Serikali iondoe vibanda vilivyo Mbele ya Biashara nyingine Kariakoo, hali mbaya

Kurunzi

JF-Expert Member
Jul 31, 2009
9,288
9,923
Hawa machinga wanatutafutia ugomvi sisi wafanyabiashara wa maduka.

Kumbuka Wenye Fremu wanalipa Kodi TRA tutashindwa kulipa Kodi kwa style hii.

Serikali waliangalie hili Jambo kwa upana zaidi.

Hapa mteja anapita wapi kuja dukani wakati duka halionekani Kodi za pango ni zaidi ya milioni kwa mwezi tunapata shida Sana kufanya biashara.

FB_IMG_1622010584359.jpg

FB_IMG_1622025242179.jpg
 
Kiukweli Machinga wanakera sanaa, na wakiguswa kidogo tuu wanakimbilia kujiona wanyonge wa mitaji midogo huku wanaumiza wenzao.

Mwenzako analipa kodi 3M unakuja kumuwekea kichanja chako kwenye mlango wa biashara yake, na pengine bidhaa ile ile anayouza kwenye fremu wewe unauza kwa bei ya debe.

Nchi haiwezi kuendeshwa kwa huruma, Serikali iondoe hawa watu, ni kero si tuu kwa wauzaji bali hata kwa wateja wengine na wapita njia.
 
Hawa machinga wanatutafutia ugomvi sisi wafanyabiashara wa maduka.

Kumbuka Wenye Fremu wanalipa Kodi TRA tutashindwa kulipa Kodi kwa style hii.

Serikali waliangalie hili Jambo kwa upana zaidi.

Hapa mteja anapita wapi kuja dukani wakati duka halionekani Kodi za pango ni zaidi ya milioni kwa mwezi tunapata shida Sana kufanya biashara.

Wapite kwenye vibaraza, au duka lako halina kibalaza?!
 
Watu wanalipa frame halafu mwingine anakuja kukuziba kwa mbele, sio sawa.

Lakini pia, kama tunataka kuwa na style ya maisha ya kustaarabika, basi tuamue kwa dhati, kama Machinga complex sasa hivi wanaishi popo tu mule, hii maana yake nini?!
 
Kutengenezwe utaratibu mzuri kwa wamachinga kufanya biashara zao,hivi ubunifu kuhusu hawa watu kufanya biashara zao kwa ubora zaidi umeshindikana kabisa au ni uvivu tu wa kufikiri...?
 
Wanatakiwa watengewe sehemu mahalum kwa ajili ya kufanya biashara zao na ili likifanyika sisi wananchi tuhamasishane kama tunanunua bidhaa kwa Machinga basi twende hayo maeneo waliyotengewa, wale watakao endelea kukaa maeneo yasiyo rasmi tusinunue bidhaa zao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawa machinga wanatutafutia ugomvi sisi wafanyabiashara wa maduka.

Kumbuka Wenye Fremu wanalipa Kodi TRA tutashindwa kulipa Kodi kwa style hii.

Serikali waliangalie hili Jambo kwa upana zaidi.

Hapa mteja anapita wapi kuja dukani wakati duka halionekani Kodi za pango ni zaidi ya milioni kwa mwezi tunapata shida Sana kufanya biashara.


View attachment 1798116
Ila kiukweli hii sio sawa....kodi anayolipa mtu wa ndani ya duka na huyo Machinga ni tofauti kabisa... kwa kweli ni uonevu mkubwa.
 
Chadema walitangaza ikifika tarehe 18/05 watawatoa machinga wote lakini wameshindwa na kulegea
 
Back
Top Bottom