Thailand
JF-Expert Member
- Nov 15, 2019
- 262
- 778
Huo hapo juu ni wizi na hujuma za waziwazi tunaofanyiwa na serikali yetu. Cost of living imekuwa kubwa, uchumi wetu wa kusuasia unazidi kuwa hoi hasa wazazi na ndugu zetu wanaotegemea mpesa, tigopesa, airtel money
kufanyiwa miamala yao. Fikiria ndani ya ada za miamala kuna 18% kodi inayoenda serikalini bado serikali imeona makusanyo hayo halali kutoka kwa wananchi hayatoshi wameona ni bora watanzania maskini waishi kama misukule ila Tozo mpya iendelee kuwanyonga watanzania.
Kama ni issue ya uzalendo, viongozi wetu wawe wa kwanza kuonesha uzalendo kwa kujipunguzia mishahara minono wanayolipana.
Kuna maoni hapa juu ya njia nyepesi serikali inaweza kuzitumia kujiongezea mapato bila serikali kutumia Tozo hii ya miamala ya simu.
SoC01 - Nini kifanyike Serikali iweze kupata pesa baada kuachana na hii tozo kandamizi na wapi pa kuwekeza
Katika hali isiyo ya kawaida maisha ya mwanadamu hasa mtanzania yanazidi kuwa magumu sana. Huku anadaiwa kodi ya nyumba na kuiendeleza familia na ndugu zake, huku anatakiwa kushiriki michango mbalimbali ya serikali ya kijiji, huku michango ya msikitini na makanisani inamsubiri yeye, huku mambo...
www.jamiiforums.com
Wananchi tuendelee kukumbuka kwamba Tozo ipo tupaze sauti kuipinga na kuwalaani viongozi wote walioleta hoja hiyo na waliohusika kuipitisha.