Serikali inaendelea kufanya ubaguzi kwenye ajira. Kama una div 1&2 au bachelor degree jua upo kwenye risk ya kutoajiriwa

Serikali mara kwa mara imekuwa ikiwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kufaulu lakini jambo la kusikitisha unapofika wakati wa ajira serikali hiyo hiyo inawabagua tena.

Tumeona kwenye ajira za polisi wanaotakiwa ni wale ambao hawakufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne. Yaani waliopata divisheni Four ila waliofaulu vizuri kwa kupata divisheni one na Two hawatakiwi.

Sanjari na hilo, kuna ubaguzi mkubwa unafanywa na serikali kwenye utoaji wa ajira hasa kwa wahitimu wenye elimu ya juu i.e bachelor degree holders kulinganisha na level zingine za kielimu kama vile diploma na certificate.

Mfano mimi nimehitimu kidato cha nne mwaka 2011. Kwakuwa nilikuwa na ndoto ya kufika mbali kielimu kama serikali inavyosisitiza, nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Sikuishia hapo, niliendelea kukazana kwa nguvu zote na maarifa yote na hatimaye nikafanikiwa kuendelea na elimu ya juu na sasa ni mhitimu wa moja ya chuo kikubwa hapa nchini

Lakini katika yote, wenzangu niliomaliza nao kidato cha nne wakapata ufaulu wa divisheni Four kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti leo hii ni waajiriwa wa serikali wanakula keki ya Taifa.

Niliomaliza nao kidato cha sita wakakosa sifa (qualifications) za kujiunga chuo kikuu wakaenda kusomea ualimu ngazi ya diploma tayari wote wameajiriwa serikalini

Lakini mimi niliyefuata ushauri wa serikali wa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa kufikia kiwango cha elimu ya juu leo naonekana sina thamani kwani serikali ile ile iliyonihamasisha kusoma kwa bidii ndio ile ile imeniweka mtaani kwa takribani miaka minne sasa. Kwa maana nyingine kiherehere changu cha kusoma kwa bidii na kufaulu leo hii ndio kinaniponza kwa sababu kama ningefeli kidato cha nne au sita leo ningekuwa ni miongoni mwa wanaofaidi keki ya Taifa.

Mwisho wa yote kama serikali haina mpango wa kuajiri wahitimu wenye bachelor degree tunaomba itamke hadharani ilikusudi vijana tujue moja kwani hata ajira zinapotangazwa wenye bachelor degree wanaoajiriwa ni wachache sana tena nafikiri ni katika jitihada za serikali kuficha dhambi ya ubaguzi wanayoifanya isijulikane kirahisi.
mkuu hapa umesema ukweli, tatizo hili yabidi kuwepo mwakilishi wa kuliwasilisha bungeni haraka sana.

Viongozi wengi ktk ngazi za juu ni mbulula na vilaza waliorisiti na kuunga elimu. Elimu zao ni za kuungia/ Kuungaunga. Unakuta kiongozi ana PhD, ila PhD yake ameipata kwa rushwa na kwa kujuana kisa tuu ni mbunge.

Hawahawa viongozi wamezaa mbulula na vilaza kama wao. Watoto wao ni form four failure, watu wa div four na zero. Hii ni kwaajili ya ugumu wa vichwa vyao kama vya baba zao na mama zao, then wanaungishwa certificate na diploma.

Hivyo basi ndo maana ajira na kazi nyingi wanapewa form four failure, div four, certificate na diploma maana wengi wao ni watoto wa viongozi.

Pia viongozi wanawakomoa wenye akili waliosoma moja kwa moja bila kuungia, kisa wao na watoto wao ni vilaza wanasoma kwa kuungia.

Hili swala ni la kusikitisha sana, wanaharakati na wabunge wenye akili timamu, ambao hawakuungia elimu walipeleke bungeni likadiskasiwe.
 
Serikali mara kwa mara imekuwa ikiwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kufaulu lakini jambo la kusikitisha unapofika wakati wa ajira serikali hiyo hiyo inawabagua tena.

Tumeona kwenye ajira za polisi wanaotakiwa ni wale ambao hawakufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne. Yaani waliopata divisheni Four ila waliofaulu vizuri kwa kupata divisheni one na Two hawatakiwi.

Sanjari na hilo, kuna ubaguzi mkubwa unafanywa na serikali kwenye utoaji wa ajira hasa kwa wahitimu wenye elimu ya juu i.e bachelor degree holders kulinganisha na level zingine za kielimu kama vile diploma na certificate.

Mfano mimi nimehitimu kidato cha nne mwaka 2011. Kwakuwa nilikuwa na ndoto ya kufika mbali kielimu kama serikali inavyosisitiza, nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Sikuishia hapo, niliendelea kukazana kwa nguvu zote na maarifa yote na hatimaye nikafanikiwa kuendelea na elimu ya juu na sasa ni mhitimu wa moja ya chuo kikubwa hapa nchini

Lakini katika yote, wenzangu niliomaliza nao kidato cha nne wakapata ufaulu wa divisheni Four kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti leo hii ni waajiriwa wa serikali wanakula keki ya Taifa.

Niliomaliza nao kidato cha sita wakakosa sifa (qualifications) za kujiunga chuo kikuu wakaenda kusomea ualimu ngazi ya diploma tayari wote wameajiriwa serikalini

Lakini mimi niliyefuata ushauri wa serikali wa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa kufikia kiwango cha elimu ya juu leo naonekana sina thamani kwani serikali ile ile iliyonihamasisha kusoma kwa bidii ndio ile ile imeniweka mtaani kwa takribani miaka minne sasa. Kwa maana nyingine kiherehere changu cha kusoma kwa bidii na kufaulu leo hii ndio kinaniponza kwa sababu kama ningefeli kidato cha nne au sita leo ningekuwa ni miongoni mwa wanaofaidi keki ya Taifa.

Mwisho wa yote kama serikali haina mpango wa kuajiri wahitimu wenye bachelor degree tunaomba itamke hadharani ilikusudi vijana tujue moja kwani hata ajira zinapotangazwa wenye bachelor degree wanaoajiriwa ni wachache sana tena nafikiri ni katika jitihada za serikali kuficha dhambi ya ubaguzi wanayoifanya isijulikane kirahisi.
Kazi ya polisi kwa Tz inahitaji mtu ambaye amefeli, sababu ni ya kutumia nguvu na siyo akili, fikiria unatumwa kwenda kumwekea madawa ya kulevya mfukoni raia ambaye hana hatia au kumpiga mpaka afe kisa amegoma kusema unachotaka wewe. sikushauri uwe polisi ni dhambi kubwa sn.
 
Wasaidizi wa Mhe.Rais mliopo humu ndani Tunaomba Sana mfikishieni Rais wetu hili jambo.Ki ukweli Kwa Ushauri wangu kama Wizara ya Mambo ya ndani imesema na kutamka kuwa Kuna Ajira 1000 za Polisi Nyingine zinakuja Kwa wale wasio na vyeo basi Hao vijana walioitwa Usaili DSM muwaangalie kwa jicho la Tatu.Wapo wachache idadi yao sio Kubwa ni elfu Moja na ushee.Naimani Serikali ya Mama Yetu Kipenzi Mhe.Samia Suluhu Hassan inaweza ikatamka lolote na hata kuitwa hao Vijana wote ni wazalendo ambao wamefuzu vigezo vya vyeti na kuwa na sifa Sahihi.Tunaomba Mama Muwape tu hizo nafasi Vijana.IGP Sirro na Viongozi wengine wa Polisi fikisheni hii na mumuombe Mama Yetu Kipenzi.Mungu Ibariki Tanzania
Yaani mm na degree yangu nikawe mlinzi bank? acha niendeshe bodaboda asee
 
Hapo inabidi watu waanze kufeli maksudi ili wapate nafasi za upolisi ....

Huwezi kuwa polisi kama hujapata zero form four ..
Labda niseme hivi: Tanzania kumekuwa na obsession ya wanafunzi kusoma ili wafaulu mitihani. Lengo la elimu siyo kufaulu mtihani bali kuelimika. Hivyo basi ajira zinatakiwa kutolewa kwa kuzingatia vigezo vingi na siyo kigezo cha ufaulu tu, kwani kama nilivyosema, kuna watu wengi wamefaulu vizuri sana lakini hawajaelimika. Nini kifanyike? Kama kuna post ya kazi ya kujaza, na sifa yake ni A level secondary, basi ni vizuri kuchagua ma-applicant kutoka kila daraja i.e. 1, 2, 3, na 4; halafu washindanishwe ili kupata watu qualified wa kujaza hizo nafasi.
 
Hiyo ni sahihi kabisa ukienda kwenye ukurasa wa tume ya utumishi unakuta nafasi za ajira kwa cheti na diploma ni nyingi zingine hata ambazo mtu mwenye degree anaweza omba lakini utasikia tunataka cheti na diploma mpaka nacheka na kujiuliza Sasa wanaogopa nini watu wa degree
 
mkuu hapa umesema ukweli, tatizo hili yabidi kuwepo mwakilishi wa kuliwasilisha bungeni haraka sana.

Viongozi wengi ktk ngazi za juu ni mbulula na vilaza waliorisiti na kuunga elimu. Elimu zao ni za kuungia/ Kuungaunga. Unakuta kiongozi ana PhD, ila PhD yake ameipata kwa rushwa na kwa kujuana kisa tuu ni mbunge.

Hawahawa viongozi wamezaa mbulula na vilaza kama wao. Watoto wao ni form four failure, watu wa div four na zero. Hii ni kwaajili ya ugumu wa vichwa vyao kama vya baba zao na mama zao, then wanaungishwa certificate na diploma.

Hivyo basi ndo maana ajira na kazi nyingi wanapewa form four failure, div four, certificate na diploma maana wengi wao ni watoto wa viongozi.

Pia viongozi wanawakomoa wenye akili waliosoma moja kwa moja bila kuungia, kisa wao na watoto wao ni vilaza wanasoma kwa kuungia.

Hili swala ni la kusikitisha sana, wanaharakati na wabunge wenye akili timamu, ambao hawakuungia elimu walipeleke bungeni likadiskasiwe.
Kuna mtu mwenye busara alishawahi kunambia kuwa ukiweka viongozi wasio na utu wataendeleza kariba yao, ukiweka wenye vyeti feki wataendeleza kariba yao kwa watakaowaleta katika mfumo, ukiweka makahaba katika uongozi watavuta makahaba wenzao kwenye uongozi.

So sijui tunatazama watu tunaowaachia kushika nyadhifa maana sijui huwa tunajisahaulisha kuwa hawa watu wakishafika kule juu hurejea asili zao....

Hivi unategemea mtu ambaye amefoji vyeti hadi kufika juu aje aweke mtendaji mwenye vyeti halali vya hadhi ya juu ili aje wajibishwa?!

Wazee wengi waliopo serikalini wana elimu za kuunga unga so wanaendeleza utamaduni huo sababu they are looking after their own kind......
 
Kwa Askari polisi ninaowafaham Mimi yaan niliotoka nao sehemu moja sikumbuki Kama Kuna mtu alienda polisi angalau akiwa hata na division three form four.

Wote walioenda polisi ni wale waliofeli form four hasa wenye division 29 ,30 ,31,na 32. Baadae nikaja gundua why polisi wanapenda waliofeli ,jibu ni kwamba wanataka kuwatumikisha kwa muda mrefu Sana maana wanajua kabisa mtu mwenye matokeo hayo hata akiamua kujiendeleza kutoboa ni mbinde Sana Zaid wanastafu huku wakiwa na mbavu mbili begani.

Kuna mdada mtaani kwetu alikuwa kilaza wa kutupwa yaan alitoka na 32 form four Leo ni Askari na anavimba balaa akijaga rikizo Ila kichwan ni zero brain na hata akiamua kujiendeleza Sina Iman km anaweza pata hizo credit tatu na kutoboa paper la six maana hamna kitu.

Hivyo ndugu yangu hiyo kaz ukiwa na vyeti Safi huwez zingatiwa maana Kwanza watakuhofia sana wale waliounga unga Sana na kupata walau diploma maana wanajua unakuja kutakeover nafas zao .kazi ya upolisi asilimia kubwa ni ya watu vilaza Sana wale toleo la mwisho kabisa ingawa wapo baadhi wenye elimu Safi kabisa Ila hao walioingia na elimu saf jua kabisa lazima Ana mtu mzito huko huko kitengoni ndio maana akingia bila shida .

Askari kalibia asilimia 90 waliingia huko wakiwa na four mbovu ,asilimia 10 waliingia na elimu Safi na ndio hao wanaowaongoza hao vilaza wengi.
 
Serikali mara kwa mara imekuwa ikiwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kufaulu lakini jambo la kusikitisha unapofika wakati wa ajira serikali hiyo hiyo inawabagua tena.

Tumeona kwenye ajira za polisi wanaotakiwa ni wale ambao hawakufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne. Yaani waliopata divisheni Four ila waliofaulu vizuri kwa kupata divisheni one na Two hawatakiwi.

Sanjari na hilo, kuna ubaguzi mkubwa unafanywa na serikali kwenye utoaji wa ajira hasa kwa wahitimu wenye elimu ya juu i.e bachelor degree holders kulinganisha na level zingine za kielimu kama vile diploma na certificate.

Mfano mimi nimehitimu kidato cha nne mwaka 2011. Kwakuwa nilikuwa na ndoto ya kufika mbali kielimu kama serikali inavyosisitiza, nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Sikuishia hapo, niliendelea kukazana kwa nguvu zote na maarifa yote na hatimaye nikafanikiwa kuendelea na elimu ya juu na sasa ni mhitimu wa moja ya chuo kikubwa hapa nchini

Lakini katika yote, wenzangu niliomaliza nao kidato cha nne wakapata ufaulu wa divisheni Four kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti leo hii ni waajiriwa wa serikali wanakula keki ya Taifa.

Niliomaliza nao kidato cha sita wakakosa sifa (qualifications) za kujiunga chuo kikuu wakaenda kusomea ualimu ngazi ya diploma tayari wote wameajiriwa serikalini

Lakini mimi niliyefuata ushauri wa serikali wa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa kufikia kiwango cha elimu ya juu leo naonekana sina thamani kwani serikali ile ile iliyonihamasisha kusoma kwa bidii ndio ile ile imeniweka mtaani kwa takribani miaka minne sasa. Kwa maana nyingine kiherehere changu cha kusoma kwa bidii na kufaulu leo hii ndio kinaniponza kwa sababu kama ningefeli kidato cha nne au sita leo ningekuwa ni miongoni mwa wanaofaidi keki ya Taifa.

Mwisho wa yote kama serikali haina mpango wa kuajiri wahitimu wenye bachelor degree tunaomba itamke hadharani ilikusudi vijana tujue moja kwani hata ajira zinapotangazwa wenye bachelor degree wanaoajiriwa ni wachache sana tena nafikiri ni katika jitihada za serikali kuficha dhambi ya ubaguzi wanayoifanya isijulikane kirahisi.
Kazi ya upolisi haiitaji ufaulu mkubwa ,nyinyi wenye madigirii mnatakiwa mjiajiri 😂😂
 
You need not regret kazi utapata tena yenye heshima kulingana na taaluma yako. Achana na upolisi kazi ambayo aina heshima mtaani. Ujue polisi wote wakisoma sana nani atalinda Benki na majumba ya ma- DC, RC, Waziri, na waheshimiwa waliofeli pia form four na six
 
Ila wabongo tunalalamika aiseeeeee.

Kwenye kila kitu. Kila kitu.
Wabongo bhana!

Mafanikio kidogo tu tayari unajiona umepatia maisha na kuanza kudharau wengine!

Hata hivyo Heri yako usiyelalamika leo maana ipo siku yaja nawe utalia na kusaga meno!
 
Kwahiyo walipata four wasiajiriwe au hawastahili kupata ajira acha ujinga nawao ni binadam na wanahaki kama wewe kama umesoma sana umefaulu vizuri pambana elimu yako ikusaidie utoke kimaisha sio uone wengine wanafaa wengine hawafai
 
Serikali mara kwa mara imekuwa ikiwahimiza wanafunzi kusoma kwa bidii na kufaulu lakini jambo la kusikitisha unapofika wakati wa ajira serikali hiyo hiyo inawabagua tena.

Tumeona kwenye ajira za polisi wanaotakiwa ni wale ambao hawakufanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne. Yaani waliopata divisheni Four ila waliofaulu vizuri kwa kupata divisheni one na Two hawatakiwi.

Sanjari na hilo, kuna ubaguzi mkubwa unafanywa na serikali kwenye utoaji wa ajira hasa kwa wahitimu wenye elimu ya juu i.e bachelor degree holders kulinganisha na level zingine za kielimu kama vile diploma na certificate.

Mfano mimi nimehitimu kidato cha nne mwaka 2011. Kwakuwa nilikuwa na ndoto ya kufika mbali kielimu kama serikali inavyosisitiza, nilisoma kwa bidii na kufanikiwa kuendelea na elimu ya kidato cha tano na sita.

Sikuishia hapo, niliendelea kukazana kwa nguvu zote na maarifa yote na hatimaye nikafanikiwa kuendelea na elimu ya juu na sasa ni mhitimu wa moja ya chuo kikubwa hapa nchini

Lakini katika yote, wenzangu niliomaliza nao kidato cha nne wakapata ufaulu wa divisheni Four kisha kujiunga na mafunzo ya ualimu ngazi ya cheti leo hii ni waajiriwa wa serikali wanakula keki ya Taifa.

Niliomaliza nao kidato cha sita wakakosa sifa (qualifications) za kujiunga chuo kikuu wakaenda kusomea ualimu ngazi ya diploma tayari wote wameajiriwa serikalini

Lakini mimi niliyefuata ushauri wa serikali wa kusoma kwa bidii na kufaulu kwa kufikia kiwango cha elimu ya juu leo naonekana sina thamani kwani serikali ile ile iliyonihamasisha kusoma kwa bidii ndio ile ile imeniweka mtaani kwa takribani miaka minne sasa. Kwa maana nyingine kiherehere changu cha kusoma kwa bidii na kufaulu leo hii ndio kinaniponza kwa sababu kama ningefeli kidato cha nne au sita leo ningekuwa ni miongoni mwa wanaofaidi keki ya Taifa.

Mwisho wa yote kama serikali haina mpango wa kuajiri wahitimu wenye bachelor degree tunaomba itamke hadharani ilikusudi vijana tujue moja kwani hata ajira zinapotangazwa wenye bachelor degree wanaoajiriwa ni wachache sana tena nafikiri ni katika jitihada za serikali kuficha dhambi ya ubaguzi wanayoifanya isijulikane kirahisi.
Haiwezi kukulipa kwa degree yako walimu mpo wengi sana
 
Hapo inabidi watu waanze kufeli maksudi ili wapate nafasi za upolisi ....

Huwezi kuwa polisi kama hujapata zero form four ..
Ukisema hivyo unakosea, semea connection mkuu.... Kama huna connection kwa maisha ya sasa mafanikio utayapata kwa kutoka jasho la meno na damu kila kona ya mwili wako! Utateseka mno ili kufanikiwa iwe kupata kazi ama michongo tu ya kukutoa kimaisha.
 
Hiyo ni sahihi kabisa ukienda kwenye ukurasa wa tume ya utumishi unakuta nafasi za ajira kwa cheti na diploma ni nyingi zingine hata ambazo mtu mwenye degree anaweza omba lakini utasikia tunataka cheti na diploma mpaka nacheka na kujiuliza Sasa wanaogopa nini watu wa degree
Upuuzi wao ni kutaka Advanced dipoloma ambayo kwa sie wa NTA level 6 inakuwa ni diploma ila sio ile advanced ya ki old school wanayotaka serikali!

Yani Diploma za vyuo vya sikuhizi ukiombea kazi ajira portal zinagoma inataka advanced diploma ya kizamani ile ambayo ni equivalent na degree sasa sijui serikali ina mawazo gani? Ifikie mahali Diploma zote ziwe acceptable sio ile tu wanayoita wao “Advanced diploma”
 
Mimi binafsi Naona suala la ajira ni mtambuka na Lina sekta yake ya ajira chakufanya shauri serikali ifanye nini ili kuboresha .LENGO LA SERIKALI NI KUCHUKUA USHAURI MZURI NA KUUFANYIA KAZI KUPITIA VYOMBO HUSIKA.NA PIA USILALAMIKE NDUGU SERIKALI NI SIKIVU MNO TENA CHINI YA SSH 💥💥 MAMBO NI FIRE JAMANI
 
Back
Top Bottom