Serikali imenunua tena mashangingi 26 mapya kimya kimya!

Lakini wakuu, gazeti la Citizen halikuchunguza kwa makini iwapo pesa ya kununulia magari hayo imelipwa yote au ni sehemu ya deni linalolipwa kidogokidogo au ni mkopo mwingine mpya kabisa.

Hizo Toyota Land Cruiser V8 ni ghali sana na inabidi ijulikane kama ni mkopo mpya kabisa mbali na mikopo mingine ambayo serkali inadaiwa na makampuni kupitia JETRO -Japan External Trade Organisation.

Kwa hizo bilioni 4.2 itakuwa ni mkopo ambao si serikali ya leo itakayolipa bali ni serikali zijazo.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Umeongea point kubwa sana. Watakuwa wamenunua kwa mkopo tu maana siku zote Serikali inapiga kelele haina pesa hivyo sidhani kama waliweza kulipa hiyo pesa kwa mkupuo. Ukiweka na riba ambayo inaweza kabisa kuwa kati ya 10% to 20% ya gharama halisi basi gharama ya magari yale ndio inazidi kupaa!!!!

Lakini wakuu, gazeti la Citizen halikuchunguza kwa makini iwapo pesa ya kununulia magari hayo imelipwa yote au ni sehemu ya deni linalolipwa kidogokidogo au ni mkopo mwingine mpya kabisa.

Hizo Toyota Land Cruiser V8 ni ghali sana na inabidi ijulikane kama ni mkopo mpya kabisa mbali na mikopo mingine ambayo serkali inadaiwa na makampuni kupitia JETRO -Japan External Trade Organisation.

Kwa hizo bilioni 4.2 itakuwa ni mkopo ambao si serikali ya leo itakayolipa bali ni serikali zijazo
.
 
Kelele za wananchi hata zikifika mbinguni serikali ya chama hiki cha mananiiiii itaendelea kutanua kama kawa. Tusubiri tu rais ajaye. Akitoka chama hikihiki cha mananiiii tutaendelea na libeneke hilihili.
 
Katika hayo matumizi ya kununua magari, nyuma ya pazia kuna siri nzito, ila sio muda mrefu watanzania watajua tu.

Kinachofanya watanzania hao wasijue kitu hicho hadi leo baada ya miaka hamsini ya kuwa huru ndicho kinachofanya ichuhukue zaidi ya miaka hamsini mingine kabla hawajakijua. Watanzania wanaamka pole pole sana kuliko wanavyotakiwa wawe.
 
Mashangingi ndo magari yenye usalama kwa viongozi wetu hata hao viongozi wa chama chenu CDM ndo wanayotumia hv unaendaje kagera na escudo hata aje nani kutawala mashangingi V8 ndo watatumia acheni wivu wa kijinga
Enzi za Nyerere V8 hazikuwepo na miundo mbinu ya barabara ilikuwa mibovu lakini kazi ilikuwa inafanyika na huko Kagera kulikuwa kunaendeka, iweje sasa hivi wakati mtandao wa barabara za lami ni Nchi nzima??? bado viongozi wetu wanaendekeza udhaifu na uzembe ktk utendaji.
 
Pasco,'
Nakushauri utoke nje ya Tanzania kwa miezi miwili tu. Utakaporudi hata mtazamo wako utakuwa umebadilika kabisa.
Watanzania wa leo sio wale waliokuwa wanafurahia t-shirt na ubwabwa.
Mkuu Jasusi, hapa sasa ndio nimeanza angalau kukuelewa, kumbe Watanzania unaowazungumzia wewe, kuwa wamebadilika, ni hawa wenzetu wenye exposure kama hawa wengi wao waliomu humu jf!, hivyo umenishauri nami nitafute fursa ya kutoka nje ya Tanzania nami nijipatie exposure japo ya miezi miwili, hivyo nitakapo rejea nchini, mtazamo wangu, utakuwa umebadilika!.

Mimi nilimaani Watanzania wapiga kura zinazo matter, hawa ni wale wenzangu na mimi ambao watoto wao huweza kuvaa nguo mpya tena za mtumbani mara moja kwa mwaka, au siku ya Iddi, au siku ya Krismasi!. Watanzania hawa ndio wale wanaishi katika lindi la umasikini uliotopea, ambao wameaminishwa "mpaji ni Mungu", na wanaishi kwa kutegemea "riski kwa Mungu", na wameridhika na umasikini wao kwa sababu ndio walichopewa na Mungu.

Hawa ndio wapiga kura walio wengi, ni hawa ndio kura zao zinazo detetermine nani anakuwa rais wa Tanzania 2015!.
Watanzania hawa wakishagawiwa zile T-shirt na kofia, na kupewa shibe ya siku moja, huiona CCM ndie mkombozi wao waliyeletewa na Mungu awakomboe, na kwa sababu siku zote, CCM is the only party they've known tangu wengi wao wamezaliwa!, na hiki ndicho chama watakacho kipigia kura maisha yao yote!.

Kama mambo yenyewe ya kubadili mtazamo ni angalau lazima mtu kajieposure, nakuhakikishia, hizo kura za hao wote wenye hako kaji exposure, bado hazitatosha kuleta mabadiliko, unless wale wote wenye hivyo viji exposure, watashuka chini ground zero, na kuwahadithia wale wenzangu na mimi kuwa umasikini wao haijatokana na Mungu, kuna dubwana ambalo ndilo chanzo cha umasikini wao, na kama wasipoliondoa, wataendelea vivyo hivyo, kuzaliwa masikini na kufa masikini kwa kutegemea t-shirt, kofia na shibe ya siku moja dhidi ya njaa ya miaka mitano mingine!, CCM itaendelea kutawala!.
 
Kwa vile Watanzania huwa wanawachagua watu kutokana na kuwatazama usoni na kuyasikiliza maneno yao matamu, majaaliwa ya CCM kuendelea kutawala ile miaka 50 mingine tuliyoelezwa humu, yanategemea atajayesimamishwa na sio sio matendo ya CCM na serikali yake katika miaka 50 iliyotangulia!.

Japo matendo hukidhi haja maridhawa kuliko maneno, Watanzania walio wengi huridhika na maneno matamu ya uwongo na hadaa za CCM mwaka hadi mwaka, ukijumlisha na ile hali ya umasikini uliotopea wa Watanzania walio wengi, zile zile T.shirt na kofia, na ile shibe ya siku moja ya kuamkia siku ya election ave, inatosha kutuletea matokeo yale yale nasi tukiendelea na nyimbo zetu zile zile huku miaka ikizidi kukatika!.

Huu ni sehemu ndogo tuu ya ukweli mchungu tunaousubiria 2015!.

"Mark my words"!.

God Bless Tanzania.

Pasco.

Nadhani uko sahihi Mkuu ila ukweli utajulikana baada ya muda kufika.Huwa nawashangaa sana wanasiasa hasa wa ccm kwa sababu:
1.Wanajua hawawezi kutekeleza lakini wanaahidi.
2.Hujiumbua wenyewe ,mwingine akiendeleza walichojiumbua humlaumu.
3.Huanzisha mipango na kuihujumu wenyewe.
4.Hawaoni shida kuiba kwenye mfuko ulio wazi na kuweka kwenye mfuko wa siri na kutegemea uwazi katika matumizi.Na mwisho wa hili ni kugeukana.
 
Mkuu Jasusi, hapa sasa ndio nimeanza angalau kukuelewa, kumbe Watanzania unaowazungumzia wewe, kuwa wamebadilika, ni hawa wenzetu wenye exposure kama hawa wengi wao waliomu humu jf!, hivyo umenishauri nami nitafute fursa ya kutoka nje ya Tanzania nami nijipatie exposure japo ya miezi miwili, hivyo nitakapo rejea nchini, mtazamo wangu, utakuwa umebadilika!.

Mimi nilimaani Watanzania wapiga kura zinazo matter, hawa ni wale wenzangu na mimi ambao watoto wao huweza kuvaa nguo mpya tena za mtumbani mara moja kwa mwaka, au siku ya Iddi, au siku ya Krismasi!. Watanzania hawa ndio wale wanaishi katika lindi la umasikini uliotopea, ambao wameaminishwa "mpaji ni Mungu", na wanaishi kwa kutegemea "riski kwa Mungu", na wameridhika na umasikini wao kwa sababu ndio walichopewa na Mungu.

Hawa ndio wapiga kura walio wengi, ni hawa ndio kura zao zinazo detetermine nani anakuwa rais wa Tanzania 2015!.
Watanzania hawa wakishagawiwa zile T-shirt na kofia, na kupewa shibe ya siku moja, huiona CCM ndie mkombozi wao waliyeletewa na Mungu awakomboe, na kwa sababu siku zote, CCM is the only party they've known tangu wengi wao wamezaliwa!, na hiki ndicho chama watakacho kipigia kura maisha yao yote!.

Kama mambo yenyewe ya kubadili mtazamo ni angalau lazima mtu kajieposure, nakuhakikishia, hizo kura za hao wote wenye hako kaji exposure, bado hazitatosha kuleta mabadiliko, unless wale wote wenye hivyo viji exposure, watashuka chini ground zero, na kuwahadithia wale wenzangu na mimi kuwa umasikini wao haijatokana na Mungu, kuna dubwana ambalo ndilo chanzo cha umasikini wao, na kama wasipoliondoa, wataendelea vivyo hivyo, kuzaliwa masikini na kufa masikini kwa kutegemea t-shirt, kofia na shibe ya siku moja dhidi ya njaa ya miaka mitano mingine!, CCM itaendelea kutawala!.
Pasco,
Labda hujanielewa, au sikujieleza vizuri. Nafasi ya kutoka nje ya nchi kwa muda inakupa perspective ambayo kwa sasa
naona huwezi kuitambua kwa sababu you are always inside the box. Nitakupa mfano mmoja tu. Dada yangu mkubwa, ambaye naye hajatoka nje ya nchi kwa miaka mingi, alikuwa mwenyekiti wa tawi la CCM pale Mugumu kwa miaka na miaka. Nilipomtembelea kabla ya uchaguzi wa 2010 nilikuta amebadilika nikamuuliza imekuwaje? Akasema viongozi wengi wa CCM pale Mugumu na Musoma ni wezi na wafanyibiashara. Freeman Mbowe alipopita pale Mugumu dada alienda kumsikiliza na baadaye akaamua kuachana na CCM. Na huyu, kama wewe, naye alikuwa akiamini kuwa CCM itatawala milele na maslahi yake yalikuwa ndani ya CCM. Lakini sasa hivi ndiye anayehamasisha akina mama waachane na CCM katika eneo lake. Nimetaja kutoka nje ya nchi kama mfano tu wa kukuondoa ndani ya sanduku. Hope unanielewa sasa.
 
profesa maji marefu hajawasaidia waje kwa Yesu kristo atawapa kila uwezo wautakao kutenda haki
 
Kuna usemi wa kiswahili usemao sikio la kufa halisikii dawa. Usemi huu hulenga matendo (ya watu/mtu/kitu) ambayo hujirudia rudia huku yakiwa hayana faida kwa mtu husika pia kwa walengwa wake.

Hii ni CCM na serikali yake hapa Tanzania. Pamoja na serikali kujinadi mahala pengi ikiwemo bungeni kuwa itaachana na ununuzi wa magari ya kifahari maarufu kama mashangingi a.k.a Kilimo Kwanza, inaonekana ununuzi wa magari hayo ni ugonjwa sugu na unaendelea kuitafuna CCM na serikali yake.

Inasemekana magari hayo yamenunuliwa tena kwa fujo safari hii kwa wateule wa hivi karibuni wakuu wa mikoa, wilaya na baadhi ya mawaziri. Kama kweli serikali ilikuwa na nia ya dhati ya kutoendelea na ununuzi wa magari hayo ya kifahari, basi ingeanza na wateule wa hivi karibuni kwa kuwanunulia RAV4 za bepari Pinda anayejificha kwenye kivuli cha mtoto wa mkulima.

Hii ni kuipa ujiko CHADEMA? Au mmetumwa kuiua CCM kwa makusudi? Au mnataka kuiua CCM ili Nyerere asahaulike?

Same sh**** everyday
 
CCM wana hela bwana issue ni namna ya kuzitumia!
Wenye wivu mjinyonge na mwaka 2015 lazima iingie ikulu kwa kishindo msipoacha tabia ya kulalamika badala ya kuact
 
Baada ya Serikali kupiga marufuku ununuzi wa magari ya kifahari maarufu kama 'Kilimo kwanza (Land Cruiser VX V8)', naona sasa Waheshimiwa wamepata mbadala!!



Prado.jpg
 
Baada ya Serikali kupiga marufuku ununuzi wa magari ya kifahari maarufu kama 'Kilimo kwanza (Land Cruiser VX V8)', naona sasa Waheshimiwa wamepata mbadala!!



View attachment 61989
Leo nimekuta dude kama hilo limebandikwa nyuma ya tairi la akiba ujumbe usemao "LIPA KODI TUJITEGEMEE" nikawa najiuliza huku kujitegemea na aina ya anasa tunazokwenda nazo tutaweza kujitegemea kweli?
 
Pasco,
Labda hujanielewa, au sikujieleza vizuri. Nafasi ya kutoka nje ya nchi kwa muda inakupa perspective ambayo kwa sasa
naona huwezi kuitambua kwa sababu you are always inside the box. Nitakupa mfano mmoja tu. Dada yangu mkubwa, ambaye naye hajatoka nje ya nchi kwa miaka mingi, alikuwa mwenyekiti wa tawi la CCM pale Mugumu kwa miaka na miaka. Nilipomtembelea kabla ya uchaguzi wa 2010 nilikuta amebadilika nikamuuliza imekuwaje? Akasema viongozi wengi wa CCM pale Mugumu na Musoma ni wezi na wafanyibiashara. Freeman Mbowe alipopita pale Mugumu dada alienda kumsikiliza na baadaye akaamua kuachana na CCM. Na huyu, kama wewe, naye alikuwa akiamini kuwa CCM itatawala milele na maslahi yake yalikuwa ndani ya CCM. Lakini sasa hivi ndiye anayehamasisha akina mama waachane na CCM katika eneo lake. Nimetaja kutoka nje ya nchi kama mfano tu wa kukuondoa ndani ya sanduku. Hope unanielewa sasa.
Mkuu Jasusi nimekuelewa, basi nami na wale mamia kwa maelfu, tunasubiria opportunity yetu kupata mwanga wa nje ya box la "CCM Itatawala Milele", ili nasi tubadilike kama Dada yako wa Mugumu, yeye angalau alimsikia Mbowe, ngoja nasi tuwasubirie watu wakuwasikia.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom