Serikali imenunua tena mashangingi 26 mapya kimya kimya!

imamu

Member
May 20, 2012
32
7
Kuna usemi wa kiswahili usemao sikio la kufa halisikii dawa. Usemi huu hulenga matendo (ya watu/mtu/kitu) ambayo hujirudia rudia huku yakiwa hayana faida kwa mtu husika pia kwa walengwa wake.

Hii ni CCM na serikali yake hapa Tanzania. Pamoja na serikali kujinadi mahala pengi ikiwemo bungeni kuwa itaachana na ununuzi wa magari ya kifahari maarufu kama mashangingi a.k.a Kilimo Kwanza, inaonekana ununuzi wa magari hayo ni ugonjwa sugu na unaendelea kuitafuna CCM na serikali yake.

Inasemekana magari hayo yamenunuliwa tena kwa fujo safari hii kwa wateule wa hivi karibuni wakuu wa mikoa, wilaya na baadhi ya mawaziri. Kama kweli serikali ilikuwa na nia ya dhati ya kutoendelea na ununuzi wa magari hayo ya kifahari, basi ingeanza na wateule wa hivi karibuni kwa kuwanunulia RAV4 za bepari Pinda anayejificha kwenye kivuli cha mtoto wa mkulima.

Hii ni kuipa ujiko CHADEMA? Au mmetumwa kuiua CCM kwa makusudi? Au mnataka kuiua CCM ili Nyerere asahaulike?
By Mkinga Mkinga | The Citizen Reporter- Dar es Salaam | Monday, 13 August 2012

The government seems to have started off on the wrong foot in its resolve to stop purchasing expensive vehicles.

Checks by The Citizen have established that recently the government received a fleet of 26 Toyota Land Cruiser V8 vehicles. Reports availed to this newspaper confirmed that the costly vehicles, also expensive to maintain, have been bought for the ministry of Justice and Constitutional Affairs for the Constitution Review Commission (CRC).

Going by the price of Sh150 million per vehicle, it means that the purchase has cost the government Sh4.2 billion.
(mhhhh! bado hatujaweka operating & maintenance cost)

Speaking exclusively to The Citizen the minister for Justice and Constitutional Affairs, Mr Mathias Chikawe, admitted that the government has bought the 28 vehicles to cater for members of the CRC to effectively discharge their responsibilities.

"Yes we have bought about 26 new vehicles after we bought two earlier for the chairman and his deputy... but the second batch consists of about 26 and will be used by commission members and supporting staff in collecting views on the new constitution," minister Chikawe said

He said his ministry was involved in buying the vehicles for the commissioners because since the last financial year the constitutional review commission had no government vote which would have allowed the purchase of facilities for the exercise.

The move comes only weeks after the Prime Minister, Mr Mizengo Pinda, told the nation that the government had resolved to do away with expensive vehicles. He said from now on it would purchase vehicles with engine capacity of 2000cc from the 3000cc which were a norm.

Tabling his office budget in august House in Dodoma, the Premier said the government plan to do away with cars which cost more for their maintenance.

Asked why his ministry had bought the vehicles against Mr Pinda's statement, Mr Chikawe said:

"The order for the vehicles was made before the Prime Minister's statement... we have decided to buy vehicles which would withstand our kind of roads because they will take the commissioners to remote areas."

He said after the CRC finishes its work, the government might decide to auction the vehicles.
(Watauziana mafisadi wenyewe)
 
Hata Mbowe kalichukuwa lake alilojidai kulirudisha, tena kalirudia kimya kimya.
 
Katika hayo matumizi ya kununua magari, nyuma ya pazia kuna siri nzito, ila sio muda mrefu watanzania watajua tu.
 
Sio kweli kuwa imeyanunua kimya kimya, tenda ilishatangazwa zamani mara baada ya uchaguzi wa 2010 na Toyota Tanzania Ltd ndio walishinda!.

Kila miaka 5 mitano serikali inayoondoka huondoka na magari yao na serikali mpyahuja na mapya!. Hata wabunge japo wangi wamerudi wale wale, zile milioni 100 za kununulia gari jipya kila mbunge amepata!. Mwaka mmoja kabla ya kuvunjwa bunge, Spika Sita alinunuliwa benzi mpya S Class 500 nyeusi. Mama Makinda naye kanunuliwa mpya S- Class 350!.

Wakuu wa wilaya mpya, wale manaibu wapya na wajumbe wa Kamati ya Kukusanya Maoni ya Katiba pia nao mashangingi mapya ni stahiki zao!.
 
Kama nikweli,I NAUMA MNO!Lakini kunasemi zababu zetu,Ukiona giza linazidi ujue asubuhi inakaribia pia Mbio zasakafuni mwisho wake kwenye ukingo!
 
Mkuu Pasco. Ishu ya msingi hapa ni ununuzi wa hayo 'mashangingi'. Serikali ya Pinda ilihaidi kupunguza ununuzi wa magari hayo, inamaana wangenunua Nissan au aina nyingine. Lkn hali halisi, magari hayo yameendelea kununuliwa, tena kwa fujo sana, sasa hapa kunakuwa na contradiction kwenye ile ahadi ya pinda. Pia, kuhusu swala la staili za viongozi, kiongozi ana staili ya gari, lakini sio lazima liwe shangingi, hata RAV4 anaweza kutumia. Hii tabia ya kununua mashangingi ni kasumba tu ya serikali ya ccm, isiyokuwa na uchungu na wananchi wake...
 
kuna wilaya zinazotumia umeme wa majenereta sasa hivi ni mgao wa kufa mtu kisa hakuna hela za kununulia mafuta. huu ujasiri wa serikali kutumia kodi zetu kununua haya mashangingi unatoka wapi!!!??? anyway, time will tell...
 
CCM CCM shika mkia., piga vita maendeleo na uadilifu ah ah ccm kufa kabisa..
Kwa ccm, kuwaletea wananchi maendeleo siyo priority. Kwao matumbo yao, ujinga kwa wananchi na amani fake ndiyo vipaumbele
 
Pasco
Mh. Lukuvi alivyokuwa anatoa taarifa kuhusu kuachana na magari ya kifahari bila shaka alijua kuwa ni stahiki yao.

Cha msingi kama serikali iko serious na statement zinazotolowa hadharani basi ni vema hayo magari ya kifahari yauzwe na atekeleze aliyoyasema.
 
Ndugu zangu if you still believe in Pinda political rhetorics then you are doomed. Jamani ni kwamba serikali haifanyi kazi kwa kauli za majukwaani za viongozi. Serikali inafanya kazi kwa kupitia waraka/secular. Kuna waraka wa serikali ambao unatumika hadi hivi sasa unaelekeza aina ya magari wanayotakiwa kununuliwa mawaziri, makatibu wakuu, RCs, DCs etc. Mpaka hadi Ijumaa waraka unaotumika ni ule wa zamani (Mashangingi).

Pinda angekuwa na nia ya dhati ya kupuguza matumizi ya serikali kwa kununua magari ya bei nafuu, angepeleka hoja hiyo kwenye baraza la mawaziri. Na kama ingepita basi waraka/secular mpya ingetoka inayoelekeza ununuzi wa magari ya viongozi. But PM is weak can't do that because he knows atakutana na vipingamizi ndani ya baraza la waziri, Because the Kikwete government is addicted in SPENDING.

Ndiyo maana hata mwaka ule alipokataa shangingi bado alinunuliwa shangingi na kuletewa. To save his face akalikataa eti wapewe wengine, lakini he coudn't do anything kwa mtu aliyenunua hilo shangingi. kwasababu anajua they guy was correct, yeye Pinda ndiye anacheza politics.

Kenya wameweza kwasababau ni suala liliokubaliwa kwenye baraza la mawaziri na kuwekewa muongozo/secular na hakuna anayethubutu kuuvunja huo muongozo. i.e kumununulia kiongozi shangingi

Nyinyi ambao mnaendelea ku-buy hizi political rhetorics za Pinda kalaghabaho. Jamaa hana nia kabisa anawazuga. Hizi zote ni dalili za chama kinachoelekea kufa hakisikii cha muazini!
 
Ndugu zangu if you still believe in Pinda political rhetorics then you are doomed. Jamani ni kwamba serikali haifanyi kazi kwa kauli za majukwaani za viongozi. Serikali inafanya kazi kwa kupitia waraka/secular. Kuna waraka wa serikali ambao unatumika hadi hivi sasa unaelekeza aina ya magari wanayotakiwa kununuliwa mawaziri, makatibu wakuu, RCs, DCs etc. Mpaka hadi Ijumaa waraka unaotumika ni ule wa zamani (Mashangingi).

Pinda angekuwa na nia ya dhati ya kupuguza matumizi ya serikali kwa kununua magari ya bei nafuu, angepeleka hoja hiyo kwenye baraza la mawaziri. Na kama ingepita basi waraka/secular mpya ingetoka inayoelekeza ununuzi wa magari ya viongozi. But PM is weak can't do that because he knows atakutana na vipingamizi ndani ya baraza la waziri, Because the Kikwete government is addicted in SPENDING.

Ndiyo maana hata mwaka ule alipokataa shangingi bado alinunuliwa shangingi na kuletewa. To save his face akalikataa eti wapewe wengine, lakini he coudn't do anything kwa mtu aliyenunua hilo shangingi. kwasababu anajua they guy was correct, yeye Pinda ndiye anacheza politics.

Kenya wameweza kwasababau ni suala liliokubaliwa kwenye baraza la mawaziri na kuwekewa muongozo/secular na hakuna anayethubutu kuuvunja huo muongozo. i.e kumununulia kiongozi shangingi

Nyinyi ambao mnaendelea ku-buy hizi political rhetorics za Pinda kalaghabaho. Jamaa hana nia kabisa anawazuga. Hizi zote ni dalili za chama kinachoelekea kufa hakisikii cha muazini!

Mkuu umesema kweli kabisa, wenzetu Kenya hakuna waziri wala nani anayetumia shangingi. Wabunge wote walipewa Volkswagen na maofisa wengine wa serikali wanatumia Corolla. Wanabana matumizi, sisi tunaongeza matumizi.

Tiba
 
Back
Top Bottom