Serikali 3 na gharama zake

Serikali 3 na gharama zake

Mchambuzi,
Ni wapi umepata wewe kuwa serikali mbili ilikuwa swala la chama? au hujui waliweza vipi kufikia maamuzi hayo?
 
Mchambuzi,
Ni wapi umepata wewe kuwa serikali mbili ilikuwa swala la chama? au hujui waliweza vipi kufikia maamuzi hayo?
Mkandara,
Serikali Mbili ni sera ya chama cha mapinduzi, ilikuwa sera bubu 1964-1977, na ikifanywa kuwa sera Rasmi ya party state 1977 ambapo katiba ya CCM ikawa ni sehemu ya katiba ya JMT.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Mkandara;10319551]Labda nirudie kusema hivi, Zanzibar wana kila sababu ya kulalamika na malalamiko yao yapo wazi kabisa. Chukulia moja Wazanzibar walidai kwamba rasilimali zetu zinazojulikana kama za Tanzania (muungano) iwe dhahabu, mafuta au gas hawafaidiki nayo, hakuna mgao maalum unaoeleweka ktk muungano huu japo jina la Tanzania linatumika.
Mkuu kwanini unatumia jicho moja kuangalia na kusoma mambo?

1. Katika jina hilo la Tanzania, znz haina mchango hata senti tano.
Hakuna ubishi kwa hilli zipo takwimu ambazo mwendawazimu peke yake atathubutu kuhoji.

2. Unaposema znz haipatai mgao wa dhahabu,mafuta na gesi hawafaidiki ni kuudanganya umma.

Znz haina bajeti ya ulinzi ya 1.2 trillion ambayo wakiambiwa wachangie 2% hawataki
Hawana bajeti ya mambo ya ndani. nje n.k.
Pesa za dhahabu na gesi ndizo zinawafikia kwa njia hiyo.
Umeme ndio huo wamelipiwa hadi wamejukuza
Achilia ada za kimatifa za mashirika yao

Katika mazingira ya sasa znz inapata 4.5 % ya pato la taifa linalotokana na hizo dhahabu na gesi ambazo hawana.

Hii maana yake ni kuwa znz inapata 4.5 ya pato la Tanganyika.

Katika pato la trilioni 12 mwaka huu, 4.5% ni karibia au zaidi ya mapato ya znz ya mwaka.
Nje yam muungano, 4.5 znz haiwezi kutengeneza kiasi hicho,

Znz inapata msaada wa bajeti achilia mbali pesa zisizo na audit.

Mwaka huu wamepewa 15 bilioni kwa ajili ya wafanyakazi wa muungano.
Yaani PAYE ya wafanyakazi wa wizara zisizo za muungano ndiyo imewapa bilioni 15.

Kwa ufupi ni kuwa znz wanapata zaidi ya kile wanachostahili kupata.

Kuna watu ambao ufikiri wao umeishia kuona pesa zinaingia bank bila kuangalia factor nyingine.

Kwa mfano, leo znz ikipewa iendeshe jeshi lake tu, 1/3 ya pato ni jeshi.Leo PAYE ya bilioni 15 hawawezi kuipata bila kutoza kodi wafanyakazi wa wizara za kilimo, afya n.k. ambazo si za muungano.

Lakini kuna kitu ambacho watu wasio ona kwa macho mawili hawakioni.
Kuwapa ajira tu ni zaidi ya kuwapa pesa.Leo asilimia 65 ya ajira za wznz zinategemea muungano.

SMZ inaajiri takribani wafanyakazi 5-10K ambao hawawezi kulipa kodi ya bilioni 1 kwa mwezi.
Wanapopewa bilioni 15 za Watanganyika ni msaada, na msaada wa kupunguiza tatizo la ajira.

Katika kuona tumeungana na watu wasioujua hesabu, sasa tunasema wana choice ambayo haituhusu wala haitugusi kwa namna yoyote.Katika muungano huu, znz hawaonewi hata sehemu moja.

Huwezi kuwa kupe mgongoni halafu ukadai ng'ombe anakuonea.Sana sana utamletea ndigana.

Mkandara huna haja ya kulalamika kwa niaba yao. Waambie kama hawataki njia nyeupe. Hebu tuambie tunawahitaji kwa lipi! tueleze Na mwisho, usiwafundishe ujinga wa kudai wakati hawajui kuchangia.

Huko ndiko kumeamsha hisia hizi na leo Watanganyika wanatambua kuwa mkoa wa Dar una mchango na uchumi mkubwa kuliko znz, lakini znz inapata mgao mkubwa wa pato la taifa kuliko Dar.

Mchango wa mikoa 21 ya Tanganyika katika uchumi wa taifa ndio uchumi wenyewe.

Ofisi ya waziri mkuu imepewa bilioni 500 kwa mikoa 21, wakati znz ambayo haina ulingano na mkoa wowote inapata kiasi cha zaidi ya bilioni 350. Huu ni ujinga ambao havumuliki

ZNZ unayosema wanaonewa, wameanzisha Maritime organization yao. Ada analipa Mtanganyika kupitia Sumatra. Unataka wapewe fungu lingine tena bank, kwa faida gani!

Yote hayo Mkandara na exposure umeyafumbia macho ukiongozwa na hisia za wababaishaji

Kama wanaonewa waondoke hatuna sababu za kuwashikilia.

Tanganyika haikwepeki ni suala la muda.


 
Nguruvi3 et al,
Nakuelewa na kuafikiana nawe...

Swali ni kwamba njia sahihi ya kuidai Tanganyika unadhani ni ipi? Unadhani msimamo wa UKAWA (which is a misnomer) kususia bunge utatusaidia kupata Tanganyika yetu? Isingekuwa vema kuteta hoja humo humo bngeni kwa uwazi na umahiri na sisi watazamaji tushawishike kupigia kura S3 na si S2?
 
Last edited by a moderator:
Mchambuzi,
Mkuu tafadhali nadhani wewe ni kati ya Great thinker wa kijiwe hiki na sii sifa ndogo hata kidogo kwani tunakutegemea utakuwa mkweli, Mzalendo, muwazi na kikubwa zaidi muadilifu ktk hayo unayoyaandika.
Kuubeza Muungano ni jambo moja na kuitaka Katiba ni jingine hivyo nakushangaa sana unapochanganya Muungano wetu na Katiba ya CCM ati ni serikali bubu iloundwa. Sisi tuliungana kwa maridhiano baina ya viongozi wa TANU (sio CCM) na Baraza la mapinduzi ambalo lilikuwa na viongozi wa ASP na wale wa Umma party. Nimeshaliweka baraza hilo kule ktk ukumbi wetu wa GT. Na Abrahman Babu alituhakikishia kwamba alikuwepo wakati wa maridhiano na yalipitishwa kweli na baraza hilo.

Swala la serikai 2, ifahamike tu kwamba hawa viongozi walitazama sababu na mahitaji yote ya kuunda serikali 1, 2 ama 3 na wametupa sababu kwa nini hawakufikia kuchagua serikali 1 ama 3 na hakuna mahala popote wameonyesha UCCM wala kwa manufaa yao isipokuwa walicholazimika kukifanya mwaka 1977 ni ku centralize madaraka ya serikali chini ya siasa ya Ujamaa. Hii ndio picha ilotufikisha hapa tulipo leo na sii serikali ngapi ndio chimbuko la Katiba mpya. Na hadi leo hi hatuna majibu ya serikali hizo kutumika maana bado population ya Zanzibar ndogo kwa asilimia karibu ile ile (mwaka 1964 ilikuwa 2.5 na leo tuna 2.9) na swala la serikali 3 bado Tanganyika itabeba mzigo ule ule ulohofiwa japo mnataka kuepa mimba hii kistaarabu.

Ndio maaana nikasema jamani swala hapa ni ku decentalize hii serikali ya CCM na ili tuweze hivyo ni lazima kwanza tutazame jinsi ya ugawaji wa mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za serikali. Iwe tuna serikali 1, 2 au 3 - fiscal decentralization inawezekana pote haihitaji Muungano kuwa Shirikisho, na wala hakuna tatizo kabisa kuwa na Fiscal federalism, isipokuwa mtihani upo katika ugawaji wa mamlaka kwa serikali zetu mbili na zile za mikoani na majimbo, vyombo na taasisi za serikali.

CCM ni kama KGB ama Chama cha Kikomunist cha China hawatakubali kuachia vitu kirahisi isipokuwa kwa mabadiliko yanayolenga kuwanufaisha wananchi na sio vyama ama kulenga kuwadhoofisha wao. Hofu ya CCM sio serikali 3 hata kidogo hili ni changa la macho tu wamepewa sababu on silver plate baada ya wajumbe wa UKAWA kuanzisha zogo la ku question Muungano wetu na hati zake. That's where they (UKAWA) went wrong na wakawapa CCM silaha ya kupigania. And they won't hasitate to use it politically kama inavyokwenda na maridhiano hayatapatikana isipokuwa UKAWA ndio watakuja gawanyika wala sii muda mrefu. CCM knows that na itafika wananchi watakubali yaishe hadi miaka ijayo.

Ebu chukulia hivi tumeunda serikali 3 na ile ya Kitaifa yenye mambo 7 ndio Dr.Slaa kashinda uchaguzi 2015, CCM wamechukua Tanganyika na CUF wameshinda Zanzibar. Sisi bara kitabadilika nini kwetu? Maana muelewe Chadema ina urahisi kushinda kiti cha Urais kuliko kushinda majimbo ama Tanganyika maana nguvu ya CCM ipo bara na vijijini msikoweza kuwafikia wananchi. Sasa hiyo serikali ya Dr.Slaa amiri Jeshi mkuu mwenye kulindwa na wakuu wa jeshi ambao ni CCM damu (KGB ya Bongo) watakuwa na sauti gani kutaka mchango wa CCM toka bara au CUF kutoka Zanzibar ili kukuza mfuko wa pamoja? - I don't think so, Hee pamoja na nani watasema! kwa hiyo ni muhimu kufikiria mfumo ambao kesho na kesho kutwa utaweza kufanya kazi sawa iwe kashinda CCM au Chadema kwa nchi husika ama Taifa zima. Kinachotakiwa sii kupunguza nguvu za CCM na kupandisha nguvu za vyama vinginevyo bali kupeleka mamlaka kunakostahili na sii kwa sababu ya kero.

Kuondoa mamlaka makubwa toka serikali ya CCM na sio serikali kuu kudhoofika pia maana focus yenu yote ni kwamba serikali kuu ni ya CCM lakini Je kesho ikiwa Chadema au CUF au NCCR mageuzi wataweza kweli kuijenga nchi pasipo vyanzo? Wataweza kweli kuondoa Ujinga, umaskini na maradhi ambayo ndio malengo yetu Kitaifa!. Wataweza kweli kuhakikisha vifo vya kina mama wajawazito vinaondoka, watoto wachanga, vifo vya ajali za magari na kadhalika. Elimu kuwa swala la nchi kweli tutafika ama nasi tunaanza alifu kwa kijiti kama Ulaya?.Haya tuna Ebola leo watapata wapi fedha za kusimamia majanga kama haya ikiwa hawana nguvu ya fedha.

Jamani leo hii, FEDHA ndio kila kitu mwenye nguvu ya fedha ndiye mwenye Dola japo sii msingi wa maendeleo lakini unapata nguvu ya kutawala. Tusianze kwa kutazama Marekani ambao katiba yao iliundwa mwaka 1788 leo wanakuja gundua mengi hayakutakiwa kuwa hivyo na ndio wanafanya amendments kila kukicha hadi haki za watu wamefanya majuzi tu baada ya miaka 200. Sisi tumekuwa katika bahati ya kukuta mambo mengi yameisha gundulika hivyo tunaendesha magari leo hi pasipo hata kuyatengeneza. Wao ilichukua karne nzima kubuni tu chombo cha moto..

Anyway niishie hapo tutaendelea baadaye. samahani msione naandika na kisha ku edit ni kwa sababu naingiliwa sana kila napoandika hoja Pc huzimika katikati..hivyo nina kipindi kifupi sana cha kuandika na kuweka hoja zangu. Why I don't know..
 
Nguruvi3, Mchambuzi et al,

Kwa kuchangia zaidi, nitoe maoni yafuatayo mintarafu ya mtafaruku huu wa S2 au S3 na hatma ya JMT:

1. UKAWA inajumuisha CUF, na CUF ndiyo iliyoshinikiza mabadilko ya Katiba ya Znz kutamka kuwa Znz ni nchi katika kile kinachojulikana kama Muafaka.

2. Naamini Watanganyika/ Watanzania Bara wengi wamezoea kuamini kuwa Znz si nchi, hivyo mfumo wa S2 unawaridhisha (conservatives). Na wengine wanasema hata hayo mabadiliko ya kusema Znz ni nchi hayana maana, kwani Znz inatambulika wapi kimataifa?

3. JK pia alichukua msimamo huu wa kubariki mabadiliko ya Katiba ya Znz bila kujua athari zake mbele ya safari, kwa upande mmoja akitaka kuonekana kama mpatanishi na ili akubalike kwa Wanzanzibari, lakini pia kwa upande mwigine akitarajia kuwa ataanzisha mchakato wa Katiba ya JMT itakayokuwa juu ya ile ya Znz: alitaka kupumua. Ikumbukwe pia kuwa Karume mtoto alikuwa na msimamo wa Znz ni nchi. Hivyo, kwa namna fulani JK ni “lame duck” kwenye utata wa suala la utaifa wa Znz.

4. Wale wanaounga mkono S3 wanafanya hivyo kwa msingi wa retaliation (a la Mchambuzi)
5. Mtaji wa CCM kwenye kukosoa Rasimu uko kwenye sehemu tatu:
a. Takwimu za Tume,
b. Hoja kuwa serikali ya Muungano itakuwa haina uhusiano na mwananchi wa kawaida (kwa madai kuwa mwananchi anataka mbolea na masoko, na panadol na chumvi na mafuta ya taa!). Binafsi sijaridhika na maelezo na utetezi wa Tume kuhusu uwakilishi wa takwimu zao na uwiano wa hoja
c. Athari/changamoto za S3 kama zilivyobainishwa na Ripoti ya Tume (hisia za utaifa nk) kwa ujumla ni “killer assumptions” za “Union Project”.
6. Naamini Tume ilipendekeza S3 ikiamini ni njia ya kuilazimsha (serikali ya) CCM ishughulikie kero za muungano za miaka nenda rudi. Iliamini pia pendekezo litaibua mjadala chanya wa umma kuhusu aina ya muundo /muungano unaofaa. Naamini, kinyume na matarajio ya Tume, hata hivyo, pendekezo hilo la S3 limeibua hisia kali, mjadala hasi na hata kuibuka kwa UKAWA.
Kwa ujumla na kwa kifupi, pendekezo hilo na jinsi lilivyobebewa bendera na UKAWA kwa upande mmoja, na msimamo wa “baadhi ya wajumbe “ wa Tume kwa upande mwingine, kumeleta mgawanyiko miongoni mwa jamii ya Watanzania. Badala ya mjadala wa Katiba mpya kuchangia kujenga jamii yenye umoja, kuna hatari ya kumalizika kwa mchakato huu tukiwa tumegawanyika zaidi. Nadhani kina Warioba sasa wanajuta kwani nchi inaweza kuingia kwenye machafuko kama misimamo hii mikali ya UKAWA na Tanzania Kwanza itaendelea.

Way Forward
1. UKAWA wakajenge hoja bungeni huku viongozi wao wengine wakiwa nje ya bunge wakielimisha wananchi. Hili litawafanya wasionekane kama kikundi cha watu wanaotaka vurugu.
2. Wajitokeze wanasheria (Lissu hawezi hili?) kujenga hoja na hata kufungua shauri mahakamani kupinga mabadiliko ya katiba ya Znz kuwa yalikiuka katiba. Najua alikuwa akipinga sana ukiukwaji huu wakatiba huko nyuma kwenye mijadala mbalimbali.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,
Mkuu wangu bado wanisikitisha sana na hoja zako ambazo kila wakati unayemlaumu ni Mkandara pasipo kurudi na majibu ya kuridhisha isipokuwa chuki yako bunafsi na Utanganyika wako ambao mwalmu alisema ni sawa na kula nyama ya mtu.

Hao Wazanzibar unawasema kila mara ni katika kundi lako hivyo sioni tofauti yako na wao hivyo mjadala wako umejengwa kwa hja zile ziole za Uzanzibar na Utanganyika, mimi hazinisaidii kupata majibu yote.

Haya sasa umekuja na hili la kwamba Zanzibar hawachangii hata sentyi moja ktk mfuko wa Taifa na unatumia Jeshi sijui hilo jeshi linapata wapi mapato yake maana nijuavyo mapato ya serikali yanatokana na vifungu hivi hivyo nakuomba uanishe hapa jinsi mapato hayo yanavyokusanywa maana pande zote mbili yaani Upande wa bara na wa Zanzibar wote wamesema moja ya kero yao ni 1. Mkanganyiko wa uchangiaji na ugawanaji wa mapato. Sasa wewe uloelewa hili kuliko hata rais alokuja kufungua Bunge la katiba na hakueleza uchangiaji na ugawanaji mapato ukoje wewe twambie unafanywa vipi. Na hata wajumbe wa tume wamefikia wao kusema uundwe mfuko wa pamoja hivyo tueleze wewe mwanzo ilikuwaje usanyaji wa mapato ya taifa na ugawajai uko vipi kiasi kwmaba wengine wote washindwe kuelewa isipokuwa wewe na wenzako.

Vyanzo vya mapato ya Taifa vletu ni hivi hapa:-
[TABLE="width: 508"]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mapato ya kodi (TRA) - 46%
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mikopo ya Misaada ya nje – 29%
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mikopo ya masharti ya Biashara - 9.4%
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mikopo ya Ndani – 9%
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mapato yasiyo ya kodi – 4%
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mapato ya Halmashauri za miji – 2.6%
[/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD]
[/TD]
[TD]
[/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,
Mkuu wangu bado wanisikitisha sana na hoja zako ambazo kila wakati unayemlaumu ni Mkandara pasipo kurudi na majibu ya kuridhisha isipokuwa chuki yako bunafsi na Utanganyika wako ambao mwalmu alisema ni sawa na kula nyama ya mtu.

Hao Wazanzibar unawasema kila mara ni katika kundi lako hivyo sioni tofauti yako na wao hivyo mjadala wako umejengwa kwa hja zile ziole za Uzanzibar na Utanganyika, mimi hazinisaidii kupata majibu yote.

Haya sasa umekuja na hili la kwamba Zanzibar hawachangii hata sentyi moja ktk mfuko wa Taifa na unatumia Jeshi sijui hilo jeshi linapata wapi mapato yake maana nijuavyo mapato ya serikali yanatokana na vifungu hivi hivyo nakuomba uanishe hapa jinsi mapato hayo yanavyokusanywa maana pande zote mbili yaani Upande wa bara na wa Zanzibar wote wamesema moja ya kero yao ni 1. Mkanganyiko wa uchangiaji na ugawanaji wa mapato. Sasa wewe uloelewa hili kuliko hata rais alokuja kufungua Bunge la katiba na hakueleza uchangiaji na ugawanaji mapato ukoje wewe twambie unafanywa vipi. Na hata wajumbe wa tume wamefikia wao kusema uundwe mfuko wa pamoja hivyo tueleze wewe mwanzo ilikuwaje usanyaji wa mapato ya taifa na ugawajai uko vipi kiasi kwmaba wengine wote washindwe kuelewa isipokuwa wewe na wenzako.

Vyanzo vya mapato ya Taifa vletu ni hivi hapa:-
[TABLE="width: 508"]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mapato ya kodi (TRA) - 46%[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mikopo ya Misaada ya nje – 29%[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mikopo ya masharti ya Biashara - 9.4%[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mikopo ya Ndani – 9%[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mapato yasiyo ya kodi – 4%[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD="colspan: 4"]Mapato ya Halmashauri za miji – 2.6%[/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Vema kabisa Mkuu.
Nikuweke sawa, taifa letu ni lipi? Znz wana taifa lao, nasisi tumo humo kwa mujibu wa katiba ya 2010?
Au taifa letu ni Tanganyika.

Twende na chanzo kimoja baada ya kingine.

Mapato ya kodi - Znz inachangia kiasi gani TRA ya taifa na Tanganyika kiasi gani
 
Vema kabisa Mkuu.
Nikuweke sawa, taifa letu ni lipi? Znz wana taifa lao, nasisi tumo humo kwa mujibu wa katiba ya 2010?
Au taifa letu ni Tanganyika.

Twende na chanzo kimoja baada ya kingine.

Mapato ya kodi - Znz inachangia kiasi gani TRA ya taifa na Tanganyika kiasi gani
Hujanijibu bado unazunguka mbuyu mkuu wangu..wewe unayesema hawachangii ndio tueleze jinsi gani fedha hizi hupatikana nimekupa vyanzo vyake halafu wewe twambie kwa takwimu ulokuwa nazo..
 
Hujanijibu bado unazunguka mbuyu mkuu wangu..wewe unayesema hawachangii ndio tueleze jinsi gani fedha hizi hupatikana nimekupa vyanzo vyake halafu wewe twambie kwa takwimu ulokuwa nazo..
Narudia tena, Salimin Awaadh, mwenyekiti wa kamati ya fedha ya BLW na mjumbe wa halamashauri kuu ya CCM kasema hivi'' Kwasasa znz haichangii hata senti moja''

Juma Duni haji, waziri wa afya wa SMZ kasema hivi 'znz haichangii kwasababu hakuna account ya pamoja''
Yule mnazi wa BBC naye kakubali kuwa hawana mchango, eti hakuna account. Account ili wachangie nini, jina!
Account pesa, account si maneno.

Tume ya Warioba imeeleza kuwa moja ya malalamiko ya Watanganyika ni znz kutochangia muungano.
Mkuu, ubishi kwa hili hauna maana.


Bandiko lako hapo juu una takwimu, umejaribu kuonyesha mapato ya taifa ikiwemo mikopo.

Mkuu, mkopo na pato ni vitu vyenye tfasi tofauti, ndio maana unaitwa mkopo.

Hili nimeshakueleza kuwa haliwezi kuwa kisingizio au mchango wa znz hata siku moja.
Mkopo ni ndege aliye mtini huwezi kusema ni wako.Tunachokiangalia hapa ni hiki

Pato la Tanganyika linaloingia katika muungano ni Trillion 12
Pato la Znz linaloingia katika bajetui ya SMZ ni bilioni 400.

Umeonyesha mikopo ya aina zote na mapato ya aina zote. Huwezi kusema kuwa znz ina mchango wa jina katika kupata mikopo, mtu mwenye akili nzuri hatakuelewa.

Muungano hauendeshwi na mikopo, na kudhani ni hivyo ni kujitoa fahamu bila kufahamu.

Ni hivi Mkandara
Kwa mujibu wa takwimu, na kwa mujibu wa kauli ya Naibu wa waziri wa fedha wa JMT, mbele ya waziri wa znz Mapato ya TRA ya znz hayavuki bahari.Mapato ya Tanganyika kutoka TRA ndiyo yanayotumika katika JMT kugharamia mambo haya

1. Wataumishi wa JMT ambao asilimia 21 ni Wazanzibar
2. Elimu ya juu ambapo wanafunzi 1700 wanadhaminiwa na JMT, huku SMZ yenye TRA yake kiaina ikidhamini 1800
3. Mapato ya Tanganyika ndiyo yanahudumia ulinzi na usalama
4. Mambo ya ndani
5. Mambo ya nje
6. Pesa za pengo la bajeti
7. Pesa ziszio na audit ( niulize swali kuhusu hili)
8, Gharama za wznz zisizowahusu Watanganyika, kama wabunge wao n.k.

Wakati znz ikichangia jina, Tanganyika inachangia gharama nzito sana.
Na huwezi kujadili mapato ukaacha madeni ya ndani na ya nje. Huo mjadala haupo kimantiki bali kiubishi.

Hili la ZNZ kuchangia tuachie hapa maana huna jibu, huna ushahidi.
Upo ushahidi kutoka kila source kwamba mchango wa znz katika muungano, ni nill, zero, buyu nothing!

Pili.
Wakati hawana mchango wowote, ni wznz hao hao wapo mbele kudai wapewe fursa zaidi za vyeo, pesa n.k. kutoka katika JMT ambayo wao hawana mchango. Nitegemezi tu, I meana mkuu ili uelewe kwa lugha rahisi ni sawa na kupe mgongoni mwa ng'ombe.

Ushahidi, siku hizi hoja za kudhulumiwa, kuonewa na kunyonywa zimekufa kifo cha mende.
Hakuna mznz mwenye akili timamu anayezungumzia hilo tena. The chapter is closed
Hata wao wanajua mchango wao ni buyu, zero nothing!

Ushahidi mwingine tunawaambia njia nyeupe, umesikia wakiandamana tena kama zamani.
Kimya na kwa adabu kabisa. Hawasemi kwasababu wanjua kuwa wamebebwa na kwamba hatuwahitaji.

Hatuwahitaji ili tupate mkopo au tuchukue hata senti tano yao. Hatuwahitaji. Waondoke kama wanataka! who cares

Tuonyeshe mchango wa znz katika JMT mbali ya jina. Ukumbi wako
 
Nguruvi3, Mchambuzi et al,

Kwa kuchangia zaidi, nitoe maoni yafuatayo mintarafu ya mtafaruku huu wa S2 au S3 na hatma ya JMT:

1. UKAWA inajumuisha CUF, na CUF ndiyo iliyoshinikiza mabadilko ya Katiba ya Znz kutamka kuwa Znz ni nchi katika kile kinachojulikana kama Muafaka.

2. Naamini Watanganyika/ Watanzania Bara wengi wamezoea kuamini kuwa Znz si nchi, hivyo mfumo wa S2 unawaridhisha (conservatives). Na wengine wanasema hata hayo mabadiliko ya kusema Znz ni nchi hayana maana, kwani Znz inatambulika wapi kimataifa?

3. JK pia alichukua msimamo huu wa kubariki mabadiliko ya Katiba ya Znz bila kujua athari zake mbele ya safari, kwa upande mmoja akitaka kuonekana kama mpatanishi na ili akubalike kwa Wanzanzibari, lakini pia kwa upande mwigine akitarajia kuwa ataanzisha mchakato wa Katiba ya JMT itakayokuwa juu ya ile ya Znz: alitaka kupumua. Ikumbukwe pia kuwa Karume mtoto alikuwa na msimamo wa Znz ni nchi. Hivyo, kwa namna fulani JK ni “lame duck” kwenye utata wa suala la utaifa wa Znz.

4. Wale wanaounga mkono S3 wanafanya hivyo kwa msingi wa retaliation (a la Mchambuzi)
5. Mtaji wa CCM kwenye kukosoa Rasimu uko kwenye sehemu tatu:
a. Takwimu za Tume,
b. Hoja kuwa serikali ya Muungano itakuwa haina uhusiano na mwananchi wa kawaida (kwa madai kuwa mwananchi anataka mbolea na masoko, na panadol na chumvi na mafuta ya taa!). Binafsi sijaridhika na maelezo na utetezi wa Tume kuhusu uwakilishi wa takwimu zao na uwiano wa hoja
c. Athari/changamoto za S3 kama zilivyobainishwa na Ripoti ya Tume (hisia za utaifa nk) kwa ujumla ni “killer assumptions” za “Union Project”.
6. Naamini Tume ilipendekeza S3 ikiamini ni njia ya kuilazimsha (serikali ya) CCM ishughulikie kero za muungano za miaka nenda rudi. Iliamini pia pendekezo litaibua mjadala chanya wa umma kuhusu aina ya muundo /muungano unaofaa. Naamini, kinyume na matarajio ya Tume, hata hivyo, pendekezo hilo la S3 limeibua hisia kali, mjadala hasi na hata kuibuka kwa UKAWA.
Kwa ujumla na kwa kifupi, pendekezo hilo na jinsi lilivyobebewa bendera na UKAWA kwa upande mmoja, na msimamo wa “baadhi ya wajumbe “ wa Tume kwa upande mwingine, kumeleta mgawanyiko miongoni mwa jamii ya Watanzania. Badala ya mjadala wa Katiba mpya kuchangia kujenga jamii yenye umoja, kuna hatari ya kumalizika kwa mchakato huu tukiwa tumegawanyika zaidi. Nadhani kina Warioba sasa wanajuta kwani nchi inaweza kuingia kwenye machafuko kama misimamo hii mikali ya UKAWA na Tanzania Kwanza itaendelea.

Way Forward
1. UKAWA wakajenge hoja bungeni huku viongozi wao wengine wakiwa nje ya bunge wakielimisha wananchi. Hili litawafanya wasionekane kama kikundi cha watu wanaotaka vurugu.
2. Wajitokeze wanasheria (Lissu hawezi hili?) kujenga hoja na hata kufungua shauri mahakamani kupinga mabadiliko ya katiba ya Znz kuwa yalikiuka katiba. Najua alikuwa akipinga sana ukiukwaji huu wakatiba huko nyuma kwenye mijadala mbalimbali.

Wakuu kuna kitu ambacho tunashindwa kusoma hapa. Kwenye suala la mabadiliko ya katiba serikali imeonesha udhaifu mkubwa. Serikali haijui inataka nini, haiko wazi kama inataka serikali moja, mbili au tatu. Kwa hiyo kimisingi haiwezi kuwa kiongozi madhuti wa mchakato wa katiba mpya.

CCM inajua inataka nini, na kwanini. Labda tatizo lake ni kuwa CCM Zanzibar ina maoni yake kutokana na msukumo kutoka kwa wananchi wa Zanzibar. CCM bara inataka kitu ambacho watanzania wa bara na visiwani hawakitaki, lakini hadi dakika hii imeshindwa kutafuta lugha ya kuwatongoz watanzania wakubali ajenda yake.

UKAWA wanajua kabisa nini wanataka, na wanachotoka ni kile wanachotaka watanzania. Na wanaweza kukitetea kwa hoja. Tatizo ni kwamba serikali na CCM wanajaribu kuwafanya wanonekane kama wajinga, na baadhi ya wajumbe wa UKAWA inaonekana kama wananunulika.

JK na Karume walifanya makosa makubwa sana kuanzisha nchi ya Zanzibar kikatiba. Kwa hiyo backlash tunayoiona sasa inatokana na Zanzibar kuwa nchi ndani ya nchi. Kwa minajili hiyo hiyo, haitakiwi kuwa nongwa kwa Tanganyika kuwa nchi ndani ya nchi.

Way forwad...let Zanzibar cease to exist, like Tanganyika did, in order to strengthen Tanzania, tuwe na serikali moja tu ambayo watanzania wote ni subjects. If not bring back Tanganyika so as we can have a just union. Magumashi ya sasa ni usaniii wa kisiasa ambao baadaye utakuwa mwiba.

Nguruvi3, mchambuzi, pasco, mkandara, bmk, mwanakijiji,
 
Mwanagenzi;10328974]Nguruvi3, Mchambuzi
1. UKAWA inajumuisha CUF, na CUF ndiyo iliyoshinikiza mabadilko ya Katiba ya Znz kutamka kuwa Znz ni nchi katika kile kinachojulikana kama Muafaka.
Hapana na si kweli. Aliyeridhia mabadiliko ya katiba ya 2010 ni makamu mwenyekiti wa CCM zanzibar, Amani Karume. Sheria ilipitishwa na BLW bila kupingwa wakiwemo CCM. Wananchi wakapiga kura ya maoni na 61% ikaridhia mabadiliko hayo. Hivyo mabadiliko ya katiba ni zao la Wazanzibar si chama kama unavyotaka umma uelewe.
Mwanagenzi;103289742. Naamini Watanganyika wamezoea kuamini kuwa Znz si nchi, mfumo wa S2.mabadiliko ya kusema Znz ni nchi hayana maana, kwani Znz inatambulika wapi kimataifa?
Unataka kusema kutotambuliwa kimataifa kunatoa fursa ya znz kuwa juu ya katiba ya JMT. Isingelikuwa nchi, ni wapi kuna taifa moja lenye wakuu wa nchi wawili wakipokezana madaraka, kuanzia maamuzi hadi ulinzi na usalama.
Hoja kubwa ni kutumia neno nchi kuvunja katiba kwanza kabla hatuvuka mipaka.
​Mwanagenzi;103289743. JK pia alichukua msimamo huu wa kubariki mabadiliko ya Katiba ya Znz bila kujua athari zake mbele ya safari, kwa upande mmoja akitaka kuonekana kama mpatanishi na ili akubalike kwa Wanzanzibari, lakini pia kwa upande mwigine akitarajia kuwa ataanzisha mchakato wa Katiba ya JMT itakayokuwa juu ya ile ya Znz: alitaka kupumua. Ikumbukwe pia kuwa Karume mtoto alikuwa na msimamo wa Znz ni nchi. Hivyo, kwa namna fulani JK ni "lame duck" kwenye utata wa suala la utaifa wa Znz.
JK alitaka kuwafurahisha wznz. Madhara ya kufanya hivyo ni wznz kuwa na mapembe dhidi yake.Mchakato aliuanzisha ili kuua mjadala wa S3. Unakumbuka Sitta alivyokumbana na kituko kule znz.Makosa ya JK ilikuwa kudhani kufanya alivyofanya ilikuwa bora, athari zake hakuziona wakati huo.
Haya tunayoyaona ni matokeo na madhara ya maamuzi ya JK kuhusu kuwafurahisha wznz.
4. Wale wanaounga mkono S3 wanafanya hivyo kwa msingi wa retaliation (a la Mchambuzi)
Si kweli, hujamtendea haki Mchambuzi.
Alichosema Mchambuzi ni kuhusu G55 na retaliations. Akaongeza, ilikuwa ni suala la matter of principle.

Mchambuzi na Bongolander wakaenda mbali kusema tatizo sasa limefikia economic injustice.
Hujamtendea haki hata kidogo kwa kuchukua nusu ya alichosema
5. Mtaji wa CCM kwenye kukosoa Rasimu uko kwenye sehemu tatu:a. Takwimu za Tume, b. Hoja kuwa serikali ya Muungano itakuwa haina uhusiano na mwananchi wa kawaida (kwa madai kuwa mwananchi anataka mbolea na masoko, na panadol na chumvi na mafuta ya taa!). Binafsi sijaridhika na maelezo na utetezi wa Tume kuhusu uwakilishi wa takwimu zao na uwiano wa hoja
CCM ilitumia takwimu chache katika tume ya Nyalali. Matokeo ya takwimu hizo hayakuangaliwa kwa namba bali kwa analysis. Hapa ndipo wengi mnapochanganya mambo

Takwimu zinasaidia katika analysis, hazisimami zenyewe kama conclusions.
Uchambuzi wa tume ulihusisha takwimu na maoni. Huwezi ku-quantify maoni, unaweza kuyafanyia qualitative analysis.

Kuhusu uhusiano wa serikali na wananchi, kumbuka ile ni serikali kuu.
Uhusiano wake umejengwa kwa serikali 2 zenye ukaribu na wananchi.

Ni sawa na sasa ambapo kuna serikali za mitaa. Je, kuna umbali na serikali kuu.
Serikali kuu kazi yake ni majukumu ya pamoja ya nchi husika.

Ndiyo maana tume ikaondoa baadhi ya mambo ili yashughulikiwe na serikali husika.
Utawezaje kuwa na wizara ya madini ikiwa znz haiwezi hata kuchoma mkaa.
Znz inahitaji wizara ya uvuvi yenye nguvu, mkazo huo hauwezi kuwa sawa na uvuvi wa Tanganyika
c. Athari/changamoto za S3 kama zilivyobainishwa na Ripoti ya Tume (hisia za utaifa nk) kwa ujumla ni "killer assumptions" za "Union Project".
Ndio maana tunasema kuna bias. Mbona hujaangalia S2 na atahri zake.

Je, kwasasa sisi ni taifa moja zaidi ya miaka 20 iliyopita au tumegawanyika.
Changamoto za tume zilikuwa kuwasaidia wajumbe kuona namna ya kukwepa hali hiyo.
Hivyo tukubaliane kuwa tume ilikuwa deep and scientific kuliko ilivyowahi kutokea.
6. Naamini Tume ilipendekeza S3 ikiamini ni njia ya kuilazimsha (serikali ya) CCM ishughulikie kero za muungano za miaka nenda rudi. Iliamini pia pendekezo litaibua mjadala chanya wa umma kuhusu aina ya muundo /muungano unaofaa. Naamini, kinyume na matarajio ya Tume, hata hivyo, pendekezo hilo la S3 limeibua hisia kali, mjadala hasi na hata kuibuka kwa UKAWA.
Tume iligundua kuwa kwasasa hakuna namna ya kunusuru muungano isipokuwa S2. Ilibaini kuwa kero zinazosemwa si kuwa zilipuuza, bali hazikuwa na majibu na ufa ni mkubwa zaidi.
Haiwezekani tume ya watu makini iamini kuwa kero za miaka 50 zinaweza kutatuliwa kwa changamoto chanya unazosema
Kwa ujumla na kwa kifupi, pendekezo hilo na jinsi lilivyobebewa bendera na UKAWA kwa upande mmoja, na msimamo wa "baadhi ya wajumbe " wa Tume kwa upande mwingine, kumeleta mgawanyiko miongoni mwa jamii ya Watanzania. Badala ya mjadala wa Katiba mpya kuchangia kujenga jamii yenye umoja, kuna hatari ya kumalizika kwa mchakato huu tukiwa tumegawanyika zaidi.
Well, wewe hulioni tatizo la kupuuzwa kwa maoni ya wananchi. Huoni tatizo linalosababishwa na CCM katika kuburuza umma. Unaridhika kabisa kuwa CCM inafanya mambo mema. Ni maoni yako na una haki
Nadhani kina Warioba sasa wanajuta kwani nchi inaweza kuingia kwenye machafuko kama misimamo hii mikali ya UKAWA na Tanzania Kwanza itaendelea.
Kama kuna tume yenye heshima ni ya Warioba. Na wala hata siku moja hawatajuta ndio maana wapo wanajibu mapigo tena kwa hoja na mantiki. Hii ni moja ya tume zenye heshima katika historia ya nchi yetu.
Way Forward
1. UKAWA wakajenge hoja bungeni huku viongozi wao wengine wakiwa nje ya bunge wakielimisha wananchi. Hili litawafanya wasionekane kama kikundi cha watu wanaotaka vurugu.
Kwani sasa UKAWA wanaonekana hivyo?
Nadhani hujaelewa maana ya kuondoka bungeni
2. Wajitokeze wanasheria (Lissu hawezi hili?) kujenga hoja na hata kufungua shauri mahakamani kupinga mabadiliko ya katiba ya Znz kuwa yalikiuka katiba. Najua alikuwa akipinga sana ukiukwaji huu wakatiba huko nyuma kwenye mijadala mbalimbali.
Kwamba unaona tatizo ni katiba ya znz na ndio maana UKAWA wapo nje!!

Mabadiliko ya katiba ya znz yalifanyika kwa mujibu wa sheria zao.
Mwenye uwezo wa kuhoji ndiye aliyewapa nafasi hiyo.

Nilidhani ungeshauri Rais awe impeached kwa kuruhusu katiba kuvunjwa.
Hili ni jambo jema sana unalosema, ingawa sina uhakika kama unamtakia mema JK.
 
Hapana na si kweli. Aliyeridhia mabadiliko ya katiba ya 2010 ni makamu mwenyekiti wa CCM zanzibar, Amani Karume. Sheria ilipitishwa na BLW bila kupingwa wakiwemo CCM. Wananchi wakapiga kura ya maoni na 61% ikaridhia mabadiliko hayo. Hivyo mabadiliko ya katiba ni zao la Wazanzibar si chama kama unavyotaka umma uelewe. Unataka kusema kutotambuliwa kimataifa kunatoa fursa ya znz kuwa juu ya katiba ya JMT. Isingelikuwa nchi, ni wapi kuna taifa moja lenye wakuu wa nchi wawili wakipokezana madaraka, kuanzia maamuzi hadi ulinzi na usalama.
Hoja kubwa ni kutumia neno nchi kuvunja katiba kwanza kabla hatuvuka mipaka. JK alitaka kuwafurahisha wznz. Madhara ya kufanya hivyo ni wznz kuwa na mapembe dhidi yake.Mchakato aliuanzisha ili kuua mjadala wa S3. Unakumbuka Sitta alivyokumbana na kituko kule znz.Makosa ya JK ilikuwa kudhani kufanya alivyofanya ilikuwa bora, athari zake hakuziona wakati huo.
Haya tunayoyaona ni matokeo na madhara ya maamuzi ya JK kuhusu kuwafurahisha wznz. Si kweli, hujamtendea haki Mchambuzi.
Alichosema Mchambuzi ni kuhusu G55 na retaliations. Akaongeza, ilikuwa ni suala la matter of principle.

Mchambuzi na Bongolander wakaenda mbali kusema tatizo sasa limefikia economic injustice.
Hujamtendea haki hata kidogo kwa kuchukua nusu ya alichosemaCCM ilitumia takwimu chache katika tume ya Nyalali. Matokeo ya takwimu hizo hayakuangaliwa kwa namba bali kwa analysis. Hapa ndipo wengi mnapochanganya mambo

Takwimu zinasaidia katika analysis, hazisimami zenyewe kama conclusions.
Uchambuzi wa tume ulihusisha takwimu na maoni. Huwezi ku-quantify maoni, unaweza kuyafanyia qualitative analysis.

Kuhusu uhusiano wa serikali na wananchi, kumbuka ile ni serikali kuu.
Uhusiano wake umejengwa kwa serikali 2 zenye ukaribu na wananchi.

Ni sawa na sasa ambapo kuna serikali za mitaa. Je, kuna umbali na serikali kuu.
Serikali kuu kazi yake ni majukumu ya pamoja ya nchi husika.

Ndiyo maana tume ikaondoa baadhi ya mambo ili yashughulikiwe na serikali husika.
Utawezaje kuwa na wizara ya madini ikiwa znz haiwezi hata kuchoma mkaa.
Znz inahitaji wizara ya uvuvi yenye nguvu, mkazo huo hauwezi kuwa sawa na uvuvi wa TanganyikaNdio maana tunasema kuna bias. Mbona hujaangalia S2 na atahri zake.

Je, kwasasa sisi ni taifa moja zaidi ya miaka 20 iliyopita au tumegawanyika.
Changamoto za tume zilikuwa kuwasaidia wajumbe kuona namna ya kukwepa hali hiyo.
Hivyo tukubaliane kuwa tume ilikuwa deep and scientific kuliko ilivyowahi kutokea.Tume iligundua kuwa kwasasa hakuna namna ya kunusuru muungano isipokuwa S2. Ilibaini kuwa kero zinazosemwa si kuwa zilipuuza, bali hazikuwa na majibu na ufa ni mkubwa zaidi.
Haiwezekani tume ya watu makini iamini kuwa kero za miaka 50 zinaweza kutatuliwa kwa changamoto chanya unazosemaWell, wewe hulioni tatizo la kupuuzwa kwa maoni ya wananchi. Huoni tatizo linalosababishwa na CCM katika kuburuza umma. Unaridhika kabisa kuwa CCM inafanya mambo mema. Ni maoni yako na una hakiKama kuna tume yenye heshima ni ya Warioba. Na wala hata siku moja hawatajuta ndio maana wapo wanajibu mapigo tena kwa hoja na mantiki. Hii ni moja ya tume zenye heshima katika historia ya nchi yetu. Kwani sasa UKAWA wanaonekana hivyo?
Nadhani hujaelewa maana ya kuondoka bungeni Kwamba unaona tatizo ni katiba ya znz na ndio maana UKAWA wapo nje!!

Mabadiliko ya katiba ya znz yalifanyika kwa mujibu wa sheria zao.
Mwenye uwezo wa kuhoji ndiye aliyewapa nafasi hiyo.

Nilidhani ungeshauri Rais awe impeached kwa kuruhusu katiba kuvunjwa.
Hili ni jambo jema sana unalosema, ingawa sina uhakika kama unamtakia mema JK.

Mkuu Nguruvi3, Mchambuzi, Mkandara

Tukiangalia huko nyuma karibu tume zote zilizoundwa na CCM zinakuwa ni tume makini. Tatizo ni kuwa CCM wanapounda tume wanasahau kuwa tume zinafanya kazi kitaaluma, sio kisiasa, ni kama kauli za kuunda tume wanazotoa viongozi wa nchi zinalenga kuonesha demokrasia, lakini sikumbuki kama kuna siku CCM imewahi kukubali maoni ya tume.

Nakumbuka tume ya Jaji Kisanga, Tume ya Nyalali na kulikuwa na tume nyingine ya Warioba kuhusu rushwa...hakuna kilichopendekezwa na tume hizo kichokubaliwa na CCM kama kuna kilichikubaliwa, basi kilikubwaliwa kidogo na kwa shingo upande. CCM iko mstari wa mbele kuunda tume na kukataa yanayopendekezwa na tume.

Kinachofanywa na tume ya Jaji Warioba kujibu mapigo ni jambo sahihi, hasa ukizingatia kuwa baada ya tume kufanya kazi zao, pamja na kufanya kazi kwa moyo wanaishiwa kupokea kejeli na kupotosha yale waliyokusanya. Kwa maoni yangu mzee Warioba yuko sahihi kabisa.

as to whether JK alifanya makosa kuruhusu ukiukaji wa katiba na kufanya nchi iote ndani ya nchi, hilo ni kweli, lakini sioni kama ndani ya CCM kuna mwenye ubavu wa kukosoa hilo. Warioba amelisema wazi mara nyingi kuwa sasa Zanzibar ni nchi kisheria, kwa hiyo umewekwa msingi wa kisheria pia kudai Tanganyika.
 
Nguruvi3,

tatizo lako wewe unapoulizwa swali unakurupuka na majibu kisha unaendelea kuzungumzia kwa nini nimeuliza. Nimekuuliza swali rahisi kabisa ya kwamba wewe unayejua Zanzibar haichangii Muungano nimetaka kujua huo Muungano uko wapi ikiwa wananchi wamekanganyikiwa kuwepo na uchangiaji ana ugawanaji wa mapato ya muungano. Sii rais wala tume wameweza kujibu hilo na ndio maana tume hiyo imekuja na wazo la kuunda mfuko wa Pamoja hivyo ni kusema hakuna kitu Muungano bali tuna serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar. Ndio maana nikauuliza kijanja ili nipate kujua huo mfuko wa Muungano ( wa pamoja)ambao Tanganyika pekee huchangia uko wapi?

Na kero ya Wazanzibar imeelezwa wazi ktk maswala yote ambayo yanaunda huu muungano ambao haupo kiuhalisia isipokuwa jina lake kutumiwa na serikali ya Tanganyika. Na kama umenifuatilia nilionyesha wazi tulikotoka na sasa tumefika wapi kiasi kwamba utaona zamani kulikuwepo ushirikiano mkubwa baina ya Tanganyika na Zanzibar wakati wa mwalimu chini ya Ujamaa lakini baada ya kuingia Ubepari na kuunda vyama vingi kimsingi tumeharibikiwa, hapa ndipo panapotakiwa kutazamwa. Kifupi serikali isokuwepo ni ya Muungano maana hakuna mfuko wa pamoja na wewe mwenyewe umeshindwa kutuonyesha wapi Tanganyika na Zanzibar wanakutana.

Hivyo kama tulikuwa na mambo 22 hatukuungana, iweje tuwe na 7 ndio tuungane wakati watu ni wale wale na akili ni zile zile?
 
Mkuu Nguruvi3, Mchambuzi, Mkandara

Tukiangalia huko nyuma karibu tume zote zilizoundwa na CCM zinakuwa ni tume makini. Tatizo ni kuwa CCM wanapounda tume wanasahau kuwa tume zinafanya kazi kitaaluma, sio kisiasa, ni kama kauli za kuunda tume wanazotoa viongozi wa nchi zinalenga kuonesha demokrasia, lakini sikumbuki kama kuna siku CCM imewahi kukubali maoni ya tume.

Nakumbuka tume ya Jaji Kisanga, Tume ya Nyalali na kulikuwa na tume nyingine ya Warioba kuhusu rushwa...hakuna kilichopendekezwa na tume hizo kichokubaliwa na CCM kama kuna kilichikubaliwa, basi kilikubwaliwa kidogo na kwa shingo upande. CCM iko mstari wa mbele kuunda tume na kukataa yanayopendekezwa na tume.

Kinachofanywa na tume ya Jaji Warioba kujibu mapigo ni jambo sahihi, hasa ukizingatia kuwa baada ya tume kufanya kazi zao, pamja na kufanya kazi kwa moyo wanaishiwa kupokea kejeli na kupotosha yale waliyokusanya. Kwa maoni yangu mzee Warioba yuko sahihi kabisa.

as to whether JK alifanya makosa kuruhusu ukiukaji wa katiba na kufanya nchi iote ndani ya nchi, hilo ni kweli, lakini sioni kama ndani ya CCM kuna mwenye ubavu wa kukosoa hilo. Warioba amelisema wazi mara nyingi kuwa sasa Zanzibar ni nchi kisheria, kwa hiyo umewekwa msingi wa kisheria pia kudai Tanganyika.
Mkuu mimi sikatai kabia kuwepo kwa serikali 3. Ila nachosema Tanganyika mnayoidai ipo na katiba hii ya Muungano ni ya Tanganyika.

Tumeonyeshwa kila jambo ndani ya katiba hii ni la Tanganyika iweje leo tukubali kirahisi kwamba katiba hii ni ya Muungano wakati waziri wa Muungano hajawahi kuitumikia Zanzibar hata katika yale ya Muungano? kwa nini hatukubali kwanza makosa hayo kisha tunapounda serikali ya 3 iwe yenye kuzitumikia serikali zote kwa ujumla wake, hayo mambo 7 hayaipi serikali ya muungano kushika mpini bali serikali ya Kifalme ambayo haina umuhimu kwa pande zote. Labda nirudi nyuma kidogo kuzungumzia ya CCM.

Unajua toka Ujamaa ufe, bado nchi hii ni ya chama kimoja japo vipo vingi vimeanzishwa! na jinsi tunavyoitetea tanganyika ni sawa kabisa na CCM wanavyojitetea wasione makosa yako wapi. Uliona wapi mgombea Urais aloshika nafasi ya pili anapigwa na Polisi kwa kuanzisha mkutano wa chama chake? Yaani tukimaliza uchaguzi mgombea huo hana kinga tena hata DC anaweza kumweka ndani bila kosa. (Yalotokeo ya Arusha).

Mali zote na ofisi zote zilizokuwa chini ya chama hiki ni mali za chama japo sote tumetoka humo. hadi leo hii CCM inamiliki karibu kila kitu, vyama vingine vikilalamika tuseme na nyie anzisheni vyenu kama vile kuna uadui?. Kuunda vyama vingi haikuwa solution bali imezaa uadui zaidi kwa sababu hatukuzingatia mambo muhimu ya kisiasa ili demokrasia ya kweli isimame, tulichofanya ni kuwaridhisha tu wanaotupa mikopo kuwa Tanzania ina vyama vingi. Tanganyika baada ya Ujamaa tumeteka mali zote kiasi kwamba hata Stamico ni ya Tanganyika, TPDC nayo hivyo umeme unauzwa kwanza Tanesco (shirika la Tanganyika) halafu ndio wauziwe Zeco badala ya Zeco na Tanesco kuwa mashirika ya umma yawe na uwezo sawa kununua moja kwa moja ili kufanisi usambazaji pande zote. Hivi kabla ya Zeco kuundwa huko Zanzibar walikuwa wakipataje Umeme?

Sasa kutokuwepo kwa usawa huo ndio maana kuna chuki kubwa baina ya vyama sawa kabisa na chuki hii baina ya Tanganyika na Zanzibar. Chako changu, changu changu ndio yalopelekea Kenya kuteka mali zote za EAC ilipovunjika, tukaambulia kuiba ndege moja tu.
 
Mkuu Kobello,

Pengine nikuulize - je, tunaweza fanya mambo yote ya Tanganyika na Zanzibar yawe ya muungano?

Kuhusu gharama - je ni Zipi hizo zitakazo ongezeka ambazo chini ya serikali Mbili hazipo?


Sent from my iPhone using JamiiForums
Samahani kwa kuchelewa kujibu.

Hatuwezi kufanya mabo yote yawe ya muungano.

Gharama za kuanzisha na kui-maintain judiciary ya Tanganyika, separate from Tanzania and the total overhaul of the court system.
Administrative costs za idara mpya zitakazoanzishwa (bearing in mind hizi zilizopo zitakuwa either za Tanganyika au Muungano) eg. Ofisi ya rais, mamlaka za kodi na ofisi zitakazosimamia wizara zote zilizopo Bara na Visiwani.

Bunge jipya na ofisi yake.
 
Samahani kwa kuchelewa kujibu.

Hatuwezi kufanya mabo yote yawe ya muungano.

Gharama za kuanzisha na kui-maintain judiciary ya Tanganyika, separate from Tanzania and the total overhaul of the court system.
Administrative costs za idara mpya zitakazoanzishwa (bearing in mind hizi zilizopo zitakuwa either za Tanganyika au Muungano) eg. Ofisi ya rais, mamlaka za kodi na ofisi zitakazosimamia wizara zote zilizopo Bara na Visiwani.

Bunge jipya na ofisi yake.
Hivi Kobello, ukimwita waziri mkuu Rais wa Tanganyika utakuwa umeongeza gharama gani? Ukiita wizara ya kilimo, afya, ujenzi n.k. wizara za Tanganyika utakuwa umeongeza gharama gani?

Judicial system itakayoongezeka ni ipi na kwa sasa iinahudumiwaje? Hapa lazima ueleze unafuu uliopo ukilinganisha na unaotarajiwa.

Administrative cost za idara mpya ni zili? Kwasasa tuna mambo 22 ambayo kiidara ni 47.
Hivi ukiwa na mambo 7 utakuwa na idara nyingi au pungufu?

Na idara za sasa zinahudumiwaje ili kusema gharama zake ni nafuu?

Kama S1 haiwezekani, S2 zinawezakanje kukiwa na dhana ya Tanganyika kuvaa koti?
 
Nguruvi3,

tatizo lako wewe unapoulizwa swali unakurupuka na majibu kisha unaendelea kuzungumzia kwa nini nimeuliza. Nimekuuliza swali rahisi kabisa ya kwamba wewe unayejua Zanzibar haichangii Muungano nimetaka kujua huo Muungano uko wapi ikiwa wananchi wamekanganyikiwa kuwepo na uchangiaji ana ugawanaji wa mapato ya muungano. Sii rais wala tume wameweza kujibu hilo na ndio maana tume hiyo imekuja na wazo la kuunda mfuko wa Pamoja hivyo ni kusema hakuna kitu Muungano bali tuna serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar. Ndio maana nikauuliza kijanja ili nipate kujua huo mfuko wa Muungano ( wa pamoja)ambao Tanganyika pekee huchangia uko wapi?

Na kero ya Wazanzibar imeelezwa wazi ktk maswala yote ambayo yanaunda huu muungano ambao haupo kiuhalisia isipokuwa jina lake kutumiwa na serikali ya Tanganyika. Na kama umenifuatilia nilionyesha wazi tulikotoka na sasa tumefika wapi kiasi kwamba utaona zamani kulikuwepo ushirikiano mkubwa baina ya Tanganyika na Zanzibar wakati wa mwalimu chini ya Ujamaa lakini baada ya kuingia Ubepari na kuunda vyama vingi kimsingi tumeharibikiwa, hapa ndipo panapotakiwa kutazamwa. Kifupi serikali isokuwepo ni ya Muungano maana hakuna mfuko wa pamoja na wewe mwenyewe umeshindwa kutuonyesha wapi Tanganyika na Zanzibar wanakutana.

Hivyo kama tulikuwa na mambo 22 hatukuungana, iweje tuwe na 7 ndio tuungane wakati watu ni wale wale na akili ni zile zile?
Wazo la mfuko wa pamoja ni matokeo ya tume ya Amina Salum si tume ya Warioba, FYI

Well, ili kuondoa kero ya wznz kwa Tanganyika kutumia jina la Tanzania ndiyo maana tunataka seikali ya Tanganyika.Unaona logic inavyojibu maswali yako kirahisi.

Huwezi kuwa na S2 ukaepuka kuvaa koti.
Logic hairuhusu hivyo ndio maana hujaweza kutumbia S2 zinafanyaje kazi na koti likawa limevuliwa.

Nakumbuka umeshauri kuwe na waziri wa Muungano halafu naibu wake awe wa Tanganyika.
Sijui maana ya hii ni kitu gani.

Yaani naibu awe mkuu wa Tanganyika halafu afanye kazi chini ya waziri wa muungano.
Yule waziri wa znz awe sawa na waziri wa muungano.
Ndiyo yale yale ya katiba ya znz kuwa juu ya katiba ya muungano.

Mkandara, huna hoja ya kueleza kero za S2 zinatatua vipi matatizo, huna hata moja.

Kuhusu gharama na maelezo ya Rais na tume, JK hakueleza kero za Watanganyika.

Alijua kusema kutaamsha hasira na chuki kutokana na economic injustice dhidi ya Watanganyika.

Halafu umesema serikali ya Tanganyika ipo, isiyokuwepo ni ya muungano.
Ni kichekesho kwasababu wznz wanapata 4.5 ya Tanganyika kwa maana hiyo, wanapata fursa zote walizo nazo kutoka Tanganyika. Huoni mkuu unaweleza watanganyika 'wake up'

Kwamba, pato la Mtanganyika ndilo la mznz kwa jina la Tanzania.
Nani kavaa koti hapo. Logic inakukutalia.

Mimi sioni sababu za kung'ang'ania znz. Hatuna mafao zaidi ya kuwa tunapoteza.
Hata S3 ni kuwasaidia. Katika huu muungano znz ni tegemezi tu na hata kusema tumeungana ni aibu

Wewe unataka S2 kwasababu unajua nje ya S2 znz itabaki bila utegemezi.

Watanganyika tunasema , muda umefika hatuwezi kuendelea na economic injustice iliyopo.

Mfano, pesa zinazotoka hazina ya Tanganyika(kwa mujibu wako) kwenda kuhudumia nchi jirani ni nyingi kuliko zinazokwena mikoa 26 ya Tanganyika.

Haiwezekani znz yenye eneo dogo na watu 1.2 milioni ipewe pesa za Tanganyika(kwa mujibu wako) huku ikichangia buyu, sifuri. Tanganyika siyo shamba la bibi na hilo lipo wazi linasubiri muda tu FYI

Hakuna muungano wa jina. Ndoa ni kuwajibika si karatasi au neno ndoa.

Leo Sumbawanga inachangia almost trilion ya pato la taifa. Katika paro la sumbawanga znz inachukua 4.5 bila kuchangia hata senti tano. Halafu mgao huo unasema ni halali.

Tanganyika inazinduka kwa sababu hizi
Matter of principal
To stop stupid economic injustice dhidi ya ka taifa kadogo kasiko na mchango wa aina yoyote kwa Mtanganyika.

Kama unadhani znz ni muhimu kwa Tanganyika, jamvi hili hapa onyesha kwa mantiki.
 
Ningependa kumjibu mwanajamvi Nguruvi3 kama ifuatavyo:


1. Hapana na si kweli. Aliyeridhia mabadiliko ya katiba ya 2010 ni makamu mwenyekiti wa CCM zanzibar, Amani Karume… Hivyo mabadiliko ya katiba ni zao la Wazanzibar si chama kama unavyotaka umma uelewe.



JK kama rais wa JMT unadhani hakuwa na habari kuhusu mabadiliko hayo ya Katiba ya Znz? Ninaposema aliridhia au alibariki simaanishi alikuwa kwenye kikao cha BLW au alitia saini muswada wa katiba. Ni wazi CC ya CCM ilibariki muafaka kabla ya Karume kutia saini na Maalim Seif.
Ni kweli mabadiliko ni zao la Wanzibari wengi kama si wote laikini usisahau hili lilitokana na msimamo wa CUF na kina Maalim Seif na ndiyo maana alipewa Umakamu wa Rias kama sehemu ya makubaliano ya Muafaka na kuunda SUK.
Ninapotoa maoni hayo simaanishi kuwa JK alifanya vema, ila nakueleza hali halisi.


2. .. Si kweli, hujamtendea haki Mchambuzi.



Nilitumia neno “retaliation” kama lilivyokuwa limetumiwa na Mchambuzi katika andiko lake liliokuwa limetangulia. Wala sipingani naye kuwa kuna wanaotaka Tanganyika as a matter of principle na wale wanaotaka as a matter of retaliation.

3. … Matokeo ya takwimu hizo hayakuangaliwa kwa namba bali kwa analysis. Hapa ndipo wengi mnapochanganya mambo. Takwimu zinasaidia katika analysis, hazisimami zenyewe kama conclusions.



Nakubaliana na hoja hii. Lakini hapo mwanzoni Tume/Warioba hakuwa amefafanua kuwa msingi wa mapendekezo ya S3 yako kwenye hoja na si takwimu za idadi ya watu waliosema wanataka S3. Hata madai ya wengi wanaounga mkono S3 wakiwemo UKAWA wanatetea hoja yao kwa madai kuwa “wananchi wengi” walitaka S3.


4. … Kuhusu uhusiano wa serikali na wananchi, kumbuka ile ni serikali kuu.
Uhusiano wake umejengwa kwa serikali 2 zenye ukaribu na wananchi.
Ni sawa na sasa ambapo kuna serikali za mitaa. Je, kuna umbali na serikali kuu.



Jibu langu ni NDIYO kuna umbali na serikali kuu! Na ndiyo maana hata sasa watu kadhaa kwa mfano (ikiwemo CHADEMA) wanataka mfumo wa MAJIMBO kwani huu unatoa fursa kubwa kwa wananchi kuwa karibu na serikali kwa mambo yanayowahusu zaidi. Na ndiyo maana wengine wanaona ni vema wawe na uwezo wa kuchagua wakuu wa wilaya zao au mikoa yao au hata wakurugenzi wa halmashauri kwa mfano. Hii yote ni kuoyesha kwa sasa wananchi wanaona kuna umbali kati yao na Dodoma au Dar es Salaam ambako ndiko kwenye “serikali”.


5. Mbona hujaangalia S2 na atahri zake



Ni kweli sikuzitaja; sikuwa na haja ya kuzitumia kujenga hoja yangu. Lakini kwa maoni yangu, mjadala wa rasimu ungejikita hapo, kuangalia faida na hatari au athari za S2 na S3.



6. Je, kwasasa sisi ni taifa moja zaidi ya miaka 20 iliyopita au tumegawanyika.


Sina shaka tumegawanyika…hasa baada ya kuja mfumo wa vyama vingi kwa upande mmoja, na CCM na serikali yake kushindwa kujenga umoja, hasa kutokana na kuongezeka kwa tofauti za kipato na hali ya maisha miongoni mwa jamii (the haves and the have not) kwa upande mwingine.
Na kwa maoni yangu, katiba mpya au la, viongozi wa vyama vya siasa, viongozi wa dini, na watu wenye kuheshimiwa katika jamii, wachukue jukumu la kushauri wapenzi, mashabiki, na wanachama wa vyama vya siasa na jamii kwa ujumla, tuachane na siasa za chuki kiasi cha watu kuumizana au kuuana kwa sababu ya tofauti za mtazamo wa kisiasa.

7. Unaridhika kabisa kuwa CCM inafanya mambo mema.
Hakuna mahali nimedai kuwa CCM wanafanya vema. Natoa maoni yangu kama mtu huru bila kuegemea ama CCM au Tanzania Kwanza wala UKAWA. Sitaki kuamini hata wewe unaweza kuchukua msimamo kuwa anayehoji Tume au UKAWA basi ni mtetezi wa CCM!



8. Kama kuna tume yenye heshima ni ya Warioba. Na wala hata siku moja hawatajuta ndio maana wapo wanajibu mapigo tena kwa hoja na mantiki. Hii ni moja ya tume zenye heshima katika historia ya nchi yetu.


Sina maoni kwa hili kwa sasa. Tuache historia itatoa hukumu. Ila ungeweza kufafanua ni nchi yetu ipi unayoizungumzia! Zanzibar, Tanganyika au Tanzania?



9. Kwani sasa UKAWA wanaonekana hivyo?



Ni kweli kuna baadhi ya wananchi wanawaona UKAWA kama kikundi cha viongozi wanaotaka kuleta vurugu!
Binafsi nisingependa waonekane hivyo na ndiyo maana kwenye maoni yangu nilishauri warudi bungeni huku wakiendeleza uhamasishaji na ushawishi huko nje ya bunge.



10. Mabadiliko ya katiba ya znz yalifanyika kwa mujibu wa sheria zao.
Mwenye uwezo wa kuhoji ndiye aliyewapa nafasi hiyo.
:cool2:


Sijakuelewa hapa mkuu! Sheria zao? Zipi? Aliyewapa nafasi hiyo ni nani?



11. Nilidhani ungeshauri Rais awe impeached kwa kuruhusu katiba kuvunjwa.


Sina hakika na jinsi katiba ya JMT inavyoelekeza juu ya hili.
Na kama akitolewa madarakani, je hatua hiyo itafanya mabadiliko ya katiba ya Znz yawe batili sawia (automatically) au lazima pawe na mchakato mwingine? Na je, hatua hiyo itasaidiaje kupatikana kwa katiba mpya?
 
Mkuu Nguruvi3, Mchambuzi, Mkandara

Tukiangalia huko nyuma karibu tume zote zilizoundwa na CCM zinakuwa ni tume makini. Tatizo ni kuwa CCM wanapounda tume wanasahau kuwa tume zinafanya kazi kitaaluma, sio kisiasa, ni kama kauli za kuunda tume wanazotoa viongozi wa nchi zinalenga kuonesha demokrasia, lakini sikumbuki kama kuna siku CCM imewahi kukubali maoni ya tume.

Nakumbuka tume ya Jaji Kisanga, Tume ya Nyalali na kulikuwa na tume nyingine ya Warioba kuhusu rushwa...hakuna kilichopendekezwa na tume hizo kichokubaliwa na CCM kama kuna kilichikubaliwa, basi kilikubwaliwa kidogo na kwa shingo upande. CCM iko mstari wa mbele kuunda tume na kukataa yanayopendekezwa na tume.

Kinachofanywa na tume ya Jaji Warioba kujibu mapigo ni jambo sahihi, hasa ukizingatia kuwa baada ya tume kufanya kazi zao, pamja na kufanya kazi kwa moyo wanaishiwa kupokea kejeli na kupotosha yale waliyokusanya. Kwa maoni yangu mzee Warioba yuko sahihi kabisa.

as to whether JK alifanya makosa kuruhusu ukiukaji wa katiba na kufanya nchi iote ndani ya nchi, hilo ni kweli, lakini sioni kama ndani ya CCM kuna mwenye ubavu wa kukosoa hilo. Warioba amelisema wazi mara nyingi kuwa sasa Zanzibar ni nchi kisheria, kwa hiyo umewekwa msingi wa kisheria pia kudai Tanganyika.
Tume zote ziliundwa na wenyeviti wa CCM.
Hakuna mapendekezo yaliyofanyiwa kazi.

Warioba yupo sahihi kabisa na alichojaribu ni kusahihisha makosa ya JK
Kuvunjwa kwa katiba

Kutoa zawadi kwa wazanzibar huku chuki ikijengeka kwa Watanganyika.

Warioba na tume wamebaini hasira za Watanganyika zinaweza kuvunja muungano kama glass.
Leo Watanganyika wanajua kiuchumi, wanaumia sana kuhudumia huu muungano.

Bado wanaambiwa kilchowaumiza miaka 50 kinatafutiwa dawa.

Dawa ni hiyo ya kuwafurahisha wzn kila siku. Kwamba kila wanapodai wanapewa, hawana uwajibikaji na wala hawajui gharama za muungano uliopo.

Hatuwezi kukaa kimya Watanganyika wakimenyeka kulipa kodi zao kwenda nchi jirani ya Zanzibar.
Tunauliza, Mtanganyika analipa gharama hizo kwa faida gani kutoka znz.

Warioba anajaribu kusahihisha makosa ya ubaguzi wanayoyafanya wazanzibar
Leo Mtanganyika ni mgeni znz, na mznz ni mwenyeji Tanganyika.

Warioba na tume wamegundua hasira za wznz zinajibika, za Watanganyika ni vunja pasua kichwa

Katika kulinda muungano, wamejaribu kuja na kitu kitakachowalamisha wznz kujua uchungu wa muungano.

Leo wznz wapo Dodoma na kwingineko wakipiga soga kwa gharama za Mtanganyika.

Wamefika mahali hawakusanyi kodi kwa kisingizio cha bandari huru kwa vile wanajua wana mgao wa kutosha kutoka kwa walipa kodi wa Tanganyika.

Watanganyika tunasema, kama watalazimisha huko Dodoma na Lumumba street hilo halina tatizo.

Tatizo ni pale Watanganyika watakapochoka na kuamua kuchukua haki yao.

Watakaolipa gharama hiyo ni wazanzibar, tena watalipa kwa mate, machozi,jasho n.k.

Hakutakuwa na muda wa majadiliano, suala litakuwa moja, tatizo ni wznz na agenda itakuwa juu yao na si muungano tena. Watakuwa katika hali mbaya sana.
 
Back
Top Bottom