Serikali 3 na gharama zake

Serikali 3 na gharama zake

Between:
1. trade
2. Foreign direct investment
3. Aid

Kipi ni bora kwa taifa? Katika yote haya, aid ni kitu cha mwisho kukipigania, unachohitaji ni more trade and investments. Sijui kwanini Watu wanapoteza muda kujadili AID kitu ambacho hakuna case study in Africa Kwamba ilisaidia taifa kujikwamua kiuchumi. Aid is beneficial only to tyrants na ndicho Wanasiasa ZnZ wanachotaka.
Hii ndio hoja ya Mkandara kuwa znz haiwezi kupewa misaada na mikopo .

Tena akieleza vyanzo vya mapato, Mkandara kaliorodhesha hili kama eneo muhimu sana. Msome hapo juu
Mkandara anasema mikopo nayo ni sehemu ya mapato, na anadai znz kutopewa fursa ya kukopa ni jambo baya sana sana sana.
Msaada ni kudhalilika, kukopa ni kudhalilika lakini watu wanaona fahari, wanasema znz inakosa fursa hizo!!!! fursa za mikopo

Nipo katika rekodi nikimwambia kuongelea misaada na mikopo ni udhalili wa hali ya juu sana.
Mkandara anasema huo ndio mchango wa znz katika muungano.

Nimemuuliza nje ya muungano znz itapata kwa kadri yake. Kwasasa wanapata 4.5% ya Trilioni 12 ambazo hawana mchango hata senti tano yaani pato la Tanganyika.

Hiyo ni zaidi ya nusu ya pato lao la mwaka. Mkandara hataki kuliona hilo anaamini ili znz iwe bora lazima iwe na kiti IMF, WB ili iweze kukopa. Kwa akina Mknadara na wazanzibar, kuwa na bendera IMF,WB ni fahaari kubwa saana.

Yaani kukopa na misaada ipo katika mawazo ya wznz na Mkandara kuliko njia za kujikwamua. Wanaamini kabisa mikopo na misaada ni neema, tena ukiangalia znz ndipo utashangaa kabisa, asset za kukopa zipo wapi? Yaani vituk

Dambisa Moyo kawaeleza vizuri sana wazungu na Waafrika kuhusu misaada.

Imefiaka mahali watu wanaorodhesha mikopo kama income, wanaorodhesha misaada kama income! teh te teh teh.

Mi nikisoma mikopo na misaada ya akina Mkandara huwa napata shaka kama kweli fikra zetu zitabadili taifa hili.
Ningeweza kuwapa benefit of doubt wavuvi na wakwezi wa znz kuhusu hili, nashangaa Mkandara anaandika kutoka majukuu na kuungana na hao wavuvi na wakwezi regardless of his exposure. duh!
 
.

..lakini wa-Znz wenyewe wanasema wanataka madaraka makubwa na mapana zaidi ili wasiwe tegemezi kwa wa-Tanganyika.
Swali ambalo Kobello huwa halijibu ni hili hapa,kwani kwasasa hivi nani analipaia gharama za S2?

Yaani Kobello anaamini ukiwa na jina Tanzania, basi gharama zinapungua kwa Mtanganyika.
Ukitenganisha S3 gharama zinaongezeka na znz inashindwa kulipa.
Kwamba, inaweza kulipa ikiwa ndani ya Tanzania na inashindwa kulipa ikiwa nje ya Tanzania.

Zanzibar wanataka madaraka kuamua mambo yao. Tume ya Warioba ilikuwa na 50%, gharama kazibeba Tanganyika 100%.

Wanataka wawe na fursa na haki katika muungano. Likija suala la kuchangia muungano mnasema hawawezi.

Muungano wa sasa ni wa kiuchumi sio muungano wa kuatafutia wazanzibar nafasi na ajira. Lazima wawajibike.

Watanganyika kama Kobello wanaamini waznz wana haki na fursa sawa, kuchangia muungano si haki yao ni zigo la Mtanganyika.

Watanganyika wamelishwa limbwata. Yanapokuja mambo ya madaraka, vyeo n.k. utawasikia wznz wote watakavyobwata.

Likja suala la kuchangia muungano utasikia hawawezi.
Sasa kama hawawezi hawapo katika muungano na hakuna maana ya wao kuwa katika muungano.

Muungano ni kusaidianaa si kubeba mmoja akila, zaidi ya wale wanaotembea.

Ninyi Watanganyika, pesa zinazokwenda znz ni zaidi ya bajeti ya mikoa 20 ya Tanganyika, hivi hamuoni hapo kuna tatizo?

Kinyume chake mikoa hiyo 20 inachingia muungano 100% na hao wznz wanachangia 0% Imean nothing, empty, nill, Nada.

Jiulizeni mna invest kwa znz kwa return gani. You have to open your eyes!

Na hao wznz hawawatambui ninyi isipkuwa wakati wa bajeti.

Wao si Watanzania wameshasema ni wznz, ninyi ndio Watanzania baada ya kuuza Utanganyika wenu.

Utanzania wenu ndio wanautumia kuwaibia, ni wezi tu hawa.Humuoni hilo?

Watanganyika mnahitaji nini ili muone?
 
Swali ambalo Kobello huwa halijibu ni hili hapa,kwani kwasasa hivi nani analipaia gharama za S2?

Yaani Kobello anaamini ukiwa na jina Tanzania, basi gharama zinapungua kwa Mtanganyika. Ukitenganisha S3 gharama zinaongezeka na znz inashindwa kulipa. Kwamba, inaweza kulipa ikiwa ndani ya Tanzania na inashindwa kulipa ikiwa nje ya Tanzania.
Yes.

Kwa sababu serikali ya T anganyika itakuja na gharama zake mpya.
 
Serikali 3 na gharama zake

Baada ya kuvunjika kwa bunge la katiba juu ya swala la muundo wa serikali, nachukua nafasi hii kutoa majibu ambayo kwa sababu zisizojulikana imeshindikana kabisa kuelezewa tofauti ya gharama baina ya serikali 2 na 3, gharama zipi zitaongozeka kulingana na mapendekezo ya rasimu ya tume ya Warioba.

Na sii lengo langu kujaribu kuukana ukweli kwamba Tanzania ya leo inahitaji serikali 3 isipokuwa kuwataarifu wananchi kuelewa jinsi gani muundo wa aina hii una mamlaka gani na unafanyaje kazi zake ktk utekelezaji wa majukumu wanayokabidhiwa kikatiba. Hii inatokana na mimi kuwasoma watu wengi kutofahamu Mamlaka ya tawala wa muundo huu ili serikali hizo ziweze kuwawakilisha wananchi wake haraka na kwa ufasaha zaidi. Hivyo lengo la kuzitaka serikali 3 linaonyesha wazi ni kutaka kutengenisha mambo ya Muungano na yasiyokuwa ya Muungano kwa bara kutokana na ukweli kwamba hadi sasa Mambo yote ya Muungano ni mambo ya bara sio ya Muungano badala ya kuziunda serikali ziwe karibu Zaidi na wananchi wake ktk utekelezaji wa matakwa yao.

Mara zote nimesikia wananchi wakidai kuwepo kwa seikali 2 hakuna tofauti ya gharama na serikali 3 na wakitumia sababu za mapngufu ya utawala uliopo ambao miaka yote baada yatangu 1984 tulipounda vyama vingi, kumekuwa na mkanganyika wa utawala ambao umewavuruga wananchi wasijue mamlaka ya vyombo vyao yana ukomo gani. Pia imewavuruga viongozi ambao kwa dhana wamekuwa wakiongeza mikoa wilaya na majibo kufikiria ndio njia rahisi ya kuwafikia wananchi wakati mamlaka bado yapo chini ya rais wa serikali kuu. Hivyo mitazamo yote hii imelenga zaidi hifadhi ya Utawala (kisiasa) kuliko sababu za ujenzi wa nyenzo za kuijenga nchi na wananchi wake ambao pia kw abahati mbaya wamevutwa katika zizi la Uchama na kupoteza Utaifa wao.
Ngoja niseme ukweli, Ukweli ni kwamba tunapoihitaji serikali ya 3 siyo serikali ya ya Tanganyika kama wanavyodai wanasiasa wengi ama wana taaluma wapambanaji isipokuwa tunaihitaji serikali ya Muungano ambayo haipo. Ukweli ni kwamba jina la Muungano lipo lakini hatuna seriikali ya Muungano toka mwaka 1984, niliwahi kulisema jhili na sasa limedhihirishwa ktk kongamano la jana. Imeelezwa katika kongamano la Mwl.Nyerere foundation ya kwamba hata hayo mambo tunayosema kuwa ni ya Muungano ni mambo ya serikali ya bara.

Hivyo mawaziri wote walioko ktk ushirika wa Muungano ni mawaziri wa serikali ya Tanganyika sio ya Muungano. Wajumbe hao walifikia hadi kuhoji ni lini wananchi wamewaona viongozi mawaziri wa Muungano wakitemebelea Zanzibar katika maswala ya Muungano?. Kwa hiyo tunazo serikali2 nazo ni serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika - Hatuna serikali ya Muungano!.. Ukweli ndio huo japo unauma.

Kwa hiyo basi ni muhimu tukubali kwamba tuchukulie kwamba hii serikali ya Muungano ni serikali ya bara, bunge lake, mahakama zake zote ni za bara, na ndio maana wapo wananchi wanahoji kuwepo kwa wabunge wa Zanzibar katika bunge la Muungano kujadili mambo yasokuwa ya Muungano bila kujua kwamba pale hakunamambo ya Muungano. Hivyo tunachokililia leo hii ni serikali ya Muungano sio Tanganyika maaa ipo.

Sasa swali linakuja - Tukiunda serikali ya 3 ya Muungano haitakuwa na gharama zake? Hizo ghrama zake ni nani atazihudumia? Na Je, bunge la serikali hii litakuwa na wajumbe wangapi, kutoka wapi na majimbo gani? Mishahara na posho zao zitagharamiwa na nani, watumishi wake watakuwa sehemu zote za Jamhuri au makao makuu tu na kadhalika… Hizi gharama za misafara ya rais ktk mialiko ya Kimataifa, mawaziri wake, mamlaka yake katika mipango ya maendeleo na kadhalika ndiyo maswala muhimu ya kujadili kuliko kuendelea kuidai Tanganyika ambayo ipo.

Je, nchi za wenzetu walokuwa na mfumo kama huu mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za serikali zake umejengwa vipi na nini nafasi ya serikali kuu ktk ujenzi wa Mataifa hayo. Nini ukomo wa mamlaka ya serikali za nchi kuendea mamlaka ya serikali kuu juu ya jambo hilo hilo. Ikiwa Nchi inahitaji uwekezaji katika Kilimo, serikali kuu itahusika vipi tofauti na hizo za kila nchi.

Nafikiri hii inatosha kwa leo tutaendelea inapobidi baada ya michango yenu.

Huwa sielewi mfumo wa serikali yetu. Tunasemaje tuna serikali 2, maraisi 2, mabunge 2, wakati maamuzi makubwa (Ulinzi,Fedha na Mambo ya nje) yanafanyika Magogoni? Je suala ni idadi ya serikali au madaraka? Bwana mkandara unasemaje kuhusu hilo?
 
Hapana rasimu imesema nchi washirika zitaruhusiwa kukopa na kuingia mikataba na mashirika au taasisi za kimataifa. Endapo JMT itahitaji basi itasaidia kwa hilo.

Kilio cha znz cha muda mrefu ni kuziwa kukopa au kukopa kupitia JMT.
Kusema hawataweza kulipa gharama za shirikisho si kweli. Wataruhusiwa kukopa hata Mkandara atathibitisha hili.
Kukopa ndio kilio chao cha muda mrefu sana, na rasimu imewapa nafasi hiyo
Kukopa kwa ajili ya maendeleo, siyo kukopa kwa ajili ya administration.
Tuwe tunaona aibu jamani.
 
Yes.

Kwa sababu serikali ya T anganyika itakuja na gharama zake mpya.
Swali ni kuwa, kwani sasa gharama hizo analipa nani katika muundo wa S2?

Pili, Tanganyika haiwezi kuongeza gharama. Hivi ukiwa na mambo 22 au 7 yapi ni mengi na yenye gharama?
 
Kukopa kwa ajili ya maendeleo, siyo kukopa kwa ajili ya administration.
Tuwe tunaona aibu jamani.
Wacha kukopa kwa maendeleo, mimi hata kuongelea kukopa naona aibu.

Waeleze akina Mknadara kuwa kukopa kuwe kwa maendeleo si utawala. Hoja ya kukopa na misaada ni yao.

Mimi siamini katika misaada hata kidogo, na wala sidhani IMF na WB wanakopesha kwasababu wanatupenda sana.

Mkandara anasema hiyo ni dhulma wanayofanyiwa wznz. Aibu
 
Swali ni kuwa, kwani sasa gharama hizo analipa nani katika muundo wa S2?

Pili, Tanganyika haiwezi kuongeza gharama. Hivi ukiwa na mambo 22 au 7 yapi ni mengi na yenye gharama?
Kwa sasa gharama hizo zinalipwa na JMT/Tanganyika.

Ingekuwa swali lako la pili lipo based on such a simple logic, labda ungepata jibu unalotarajia. Na ndivyo inavyozungumzwa huko mjini. Kuwa mambo ya muungano yamepungua kwa hiyo mambo ya muungano yatapunguza gharama. Huo ni uongo mtakatifu!!

Serikali ya muungano lazima itashughulikia International trade, Statistics,Climate, Research,Industrial licensing, Environmental Protection (Mimi ningependekeza ipewe National Parks na Game Reserves zote), Kilimo na mifugo, Uvuvi, Mawasiliano na Uchukuzi, Sheria, Hazina (meaning fedha apart from currency, yaani taxation,mikopo na madeni etc), Social Welfare, Elimu etc....

Msiwasikilize hao wajumbe wa Tume ya Katiba, hawawaambii ukweli na wameficha mambo fulani. I can sense that.
 
Hapana rasimu imesema nchi washirika zitaruhusiwa kukopa na kuingia mikataba na mashirika au taasisi za kimataifa. Endapo JMT itahitaji basi itasaidia kwa hilo.

Kilio cha znz cha muda mrefu ni kuziwa kukopa au kukopa kupitia JMT.
Kusema hawataweza kulipa gharama za shirikisho si kweli. Wataruhusiwa kukopa hata Mkandara atathibitisha hili.
Kukopa ndio kilio chao cha muda mrefu sana, na rasimu imewapa nafasi hiyo

Kadri tunavyojadiliana na kujenga ufahamu vivyo hivyo ndipo baadhi ya maswali ambayo mengine, pengine wawezadhani yana majibu ya wazi, ndivyo yanavyojitokeza. Kwa mfano: Je, rasimu inatambua/inathibitisha/inapendekeza uwepo wa nchi ngapi? 3, 2 au nchi 1? Kumbuka sizingumzii Serikali!
 
Serikali ya muungano lazima itashughulikia International trade, Statistics,Climate, Research,Industrial licensing, Environmental Protection (Mimi ningependekeza ipewe National Parks na Game Reserves zote), Kilimo na mifugo, Uvuvi, Mawasiliano na Uchukuzi, Sheria, Hazina (meaning fedha apart from currency, yaani taxation,mikopo na madeni etc), Social Welfare, Elimu etc....

Msiwasikilize hao wajumbe wa Tume ya Katiba, hawawaambii ukweli na wameficha mambo fulani. I can sense that.

Kwa maoni yako kuongezeka kwa "mambo ya muungano" ni kujenga muungano au kudhoofisha muungano?

Mimi naamini mambo yakiongezeka maana yake ni kuwa washirika wanaukaribia zaidi muungano wa kweli, kwani mwisho wa siku taasisi zinazoshughulikia masuala ya muungano nazo inatakiwa ziungane!

What do others think? Mchambuzi, Mkandara and Nguruvi3 especially!
 
Kwa maoni yako kuongezeka kwa "mambo ya muungano" ni kujenga muungano au kudhoofisha muungano?

Mimi naamini mambo yakiongezeka maana yake ni kuwa washirika wanaukaribia zaidi muungano wa kweli, kwani mwisho wa siku taasisi zinazoshughulikia masuala ya muungano nazo inatakiwa ziungane!

What do others think? Mchambuzi, Mkandara and Nguruvi3 especially!
Hapa mnasahau ukweli kuwa ndivyo ilivyokuwa hadi tukawa na mambo 22.

Wazanzbar wakaandika katiba ya 2010 inayowapa uwezo wa kuondoa au kuacha mambo ya muungano katika JMT.
Kwa mfano, wameunda baraza lao la mitihan, ZBR, ZMO,shirika lao la bandari na Anga
Na orodha ni ndefu sana.

Katika mazingira hayo, znz inapewa uwezo wa kuamua nini kiwemo ndani ya muungano na kipi kisiwepo.
Kwa mfano, hutasikia wakizungumzia ulinzi na usalama kwasababu kwao ni nafuu.

Hata katika mashirika na taasisi walizounda, wazanzibar wamebaki kuwa tegemezi kwa kuvizia.
Kwa mfano, ZMO inahudumia znz lakini ada zake zinalipiwa na JMT

Hivi baraza la mitihani la taifa NECTA linasababu gani kuwa na wajumbe kutoka znz ikiwa wana baraza lao
Kuna sababu zipi za kuwa na wajumbe katika bandari, anga, TBS na taasisi nyingine

Hapa maana yake ni Wzn wanatumia JMT kama eneo La kupunguza tatizo la ajira, wala si kuongeza ukaribu wa muungano.

Labda nikuulize, wizara ya kilimo inawahusu nini wazanzibar hadi wabunge wao wajadili na wawe na wafanyakazi wao.

Katika kuhakikisha wanaitumia vema JMT, wazanzibar wanadaia wapewe kodi za wafanyakazi wa muungano.

Tunajua wafanyakazi wa muungano wanahusisha wizara nne tu kwa hali ilivyo sasa.

Utashangaa wamepewa bilioni 15 kama kodi za wafanyakazi wa wizara za kilimo, afya, ujenzi, akina mama na watoto, maliasili na utalii, nishati n.k. Hizo hazipo katika mambo ya muungano, kwanini walipwe kodi za wafanyakazi wasiowahusu.

Kwa maana nyingine licha ya kwamba tunasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa gharama za wananchi wa Tanganyika(wanakosa nafasi) bado tunawalipa kwa kupunguza tatizo la ajira kwao.

Hakuna maana yoyote ya kuwa na mambo ya pamoja ikiwa znz ina mambo yao.

Ndipo inapokuja hoja ya matter of principla. Kuwa Tanganyika ina deserve fiscal autonomy yake ili (ii) ku-manage economy yake.

Hivyo wazanzibar hawataki mambo yawe ya muungano, kudhani hilo linawezekana ni kujidanganya.
Ni sawa na kusema tuwe na serikali moja.

Hatuwezi kuwa na JMT yenye mambo yote huku mambo hayo yakiwa ni rasilimali na mipango ya Tanganyika tu.

Njia nzuri ya kuwa na muungano fair ni kutenga mambo na kila serikali ishughulikie mambo yake.

Kwa hali ilivyo, Watanganyika wanadhulumiwa na kuonewa. Kwabahati mbaya wao kama alivyo Mwanagenzi hawaoni dhulma hiyo.

Wanachokitaka ni kuwa na JMT tu hata kama ni kwa gharama za watoto wao.

Huwezi kuwa na mambo yote ya muungano, wakati Zanzibar wameshijitoa katika muungano

Hawajitambulishi kama Watanzania bali wazanzibar.

Vipi unaweza kuwa na mambo yote ikiwa wao hawakubali huo Utanzania isipkuwa wanapotaka mafao, fursa na utegemezi?
 
Kobello,

Kuhusiana na hoja kwamba serikali ya Tatu itaongeza gharama, tuliangalie kwa mfano jeshi la polisi, utaratibu na allocations ya kimataifa ni Askari mmoja kwa kila Watu, raia au wananchi Mia nne; serikali tatu zitaongeza gharama gani Katika suala hili?

katiba ya sasa ya JMT Inasema wazi Kwamba serikali ya muungano ndiyo inasimamia pia mamlaka ya Tanganyika/Tanzania bara, kwa maana hii, gharama za Tanganyika Zipo na zinatambulika kikatiba, sasa cha ajabu nini kuhusiana na gharama za Tanganyika Kwamba kutakuwa na gharama Wakati katiba inaweka wazi Kwamba kuna gharama za Tanzania bara za kusimamia? Gharama hizi Zipo tu...

Na Isitoshe, kwa Mujibu wa rasimu, wizara za muungano zitakuwa ni nne tu tofauti na Hali ya sasa chini ya serikali Mbili ambapo Zipo za muungano, zipo mchanganyiko baina ya Tanganyika na muungano, na Zipo za Zanzibar...



Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
Kobello,

Kuhusiana na hoja kwamba serikali ya Tatu itaongeza gharama, tuliangalie kwa mfano jeshi la polisi, utaratibu na allocations ya kimataifa ni Askari mmoja kwa kila Watu, raia au wananchi Mia nne; serikali tatu zitaongeza gharama gani Katika suala hili?

katiba ya sasa ya JMT Inasema wazi Kwamba serikali ya muungano ndiyo inasimamia pia mamlaka ya Tanganyika/Tanzania bara, kwa maana hii, gharama za Tanganyika Zipo na zinatambulika kikatiba, sasa cha ajabu nini kuhusiana na gharama za Tanganyika Kwamba kutakuwa na gharama Wakati katiba inaweka wazi Kwamba kuna gharama za Tanzania bara za kusimamia? Gharama hizi Zipo tu...

Na Isitoshe, kwa Mujibu wa rasimu, wizara za muungano zitakuwa ni nne tu tofauti na Hali ya sasa chini ya serikali Mbili ambapo Zipo za muungano, zipo mchanganyiko baina ya Tanganyika na muungano, na Zipo za Zanzibar...



Sent from my iPhone using JamiiForums
Polisi, jeshi, currency, uhamiaji, vyama vya siasa na katiba havitaongeza wala kupunguza gharama zake za uendeshaji kwa sababu vyombo hivi vitakuwa chini ya serikali moja.

Lakini katika mfumo wa Federation, serikali kuu itakuwa na Treasury yake na Serikali ya Tanganyika pia. Simaanishi kuwa Treasury ya Union itasimamia currency tu (yaani itasimamia Central Bank na Monetary Policy tu) bali itabidi isimamie Fiscal Policies zake na lazima itakuwa na departments na wafanyakazi wake tofauti na Tanganyika. Tanganyika itakuwa na Fiscal autonomy yake kwa hiyo nayo itahitaji vyombo vyake na wafanyakazi wake. Kwa sasa hivi, monetary policies zipo chini ya BOT na Fiscal policies zipo chini ya Hazina. Tukianzisha serikali ya Tanganyika, itabidi tuwe na Hazina ya Tanganyika ambayo itasimamia fiscal policies za Tanganyika independent of and under the jurisdiction of both Zanzibar and Union governments respectively. Kwa hiyo utahitaji chombo kipya chenye wafanyakazi wake na administration costs mpya kwa mwananchi wa Tanganyika.

Kuna Suala la International Trade, hili suala lazima nalo lisifichwefichwe kwa sababu huwezi kuondoa International trade kwenye Union. Lazima Union itakuwa na international trade kwa hivyo hilo ni la nane tayari panga pangua.For example,
Tanganyika ikiamua kujenga bomba la mafuta kwenda Mombasa kupitia Tanga, hiyo tayari ni international trade ambayo ipo chini ya jurisdiction ya Mipaka ya Serikali kuu ya Muungano, yaani mipaka ya Tanzania na Serikali ya muungano lazima ihusike. hata biashara za binafsi zinazovuka mipaka lazima ziwe controlled na Union government chini ya uhamiaji na customs. Kwa hiyo international trade itakuwa na chombo chake Tanganyika na Muungano (sizungumzii mambo ya mabalozi, kwa sababu hawa ni constant kwa union peke yake).

Mambo ya kilimo na mifugo, lazima kuwe na department yake kwenye Muungano na Tanganyika. Hasa kwenye issue ya Ghala la Taifa (food security), kwenye stabilization ya bei, emergencies, disease and pest control etc .. lazima Union iwe na chombo cha kusimamia haya mambo, haiwezi kuziachia Tanganyika na Zanzibar ziwe too independent kwenye masuala haya. They have to be harmonized.

Hapo bado kuna kupangua na kupanga court system ili kukabili changamota za Federal systems. Especially constitutionality issues na Inter-state trade na arbitrations nyingine kwa sababu migongano itakuwa mingi na efficiency ya mahakama zetu sidhani kama ipo tayari. Mfumo wa Federation (hasa tunaoutaka sisi ambao ni tofauti na federations kama za Nigeria etc...) ni mfumo unaotokana na nchi mbili zilizokwisha kuwa huru na wala siyo Kano na Biafra au Kivu na Katanga.

Costs zitaongezeka, tena sana na tusipende kukariri talking points za idadi ya Polisi na idadi za mawaziri. Waziri mmoja hata akilipwa milioni 200 kwa mwaka wakiwa kumi ni bilioni 2 kwa mwaka. Hatuzungumzii bilioni mbili kwa mwaka, tunazungumzia trilions.


Talking points zingine ni kukopa. Hivi watu wazima wanaweza kukaa chini na KUSEMA KUWA TUKISHINDWA TUTAPEWA MISAADA?? Mimi sioni kama ni jambo linalofaa hata kuzungumzwa na kiongozi yeyote yule.
 
..naunga mkono hoja zako kwa asilimia 100.

..imetokea mara nyingi wa-Znz kushindwa kuendesha mambo yao na Tanganyika ikalazimika kuwasaidia.

..lakini wa-Znz wenyewe wanasema wanataka madaraka makubwa na mapana zaidi ili wasiwe tegemezi kwa wa-Tanganyika.

Mkuu that is a fact, ndio maana ukiangalia post zangu zote mimi naelekea zaidi kwenye serikali moja ya Tanzania. Mara kadhaa nimesikia serikali ya Zanzibar inaomba hela kwa Bakhresa kulipa mishahara wafanyakazi wa serikali, hii inaonesha kabisa kuwa bado hakuna uwezo wa kuendesha serikali makini.
 
Polisi, jeshi, currency, uhamiaji, vyama vya siasa na katiba havitaongeza wala kupunguza gharama zake za uendeshaji kwa sababu vyombo hivi vitakuwa chini ya serikali moja.

Lakini katika mfumo wa Federation, serikali kuu itakuwa na Treasury yake na Serikali ya Tanganyika pia. Simaanishi kuwa Treasury ya Union itasimamia currency tu (yaani itasimamia Central Bank na Monetary Policy tu) bali itabidi isimamie Fiscal Policies zake na lazima itakuwa na departments na wafanyakazi wake tofauti na Tanganyika. Tanganyika itakuwa na Fiscal autonomy yake kwa hiyo nayo itahitaji vyombo vyake na wafanyakazi wake. Kwa sasa hivi, monetary policies zipo chini ya BOT na Fiscal policies zipo chini ya Hazina. Tukianzisha serikali ya Tanganyika, itabidi tuwe na Hazina ya Tanganyika ambayo itasimamia fiscal policies za Tanganyika independent of and under the jurisdiction of both Zanzibar and Union governments respectively. Kwa hiyo utahitaji chombo kipya chenye wafanyakazi wake na administration costs mpya kwa mwananchi wa Tanganyika.

Kuna Suala la International Trade, hili suala lazima nalo lisifichwefichwe kwa sababu huwezi kuondoa International trade kwenye Union. Lazima Union itakuwa na international trade kwa hivyo hilo ni la nane tayari panga pangua.For example,
Tanganyika ikiamua kujenga bomba la mafuta kwenda Mombasa kupitia Tanga, hiyo tayari ni international trade ambayo ipo chini ya jurisdiction ya Mipaka ya Serikali kuu ya Muungano, yaani mipaka ya Tanzania na Serikali ya muungano lazima ihusike. hata biashara za binafsi zinazovuka mipaka lazima ziwe controlled na Union government chini ya uhamiaji na customs. Kwa hiyo international trade itakuwa na chombo chake Tanganyika na Muungano (sizungumzii mambo ya mabalozi, kwa sababu hawa ni constant kwa union peke yake).

Mambo ya kilimo na mifugo, lazima kuwe na department yake kwenye Muungano na Tanganyika. Hasa kwenye issue ya Ghala la Taifa (food security), kwenye stabilization ya bei, emergencies, disease and pest control etc .. lazima Union iwe na chombo cha kusimamia haya mambo, haiwezi kuziachia Tanganyika na Zanzibar ziwe too independent kwenye masuala haya. They have to be harmonized.

Hapo bado kuna kupangua na kupanga court system ili kukabili changamota za Federal systems. Especially constitutionality issues na Inter-state trade na arbitrations nyingine kwa sababu migongano itakuwa mingi na efficiency ya mahakama zetu sidhani kama ipo tayari. Mfumo wa Federation (hasa tunaoutaka sisi ambao ni tofauti na federations kama za Nigeria etc...) ni mfumo unaotokana na nchi mbili zilizokwisha kuwa huru na wala siyo Kano na Biafra au Kivu na Katanga.

Costs zitaongezeka, tena sana na tusipende kukariri talking points za idadi ya Polisi na idadi za mawaziri. Waziri mmoja hata akilipwa milioni 200 kwa mwaka wakiwa kumi ni bilioni 2 kwa mwaka. Hatuzungumzii bilioni mbili kwa mwaka, tunazungumzia trilions.


Talking points zingine ni kukopa. Hivi watu wazima wanaweza kukaa chini na KUSEMA KUWA TUKISHINDWA TUTAPEWA MISAADA?? Mimi sioni kama ni jambo linalofaa hata kuzungumzwa na kiongozi yeyote yule.

Mkuu kuna watu bila hata aibu wanasema serikali ya Muungano inaizuia Zanzibari kuomba nje, wengine wanasema wazi kabisa kuwa Zanzibar ikiwa nje ya muungano itaendeshwa kwa misaada. You can not believe this, but this is what is being said.
 
Kwa sasa gharama hizo zinalipwa na JMT/Tanganyika.

Ingekuwa swali lako la pili lipo based on such a simple logic, labda ungepata jibu unalotarajia. Na ndivyo inavyozungumzwa huko mjini. Kuwa mambo ya muungano yamepungua kwa hiyo mambo ya muungano yatapunguza gharama. Huo ni uongo mtakatifu!!

Serikali ya muungano lazima itashughulikia International trade, Statistics,Climate, Research,Industrial licensing, Environmental Protection (Mimi ningependekeza ipewe National Parks na Game Reserves zote), Kilimo na mifugo, Uvuvi, Mawasiliano na Uchukuzi, Sheria, Hazina (meaning fedha apart from currency, yaani taxation,mikopo na madeni etc), Social Welfare, Elimu etc....

Msiwasikilize hao wajumbe wa Tume ya Katiba, hawawaambii ukweli na wameficha mambo fulani. I can sense that.
Hapa ndipo sikubaliani na Watanganyika wengi. JMT ni Tanganyika na Zanzibar. Gharama za sasa zinalipwa na Mtanganyika 100%. Hakuna mahali wala mtu anayekataa ukweli huu.

Pamoja na kuwa znz ina fiscal autonomy yake, mambo kama ya kodi(TRA) hayaingii katika muungano yanabaki znz.
Kwa mantiki hiyo kodi ya kuhudumia muungano kaibeba Mtanganyika 100%
Hivyo, jibu lako la kusema anayegharamia muungano ni JMT hilo ni kutaka kuficha ukweli na ndilo hasa ninawasikitikia Watanganyika.

Wanajidanganya wakijua kuwa watanganyika wanalazimika kulipa kodi kwenda nchi jirani isiyowahusu kwa namna yoyote.
Hakuna sababu ya kumbebesha Mtanganyika kodi kwenda kuhudumia znz. Hakuna sababu kabisa isipokuwa ujinga tu!

Pili, Zanzibar wanataka mamlaka yao ya International trade. Znz wana bureau of statistic, wana climate depart, research institute zao, industrial license, environ protection, kilimo na mifugo, mawasiliano na uchukuzi, ZRA, baraza la mitihani, Bandari, Anga, utalii n.k. Tayari wanazo.

Unaposema eti hayo ni sehemu ya mambo ya muungano, unachotaka kusema ni kuwa uwepo wake ni kwa faida ya wote lakini gharama zake abebe Mtanganyika. Na kwamba znz ina haki ya kuwa na mambo yake, yale ya Watanganyika yawe ya wote.
Huu uzezeta wa Watanganyika utaisha lini?

Huwezi kuwa na muungano wa mambo yote huku sehemu moja ikiwa na mambo yake. Hili halipo popote duniani.

Ukiataka hivyo ni lazima uwe na ya Tanganyika ili baadaye kuwe na chombo cha pamoja.
Wazanzibar hawataki sasa ninyi mnalazimisha. Hivi hamuoni manaleta tatizo?

Nimekuuliza, mambo 22 sasa ni 7 (rasimu). Ni yapi yaliyoondolewa(15 ) ambayo Tanganyika inaona yameongeza gharama?

Katika mambo 22 ambayo kiidara ni 47 naomba uniambie kuhusu hili.

1. Zanzibar ilipoondoa bandari, anga, statistic, baraza la mitihani, ZBS n.k. gharama gani zimeongezeka kwa Tanganyika?

2, Hoja ya msingi hapa ni kuwa yalipopunguzwa mambo 22 a kubaki 7, kwa maana yaliondolewa 15, Tanganyika imeingia vipi gharama. I mean sasa tuna mambo ya Tanganyika na znz katika maeneo fulani, Tanganyika imeingia vipi gharama za ziada?

3. Katika mambo 7 ya tume, tunaomba utuonyeshe kuwa yanapokuwa ya ushirika Tanganyika itaingia gharama zaidi.
Hapa tuna ulinzi na usalama, mambo ya ndani, mambo ya nje, katiba, uraia na uhamiaji

Hapa tunataka utueleze, mambo hayo yanapokuwa ya shirikisho Tanganyika inaongeza vipi gharama.
 
Pili, Zanzibar wanataka mamlaka yao ya International trade. Znz wana bureau of statistic, wana climate depart, research institute zao, industrial license, environ protection, kilimo na mifugo, mawasiliano na uchukuzi, ZRA, baraza la mitihani, Bandari, Anga, utalii n.k. Tayari wanazo.

Unaposema eti hayo ni sehemu ya mambo ya muungano, unachotaka kusema ni kuwa uwepo wake ni kwa faida ya wote lakini gharama zake abebe Mtanganyika. Na kwamba znz ina haki ya kuwa na mambo yake, yale ya Watanganyika yawe ya wote.
Huu uzezeta wa Watanganyika utaisha lini?

Huwezi kuwa na muungano wa mambo yote huku sehemu moja ikiwa na mambo yake. Hili halipo popote duniani.

Ukiataka hivyo ni lazima uwe na ya Tanganyika ili baadaye kuwe na chombo cha pamoja.
Wazanzibar hawataki sasa ninyi mnalazimisha. Hivi hamuoni manaleta tatizo?

Nimekuuliza, mambo 22 sasa ni 7 (rasimu). Ni yapi yaliyoondolewa(15 ) ambayo Tanganyika inaona yameongeza gharama?

Katika mambo 22 ambayo kiidara ni 47 naomba uniambie kuhusu hili.

1. Zanzibar ilipoondoa bandari, anga, statistic, baraza la mitihani, ZBS n.k. gharama gani zimeongezeka kwa Tanganyika?

2, Hoja ya msingi hapa ni kuwa yalipopunguzwa mambo 22 a kubaki 7, kwa maana yaliondolewa 15, Tanganyika imeingia vipi gharama. I mean sasa tuna mambo ya Tanganyika na znz katika maeneo fulani, Tanganyika imeingia vipi gharama za ziada?

3. Katika mambo 7 ya tume, tunaomba utuonyeshe kuwa yanapokuwa ya ushirika Tanganyika itaingia gharama zaidi.
Hapa tuna ulinzi na usalama, mambo ya ndani, mambo ya nje, katiba, uraia na uhamiaji

Hapa tunataka utueleze, mambo hayo yanapokuwa ya shirikisho Tanganyika inaongeza vipi gharama.
Kabla ya kukujibu maswali yako matatu, itabidi niweke mambo fulani sawa,

Kama Znz walivyo na idara zao independently, ndivyo hivyohivyo Tanganyika itakuwa na mambo yake independently hata kama serikali ya muungano itakuwa inasimamia hayo mambo.

Vilevile, Serikali ya muungano itabidi iwe na vyombo vya kusimamia mambo yasiyo ya muungano. Hiyo tume iliyopendekezwa itakuja kuwa one of the biggest bureaucracies in Tanzanian history (May be close to PM's office now or even more).Na mawaziri wake lazima watakuwa na wakurugenzi au mawaziri wadogo wataosimamia workforce kubwa na yenye bajeti kubwa kuliko neno "Tume" linavyofikiriwa. Ni sawa na President's Office leo ilivyo na mawaziri na wakurugenzi lukuki, kiasi kwambA unajiuliza President's Office ni Office au institution kubwa????

Kuhusu hapo nilipo-bold na kupaka rangi nyekundu, kuna Department of Transport, Department of Health and Human Services, Department of Treasury etc ... kwenye Federal level United States. Na States zina departments zake hizo hizo ukiondoa Homeland Security, Defence na Department of State (Foreign Affairs). Na States mbalimbali zinafanya international trade independent na Federal government, hata pia Inter-state trade zipo independent but regulated na Federal government. Hii ipo US na mimi ni mfanyakazi wa State government, so trust me.

Nikija kwenye maswali yako,
Zanzibar ilipoondoa Bandari, na hayo mambo mengine, gharama zitakuwa zimepungua (for at least 5%) ingawa mambo yaliyoondolewa ni source of income kwa nchi especially Bandari, Anga etc.. na administration yake haiwezi kuwa completely on Zanzibar kwa sababu Defense ya Anga, Traffic control na Radar bado zitakuwa managed na Muungano. Pia Maritime issues nyingi zitakuwa controlled na JMT bado. Tanganyika ikianzisha serikali yake itataka kuanzisha utaratibu wake wa anga na maji ambao lazima utaipa fungu fulani Tanganyika na fungu fulani Muungano na hii itahitaji usimamizi wa vyombo tofauti vyenye gharama tofauti. It's the administration that matters na hapo ndiyo cost inapoongezeka.

Swali la pili na la tatu yana uhusiano na la kwanza ila nitakujibu hivi kwa pamoja,

Mambo hayo 15 unayoyazungumzia, lazima yatakuwa na vyombo vyake vya kuyasimamia kwenye Jamhuri ya Muungano. Tume imejaribu ku- sugar-coat na kuipa madaraka tume itakayokuwa chini ya mawaziri wawili wanaoshughulikia Muungano. Yaani kama ilivyo kwa Waziri wa nchi VP's Office anayeshughulikia muungano. Hii haitakuwa rahisi hivi kwa sababu hizi zitakuwa States mbili tofauti zenye policies mbili tofauti kwenye kila jambo na policies hizo zitatungiwa legislations tofauti kwa kila serikali kuzitekeleza. Na legislations hizo zitatekelezwa na executive instruments tofauti ambazo itabidi ziwe regulated na harmonized na chombo superior cha muungano. Mambo yanayohusu Agriculrture, transportation, communications, licensing bureaus etc etc zote lazima ziwe harmonized na haziwi regulated na katume kadogo kama tunavyoaminishwa. That Union government will grow and grow and grow kutokana na mahitaji na lazima tuambiane hilo.
 
Kobello
Kwahiyo tumekubaliana kuwa kuondoa mambo 15 katika 22 kumepunguza gharama kwa Tanganyika na si kuongeza.
Sijui umeateje punguzo la 5% lakini tunakubaliana punguzo hilo ni ongezeko kwa Tanganyika. Hili tumekubaliana.

Kwa muundo ulisema wa Marekani, serikali kuu ni ndogo kwasababu mambo mengi yapo katika state level.
Hakuna state ambayo ina mambo yake tofauti na federal policy at least ingawa kuna legislation tofauti.
Hapa kwetu Zanzibar hawataki hilo, wanachotaka ni kuwa independent. Kwa mwendo huo mfano wa Marekani ni mfu.

Pili, kwasasa Maritime ni tofauti. Mfano, Zanzibar wana ZMO. Tanganyika wana SUMATRA kwa jina la JMT.
Znz wanasajili meli na shughuli nyingine na kubaki na mapato yao. Waliposajili meli za Iran, kiasi walichokusanya ni dollar 500,000. Gharama za JMT kule IMO zinalipwa na Tanganyika. Hivyo makusanyo ni znz malipo kwa Mtanganyika.
Hapo huoni kuna tatizo? Hivi ada ya JMT kule IMO ikiwa ni 100,000, kwa kiasi cha 500,000 walizokusanya znz kuna uhalali wa kutolipa hata 25,000? Kuna sababu gani unazoweza kutuambia zinahalilisha znz kutolipa na Tanganyika kulipa?

Kuhusu tume ya uratibu, hapa hujaitendea haki tume. Ukisoma rasimu tume hiyo haikuundwa kuweka mambo pamoja.
Imeundwa kuleta uwiano wa shughuli zinazokinzana. Elewa kuna mambo yatakayobidi yaoanishwe kwa faida ya washirika.
Hawaoanishi sera bali yale yanayohitajika kuleta uwiano. Znz wakisema ardhi si ya muungano, Tanganyika wasema hivyo.
Kunahitajika chombo kitakachohakikisha kama ni hivyo hakuna kualaumiana bali makubaliano.

Mfano, znz wakisema ardhi si muungano, tume itahakikisha kuwa sheria hizo zinatumika Tanganyika tofauti na ilivyo sasa. Kwasasa ardhi ni mali ya znz, ya Tanganyika ni ya wote kwasababu ni ya JMT. Tume iatkuwepo kuhakikisha kuwa hakuna misuse ya sheria au taratibu za upande mmoja.

Nimekuuliza kupunguzwa kwa mambo 15 kumeathiri vipi Tanganyika. Jibu lako hakuna. Sasa gharama zinazosemwa zitaongezeka ni zipi?

Hadi sasa mahakama zote hadi ya rufaa ni za Tanganyika na Zanzibar wanayakwao. Mahakama itakayokuwa ya pamoja ni mahakama kuu ambayo ipo hadi sasa ikihudumiwa na Tanganyika. Hivi utakapoitaka Zanzibar ichangie mahakama ku, utakuwa unaongeza au unapunguza gharama ?

Kuna bunge la JMT ambalo lina Wazanzibar 81. Kwa gharama za mbunge mmoja kuanzia uchaguzi ni za Mtanganyika.
Mshahara wa mbunge (10,000 ,000 kwa mujibu wa Zitto MB) kwa mwezi ni sawa na milioni 810. Hizo zinatoka Tanganyika peke yake.

Tutakapokuwa na bunge la shirikisho, Tanganyika itakuwa na wabunge 50 ambao gharama zao ni chache kuliko 81.
Zanzibar itahudumia wabunge wake kama ilivyo sasa BMK. Hapa gharama zinaongezeka au zinapungua kwa Tangayika?

Sasa hivi kuna wanafunzi 1,700 wa znz wanaopewa grant kutoka Tanganyika. Ukitumia hesabu rahisi za gharama ya milioni 5 kwa kila mmoja, maana yake ni kuwa Tanganyika inalipa Bilioni 85 za elimu ya juu ambalo si jambo la muungano. Unapoondoa hilo katika muungano, unapunguza au unaongeza gharama kwa Tanganyika?

Nimejaribu kukupa vitu vichache ili kukuonyesha kuwa kwa namna yoyote gharama za shirikisho zitakuwa offset na gharama ndogo ndogo zitakazo ondoka katika muungano wa sasa.
Hivyo hofu kwa Tanganyika haipo, labda utueleze hofu ipo eneo gani ?

Hoja yangu kubwa hapa ni kuwa hadi sasa Tanganyika inasimama yenyewe bila Zanzibar kwa kubeba gharama za ''shirikisho'' la sasa. Tutakapotenga Tanganyika na Zanzibar, tutapunguza mzigo kwa Tanganyika.

Mfano, kama kuendesha mahakama kuu kwa sasa Tanganyika inatumia Bilioni 100, tukiwa na shirikisho Zanzibar ikachangia Bilioni 10, gharama za Tanganyika ni Bilioni 90.
Wapi gharama zinaongezeka?

Ndio msingi wa swali langu ulilokubali kuwa hadi sasa Tanganyika ndiyo inalipia muungano huu, kukiwa na shirikisho ni kubadili jina na nafuu kwa Tanganyika. Nafuu ni kuwa znz haitajificha katika chaka la JMT, itakuwa wazi na mchango wake utatakiwa kuonekana.
 
Sheikh Ngruvi3 naona bado "hujanfahamu": mimi siungi mkono "udhalimu" wa Zenj dhidi ya Tanganyika.
Mimi ni muumini wa Muungano. Hofu yangu ni kwamba tukiwa na 3 basi muungano utakufa.
Ninaunga mkono 2 (zisizo na unyonyaji) kama "transitory process towards 1". Naamini baada ya miaka mingi ijayo ndoto hiyo itatimia...baada ya wale wenye "uchu wa madaraka" (kama waitwavyo) na wale "wenye uchungu sana na mapinduzi daima" kuwa wamepisha kizazi kingine ambacho kitajali zaidi maendeleo kwa wananchi kuliko historia.


Ila, kama plan B, ikiwa tumeshindwa kuafikiana kwa 2 au 3, tutafute namna ya kuachana kwa amani. Tujipe kama miaka 10 kama twataka Muungano na kwa muundo upi. Tutaachana kwa kura ya maoni kwa wananchi, na tujiulize baadaye kwa kura ya maoni kama twataka kuungana tena kwa mtindo upi. Katika kipindi hicho cha miaka 10 kila upande uendeshe mambo yake na baada ya miaka 10 iitishwe kura ya maoni.
 
Kobello,
Labda wewe mkuu wangu utawezana na hawa watu maana mimi nimejaribu sana kuwafahamisha lakini imekuwa vigumu sana na nadhani sababu ni kwamba hawajawahi kuona muundo wa serikali 3 zinapoundwa mamlaka gani huwa chini ya serikali hizi dhidi ya serikali kuu maana wanachukulia sana wepesi wa kupunguza matumizi.

Swala la Mikopo, hili hatuwezi kuliepuka hata kidogo ikiwa serikali yetu leo hii inakopa zaidi ya asilimia 40 kwa matumizi ya mambo ya ndani na asilimia 80 kwa ajili ya maendeleo. Iwe aibu ama sio aibu ukweli unabakia tunakopa fedha hizo na zinatakiwa zitumike ipaswavyo maana hatuwezi kusema kesho tutaacha tukiwa na serikali 3. Hata nchi za Asia kina Maleysia zilikopa mfuko wa Tiger kama mfanyabishara anavyoweza kopa benki kwa kuanzisha miradi yake. Tatizo ni sisi wenyewe kuwa na matamanio zaidi ya uwezo wetu. Tunakusudia kukusanya bil.3 tunapanga matumizi ya bil. 5 hizo za ziada zitoke wapi? na Je kweli viongozi wetu wapo tayari kutumia bil. 3 zinzzokusudiwa kukusanywa waache hayo wa VX, posho, misafara, kurusha Hellikopta kwa kodi za wananchi? sidhani sio hawa Wadanganyika niwajuao.

Hivyo kinachonikosha miye ni kwamba inaonyesha kama tukiwa na serikali 3 basi hiyo mikopo haitakuwepo ama inahusiana na serikali 2, wakati viongozi na mawazo yetu ni yale yale ya utumwa wa ukoloni mamboleo. Kama tumekopa kwa ajili ya maendeleo ni lazima fedha hizo zitumike vizuri na Zanzibar wao wameeleza sababu zao sisi bara tunapigana nao badala ya sisi kutunga sheria ambayo uadilifu na uwajibikaji uwezeshe matumizi bora ya mikopo hiyo hadi tufikie uwezo wa kujitegemea.

Kati ya nchi nyingi zilizokuwa ndani ya federation huwa wana katiba kama ya zanzibar sema katika yetu ya Taifa imelega na kuonekana kama ni katika ya Tanganyika, hivyo imepwaya kuwa katiba ya taifa hivyo binafsi yangu maadam ina serve Tanganyika kwa mambo yote nachukulia katiba hiyo ni ya Tanganyika. na ndio maana tunataka katiba ya taifa ambayo ina mamlaka juu ya hizi nchi 2 hasa katika mambo ya uzalishaji ili uchangiaji na ugawanaji uwe ni conditional. Maana hatukuwa na mfumo wa uchangiaji na ugawanaji tumefahamu wapi makosa yetu yalikuwa. Zanzibar kuwa na kiongozi wao sio kosa ila kosa ni kumwita kiongozi huyo rais lakini rasimu imependekeza marais watatu watu hawaoni kosa ila tukusema tunaweza kuwaita mawaziri wakuu. Well, ikifikia hivyo Zanzibar watabadilisha nao lakini at the time being walihitaji kiongozi wao na jina la rais lilikuwa rahisi kwao kama ilivyopendekezwa ktk rasimu hii.

Na hatuwezi kuwashutumu zanzibar ikiwa imebainika wazi kwamba hadi leo hii tulikuwa hatuna mfuko wa pamoja jambo ambalo limependekezwa sasa hivi. Zamani kila kitu kilimilikiwa na serikali hivyo mfuko ulikuwa wetu sote hatukutegemea kodi za wananchi serikali ilimiliki njia kuu za uchumi, hii inaonyesha wazi kwa nini Zanzibar baada ya mageuzi haya kutokea na hatukufanya marekebisho makubwa walihitaji katiba mpya maana wao wanapungukiwa mambo 22 ya kimamlaka ambayo yapo kwenye serikali ya JMT lakini yanatumiwa na Tanganyika peke yake. Hivyo kudai kuwa nayo wao haimaanishi hawataki tuwe pamoja isipokuwa hawana hivyo aidha wapewe ama wafaidike nayo ndani ya Muungano.

Sisi tumechagua kutenganishe wote tuwe na hayo mambo jambo ambalo litakuja leta msukosuko wakati zanzibar watakuwa na mamlaka ya kufanya mikataba nje ambayo kwetu bara itaonekana kama ni kuuza nchi na hapo ndipo tutakapo anza kuvutana mashati. Imetoke kwenye OIC lakini kama hili swala lingekuwa na manufaa kwa Tanzania yote na wakawa monitored na chombo cha Kitaifa sidhani kama bara tunngelipiga vita isipokuwa kusikia ni chombo cha kiislaam na wanaingia zanzibar fikra na woga wa Udini ukatuingia.

Mimi naamini kabisa kwamba sisi tumeingiwa sana na chuki ambayo imetokana na Udini, kwanza ile kuchomwa kwa makanisa Zanzibar, kuchomwa kwa misahafu, kuvamia misikiti na makanisa, kudhuru wachungaji na kadhalika inapeklekea kutoaminiana baina ya waislaam na waklristu jamboamablo limetokana na udhaifu kubwa wa utawala huu na tukiendelea kushinikiza serikali 2 au 3 wakati kuna mambo muhimu zaidi ya bkuyatazama tutafika mahala tutakula nyama kama mwaliimu alivyosema.

Mwisho, Mfuko wa pamoja hauhitaji idadi ya serikali kuongezeka ama kupungua. Tunaweza unda mfuko wa pamoja ktk seirklai 1 2 ama 3 isipokuwa tutazame nini haswa tulipotaka kuelekea ktk Muungano wetu ambao hauhusiani kabisa na wingi wa serikali bali UMOJA wetu na mshikamano. Sidhani kama serikali 3 ni suluhisho la kuunda mfuko wa pamoja ila ni kuleta matatizo mengine ambayo hayakuwepo.
 
Back
Top Bottom