Kobello,
Mkandara,
..mimi nadhani badala ya kuangalia Canada mngeangalia hapa nyumbani.
..serikali ya mapinduzi ya Zanzibar na wizara zake inaweza kutusaidia kujua nini kitakuwepo kwenye serikali ya Tanganyia ikiwa CCM wataridhia ianzishwe.
..sasa sina uhakika kama SMZ ina wizara zote ambazo zipo ktk serikali ya muungano, na zinabainishwa kwamba wizara zinazohusiana na masuala ya muungano.
..kwenye SMZ kuna wizara ya fedha, na suala hilo linaeleweka. lakini SMZ hawana wizara ya ulinzi, wizara ya mambo ya ndani, idara yake yenyewe ya uhamiaji, pamoja na wizara nyingine ambazo zimebainishwa kushughulikia masuala ya muungano.
..pamoja na maoni yangu hayo, mimi nawashauri mrudi kwenye rasimu muangalie ni mambo gani yamependekezwa yawe ya muungano, halafu mjiridhishe kama serikali za Tanganyika na Zanzibar zitalazimika kuwa na wizara zake zenyewe zinazoshughukia masuala yaliyopendekezwa kuwa ya muungano.
cc
Mchambuzi,
Nguruvi3
Mkuu wangu sidhani kama ni busara kuwasikiliza Zanzibar ikiwa tunaelewa muundo wa serikali 3 ndani ya SHIRIKISHO unaundwaje na inakuwa vipi na ndio chanzo cha mjadala huu maana tayari tunayo rasimu ilopendekeza. Kama kweli tutashirikiana katika mambo yale tu yaloorodheshwa na sii kinyume ina maana tunaunda JUMUIYA baada ya kuvunja muungano. Ni ushirikiano kama ilivyo Jumuiya ya EAC kila mtu ana chake, na tutashirikiana tu kwa yale ambayo yamekubaliwa.
Sasa ya nini yote haya ikiwa tunayo EAC halafu tunaunda tena Jumuiya ya Tanganyika na Zanzibar? maana haiwezekani tukawa na shirikisho tukakutana kwenye mambo hayo, Tanganyika na Zanzibar zikalazimika kutokuwa na waziri wa fedha kwa sababu atakuwepo wa serikali kuu ya Muungano, Hizo bajeti za nchi zao zitawakilishwa vipi? na je sio ndio kurudisha makosa yale yale tulokuwa nayo ila tumeyapa jiko moja zaidi?. Na zaidi ya yote, hata hiyo Jumuiya ya EAC, Kenya wana vyombo vyao vya kukusanya ushuru, sisi tuna yetu, Uganda vile vile tunachokubaliana ni sheria moja itumike kutunufaisha sote. Haiwezekani kabisa kesho tukawa na shirika moja la ndege la EAC ndipo tutaanza kuumizana vichwa tena.
Na muda wote nimekuwa nikiwaeleza ya kwamba maadam tumegundua kuwa mambo yote ya Muungano hayakuwa ya Muungano ila ya Tanganyika, hii inadhihirisha kwamba mfumo wetu ndio ulokuwa na kasoro, sio serikali ngapi kwani dhamana walopewa serikali ya Muungano kwa nchi hizi mbili waliitumia kwa maslahi ya Tanganyika tu. na hawakuwaruhusu wao waunde wizara hizo ndani isipokuwa za serikali ya Muungano ambayo haikuwahudumia. Sielewi kama ilikuwa kosa la kimfumo ama viongozi wetu na Ubinafsi wao waliamua kufanya hivyo baada ya kubadilisha mfumo wa kiuchumi na kisiasa. Kwa hiyo ndio maana mimi toka mwanzo niliyaelewa malalamiko ya Wazanzibar, na kukubali kuwa dhamana ilopewa serirali kuu, sisi Bara tuliitumia vibaya kujinufaisha.
Hii inanipa wasiwasi sana na muundo huu ulopendekezwa na utakuwa wa kipekee vile vile, na ndio maana nimekuwa nikiwasikiliza
Mchambuzi na
Nguruvi3 ambao wao wamependekeza tuvunje huu muungano tugawane mbao na kuunda Jumuiya kama itahitajika kutokana na chuki ilotokea baina yetu (yale alotuasa mwalimu). Na ukweli ni kwamba kilichotakiwa ni kuhakikisha yale mambo 22 yalokuwepo yatunufaishe sote kama taifa moja na kama chaguo ni serikali 3 tukubali pia kuna gharama zake badala ya kuudanganya Umma.
Hivi kweli kuna watu walifikiri kina Mwalimu walikuwa wajinga kiasi gani kusema serikali 3 zina gharama kubwa na itakuwa mzigo kwa Tanganyika? Hivi kweli hao wanasiasa wetu na hasa UKAWA wanaweza kutuambia maneno yale yalikuwa na maana gani? Kwa nini kina Nyerere walisema serikali 3 itakuwa mzigo kwa Tanganyika, wao walielewa vipi? na nanyi nyote mnaopendekeza serikali 3 mlielewa vipi kuhusu muundo wa serikali 3 zilizokataliwa na waasisi wetu wa Muungano - Ukweli ni kwamba Waasisi walitazama mzigo huo utakuwa wa wananchi, lakini wanasiasa wa leo wanatazamia sana mapato ya gas na mafuta!
Jingine, ukiisoma rasimu vizuri utakuta wametumia sana neno NCHI moja ya Tanzania, hii inazua mkanganyiko mwingine juu ya NCHI hii kwa sababu mara nyingi nchi huwa haina Soveregnity, ni state ndani ya Taifa -Sasa kama Tanzania ni nchi sio Taifa, yenye sovereign ni nini?