Kobello
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 9,223
- 8,907
Inaelekea bado kidogo kwenye mambo ya serikali.Hivi Kobello, ukimwita waziri mkuu Rais wa Tanganyika utakuwa umeongeza gharama gani? Ukiita wizara ya kilimo, afya, ujenzi n.k. wizara za Tanganyika utakuwa umeongeza gharama gani?
Judicial system itakayoongezeka ni ipi na kwa sasa iinahudumiwaje? Hapa lazima ueleze unafuu uliopo ukilinganisha na unaotarajiwa.
Administrative cost za idara mpya ni zili? Kwasasa tuna mambo 22 ambayo kiidara ni 47.
Hivi ukiwa na mambo 7 utakuwa na idara nyingi au pungufu?
Na idara za sasa zinahudumiwaje ili kusema gharama zake ni nafuu?
Kama S1 haiwezekani, S2 zinawezakanje kukiwa na dhana ya Tanganyika kuvaa koti?
Waziri mkuu wa Tanganyika ni jina tu la cheo na aina ya mamlaka. Hii haimaanishi kuwa "Execution of legislations" itakuwa eliminated. Kwa mfumo wa sasa hivi, waziri mkuu ni sehemu ya Executive branch.
Waziri mkuu Mizengo Pinda gharama zake zipo chini ya rais. Madaraka yake na kazi zake anapangiwa na Rais. Ni mtumishi mmoja tu ambaye amepewa baadhi ya wafanyakazi wa "Executive Branch wawe chini yake". Ukimuondoa Rais, haimaanishi kuwa hakutakuwa na kiongozi wa juu atakayekuwa na watumishi wanaosimamia "Executive Branch" ya Tanganyika, be it The Prime Minister or The President.
The same goes to the Judicial System. Tanganyika will have her own judicial system and the union will have her own courts too. Kutakuwa na mahakama kubwa ya muungano kwa kila mahakama ndogo. mahakama ya juu itakuwapo ya muungano na ya Tanganyika(Kama ambavyo Zanzibar ina zake) na mahakama, ili kupunguza mzigo na kuongeza ufanisi sitashangaa kama kutakuwa na Kanda kwa mahakama za Muungano. Rais wa muungano lazima atakuwa na Majaji wake kwenye masuala mbalimbali. natabiri mkaraganyo mkubwa kwenye mahakama za Biashara, katiba, na mabo ya maritime.
Tanganyika lazima itakuwa na SUMATRA/TRA/ na other regulatory bodies zake independent of the Union government.
Mkuu usipende kuweka sana siasa na kufuata maneno ya wanasiasa, gharama za uendeshaji ni lazima zitaongezeka, panga pangua. hata rasimu inalikubali hilo.
Kupunguza mawaziri ni dhana ya kitoto sana kwa sababu mambo yanayohitaji mkono wa serikali yatabaki palepale. Mambo ya kilimo, Elimu, CommWorks etc... lazima pia yatakuwa na idara zake Tanganyika na Muungano.
Uliahidi kuleta uzi humu lakini nadhani umesahau. tujaribu kujenga serikali bandia, uone jinsi gharama zitakavyoongezeka. Kelele tu hazitasaidia lolote.