Serikali 3 na gharama zake

Serikali 3 na gharama zake

Muungano haulazimishwi sio utumwa.....wananchi waulizwe kama wanautaka au la...na kwa muundo gani.
Kwangu mie tuwe na mashirikiano ya karibu katika masuala ya usalama na uchumi bila ya kuwa na serikali ya kuyaratibu.
 
Tuna mashirikiano ya karibu ya kidugu na kiuchumi na nchi tulizopakana nazo bila ya kuwa na muungano wa kiserikali wowote. Aidha, shirikisho la afrika mashariki pia ni aina mojawapo ya ushirikiano ktk mambo mbalimbali kwa ufasaha na utaratibu unaoeleweka. Tunaweza kuwa na uhusiano wa namna hio baina ya zanzibar na tanganyika na sio muungano huu wa mazingaombwe kimuundo na kukosa uwajibikaji kwa watawala.

Kama muungano ni vyema baina yetu basi tuwe na serikali moja.
 
Mimi ningependekeza kama tuwe na serikali ya tanganyika, ya znz chini ya mawazir wakuu. Na katika masuala ya muungano huyo wazir mkuu awe rais na mwenzie wa znz awe makamu, na hivo hivo kwa wizara za muungano
 
Ofcourse gharama itaongezeka ila haitaongezeka kama watu wanavyosema sababu mambo ya muungano sio mengi na sio kwamba sasa hivi hayafanyiki.

Pili tukitenga tutajua ni pesa ipi inakwenda wapi na inafanya nini (kuongeza accountability) na sio necessarily kwamba kodi zitaongezeka sababu kuna option ya kupunguza matumizi yasiyo ya lazima AKA kufuja pesa hence kufunga mikanda kwa hawa wasaka utawala na kama pesa itakuwa ndogo basi hiyo misafara, posho, mishahara n.k. ndio itabidi ipungue kwa hao viongozi, ambao nadhani hawalazimishwi wakiona Siasa hailipi tena basi warudi kufanya shughuli nyingine

Cha kujiuliza ni kwamba faida ya Serikali Tatu ni kubwa au ndogo kulinganisha na faida inayopatikana in so called kuepuka gharama wakati hilo punguzo linaishia kwenye matumbo ya watu wanaojificha kwenye hii confusion ya sasa ?
Mkuu shukuran at least wewe umekuja kujadili kuliko BAK yeye anatanguliza Profesa Lipumba kuwa ndiye suluhisho kana kwamba aloyasema ndio rasimu ya wananchi ama huyu ndiye mwenye majibu ya serikali ya 3 tukamuulize yeye. Mimi najua fika kwamba hadi sasa matumizi ya kugharamia serikali ya Muungano yanafanywa kwa asilimia kubwa na Tanganyika pengine zaidi ya asilimia 99. Na vyanzo vyake ni vile ambavyo vimo ktk mambo ya muungano na inafahamika sasa hivi kuwa JMT ni Tanganyika yenyewe hilo halina shida, hivyo mimi nimeyaweka matumizi ya JMT ya sasa hivi iwe kama Tanganyika lakini ile ya Muungano mpya wa serikali ya 3 itakayo undwa haitakuwa na vyanzo tofauti na serikali iliyopo. Hivyo kuna tofauti kubwa sana kusema leo hii gharama hizo zinatumikia serikali ya muungano ambayo ni Tanganyika, ila tutakapo unda hii ya 3 itategemea sana serikali za Tanganyika na Zanzibar kuchangia mfuko wa kuendesha serikali hiyo na hapo ndipo maswali yanapokuja.

Je serikali hizi zitatoa wapi fedha za kuchangia mfuko huu ikiwa vyanzo vyote hivyo sio ktk mambo ya Muungano? Na itatofautisha kipi kati ya leo na kesho ikiwa toka Muungano wetu yenye vyanzo hivyo vilikuwa vikichangia karibu robo tatu ya matumizi ya serikali (recurrent expenditure) leo hii imeshuka kiasi kwamba asilimia karibu 40% ni misaada kutoka nchi za nje kwa mambo haya haya ya matumizi ya ndani acha mbali Maendeleo. Ukiyasoma malalamiko ya Watanganyika ni pamoja na mchango wao mkubwa ktk serikali ya muungano japo mambo yote ya Muungano ni yao sasa iweje rahisi kuchangia serikali ambayo wao hawaihitaji kutokana na uwezo mdogo wa vyanzo vyao kukidhi mahitaji ya serikali yao!. sijui kama umenielewa?

Sasa Kesho itakapo changia Zaidi kwa asilimia 97.7 kutokana na population yetu dhidi ya Zanzibar (45mil vs 1.3 mil) tutakuwa tumeepuka Kipi? Laa sivyo hiyo serikali ndogo ya muungano itakuwa na udogo gani kiasi kwamba iwe na mamlaka juu ya kugharamiwa kuendeshwa wakati huo huo isitugharimu sana kama wanavyosema ilihali mabunge pekee ya bara na Muungano tunazungumzia wabunge wa majimbo yote ya Tanzania bara na wale wa serikali ya Tanganyika kufikia at least 600, na kama sivyo ndio maana nauliza kutakuwa na wabunge wangapi na kutoka sehemu gani kuunda bunge hili la muungano, Jeshi la Polisi lazima liwepo la askari wa serikali ya Tanganyika na lile lenye mamlaka ya Kitaifa yaani kuweza kutumikia Muungano na sehemu nyinginezo maana kila wizara ina idara zake na taasisi zake zote zijumlishwe humo. Udogo huu wa kugharamia haya ni upi?

Sasa iweje serikali ambazo hazijitoshelezi leo kwa kuomba misaada ziweze kuihudumia serikali ya muungano ambayo haina mamlaka yoyote ktk vyanzo vya mapato ya serikali hizi isipokuwa wanategemea ushuru wa bidhaa zisizo za kodi jambo ambalo litaweza kuwepo ktk shirikisho la EAC? Lakini leo hii wategemee mchango wan chi ambazo zinategemea misaada kujiendesha zenyewe kutoa fungu lao ili kuchangia mfuko wa pamoja? Does it make sense kweli?

Mimi nachoomba ni darasa tu siko hapa kubishana isipokuwa kufahamishwa yale yalonikinza kichwani.
 
Labda ktk kuweka usemi wangu sawa niseme tu mapendekezo yangu kuwa kuwepo kwa serikali 3 lakini katika Muungano sio shirikisho, hilo moja na pili serikali kuu iwe na mamlaka kamili juu ya vyanzo vyote vya mapato, isipokuwa shughuli za utekelezaji wa kukusanya mapato hayo yatapewa mamlaka ya nchi na kila nchi itachangia mfuko huu moja kwa moja tokana na kodi zote kwa asilimia itakayowekwa.
 
Sasa iweje serikali ambazo hazijitoshelezi leo kwa kuomba misaada ziweze kuihudumia serikali ya muungano ambayo haina mamlaka yoyote ktk vyanzo vya mapato ya serikali hizi isipokuwa wanategemea ushuru wa bidhaa zisizo za kodi jambo ambalo litaweza kuwepo ktk shirikisho la EAC? Lakini leo hii wategemee mchango wan chi ambazo zinategemea misaada kujiendesha zenyewe kutoa fungu lao ili kuchangia mfuko wa pamoja? Does it make sense kweli?

Mimi nachoomba ni darasa tu siko hapa kubishana isipokuwa kufahamishwa yale yalonikinza kichwani.

Naona hapo juu umesema kwamba wabunge 600 jumla namba ambayo sidhani kama ni lazima iwe hio, inaweza ikawa pungufu (ukizingatia bado kutakuwa na Katiba ya Tanganyika ambayo huenda ikatuondolea mizigo minginge ya kufuja pesa kama wakuu wa wilaya) anyway according to Rasimu wabunge wa Jamuhuri watakuwa kama 60 ambao am sure kutokana na vitu vya muungano sio vingi na pesa itakuwa sio nyingi ya muungano hata vikao vyao havitakuwa vya muda mrefu na kuhusu Uongozi as far as I know just imagine sasa hivi huyu JK ndio angekuwa raisi wa Muungano (minus safari zake za kila siku sababu washirika wasingekubali asafiri hivi kwa kutumia pesa zao) Pinda angekuwa kiongozi wa Bara na Zanzibar wangekuwa na kiongozi wao (tuondokane na haya mambo ya Makamu wa Raisi na upuuzi kama huo).

Alafu unasahau hapa issue sio kwa upande wa Bara tu hata Zanzibar ambao kwa sasa wanaona Bara inawanyonya tukiwaridhisha kwa yote wanayoyataka ni dhahiri kwamba Bara watu wataanza kunungunika.., Kwahio kama kweli tunataka kuepuka gharama basi tufanye serikali moja..., kama haiwezekani basi ni tatu na kama hio ya Muungano itakosa pesa ya watu kujinafasi am sure kuna wazalendo ambao watakuwa tayari kuwa kiongozi wa hii serikali kama symbolic tu hata kama kutakuwa hakuna marupu rupu ya kutosha. Na kama Serikali 3 itakuwa ni njia ya Muungano kuvunjika hapo baadae and so be it....
 
kama serikali ya Tanganyika ipo ni kwanini wazanzibar wanaajiriwa Tanganyika na hakuna mtanganyika anayeajiriwa serikali ya zanzibar? hatutaki mambo ya kivuli sijui mwamvuli, tunataka the government of Tanganyika. Rasimu ya warioba imeelezea kabisa idadi ya wabunge wa muungano na namna watavyopatikana.

Gineous
 
kama serikali ya Tanganyika ipo ni kwanini wazanzibar wanaajiriwa Tanganyika na hakuna mtanganyika anayeajiriwa serikali ya zanzibar? hatutaki mambo ya kivuli sijui mwamvuli, tunataka the government of Tanganyika. Rasimu ya warioba imeelezea kabisa idadi ya wabunge wa muungano na namna watavyopatikana.

Unafikiri ajira ziko Serikalini tu?

Hakuna Mtanzania bara anaetaka aajiriwe na Serikali ya Zanzibar, mishahara Serikalini Zanzibar ni midogo sana kulinganisha na Serikali ya Muungano.

Watanzania bara wengi sana wameajiriwa katika sekta binafsi Zanzibar na wengi wao wapo kwenye mahoteli na makampuni yanayoshughulikia utalii.
 
government ya tanganyika ipo mzee soma iyo makala vizuri, kitakachobadilika ni jina tu, kimbembe hiyo ya muungano na gharama zake
 
Mhhh... Nadhani BAK unakwepa wajibu.
Kwenye mjadala kila mtu ana wajibu wa kuweka ushahidi wake hadharani na kuhakikisha unaeleweka na mnaye jadiliana naye! Yawezekana kabisa Mkandara kamsikia Lipumba; lakini kamwelewa alivyomwelewa,na hajaona uzito wa hoja za huyo Lipumba. Inaonekana unazielewa vyema zaidi na unadhani MKandara angezielewa (kama wewe ulivyozielewa) angekubaliana na wewe... Kiusomi kabisa; ni wajibu wako kumwelewesha Mkandara ulivyoelewa + kwa nini hoja hizo zinakuelea zaidi!
Mpe shule MKandara aelewe; achan na haya ya "sina muda" - unao ila aidha hutaki au hata wewe hukumwelewa vizuri Lipumba, au hujui kabisa na ulisikia tu mtu akitumia hiyo kama hoja!

cheers
 
Last edited by a moderator:
Naona hapo juu umesema kwamba wabunge 600 jumla namba ambayo sidhani kama ni lazima iwe hio, inaweza ikawa pungufu (ukizingatia bado kutakuwa na Katiba ya Tanganyika ambayo huenda ikatuondolea mizigo minginge ya kufuja pesa kama wakuu wa wilaya) anyway according to Rasimu wabunge wa Jamuhuri watakuwa kama 60 ambao am sure kutokana na vitu vya muungano sio vingi na pesa itakuwa sio nyingi ya muungano hata vikao vyao havitakuwa vya muda mrefu na kuhusu Uongozi as far as I know just imagine sasa hivi huyu JK ndio angekuwa raisi wa Muungano (minus safari zake za kila siku sababu washirika wasingekubali asafiri hivi kwa kutumia pesa zao) Pinda angekuwa kiongozi wa Bara na Zanzibar wangekuwa na kiongozi wao (tuondokane na haya mambo ya Makamu wa Raisi na upuuzi kama huo).

Alafu unasahau hapa issue sio kwa upande wa Bara tu hata Zanzibar ambao kwa sasa wanaona Bara inawanyonya tukiwaridhisha kwa yote wanayoyataka ni dhahiri kwamba Bara watu wataanza kunungunika.., Kwahio kama kweli tunataka kuepuka gharama basi tufanye serikali moja..., kama haiwezekani basi ni tatu na kama hio ya Muungano itakosa pesa ya watu kujinafasi am sure kuna wazalendo ambao watakuwa tayari kuwa kiongozi wa hii serikali kama symbolic tu hata kama kutakuwa hakuna marupu rupu ya kutosha. Na kama Serikali 3 itakuwa ni njia ya Muungano kuvunjika hapo baadae and so be it....
Sawa mathlan kutakuwa na wabunge 60, hawa wabunge watachaguliwa kwa vigezo gani na kazi yao haswa ni ipi? Je, ni kuwakilisha wananchi ama kuiwakilisha serikali ya Jamhuri maana ukiwa na wabunge sawa na wizara na idara za seriiali hiyo ina maana tutapoteza maana ya uchaguzi wa wabunge ambao huwakilsha wananchi na sio serikali. Na kama ni maana ya wananchi swali langu ni Je wabunge 60 wanatosha kutunga sheria za serikali ya muungano na sheria hizo zikakubaliwa nchi zote za Muungano? watasimamia vipi bajeti ya mambo ya maendeleo ya nchi zetu ikiw ani pamoja na mikataba! mtanisamehe kwa maswali haya maana najaribu kutazama mbele kuelewa tunachokifanya.

Pili, Hata hiyo serikali ya Tanganyika haiwezi kuepuka wakuu wa wilaya bali tutawajenga upya maana rais ni lazima awe na wawakilishi wake, sasa hao mikoani na wilayani hawa wataitwa kina nani? maana haiwezekani serikali kuu iwe makao makuu tu pasipo uwakilishi wake mikoani kazi ataifanya vipi? au ndio ule u - ceremonial role ambao Wapambanaji makamanda watamkataa mapema kabisa kuwa na mtawala wa kifalme. think about it unamtaka kweli rais mfalme?..Je Hao mawaziri wake wataweza vipi kuitembelea mikoa ikiwa hakuna mawasilino nayo? yaani kusema kweli bado kabisa sijaelewa huu muundo utakuwaje na utatusaidia vipi kuuboresha maisha ya wananchi na Muungano.

Mwisho, Labda ifikie mahala UKAWA wakubali kupoteza moja nalo ni SHIRIKISHO na CCM wakubali kupoteza moja nalo ni serikali 2 ili tuwe na MUUNGANO wenye SERIKALI 3 na tusiogope matumizi makubwa ya serikali hizi kwa sababu ndivyo itakavyo kuwa na hatuwezi kuepuka matumizi kwa kupunguza uwakilishi wa wananchi isipokuwa kwa sheria kali na miiko ya uongozi itakayo wabana wao kuongoza na sii kutawala. Lengo la hoja yangu ni kuwaeleza wananchi kwamba hatuwezi kuepuka gharama tukaipata katiba Bora -Haiwezekani, ila tutapata bora katiba toka rasimu hii sehemu hizi mbili tunazoshindana kulingana na maelezo nilokwisha yaona.

Ama kuna njia niloisema miye ambalo ni karibu sana na kuwa na serikali moja isipokuwa tunagawana majukumu ya shughuli za serikali na ukusanyaji wa mapato ambao kila nchi inachukua asilimia yake na kupeleka asilimia ilobakia serikali kuu.
 
Mkandara umesema sahihi mwanzoni - kisichokuwapo ni serikali ya muungano. Yaani mawaziri wote na Rais wao wanafanya mambo ya bara pamoja na kusemwa kuwa ni wa muungano. Kwa mfano Chikawe - Waziri wa Mambo ya Ndani - ni waziri wa muungano - lkn kila mara anashughulika na mambo ya bara tu! Sawa kabisa nami nakubali. Sasa huoni kuwa wanaopendekeza serekali tatu wanataka ufanisi zaidi kwa mambo ya muungano? Ili Chikawe akiwa waziri wa muungano asijisahau na kufanya ya bara tu huku kavaa kofia ya muungano.

Kuhusu gharama. Nilimsikiliza vizuri Awadh Said mjumbe wa iliyokuwa Tume ya Warioba. Anasema walichopendekeza ni kumweka Chikawe wazi - Waziri katika serikali ya muungano anayeshughulikia mambo ya ndani. Anahama toka serikali ya sasa hivi - ya bara na muungano- kwenda kwenye serikali ya muungano pekee. Kumbuka bara hawatakuwa na wizara ya mambo ya ndani. Gharama gani zinaongezeka hapo?
 
Sawa mathlan kutakuwa na wabunge 60, hawa wabunge watachaguliwa kwa vigezo gani na kazi yao haswa ni ipi? Je, ni kuwakilisha wananchi ama kuiwakilisha serikali ya Jamhuri maana ukiwa na wabunge sawa na wizara na idara za seriiali hiyo ina maana tutapoteza maana ya uchaguzi wa wabunge ambao huwakilsha wananchi na sio serikali. Na kama ni maana ya wananchi swali langu ni Je wabunge 60 wanatosha kutunga sheria za serikali ya muungano na sheria hizo zikakubaliwa nchi zote za Muungano? watasimamia vipi bajeti ya mambo ya maendeleo ya nchi zetu ikiw ani pamoja na mikataba! mtanisamehe kwa maswali haya maana najaribu kutazama mbele kuelewa tunachokifanya.
Hao wabunge 60 ni according na TUME ila binafsi hata mimi naona hawa ni wengi sana ukizingatia mambo ya Muungano yapo 7 binafsi ningependa hii irekebishwe hii namba ipungue zaidi au watu wapewe kofia mbili yaani katika hao hao wabunge wa Zanzibar na Bara baadhi yao (lets say 7) wawe wanakaa kwenye vikao vya Muungano ambavyo navyo viwe vichache sioni faida ya kuwa na kila mwakilishi wa Muungano katika kila jimbo
 
Mkandara umesema sahihi mwanzoni - kisichokuwapo ni serikali ya muungano. Yaani mawaziri wote na Rais wao wanafanya mambo ya bara pamoja na kusemwa kuwa ni wa muungano. Kwa mfano Chikawe - Waziri wa Mambo ya Ndani - ni waziri wa muungano - lkn kila mara anashughulika na mambo ya bara tu! Sawa kabisa nami nakubali. Sasa huoni kuwa wanaopendekeza serekali tatu wanataka ufanisi zaidi kwa mambo ya muungano? Ili Chikawe akiwa waziri wa muungano asijisahau na kufanya ya bara tu huku kavaa kofia ya muungano.

Kuhusu gharama. Nilimsikiliza vizuri Awadh Said mjumbe wa iliyokuwa Tume ya Warioba. Anasema walichopendekeza ni kumweka Chikawe wazi - Waziri katika serikali ya muungano anayeshughulikia mambo ya ndani. Anahama toka serikali ya sasa hivi - ya bara na muungano- kwenda kwenye serikali ya muungano pekee. Kumbuka bara hawatakuwa na wizara ya mambo ya ndani. Gharama gani zinaongezeka hapo?
Mkuu hapa ndipo watu wengi hawaelewi ama wanachanganya madawa na hivyo kuleta mkanganyiko. Sababu kubwa ya kuitaka serikali ya 3 ni kuwezesha seriiali hizo zijue malaka yake na mipaka yake na sii kugawana mambo. Leo Hii Chikawa ni waziri wa mambo ya ndani ya serikali ya Jamhuri (mambo yaliyopo ktk Muungano) lakini amekuwa akiitumikia bara kutokana na madai kwamba tuna serikali 2 ndiyzo zilizosababisha. Sasa ili kusahihisha makosa kama haya ndipo swala la serikali 3 limejitokeza ili Tanganyika iwe na mkuu wake na Zanzibar iwe na mkuu wake chini ya serikali kuu inayoongozwa na Chikawa.

Hivyo ni lazima Tanganyika nayo iwe na wizara yake ya mambo ya ndani ambayo kisheria haitakiuka sheria mama yaani katiba ya Muungano. Kifupi Chikawa atakuwa kama kiongozi wa hata FBI kwa nchi ya Marekani yaani kwa mambo yaliyo juu ya sheria za nchi husika japo kila nchi ina mku wake na hutekeleza majukumu yake kulingana na sheria za hapo, tena badi kila Mji una polisi yake na mamlaa yake polisi wa Mwanza haweza kuwa na mamlaka Kilimanjaro unless amehamishiwa huko ila Polisi wa taifa anaweza kufanya kazi yake mahala popote na wakati wowote wanaingia sehemu yoyote within mipaka yetu..

Hivyo, maelezo ya Awadh Said ni ya kupotosha zaidi kwa sababu huwezi kuonyesha Chikawa awe wa Muungano ambavyo ndivyo tulivyo ukaiacha Tanganyika haina mambo ya ndani ni yale yale ya serikali 2, ni sawa na tummetoa mfuko mmoja wa suruali na kumweka mfuko mwingine na kuuacha mfuko ule wazi hauna kitu. Kuna tofauti kubwa kati ya kugawna malamaka na kugawana mambo mana unaweza kuwa na mambo yote lakini mamlaka yake yakashuka hadi serikali za mitaa haina maana tumegawana mambo ya Utanganyika au Uzanzibar, ila shughuli zetu ndizo zinaweza kuwa ktk makundi ya mipaka na maeneo.

Kifupi tu ni kwamba muundo huu wa serikali 3 uloainishwa na rasimu hauwezi kutekelezeka ipaswavyo kwa sababu tumegawa mamlaka hayo kwa nchi ndogo na tukaiacha serikali kubwa bila meno maana hata ukichukuliasheria mama ya kuwaendeleza na kuwanufaisha wakulima/ wavuvi na wafugaji wakati haya sii mambo ya muungano, serikali kuu itaweza vipi kusimamia shughuli zao iwe hata kutoa mafao (subsidies) kwa walengwa ilihali sii kazi yao?. Zaidi ya hapo hili swala la kuunda sera ya Kitaifa kama lengo kuu ni kuwanufaisha kundi la watu ili kuwainua ni swala la vyama vya siasa kiitikadi. Chama ndicho kinaweza kuweka malengo hayo kama dira yao pindi wakishika uongozi na vyama vingine vikawapa kipaumbele Wawekezaji na Wajasiriamali ama hata Matajiri maadam malengo hayo wananchi wengi watayachagua.

Mimi sii mwanasiasa lakini kwa jinsi navyoliona swala hili linavyokwenda na ujadiliwa naona kama tunazidi kupotoshwa zaidi. Serikali kuu yenye mambo 7 haiwezi kabisa kuwa na nguvu juu ya serikali ndogo wala kuendesha Jeshi letu lenye matumizi makubwa kuliko wizara zote ukizingatia siasa za leo na mahitaji yake.
 
Mkuu hapa ndipo watu wengi hawaelewi ama wanachanganya madawa na hivyo kuleta mkanganyiko. Sababu kubwa ya kuitaka serikali ya 3 ni kuwezesha seriiali hizo zijue malaka yake na mipaka yake na sii kugawana mambo. Leo Hii Chikawa ni waziri wa mambo ya ndani ya serikali ya Jamhuri (mambo yaliyopo ktk Muungano) lakini amekuwa akiitumikia bara kutokana na madai kwamba tuna serikali 2 ndiyzo zilizosababisha. Sasa ili kusahihisha makosa kama haya ndipo swala la serikali 3 limejitokeza ili Tanganyika iwe na mkuu wake na Zanzibar iwe na mkuu wake chini ya serikali kuu inayoongozwa na Chikawa.

Hivyo ni lazima Tanganyika nayo iwe na wizara yake ya mambo ya ndani ambayo kisheria haitakiuka sheria mama yaani katiba ya Muungano. Kifupi Chikawa atakuwa kama kiongozi wa FBI kwa nchi ya Marekani yaani kwa mambo yaliyo juu ya sheria za nchi husika japo kila nchi ina mku wake na hutekeleza majukumu yake kulingana na sheria za hapo, tena badi kila Mji una polisi yake na mamlaa yake polisi wa Mwanza haweza kuwa na mamlaka Kilimanjaro unless amehamishiwa huko ila Polisi wa taifa anaweza kufanya kazi yake mahala popote na wakati wowote wanaingia sehemu yoyote within mipaka yetu..

Hivyo, maelezo ya Awadh Said ni ya kupotosha zaidi kwa sababu huwezi kuonyesha Chikawa awe wa Muungano ambavyo ndivyo tulivyo ukaiacha Tanganyika haina mambo ya ndani ni yale yale ya serikali 2, ni sawa na tummetoa mfuko mmoja wa suruali na kumweka mfuko mwingine na kuuacha mfuko ule wazi hauna kitu. Kuna tofauti kubwa kati ya kugawna malamaka na kugawana mambo mana unaweza kuwa na mambo yote lakini mamlaka yake yakashuka hadi serikali za mitaa haina maana tumegawana mambo ya Utanganyika au Uzanzibar, ila shughuli zetu ndizo zinaweza kuwa ktk makundi ya mipaka na maeneo.

Kifupi tu ni kwamba muundo huu wa serikali 3 uloainishwa na rasimu hauwezi kutekelezeka ipaswavyo kwa sababu tumegawa mamlaka hayo kwa nchi ndogo na tukaiacha serikali kubwa bila meno maana hata ukichukuliasheria mama ya kuwaendeleza na kuwanufaisha wakulima/ wavuvi na wafugaji wakati haya sii mambo ya muungano, serikali kuu itaweza vipi kusimamia shughuli zao iwe hata kutoa mafao (subsidies) kwa walengwa ilihali sii kazi yao?. Zaidi ya hapo hili swala la kuunda sera ya Kitaifa kama lengo kuu ni kuwanufaisha kundi la watu ili kuwainua ni swala la vyama vya siasa kiitikadi. Chama ndicho kinaweza kuweka malengo hayo kama dira yao pindi wakishika uongozi na vyama vingine vikawapa kipaumbele Wawekezaji na Wajasiriamali ama hata Matajiri maadam malengo hayo wananchi wengi watayachagua.

Mimi sii mwanasiasa lakini kwa jinsi navyoliona swala hili linavyokwenda na ujadiliwa naona kama tunazidi kupotoshwa zaidi. Serikali kuu yenye mambo 7 haiwezi kabisa kuwa na nguvu juu ya serikali ndogo wala kuendesha Jeshi letu lenye matumizi makubwa kuliko wizara zote ukizingatia siasa za leo na mahitaji yake.
Kwani tunauunganisha kila kitu? Nijuavyo mimi tunaunganisha baadhi tu ya mambo na ndivyo walivyokubaliana waasisi. Hatuunganishi kilimo na ufugaji, hatuunganishi tawala za mikoa na serikali za mitaa, hatuunganishi rasilimali nk. Tunaunganisha ulinzi na usalama, tunaunganisha mambo ya nje. Yale mambo ambayo huunganishi yatashughulikiwa na serikali washirika. Yale tunayounganisha yatashughulikiwa na serikali ya muungano. Ugumu unatoka wapi? Kwanini unanga'ng'ania serikali ya Tanganyika iwe na Wizara za muungano pia? Kwa nini leo hii Zanzibar haina Membe wao? Mimi nadhani tunachamba mno na matokeo yake ndiyo haya.
 
Mkandara,niemeufuatilia mjadala na namna unavyojibu hoja za jamaa wanaochangia uzi wako. Nime-notice kitu kimoja kutoka kwako ambacho ni hofu.

Una hofu kubwa kwa sababu kilichopendekezwa ni kipya. Na hofu uliyonayo ndiyo ambayo wajumbe wengi wa BMLK waliobaki Dodoma leo na baadhi ya watu wanaoipinga rasimu ya Tume ya Jaji Warioba inayopendekeza muungano wa muundo wa serikali 3.

Tofauti yake ni kwamba,wewe hofu yako at least inakuja na suluhu pasipo kubomoa msingi mkuu wa rasimu, kwamba serikali zilizopo sasa ni 2 ambazo ni (anganyika (au sema Tanzania Bara) chini ya Rais J.Kikwete na ile ya Zanzibar chini Daktari Shein. Kwa mujibu wa maoni yako inayokosekana hapa ni serikali ya Muungano. Na sasa unajiuliza hii serikali Muungano itakayokuja itakuwaje na chanzo cha mapato ya kuindesha yatatoka wapi!!??....

Na kwa maoni yako Rasimu ya Warioba haijaliweka sawa hili na kama imeweka ni kwa kiwango kidogo sana ambapo itaiweka serikali ya Muungano katika namna ya kuanguka wakati wowote kwa kukosa mapato ya kuiendesha....Hii ndiyo hofu yako kuu,hofu ya Kikwete,hofu ya CCM na wabunge wake waliobaki katika BMLK, au siyo?

Lakini hawa wenzetu wanachoharibu wanatupa suluhisho la hofu zao kwa kutupa majibu ya kuturudisha kulekule tunakotaka tutoke.....Muundo wa Muungano wa serikali mbili ya Muungano + Tanganyika kwa wakati mmoja na ile ya Mapinduzi ya Zanzibar. Mgogoro upo hapa!!

Mimi nilidhani kwamba badala ya kusema muundo wa serikali tatu, usimamimizi na uendeshaji wake ni mgumu hautekelezeki, wote kwa pamoja tungejaribu kuangalia ni mianya ipi ambayo Rasimu imeacha ulegelege na kuiziba kwa madhumuni ya kuiboresha zaidi pasipo kuwa na mtifuano usio na sababu!!..

Hata hivyo mimi natofautina kidogo na wewe juu ya maoni ya Awadhi aliyekuwa mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba na M/kiti wa Chama cha Wanasheria Zanzibar aliyoyatoa katika mdahalo uliofanyika j'tatu tarehe 4 - Ubungo Plaza na kurushwa moja kwa moja na baadhi ya vyombo vya habari na mimi niliyeko huku Monduli kusikia na kuona.

Binafsi nilimuelewa kwani alisema walichokifanya wao kama Tume baada ya kuchambua maoni ya wananchi,kupima uzito wa hoja na kuandaa rasimu ya mwisho ni kutenganisha mamlaka ya nchi hizi mbili zilizoungana mwaka 1964 kwa kuziundia serikali zenye mamlaka kamili za kikatiba na kuiweka wazi ile ya Muungano ambayo hawa washirika wa Muungano watawajibika kwayo kuhakikisha inakuwepo na inakuwa na nguvu. Hapa ni vyema ukakumbuka kwamba serikali ya Muungano ndiyo itakokuwa na mamlaka ya juu kabisa kwa serikali zote za washirika na kumbuka mambo ya ulinzi, usalama wa taifa,Mambo ya nje na Polisi ni mambo ya Muungano!!

ISHU YA GHARAMA JE?

Kutenganishwa kwa mamlaka ya serikali ya Muungano,Tanzania Bara (Tanganyika) na Zanzibar hakuongezi wala hakupunguzi eneo la nchi hizi washirika wa Muungano. Kwa mujibu wa Awadhi kwa niaba ya Tume shughuli za maendeleo na kiutawala zinazofanyika leo chini ya mfumo tulio sasa wa serikali 2 zitaendelea kubaki vilevile isipokuwa Rasimu ya katiba hii yenye muundo serikali 3 inaleta ufanisi zaidi ktk usimamizi wa shughuli hizo kwa lengo la kuwahudumia wananchi wa nchi hizi mbili. Na kwa maana hiyo hata gharama za kuindesha serikali ya Muungano bado zinabaki zilezile kutoka katika vyanzo vilevile!!

Ni ukweli ulio wazi kuwa eneo la Tanganyika ni kubwa mara zaidi ya elfu nne kulinganisha na Zanzibar. Ina idadi kubwa ya wakaazi mara elfu zaidi ya nne. Ni wazi hata shughuli nyingi za Mungano zitakuwa zinafanyikia Tanzania Bara na kwa maana hiyo bado huyu atakuwa atakuwa mchangiaji mkuu wa shughuli za muungano. Lililo muhimu hapa ni kutengeneza katiba yenye nguvu kuilinda serikali ya Muungano na kutowapa nafasi nchi washirika kuuchokonoa muungano kwa namna yoyote ile aidha kwa kukwepa kuchangia kwa nia ya kutaka kuuvunja!!

Lililo muhimu zaidi ni kuheshimiana na tukubaliane..........Turidhiane. Haya mengine ni hofu za watu flaniflani tu na hasa watawala walioko madarakani kwa hofu ya kupoteza fursa walizo nazo za kifisadi!!
 
Kwani tunauunganisha kila kitu? Nijuavyo mimi tunaunganisha baadhi tu ya mambo na ndivyo walivyokubaliana waasisi. Hatuunganishi kilimo na ufugaji, hatuunganishi tawala za mikoa na serikali za mitaa, hatuunganishi rasilimali nk. Tunaunganisha ulinzi na usalama, tunaunganisha mambo ya nje. Yale mambo ambayo huunganishi yatashughulikiwa na serikali washirika. Yale tunayounganisha yatashughulikiwa na serikali ya muungano. Ugumu unatoka wapi? Kwanini unanga'ng'ania serikali ya Tanganyika iwe na Wizara za muungano pia? Kwa nini leo hii Zanzibar haina Membe wao? Mimi nadhani tunachamba mno na matokeo yake ndiyo haya.
Mkuu nakuomba sana unisome kwa taratibu upate kunielewa. Sing'ang'anii kitu chochote ila hunielewi tu. Kila jambo na wakati wake mkuu wangu hakuna nchi serikali kuu na hasa chombo kama TRA hawana mamlaka ya kodi ya wananchi wake ila nchi washirika ndiyo mambo yao! na kodi zetu zipo katika kila jambo hivyo umuhimu wa serikali kuu kuwa ni yake pia upo. Hii habari ya mfuko wa pamoja sijui nchi zichangie mfuko wa hazina inatisha!

Narudi kwa Waasisi wetu na historia kwa ufupi.

Waasisi wetu waliandika katiba hii ya mwaka 1977, awali katiba hii ilitanguliwa na katiba kama nne hivi toka Uhuru wetu na kama sikosei ni katiba ya mwaka 1964 baada ya Muungano ndio ilikuwa na mambo 11 tu kutokana na kwamba tulikuwa na Jumuiya ya Afrika mashariki ambayo ndio ilishika mambo mengine 11. Hivyo Zanzibar ikawa mshirika moja kwa moja wa Jumuiya hiyo ndani ya Tanzania na hayo mambo 22 yalikuwemo vile vile ktk ushirika wetu. Pili, Zanzibar haikuwa na katiba yake ila ikiongozwa na Amri za Rais (Presidential Decrees) hivyo chama cha ASP na baraza la mapinduzi ndio walokuwa executive council na law maker kwa muda wote kabla na baada ya katiba ya mwaka 1977.

Hivyo katiba hii ya mwaka 1977 ilitokana na kuungana vyama vya TANU na ASP na kufuatiwa kuvunjika kwa Jumuiya ya Afrika mashariki mwaka huo huo. Hawa wanaouliza haya mengine 11 yametoka wapi ni kutokana na kutofuatia Historia ya muungano wetu na tumetoka wapi na tulikuwa tukienda wapi. Utawala wa CCM waliweka msingi mikuu ya Utawala wao wa Kiumla, chama kimoja, kujenga Ujamaa na muundo wa serikali mbili ilihali Zanzibar hawakuwa na katiba nadhani hadi hapo utaona waasisi wetu walielekea wapi. Misingi yote hii ilikuwa ndio kiini cha kuandikwa katiba hiyo ya Taifa na ikaitwa katiba ya kudumu. Kwa hiyo katiba hii ilipitishwa na bunge maalum lililoteuliwa na Rais baada ya masaa machache sana, kutokana na mwongozo na mwelekeo wa chama chao bila ridhaa ya wananchi.

Kwa hiyo katiba ya mwaka 1977 iliandikwa katika wakati tofauti kabisa na mazingira ya leo, walilazimika kufanya hivyo kutokana na hali halisi ya wakati ule bado siasa ya Ujamaa uliipa serikali milki ya kuhodhi njia zote za uchumi. Kila dola ilikuwa bado ikitaka kujua inamiliki vitu gani na hivyo maridhiano ya katiba ile ilikuwa baina ya viongozi wa ASP na viongozi wa TANU ilihali leo tunasema katika nchi ya kidemokrasia msingi mkuu wa Katiba ni ule unaoweka mamlaka yote mikononi mwa wananchi. Na wananchi wenyewe ndio sisi Watanzania sio Utanganyika wala Uzanzibar Je utayaweka vipi mamlaka hayo kwa wnanchi kwa kugawa kwanza mambo ya Muungano wao kama sii kuwagawa wao ili wagawane umaskini?

Hivyo katiba hii lazima itupe mwanga na maono ya mbele, inaondoa utawala wa kiumla, chama kimoja, Ujamaa wa seerikali kuhodhi njia za uzalishaji, haki sawa, ubaguzi, idumishe udugu wetu, na iwe sheria mama kwa nchi washirika hivyo sheria za nchi hazitakiwi kukinzana nayo hata kidogo. Hivyo kutokea kwa mapungufu haya ya katiba ya mwaka 1977 yalosababisha kuandika kwa katiba mpya ya Zanzibar ilokinzana na katiba hii ni kutokana na ukweli kwamba katiba hii haikidhi mahitaji ya sasa ambayo yametokana na mabadiliko makubwa ktk mfumo wa kisiasa na Kiuchumi. Sasa wenzetu hawakutaka kuendelea na sheria mama ilowabana ktk utawala wa kiumla, utawala wa chama kimoja, na Ujamaa ambao sisi bado ndio unaweka pamoja. Huu ni wakati tofauti kabisa mkuu wangu lazima tuone mbali..
 
Kitaturu,

Mkuu swala la jeshi na mengineyo hata King Mswati na Malkia wanayo mamlaka hayo, lakini Je wananchi wetu wako tayari kuwa na Ufalme? Je nchi husika zitafuata sheria mama ya mfalme (muite mtakavyo) wanayemchagua kuwa kiongozi wa mambo 7 wakati hawamhitaji hivyo? Ni wapi panapoonyesha ndani ya rasimu hii kuwa serikai kuu itakuwa na mamlaka juu ya serikali hizi ikiwa ni SHIRIKISHO maana shirikisho lina tafisri yake. nachelea tu kusema haya tujihadhari na maamuzi ya leo.

Mimi naziona nchi za wenzetu swala la kodi utafuatwa na IRS au Revenue Canada popote unapokwenda na sio swala la nchi mshirika pekee, leo hii unategemea vipi serikali kuu iwe na nguvu hizo wakati sii mambo ya muungano na haina vyanzo? Kuna mambo gani ambayo sii ya wananchi maana hata mkulima, mfugaji mfanyakazi, mjariamali, mvuvi, mwekezaji yaani kila mtu ni lazima alipe kodi na hii sisi sio ktk mambo ya muungano. Tutaweka vipi malengo ya katiba hii ili kuondoa maadui wetu kama Ujinga, maradhi na umaskini kama sio mambo ya muungano? hatuwezi kuepuka matumizi makubwa kwa kudharau yale waloyaona waasisi wetu kuigharamia serikali kuu ambayo ni mzigo kwa Tanganyika, laa tukubali matumizi haya halafu tuone mbele itakuwaje.

Wewe soma sura ya 18 ibara ya 130 na 131 kisha nambie huo ushuru usio na kodi utaweza vipi kuendesha serikali hii ambayo mnadanganywa kuwa itakuwa ndogo tu na ifanye kazi kwa ufanisi. Hilo Jeshi mnajua mahitaji yake ama udogo wa jeshi ndio kusema halihitaji fedha? Je sio rasimu hii inayopendekeza miaka 40 kwa mgombea Urais tukifika huko mtaikubali pia au tutaanza mjadala mwingine wa vijana? sio kila kilichoandikwa ktk rasimu hii ni muarobaini lazima tuijadili na kuona wapi turekebishe ili wananchi kwa pamoja tuikubali.
 
Mukandara;

Nimekusoma na kukuelewa na kwa hakika umekuja kwenye hoja yangu kwamba; Si ndiyo hayo mambo ambayo tunatakiwa kuyaweka sawa kama mapungufu katika Rasimu hii ya Tume ya Jaji Warioba ili ikae vizuri zaidi kisha tusonge mbele? Tatizo letu nini hasa?

Katika ishu ya Jeshi na ufalme wa King Msawati hata sijakuelewa na kama nimekuelewa basi ni wazi unafikiria vibaya. Nasema hivyo kwa sababu hata sasa Jeshi liko chini ya mamlaka ya Muungano na tuna Amiri Jeshi mmoja tu ambaye ndiye Rais wa JMT na katika Rasimu hii ndicho kinachopendekezwa. Vinginevyo unaweza kunielewesha katika lugha rahisi zaidi ili nikuelewe

Ndiyo, na kama tunaona kuwa ishu ni Rasimu kutokuweka mfumo na vyanzo thabiti vya mapato ya kuindesha serikali ya Muungano ni wakati wa kurekebisha sasa kwa sababu huu ni muungano wetu sisi wana wa nchi hizi mbili na kwa hakika tuliungana kwa hiari hatuna sababu yeyote ya kushindwa kukubalianana kuanza kufikiri kusalitiana huko mbeleni. Na hili ndilo tatizo lililopo sasa kutokuaminiana na kama ni hivyo hata walioko huko Dodoma kwa sasa na wakawa na fikra hizi, ni wazi hakuna watakachokitengeneza!!
 
Back
Top Bottom