andara;10296423]
Nguruvi3Nachopinga mimi ni muundo wa serikali 3 unaoweka mambo 7 yasokuwa na umuhimu kwa nchi husika kuunda muungano wetu isipokuwa ni kuubomoa na kuunda shirikisho kama NATO ama nchi za Ulaya la majeshi na maswala ya mambo ya nje of which Zanzibar na Tanganyika hatuna haja wanaweza yamudu wenyewe na sii priority ya wananchi.
Mkandara , wzn wamelalamika 22 ni mengi, leo unaendaje kuwaambia yote ni ya muungano? Sio wewe uliyewahi kusema Tanganyika imeingiza mambo kinyemela. Leo unabadilisha poisition. Mkuu ! please unachanganya umma. Hatuna tatizo kama unajichanganya, unapogusa umma inatuuma Na nasema wazi kwamba tukitaka serikali 3 basi ni lazima mambo yote yawe ya Muungano kama walivyopanga waasisi wetu kama hatua ya kufikia muungano kamili ambayo inapelekea hisia za serikali moja, lakini sisi tutagawa mamlaka ya kuendesha shughuli za serikali uwe wa pande mbili kwa
serikali ya Bara na Zanzibar. Ok, nimekuelewa! yaani tuwe na serikali ya Tanganyika na Zanzibar halafu serikali moja ambayo ni ya shirikisho.
Hapa nimekuelewa vema.
Wingi wa serikali hauondoi watataizo ya wananchi bali malengo ya kuunda serikali hizo ni kuboresha utekelezaji wa shughuli zake na hapa sioni kabisa fikra hizo zikitumika kujenga hoja. Tuna serikali hadi za mitaa na hazitazamwi kuboreshwa kwake isipokuwa Utanganyika na Uzanzibar.
Upo katika rekodi zangu nilizoangalia leo ukisema kuwa, znz ipewe nafasi ya kumiliki uchumi wake. Kwamba, JMT imeinyima nafasi. Znz haiwezi kukopa wala kupata misaada. Sasa mkuu, huoni malengo ya serikali 3 ni kuboresha shughuli zake kama ulivyosema kwa Zanzibar.
Ndio maana Watanganyika tunasema, tunataka fiscal autonomy kwasababu kuu mbili
1. Kuacha kuwa ndani ya koti, na hivyo kuwapa znz nafasi ya kujiendeleza kiuchumi
2. Tanganyika kuwa na fiscal autonomy ili nayo kama znz iweze kupanga shughuli zake bila wasi wasi kama ilivyo sasa.
Unajua zamani toka tuunde Muungano wetu tulikuwa na rais na makamu wa rasi wawili, Jumbe akiwa makamu wa kwanza na rais wa Zanzibar na Kawawa akiwa makamu wa pili na msimamizi wa mambo ya Tanganyika. Hivyo tukawa na Utatu ndani ya nchi 1 jambo ambalo halikuleta utata hadi mwaka 1977 tulipoandika katiba Mpya.
Mkuu naona kumbu kumbu zako zina 'rust'. Utata wa muungano ulianza siku nyingi. Hayo mambo 11 yalipofikia 2o ilikuwa wakati huo unaosema utatu haukuwa na shida. Hapa umepotosha vizuri sana
Hivyo basi, tukubali kwanza uwepo wa serikali 3 utakuwa na manufaa gani katika Muungano wetu badala ya kuanza kunyoosheana vidole kwa sababu tu Mnaitaka Tanganyika. Hakuna mahala napingana na wazo la serikali 3 isipokuwa siii kwa Utanganyika bali kama sababu zitakuwa ni kurahisisha utekelezaji wa shughuli za serikali maana wananchi wanayataka maendeleo lakini muundo uliopo umekuwa kikwazo cha maendeleo hayo.
Mkuu, kwani Utanganyika unakuuma nini?
Kwanini usizungumzie uzanzibar unadhani Utanganyika ni uhalifu.
Mkuu nani amepanda mbegu ya Utanganyika? Nani amekuza jina la Tanganyika.
Kwani huelewei ni haramu mzn kuwa Mtanzania.
Pili, haiwezekani hata siku moja ukwa na JMT yenye znz halafu ukasema kuna Tanganyika nje ya hapo.
Mkuu huko ndio kuvaa koti kwenyewe tunakotaka kuvua.
Sijui ni kitu gani kinakuuma kuzinduka kwa Tanganyika hadi unafikia mahali kuita Tanzania bara, nchi isiyojulikana isipokuwa kwako tu mwenyewe.
Hatuwezi kuishi na malalamiko ya wzn kila siku. Tunashindwa kufanya shughuli za nchi yetu tukihangaika kuwapendeza na vikao visivyo isha. Tunatatukanwa tukiwa tumewabeba mgongoni.
Yote hayo hayana return ya aina yoyote kwa Mtanganyika
Tunataka kuvua koti Mkandara, na wznz wantaka tuvue koti. Kipi unaona kina tatizo?