Serikali 3 na gharama zake

Serikali 3 na gharama zake

Mkandara ,
Naomba niweke kumbu kumbu sawa kwa faida ya wanajamvi.
1. Wewe umesimamia S2 siku zote ukisema hakuna sababu ya kurudisha serikali ya Tanganyika
a) Itua uzalendo wa nchi
b) Italeta mgawanyiko miongoni mwa Watanzania
c) Mambo yote yawe ya muungano chini ya Tanzania lakini znz ibaki kama ilivyo. (Si chini ya Tanganyika)

2. Upo katika rekodi ukisema kuzinduka kwa Tanganyika kutaongeza gharama. Hapa uliamini uwepo wa Tanzania muungano

3. Kwamba, Tanganyika imevaa koti la muungano na kuwanyima wznz misaada na mikopo.
Kwa maneno yako ya bandiko hapo juu, una maana Tanganyika inakopa na kuwanyima wznz misaada na mikopo yao.

4. Umeeleza kuwa, znz inaweza kuchangia muungano kama itapewa kipaumbele cha bandari na biashara n.k.
Kwa maneno yako ya juu, una maana ZNZ inaweza kuwachangia Watanganyika!!!!

5. Hakuna taifa la Tanganyika, ukiungana na Shivji katika hilo.
Leo unasema taifa ulilosema halipo, ndilo lililopo.

Mifano ni zaidi ya 10 ikionyesha jinsi unavyobailika na kubadilisha position yako kila alfajiri na magharibi.

Nadhani ni ngumu kwangu na wengine kukuelewa hasa unasimamia nini, unazungumza nini na una tetea nini.

Tunachokijua ni kubadili position na kama utahitajika ushahidi upo wa kutosha.

Tanganyika
Kusema kuwa Tanganyika ipo isiyokuwepo ni muungano, hilo ni tusi kubwa sana kwa Watanganyika.

Kwanza, nikukumbushe kuwa umeangalia mjadala kwabahati mbaya hukuelewa au umeelewa vibaya dhana zilizojadiliwa

Pili, unajaribu kupotosha umma kwa kucheza na maneno zaidi ya facts

Mfano, unapodai Tanganyika ipo, isiyokuwepo ni muungano, una maana madai ya wznz ni dhidi ya Watanganyika na si muungano.

Mfano, wznz wanadai asilimia 21 ya ajira za Tanganyika, wanagharamiwa mambo ya wizara nyeti kwa gharama za Mtanganyika n.k. Hili ni tusi kwa Watanganyika na linahimiza kuzinduka kwake

Mkandara, elewa kuwa kinachotakiwa hapa fiscal autonomy kwa Tanganyika.

Hiyo itapatikana Tanganyika ikiwa inatambulika rasimi na kuwa na mwongozo wake kama ilivyo znz.

Hatutaki kuwa na dude Tanzania ambalo znz inalitumia kumuumiza Mtanganyika.
Elewa dhana ya fiscal autonomy na identity.

Kuhusu tume, walichosema ni kuwa kwa hali ya S2 muungano sasa haupo.
Wazanzibar wameondoa mambo mengi, na tume wameona ni kujidanganya kama tuna Sumatra na Zanzibar Maritime.
Hapa uelewe znz ipo Tanzania ili kullipiwa ada kule IMO na wala si muungano.Kwa

Ni kwa msingi huo tume ikasema, kuendelea na muungano wa kujidanganya huku Tanganyika ikibeba mzigo na Wazanzibar wakiungana kwa jina si kutenda haki. Na ni kwa jina hilo hilo wznz wanawajibika kupitia ili kuweza kujikwamua kwa mambo yao.

Prof Kabudi aliposema Watanganyika wana yao mezani alimaanisha hili.

Gharama za S3
Huko nyuma ulisema JMT inabeba gharama za S2 na ni rahisi. Tulikuuliza mara nyingi kwani gharama hizo zinachangiwaje? Hukuwa na jibu. Leio unasema S3 zitakuwa na gharama ukisahau hukuweza kutueleza gharama za sasa analipia nani.

Hoja yangu hapa si kujibu hoja zako, ni kukutaka utueleze unasimamia nini ili tuweze kujadiliana vema.
Kwa sasa kila jibu litakuwa na position tofauti na hilo litakuwa gumu sana the least to say.

Hebu tueleze, wewe unadhani nini kifanyike katika mazingira unayoyasema.
 
Mkandara ,
Naomba niweke kumbu kumbu sawa kwa faida ya wanajamvi.
1. Wewe umesimamia S2 siku zote ukisema hakuna sababu ya kurudisha serikali ya Tanganyika
a) Itua uzalendo wa nchi
b) Italeta mgawanyiko miongoni mwa Watanzania
c) Mambo yote yawe ya muungano chini ya Tanzania lakini znz ibaki kama ilivyo. (Si chini ya Tanganyika)

2. Upo katika rekodi ukisema kuzinduka kwa Tanganyika kutaongeza gharama. Hapa uliamini uwepo wa Tanzania muungano

3. Kwamba, Tanganyika imevaa koti la muungano na kuwanyima wznz misaada na mikopo.
Kwa maneno yako ya bandiko hapo juu, una maana Tanganyika inakopa na kuwanyima wznz misaada na mikopo yao.

4. Umeeleza kuwa, znz inaweza kuchangia muungano kama itapewa kipaumbele cha bandari na biashara n.k.
Kwa maneno yako ya juu, una maana ZNZ inaweza kuwachangia Watanganyika!!!!

5. Hakuna taifa la Tanganyika, ukiungana na Shivji katika hilo.
Leo unasema taifa ulilosema halipo, ndilo lililopo.

Mifano ni zaidi ya 10 ikionyesha jinsi unavyobailika na kubadilisha position yako kila alfajiri na magharibi.

Nadhani ni ngumu kwangu na wengine kukuelewa hasa unasimamia nini, unazungumza nini na una tetea nini.

Tunachokijua ni kubadili position na kama utahitajika ushahidi upo wa kutosha.

Tanganyika
Kusema kuwa Tanganyika ipo isiyokuwepo ni muungano, hilo ni tusi kubwa sana kwa Watanganyika.

Kwanza, nikukumbushe kuwa umeangalia mjadala kwabahati mbaya hukuelewa au umeelewa vibaya dhana zilizojadiliwa

Pili, unajaribu kupotosha umma kwa kucheza na maneno zaidi ya facts

Mfano, unapodai Tanganyika ipo, isiyokuwepo ni muungano, una maana madai ya wznz ni dhidi ya Watanganyika na si muungano.

Mfano, wznz wanadai asilimia 21 ya ajira za Tanganyika, wanagharamiwa mambo ya wizara nyeti kwa gharama za Mtanganyika n.k. Hili ni tusi kwa Watanganyika na linahimiza kuzinduka kwake

Mkandara, elewa kuwa kinachotakiwa hapa fiscal autonomy kwa Tanganyika.

Hiyo itapatikana Tanganyika ikiwa inatambulika rasimi na kuwa na mwongozo wake kama ilivyo znz.

Hatutaki kuwa na dude Tanzania ambalo znz inalitumia kumuumiza Mtanganyika.
Elewa dhana ya fiscal autonomy na identity.

Kuhusu tume, walichosema ni kuwa kwa hali ya S2 muungano sasa haupo.
Wazanzibar wameondoa mambo mengi, na tume wameona ni kujidanganya kama tuna Sumatra na Zanzibar Maritime.
Hapa uelewe znz ipo Tanzania ili kullipiwa ada kule IMO na wala si muungano.Kwa

Ni kwa msingi huo tume ikasema, kuendelea na muungano wa kujidanganya huku Tanganyika ikibeba mzigo na Wazanzibar wakiungana kwa jina si kutenda haki. Na ni kwa jina hilo hilo wznz wanawajibika kupitia ili kuweza kujikwamua kwa mambo yao.

Prof Kabudi aliposema Watanganyika wana yao mezani alimaanisha hili.

Gharama za S3
Huko nyuma ulisema JMT inabeba gharama za S2 na ni rahisi. Tulikuuliza mara nyingi kwani gharama hizo zinachangiwaje? Hukuwa na jibu. Leio unasema S3 zitakuwa na gharama ukisahau hukuweza kutueleza gharama za sasa analipia nani.

Hoja yangu hapa si kujibu hoja zako, ni kukutaka utueleze unasimamia nini ili tuweze kujadiliana vema.
Kwa sasa kila jibu litakuwa na position tofauti na hilo litakuwa gumu sana the least to say.

Hebu tueleze, wewe unadhani nini kifanyike katika mazingira unayoyasema.

Naamini hakuwepo kwenye tume ya kukusanya maoni vinginevyo angewavuruga sana wajumbe.
 
Nguruvi3,
Mkandara ,
Naomba niweke kumbu kumbu sawa kwa faida ya wanajamvi.
1. Wewe umesimamia S2 siku zote ukisema hakuna sababu ya kurudisha serikali ya Tanganyika
a) Itua uzalendo wa nchi
b) Italeta mgawanyiko miongoni mwa Watanzania
c) Mambo yote yawe ya muungano chini ya Tanzania lakini znz ibaki kama ilivyo. (Si chini ya Tanganyika)

2. Upo katika rekodi ukisema kuzinduka kwa Tanganyika kutaongeza gharama. Hapa uliamini uwepo wa Tanzania muungano

3. Kwamba, Tanganyika imevaa koti la muungano na kuwanyima wznz misaada na mikopo.
Kwa maneno yako ya bandiko hapo juu, una maana Tanganyika inakopa na kuwanyima wznz misaada na mikopo yao.

4. Umeeleza kuwa, znz inaweza kuchangia muungano kama itapewa kipaumbele cha bandari na biashara n.k.
Kwa maneno yako ya juu, una maana ZNZ inaweza kuwachangia Watanganyika!!!!

5. Hakuna taifa la Tanganyika, ukiungana na Shivji katika hilo.
Leo unasema taifa ulilosema halipo, ndilo lililopo.
Sitopenda kuendelea kubishana na mtu asoweza kusoma maelezo ya watu akayaelewa kwanza kabla ya kutoa hoja zake. Haya yote sii maswali yangu mimi bali maswali ya wananchi walokusanya tume ya Warioba na ndio chanzo cha kuandika rasimu hii. Tunaijadili rasimu ya warioba na sii mawazo ya Mkandara hapa ila kubaliana ama pingana name kwa kufuata utafiti wa tume ya warioba.

Mimi nayajadili tu kwa mapana yake ktk kuubaliana na kutokubaliana. Sasa nakushangaa wewe unapokuja na hoja ambazo umetunga wewe. Kukataa kwamba Tanganyika haikuvaa koti la Muungano ili hali Warioba mwenyewe katika kongamano la juzi kasema kuna ukweli huo, labda fuatilia mada iloanzishwa hapa. Kasema wazi kwamba mambo yote ya Muungano ni mambo ya Tanganyika ama nikuwekee dondoo zake kuwa alisema hivi.
=>Jaji warioba anasema hakuna mawaziri wa muungano wanaotembelea Zanzibar kwa ajili ya mambo ya Muungano.
Mambo yote ya muungano ni ya bara.
=>Anasema Nchi mbili zimeunganika lakini moja haina Sovereignty, Tanganyika iko huru kufanya mambo yake ya maendeleo lakini Zanzibar mpaka iombe ridhaa ya Bara.
Sasa sielewi wewe unaelewa vipi kuhusu hili neno Muungano na mambo yake kuwa ya Muungano?

Pili, nakuomba wewe sasa twambie Warioba alipotoa maswali yake saba kwa wale wanaombeza na la pili akisema kuwa - "Hoja ya wananchi ni kwamba Tanganyika imevaa koti la Muungano, wakisema serikali ya sasa sio ya muungano ila ni ya Tanganyika." Na maelezo ya Warioba yanathibitisha hivyo na ndio sababu ya kupendekeza muundo wa serikali 3, wewe huna sababu isipkuwa ya Utanganyika tu. Nachopinga mimi ni muundo wa serikali 3 unaoweka mambo 7 yasokuwa na umuhimu kwa nchi husika kuunda muungano wetu isipokuwa ni kuubomoa na kuunda shirikisho kama NATO ama nchi za Ulaya la majeshi na maswala ya mambo ya nje of which Zanzibar na Tanganyika hatuna haja wanaweza yamudu wenyewe na sii priority ya wananchi.

Na nasema wazi kwamba tukitaka serikali 3 basi ni lazima mambo yote yawe ya Muungano kama walivyopanga waasisi wetu kama hatua ya kufikia muungano kamili ambayo inapelekea hisia za serikali moja, lakini sisi tutagawa mamlaka ya kuendesha shughuli za serikali uwe wa pande mbili kwa serikali ya Bara na Zanzibar. kaa haiwezekani basi serikali 2 ziendelee tuipate katiba mpya yenye kuondoa hitilafu kubwa zinazowakwaza wananchi na sio kung;ang;ania kitu ambacho hatutaweza kufikia maridhiano. Wingi wa serikali hauondoi watataizo ya wananchi bali malengo ya kuunda serikali hizo ni kuboresha utekelezaji wa shughuli zake na hapa sioni kabisa fikra hizo zikitumika kujenga hoja. Tuna serikali hadi za mitaa na hazitazamwi kuboreshwa kwake isipokuwa Utanganyika na Uzanzibar.

Unajua zamani toka tuunde Muungano wetu tulikuwa na rais na makamu wa rasi wawili, Jumbe akiwa makamu wa kwanza na rais wa Zanzibar na Kawawa akiwa makamu wa pili na msimamizi wa mambo ya Tanganyika. Hivyo tukawa na Utatu ndani ya nchi 1 jambo ambalo halikuleta utata hadi mwaka 1977 tulipoandika katiba Mpya.

Katiba hiyo iliondoa wadhifa wa makamu wa pili wa rais hivyo hatukuwa na makamu warais wa pili kwa tanganyika toka mwaka 1978 hadi 1984, tukaunda waziri mkuu ambaye Sokoine akawa ndiye kiongozi wa bara. Lengo la kufanya hivi ilikuwa katika kuelekea kuunda serikali moja jambo ambalo liliteka kero za mwanzo kabisa, Jumbe akitaka serikali 3 badala ya moja na Zanzibar wakaandika katiba yao ya kwanza kabisa mwaka 1979. These are facts na za siii kugushi.

Kuelekea uchaguzi wa mwaka 1984, Nyerere alikuwa na vijana wake watatu mkononi salim, Sokoine na Maalim Seif, hivyo tufahamu ya kwamba hata Jumbe kusemekana kutaka kuuvunja Muungano ni kutokana na sio hoja ya serikali 3 bali maalim Seif alitaka kuchukua nafasi hiyo maana Jumbe ndiye alikuwa kikwazo. Ikauzwa kama uhaini wa muungano kwa sababu wazo pasipo mwongozo wake ni hoja potofu na ilipouzwa mwalimu akajaa tele. Alolishwa zaidi mwalimu hata akaamini siyajui na ndipo Jumbe akawekwa kizuizini tena Tanganyika na sio kwao Zanzibar, hili watu hawalitazami kwa sababu Fitna ilianzishwa Zanzibar na sii Tanganyika, hivyo Jumbe Mzanzibar alohamia bara amekuwa adui wa Muungano na Tanganyika.

Kufikia uchaguzi wa mwaa 1985, Sokoine hatukuwa naye tena na Jumbe ndio hivyo kwa hiyo Seif na Salim wakawa kipenzi cha mwalimu lakini hawakubaliki na baraza la mapinduzi. Ndipo Mwinyi kuingia Ikulu na kuvunjika kwa fikra za serikali 3 na zanzibar kuandika upya. Ujio wa vyama vingi swala la makamu wa rais kuwa rais wa zanzibar likaondolewa kwa sababu kule Zanzibar wanaweza kupitisha chama kingine na ikawa mkanganyiko. Hivyo tutaanza kutoka ktk dira yetu na katiba ikawa haikidhi tena mahitaji yetu kiuchumi na kidemokrasia.

Hivyo basi, tukubali kwanza uwepo wa serikali 3 utakuwa na manufaa gani katika Muungano wetu badala ya kuanza kunyoosheana vidole kwa sababu tu Mnaitaka Tanganyika. Hakuna mahala napingana na wazo la serikali 3 isipokuwa siii kwa Utanganyika bali kama sababu zitakuwa ni kurahisisha utekelezaji wa shughuli za serikali maana wananchi wanayataka maendeleo lakini muundo uliopo umekuwa kikwazo cha maendeleo hayo.

Na kugawana mali sii suluhu ndicho nachokazania. Wingi wa serikali pasipo kuwa na nia nzuri ni sawa na maneno ya Prof. Shivji kuwa The road to hell is paved in good intention!.
 
Mukandara;

Nimekusoma na kukuelewa na kwa hakika umekuja kwenye hoja yangu kwamba; Si ndiyo hayo mambo ambayo tunatakiwa kuyaweka sawa kama mapungufu katika Rasimu hii ya Tume ya Jaji Warioba ili ikae vizuri zaidi kisha tusonge mbele? Tatizo letu nini hasa?

Katika ishu ya Jeshi na ufalme wa King Msawati hata sijakuelewa na kama nimekuelewa basi ni wazi unafikiria vibaya. Nasema hivyo kwa sababu hata sasa Jeshi liko chini ya mamlaka ya Muungano na tuna Amiri Jeshi mmoja tu ambaye ndiye Rais wa JMT na katika Rasimu hii ndicho kinachopendekezwa. Vinginevyo unaweza kunielewesha katika lugha rahisi zaidi ili nikuelewe

Ndiyo, na kama tunaona kuwa ishu ni Rasimu kutokuweka mfumo na vyanzo thabiti vya mapato ya kuindesha serikali ya Muungano ni wakati wa kurekebisha sasa kwa sababu huu ni muungano wetu sisi wana wa nchi hizi mbili na kwa hakika tuliungana kwa hiari hatuna sababu yeyote ya kushindwa kukubalianana kuanza kufikiri kusalitiana huko mbeleni. Na hili ndilo tatizo lililopo sasa kutokuaminiana na kama ni hivyo hata walioko huko Dodoma kwa sasa na wakawa na fikra hizi, ni wazi hakuna watakachokitengeneza!!
Mkuu samahani nilichanganya mada kidogo na ya mwandishi wa kwanza. Unajua mimi nautazama Muungano wetu kama ni wa WATU na NCHI kutokana na historia yetu na hivyo hatuungani kwa sababu za kiuchumi ama kisiasa kama inavyodaiwa na wengi ambao ni wanasiasa uchwara. Hawa wanajaribu kwa kila hila kulifanya swala hili la Muungano kuwa ni wa kisiasa kutokana na walivyolishwa ama maslahi ya nchi za nje kutugawa ili watutawale kiuchumi. It all start with UCHUMI kutokea kutoelewana na kugawana mali kwa nchi zenye muungano na bahati mbaya tunachochewa na nguvu za mataifa makubwa zaidi yetu.

Mimi nimezaliwa na kukulia bara, tena nimmekulia Mwibara ambako marafiki wangu wakubwa walikuwa ni waarabu wenye asili ya Oman wakiwa na maduka yao pale mjini Kibara. Hawa walinambia hata wazazi wao wenyewe walizaliwa pale Kibara sasa hiyo ilikuwa miaka ya 60, Huo Ukerewe vile vile tulikuwa na majirani na marafiki waarabu wa Oman walohamia pale toka miaka ya 40, Leo hii hawa watu wamerudi Arabuni kutokana na siasa hizi za chuki zilizojengwa maana walikuwa wakiishi bara na sii zanzibar na salama hadi Uhujumu Uchumi ulipokuja miaka ya 80. Kama yalifanyika makosa basi ni kazi yetu kuyarekebisha na sii kuendelea kuweka chuki baina yetu ilhali sisi tuna historia ndefu sana ambayo imetujenga sisi kama taifa. Marekani ile pale kuna mataifa mangapi? naweza sema mataifa yote na wote wako proud to be American sisi ndio kwanza na Utanganyika!

Inanikera sana kuona niko huku nchi za wageni najiona raia na umoja mkubwa umejengwa kushinda nyumbani nilikozaliwa!
 
Nilitegemea utakuja na jibu la hofu ya ccm juu ya gharama za serikali ya Muungano. Analysis yako kwa sehemu iko sawa na kwa sehemu haiko sawa kutokana na mfumo halisi ambao umekuwa ukiendesha nchi hii tangu 1964, na nchi hizi tangu 2010.

Falsafa ya uchambuzi wa majina utawala gani unaitwa serikali gani si jambo la msingi hapa. Hakuna mtu asiyefahamu kwamba kuna SMZ and Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo essentially inahusika na masuala ya Muungano na ya Tanzania bara ama Tanganyika.

Ukweli ni kwamba Serikali ya Tanganyika haipo. Iliyopo ni ya Jamhuri ya Muungano na ya Zanzibar. Kuchapatisha masuala ya tanzania bara kwenye muungano ndiyo mwanzo wa confusions hizi na uwajibikaji usio tija wa serikali ya Muungano kwa Zanzibar.

Kinachotakiwa ni kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ambayo haipo na kuimarisha serikali ya Muungano ili iweze kusimama kama nguzo ya uwepo wa hizi serikali mbili washirika.

Naungana na wewe katika hoja ya kujadili masuala muhimu ya uimarishaji wa serikali ya Muungano.


Serikali 3 na gharama zake

Baada ya kuvunjika kwa bunge la katiba juu ya swala la muundo wa serikali, nachukua nafasi hii kutoa majibu ambayo kwa sababu zisizojulikana imeshindikana kabisa kuelezewa tofauti ya gharama baina ya serikali 2 na 3, gharama zipi zitaongozeka kulingana na mapendekezo ya rasimu ya tume ya Warioba.

Na sii lengo langu kujaribu kuukana ukweli kwamba Tanzania ya leo inahitaji serikali 3 isipokuwa kuwataarifu wananchi kuelewa jinsi gani muundo wa aina hii una mamlaka gani na unafanyaje kazi zake ktk utekelezaji wa majukumu wanayokabidhiwa kikatiba. Hii inatokana na mimi kuwasoma watu wengi kutofahamu Mamlaka ya tawala wa muundo huu ili serikali hizo ziweze kuwawakilisha wananchi wake haraka na kwa ufasaha zaidi. Hivyo lengo la kuzitaka serikali 3 linaonyesha wazi ni kutaka kutengenisha mambo ya Muungano na yasiyokuwa ya Muungano kwa bara kutokana na ukweli kwamba hadi sasa Mambo yote ya Muungano ni mambo ya bara sio ya Muungano badala ya kuziunda serikali ziwe karibu Zaidi na wananchi wake ktk utekelezaji wa matakwa yao.

Mara zote nimesikia wananchi wakidai kuwepo kwa seikali 2 hakuna tofauti ya gharama na serikali 3 na wakitumia sababu za mapngufu ya utawala uliopo ambao miaka yote baada yatangu 1984 tulipounda vyama vingi, kumekuwa na mkanganyika wa utawala ambao umewavuruga wananchi wasijue mamlaka ya vyombo vyao yana ukomo gani. Pia imewavuruga viongozi ambao kwa dhana wamekuwa wakiongeza mikoa wilaya na majibo kufikiria ndio njia rahisi ya kuwafikia wananchi wakati mamlaka bado yapo chini ya rais wa serikali kuu. Hivyo mitazamo yote hii imelenga zaidi hifadhi ya Utawala (kisiasa) kuliko sababu za ujenzi wa nyenzo za kuijenga nchi na wananchi wake ambao pia kw abahati mbaya wamevutwa katika zizi la Uchama na kupoteza Utaifa wao.
Ngoja niseme ukweli, Ukweli ni kwamba tunapoihitaji serikali ya 3 siyo serikali ya ya Tanganyika kama wanavyodai wanasiasa wengi ama wana taaluma wapambanaji isipokuwa tunaihitaji serikali ya Muungano ambayo haipo. Ukweli ni kwamba jina la Muungano lipo lakini hatuna seriikali ya Muungano toka mwaka 1984, niliwahi kulisema jhili na sasa limedhihirishwa ktk kongamano la jana. Imeelezwa katika kongamano la Mwl.Nyerere foundation ya kwamba hata hayo mambo tunayosema kuwa ni ya Muungano ni mambo ya serikali ya bara.

Hivyo mawaziri wote walioko ktk ushirika wa Muungano ni mawaziri wa serikali ya Tanganyika sio ya Muungano. Wajumbe hao walifikia hadi kuhoji ni lini wananchi wamewaona viongozi mawaziri wa Muungano wakitemebelea Zanzibar katika maswala ya Muungano?. Kwa hiyo tunazo serikali2 nazo ni serikali ya Zanzibar na serikali ya Tanganyika - Hatuna serikali ya Muungano!.. Ukweli ndio huo japo unauma.

Kwa hiyo basi ni muhimu tukubali kwamba tuchukulie kwamba hii serikali ya Muungano ni serikali ya bara, bunge lake, mahakama zake zote ni za bara, na ndio maana wapo wananchi wanahoji kuwepo kwa wabunge wa Zanzibar katika bunge la Muungano kujadili mambo yasokuwa ya Muungano bila kujua kwamba pale hakunamambo ya Muungano. Hivyo tunachokililia leo hii ni serikali ya Muungano sio Tanganyika maaa ipo.

Sasa swali linakuja - Tukiunda serikali ya 3 ya Muungano haitakuwa na gharama zake? Hizo ghrama zake ni nani atazihudumia? Na Je, bunge la serikali hii litakuwa na wajumbe wangapi, kutoka wapi na majimbo gani? Mishahara na posho zao zitagharamiwa na nani, watumishi wake watakuwa sehemu zote za Jamhuri au makao makuu tu na kadhalika… Hizi gharama za misafara ya rais ktk mialiko ya Kimataifa, mawaziri wake, mamlaka yake katika mipango ya maendeleo na kadhalika ndiyo maswala muhimu ya kujadili kuliko kuendelea kuidai Tanganyika ambayo ipo.

Je, nchi za wenzetu walokuwa na mfumo kama huu mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za serikali zake umejengwa vipi na nini nafasi ya serikali kuu ktk ujenzi wa Mataifa hayo. Nini ukomo wa mamlaka ya serikali za nchi kuendea mamlaka ya serikali kuu juu ya jambo hilo hilo. Ikiwa Nchi inahitaji uwekezaji katika Kilimo, serikali kuu itahusika vipi tofauti na hizo za kila nchi.

Nafikiri hii inatosha kwa leo tutaendelea inapobidi baada ya michango yenu.
 
Jamani mambo ya kulazimishana yamepitwa na wakati, Mwezi unaokuja Scotland wanapiga kura kuvunja muungano wao na England au kuweno kwenye muungano huo. Wazanzibari nao wapewe njia hiyo waamue kama wanataka muungano au vipi? Tanganyika au Tanzania Bara na wao waulizwe kama wanataka muungano wa kuwabeba wazanzibar kwa hali na mali.
 
Nilitegemea utakuja na jibu la hofu ya ccm juu ya gharama za serikali ya Muungano. Analysis yako kwa sehemu iko sawa na kwa sehemu haiko sawa kutokana na mfumo halisi ambao umekuwa ukiendesha nchi hii tangu 1964, na nchi hizi tangu 2010.

Falsafa ya uchambuzi wa majina utawala gani unaitwa serikali gani si jambo la msingi hapa. Hakuna mtu asiyefahamu kwamba kuna SMZ and Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo essentially inahusika na masuala ya Muungano na ya Tanzania bara ama Tanganyika.

Ukweli ni kwamba Serikali ya Tanganyika haipo. Iliyopo ni ya Jamhuri ya Muungano na ya Zanzibar. Kuchapatisha masuala ya tanzania bara kwenye muungano ndiyo mwanzo wa confusions hizi na uwajibikaji usio tija wa serikali ya Muungano kwa Zanzibar.

Kinachotakiwa ni kuundwa kwa serikali ya Tanganyika ambayo haipo na kuimarisha serikali ya Muungano ili iweze kusimama kama nguzo ya uwepo wa hizi serikali mbili washirika.

Naungana na wewe katika hoja ya kujadili masuala muhimu ya uimarishaji wa serikali ya Muungano.
Mkuu wangu ulisikiliza mdahalo wa Nyerere foundation hivi majuzi na maelezo aloyatoa Warioba? nakuomba msikilize tena chukua muda wako kumuelewa na inakuwaje tena leo mnakataa utafiti wake. https://www.youtube.com/watch?v=bDbUTYbPMc4
 
Gharama ya serikali ya muungano kwa mujibu wa data kutoka hazina ni 1.8b.

1.8 trillion. Na sehemu kubwa ya gharama hizi zitakuwepo hata Kama muungano utavunjika na kila upande kubeba mbao zake.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna mtu yoyote Mwenye clip ya butiku Akijibu maswali atusaidie?


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kama serikali 3 ni gharama basi hata 2 ni gharama pia. Mtuletee serikali moja ndio tutawaelewa hizi mbili miaka 50 hakuna tija yoyote
 
Kwangu mimi naona gharama isiwe sababu/kigezo kikuu cha kuamua ni aina gani ya muungano unatufaa. Ingekuwa hivyo, watu tusingeoa kwani usela ni gharama ndogo kuliko kuoa, kusomesha watoto n.k. Serikali tatu naona ni muafaka fulani tu wa kuushikilia muungano usivunjike, kwani haileti sense baada ya miaka 50 ya muungano ya kuwa na serikali mbili, ndo tunataka kuwa na serikali tatu. Hapo tunaenda mbele au tunarudi nyuma? Ingebidi tuwe tunaelekea kwenye serikali moja sasa. Serikali tatu ni jibu na compromise ya Watanganyika baada ya kuona wenzao kwa maneno wanataka muuungano ila kwa matendo hawautaki. Hata kama ni gharama zaidi, lakini imefika wakati identity ya Watanganyika itambulike at the same level na ya Wazanzibar. Lakini ideal solution ni serikali moja au kila mtu aende kivyake.
 
Mkuu wangu wewe unajua alisema nini unaona shida gani kuyaweka hapa. Wewe sii uliridhika na majibu yake ina maana unayajua sasa iweje mimi nikatafute majibu wakati wewe ulikubaliana na majibu yake hii ina maana unayajua,unachoficha hapa ni kipi.

Hayo ya Maccm na ufisadi wake ni mada nyingine sijasema nakubaliana nao isipokuwa nahoji serikali 3 kama mwananchi ambaye ni mlipa kodi na najua kodi zetu zitaongezeka kugharamia serikali hiyo.

Mboa haya mambo ya serikali tatu yalishafafanuliwa sana namna ya uendeshaji wake, sasa mimi naanza kukubaliana na yule aliyekutaka kuwa serious na kwamba hapa ni kwa great thinkers, umeelekezwa sources za kupata majibu bado unataka spoon feeding? au ndio ule ubishi ulioelezwa kuwa ni wa ki........
 
Nyamanoro, Hivi wewe ukiitwa Kirumba kesho, ina maana utakuwa mtu tofauti? aaah watu wengine bana..

Labda niwaulizeni nnyie mnaoitwa great thinkers. Ikiwa tume ya Warioba imewakillishwa na warioba mwenyewe, Butiku na Awadh katika kongamano la Nyerere foundation wamesema wazi kwamba yale mambo 22 ya muungano sii ya Muungano ila ni ya Tanganyika. Je, kama hayo sii ya Muungano, nambieni nyie ni yapi mambo yalobaki ambayo ya Muungano?.

Kuna watu mnailalamikia Zanzibar kwa katiba yake ilovunja katiba yetu ya Muungano, lakini je kama hayo mambo 22 hayakuwahusu hadi hivi sasa, ilitaka wao waendeshe vipi nchi yao ndani ya Muungano huu? Na turudi katika ukweli ya kwamba kuwepo kwa mambo 7 ya Muungano hivi kweli muundo huu unaiwezesha Chadea kuongoza Zanzibar? Au CUF Tanganyika? Maana kinachotakiwa ni kuunda muundo unaoweka majibu ya demokrasia yakwei ambayo tuliianza mwaka 1993 lakini kutokana na mfumo ulotangulia uliondoa uweekano huo. Je kweli seriali 3 yenye mambo 7 inavisaidia nini vyama vyingine vya upinzani kushiriki sawa katika uchaguzi. Hivi kweli Chadema inaweza kuongoza Zanzibar? na kwa mambo gani ambayo yatwapa kura kuwawezesha kushinda huko ama bara.

Na muundo uliopo hadi sasa japo Chadema wameshinda uchaguzi mikoa ya Arusha, Mwanza, Kigoma na kadhalika chama hicho kimeshindwa kuwa na mamlaka ya uendeshaji wa serikali za sehemu hizo kutokana na mfumo uliopo na sio serikali 2 wala 3. Ma Meya wote wa wilaya zetu wana mamlaka gani? kama sio kila sehemu kutegemea rais wa JMT ambaye sijui ni lipi kalifanya huko Zanzibar kiasi kwamba Wazanzibar kesho waseme serikali ya Muungano imetuwezesha hili ama lile. Mimi siwaelewi kabisa mnapokuja na maswali mengi juu ya mambo yamuungano wakati majibu tumeshapewa kuwa sii ya Muungano na hayajawahi kuwa ya Muungano sasa hayo saba (7) mna hakika gani yatakuwa ya muungano.
 
Serikali 3 na gharama zake

...................... Sasa swali linakuja - Tukiunda serikali ya 3 ya Muungano haitakuwa na gharama zake? Hizo ghrama zake ni nani atazihudumia? Na Je, bunge la serikali hii litakuwa na wajumbe wangapi, kutoka wapi na majimbo gani? Mishahara na posho zao zitagharamiwa na nani, watumishi wake watakuwa sehemu zote za Jamhuri au makao makuu tu na kadhalika… Hizi gharama za misafara ya rais ktk mialiko ya Kimataifa, mawaziri wake, mamlaka yake katika mipango ya maendeleo na kadhalika ndiyo maswala muhimu ya kujadili kuliko kuendelea kuidai Tanganyika ambayo ipo.

Je, nchi za wenzetu walokuwa na mfumo kama huu mamlaka ya uendeshaji wa shughuli za serikali zake umejengwa vipi na nini nafasi ya serikali kuu ktk ujenzi wa Mataifa hayo. Nini ukomo wa mamlaka ya serikali za nchi kuendea mamlaka ya serikali kuu juu ya jambo hilo hilo. Ikiwa Nchi inahitaji uwekezaji katika Kilimo, serikali kuu itahusika vipi tofauti na hizo za kila nchi.

Nafikiri hii inatosha kwa leo tutaendelea inapobidi baada ya michango yenu.

Nimeondoa bla-bla zingine na kutaka kukuonyesha kwamba wewe hujafikilia kabla ya kutuuliza swali la kizembe kama hilo. Wengi tunadhani tunafikilia, lakini kumbe sivyo.

Hizo nchi za wenzetu unazotaka ziwe mfano hujui kwamba kuna nchi zina serikali zaidi ya 30? USA ina serikali ngapi ndani ya Federal?

Hapo unapoona serikali mbili ni gharama kubwa na kwamba ya tatu itaongeza gharama zaidi, yaani umeamini kwamba tutaendelea kuwa na marais waizi kama hawa tulionao ambao wanajichotea tuuu pesa ya safari bila hata audit? Hata kama utabakiza serikali moja kwa kuwa na rais wa aina hii ambaye haoni tofauti ya pesa yake na ya serikali, mzigo ni mkubwa kuliko hata serikali 10.
 
1.8 trillion. Na sehemu kubwa ya gharama hizi zitakuwepo hata Kama muungano utavunjika na kila upande kubeba mbao zake.

Sent from my iPhone using JamiiForums

Heba sema kama kweli, kuna sababu yoyote ya kuendesha serikali kwa gharama kubwa kiasi hicho? Hizi ni nchi maskini, lazima Rais awe na matumizi yanayo angaliwa, siyo hali ya sasa hivi ambayo anaonekana hawezi tofautisha kipato chake na kile cha taifa. Anachota na kutumia kama kijiwe chake bila ukaguzi. Ni kama Mobutu!

Mawaziri nao wanachota watakavyo. kila wizara ina pesa za chai jumla yake ni kubwa kuliko bajeti ya Elimu. Hayo ndo matumizi makubwa ya serikali wanayotumia kutuogopesha. Nonsense!
 
Nimeondoa bla-bla zingine na kutaka kukuonyesha kwamba wewe hujafikilia kabla ya kutuuliza swali la kizembe kama hilo. Wengi tunadhani tunafikilia, lakini kumbe sivyo.

Hizo nchi za wenzetu unazotaka ziwe mfano hujui kwamba kuna nchi zina serikali zaidi ya 30? USA ina serikali ngapi ndani ya Federal?

Hapo unapoona serikali mbili ni gharama kubwa na kwamba ya tatu itaongeza gharama zaidi, yaani umeamini kwamba tutaendelea kuwa na marais waizi kama hawa tulionao ambao wanajichotea tuuu pesa ya safari bila hata audit? Hata kama utabakiza serikali moja kwa kuwa na rais wa aina hii ambaye haoni tofauti ya pesa yake na ya serikali, mzigo ni mkubwa kuliko hata serikali 10.
Mkuu unazungumzia wao wenye serikali 50 lakini wao mambo yao yote ya muungano yanazinufaisha nchi zote 50 sio kwetu sisi na wao hawakuanza na muundo wa chama kimoja na Ujamaa, vyama viwili kuungana na kadhalika.

Sisi tumepitia mifumo ya utawala ambayo mabadiliko yake lazima yazingatie kwanza tumetoka wapi, tumesimama wapi na tulitaka kwenda wapi. Swali langu dogo tu, leo tukiwa na serikali 3 itawezaje kusaidia sehemu tuloshindwa ikiwa hayo mambo 22 tunayodai ni ya Muungano sii ya Muungano ktk utekelezaji wake? Je, sio kwamba kuna tatizo sehemu nyinginezo. Hivi kweli swala la mamlaka ya serikali kuu ni geni kwetu kiasi kwamba tushindwe kuliona? NEC hawana mamlaka kamili, TISS, Mameya na kadhalika kipi kipya kwenu haswa msokijua. Je, huko majuu kweli nao wanaendesha serikali zao kama kwetu kiasi kwamba kuna Utanganyika na Uzanzibar?

Nimeuliza vizuri tu ya kwamba Chadema wameshinda uchaguzi mikoa ya Arusha na Mwanza 2010, Je kweli wanayo mamlaka ya kutekeleza shughuli za serikali ktk mikoa hiyo ama ni watega bakuli na kutazama kama ahadi za JK zimefika ktk majimbo yao? Labda nyie mnajua zaidi nambieni hivi Chadema wamefanya nini Arusha na Mwanza zaidi ya RC na DC wa mikoa na wilaya zake. Sasa wao wataweza vipi kupeleka mabadiliko ktk majimbo hayo pasipo CCM kuidhinisha! ndio haya walokuwa nayo zanzibar miaka yote lazima kitu kipitishwe na bara na mambo 22 tumethibitishiwa kuwa sii ya Muungano bali ni ya bara. Kayasema yote haya Warioba lakini bado hamkubali na Utanganyika wenu ambao hauwasaidii kitu isipokuwa kurudisha jina.
 
Ni lazima tuanze kutatua mambo madogo madogo kabla hatujawaza makubwa. Mambo ya Muungano na yale ya Tanganyika yanatekelezwa na serikali ya Muungano iliyopo.
Ni rahisi sana kuyatenganisha kama kuna utashi wa kisiasa.
Rais wa JMT yupo na gharama zake zinajulikana.
Rais wa Tanganyika ni sawa na Waziri Mkuu wa JMT na yupo na gharama zinajulikana.
Rais wa Zanzibar yupo na gharama zake ni zile zile.
Majeshi yote yapo na gharama haziongezeki.
Wafanyakazi na vitendea kazi vya SMZ hakuna badiliko.
Wafanyakazi wa wizara za Muungano wapo, wale wanaoshughulikia mambo ya Bara wapo, vitendea kazi na gharama zao ni zile zile.
Ni mambo machache sana ya kutumia gharama mpya, kwa mfano mahakama. Hivyo kama kuna makubaliano, utekelezaji unaweza kuanza kidogo kidogo hata kesho asubuhi.
Tatizo hapa ni malengo ya wanasiasa, ubinafsi wa wachache na walio wengi kukaririshwa kuimba serikali tatu au mbili bila kuelewa wanachokisema. Serikali 3,2 au moja zinawezekana kuendeshwa kwa rasilimali zilizopo!
 
Heba sema kama kweli, kuna sababu yoyote ya kuendesha serikali kwa gharama kubwa kiasi hicho? Hizi ni nchi maskini, lazima Rais awe na matumizi yanayo angaliwa, siyo hali ya sasa hivi ambayo anaonekana hawezi tofautisha kipato chake na kile cha taifa. Anachota na kutumia kama kijiwe chake bila ukaguzi. Ni kama Mobutu!

Mawaziri nao wanachota watakavyo. kila wizara ina pesa za chai jumla yake ni kubwa kuliko bajeti ya Elimu. Hayo ndo matumizi makubwa ya serikali wanayotumia kutuogopesha. Nonsense!
Mkuu wambo mengine tumnalaumu serikali 2 bure kabisa. Kwa nini tunashindwa kujenga hoja za msingi ili tuwe na serikali 3? Wakati tunajua kabisa kwamba hakuna mambo ya muungano hivi sasa isipokuwa msahafuni kama vile Muislaam/Mkristu nayebeba Quran/Biblia na asiifuate ibada tutalaumu Quran au Biblia? Utalaumu kuwepo kwa madhehebu mengi kuwa sababu ama kuongeza madhehebu zaidi ndio itasaidia? Jamani sisi hatufuati katiba yetu wenyewe ni watu wasokuwa na dira wala uzalendo.

Matatizo yetu yapo ktk mfumo mzima wa Utawala, hakuna Uwajibikaji, Uzalendo, uwazi wala usawa kiasi kwamba serikali kuu inachoamua wao ndicho kinafanyika. Kama Ntarahamwe au AlShabab wanachokiamini wao japo kinyume cha Imani za dini wao hutafuta sababu za kuhalalisha na watu wakaamini na sasa tuna makundi hayo nchini na yanatuvuruga.

Serikali hizi hizi chini ya Nyerere, Mwinyi na Mkapa haikuwa na matumizi kama haya tena wamesema wazi kwamba mwalimu alikufa maskini ebu tazama viongozi wa leo wakoje? Mbunge wa jimbo dogo tu anapokea mshahara mkubwa kuliko CEO wa Benki zetu. Acha hao mawaziri na manaibu halafu kweli mnakuja singizia serikali 2. Huyo Mzee Mtei mwenyewe muulizeni alikuwa akichukua mshahara kiasi gani akiwa wazir wa fedha!..wabunge wetu mawaziri na kadhalika leo tuje singizia muundo wa serikali 2!

Na je tukiwa na serikali 3 nani ata control matumizi ya rais maana atakuwa ceremonial hiyo misafara ataipanga nani? Jamani mwee jaribuni kujenga hoja maana hatuwezi kuepuka matumizi ya serikali 3 kwa kurudia makosa yale yale ambayo hata hayo mambo 7 ndio yalomfanya rais kuwa John Mtembezi. Kwa nini asiwajibike, kwa nini kionmgozi yeyote wa bara ama viziwani awekewe kipimo cha Uwajibikaji ambacho kitaondoa rabsha hizi.

Mangapi tulowahi kuamua kwa fikra za kupingana na waasisi wetu kiasi kwamba kuna watu wanaamini HydroPower haitufai tena wakati ina uwezo wa kuzalisha mega watts 3,000 hivyo tumeiacha ife tukakimbilia Uzaklishaji wa gas kwa matumizi ya ndani. Matatizo ya umeme yako pale pale miaka nenda miaka rudi. Mabillioni yalojenga Hydro yamekufa wakati tunajua kabisa mitambo hiyo inazalisha chini ya kwango kutokana na kuto karabatiwa kwa miaka mingi hadi michanga imejaa. Sisi tumesingizia maji sasa maji yatakaa vipi ikiwa bonde limejaa michanga kama mto wa jangwani. Kama tungetaka mto wa jangwani uwepo tungeweza lakini badala yake tumefanya kila juhudi kuhakikisha bonde hilo linakufa ili tujenge nyumba za makazi.
Yaani hata sijui nianzie wapi na nimalizie wapi ili mnifahamu..
 
1.8 trillion. Na sehemu kubwa ya gharama hizi zitakuwepo hata Kama muungano utavunjika na kila upande kubeba mbao zake.


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mkuu nakuomba sana wewe na Nguruvi3, kina jassu na wengine msikilizeni hotuba ya mwalimu kwa makini isha jifikirieni nyie mmesimama wapi..Hotuba
 
Binafsi yangu hainishangazi hata kidogo kuona mchakato wa katiba umekwama na hakuna maelewano wala hayatakuwepo kwa sababu sisi wenyewe hapa JF ni reflection ya wajumbe wa baraza maalum la katiba, hatuelewani na wala hatutaelewana. Hivi Ndivyo Miafrika tulivyo na haishangazi hata kidogo kwa siku zote maisha yetu yapo katika majuto ni mjukuu. Hakuna swali hata moja lilopewa jibu, hakuna isipokuwa kuzungushana ati nenda kasome rasimu kana kwamba kule kuna majibu. Labda nyie wenyewe rudieni kuisoma rasimu kisha wekeni majibu mloyasoma maana mimi nimeuliza kutokana na rasimu yenyewe na kama unayajua majibu kuna tatizo gani kujibu.

Mimi nimechukua muda sana kutafakari swala hili na kukosa majibu ktk maswala ambayo nimeyaorodhesha hapo juu lakini badala ya watu kunipa majibu yamekuja maswali na maelezo ya kukebehi na kdhalika kwa sababu hata wao hawana majibu isipokuwa wanataka tu serikali 3 kwa sababu ya Ushabiki. Ni rahisi kabisa kujiuliza serikali yenye mambo 7 itakuwa ana bunge la aina gani? wabunge hao watatoka majimbo gani? na watazungumzia mambo yapi ktk maendeleo ya taifa zima.

Mimi sii mshabiki wa vyama wala sintokubali kuburuzwa na upande wowote isipokuwa kuelewa tunaingia ktk muundo ambao hautawagharimu wananchi walipa kodi. Hii habari ya kwamba fedha zipo hazina pasipo kujua hizo fedha ni kodi zenu na zipo pale kwa mautumizi ya mwaka huu ni upumbavu mkubwa kutumia sababu kama hizo kujenga hoja wakati leo hii hatuna serikali ya 3 wala fungu lilotengwa kwa minajiri hiyo. hata kama kuna surplus hazina bado haioneshi ni jinsi gani tutagharamia serikali hiyo kwa miaka 50 au 100 ijayo.

Wengine wamehoji kama nimeisoma rasimu ya katiba wakati wanajua fika kwamba rasimu hiyo haijakamilika, hata hiyo Sura ya sita ya rasimu inatoa tu mapendekezo ambayo ibara ya 2 na ya 3 zinazungumzia mihimili ya serikali hiyo pasipo namba za watumishi wake, muundo na madaraka ya serikali hiyo pia utategemea mamlaka ya serikali 2 za muungano (serikali ya Zanzibar na Ya Bara kufikia muafaka wake. Hakuna kikao chochote baina ya serikali ya bara wala visiwani (kwa sababu hazipo) walofikia kuanisha muundo na madaraka ya serikali hii ya 3 isipokuwa kuweka mambo 7 yatakayo kuwa na Muungano na rais ambaye hatakuwa na mamlaka juu ya mambo yasokuwa ya Muungano. Hivyo sio tu rais anaondolewa nguvu yake bali uanapunguziwa hata uwezo wa kuendesha nchi.

Ifahamike tu ya kwamba gharama za kuendesha serikali ni kodi za wananchi, huko hazina kuna makusanyo ya kodi kwa ajili ya matumizi ya serikali zilizopo na sii vinginevyo. Hata bajeti inaposomwa sio kwamba fedha hiz ziko hazina bali makadirio ya makusanyo na mapato ili kuweza kujenga matumizi ya mwaka unaofuata. Na kwa Zaidi ya miaka 20 serikali zetu hizi mbili zimekuwa zikitumia Zaidi ya makadirio, hivyo miaka yote kulikuwa na deficit iweje leo tuongeze serikali ya 3 ionekane rahisi kihivyo? Kwa gharama zozote zitakazo jitokeza ni kodi zenu wananchi ndizo zitaendesha serikali ya 3 hivyo ni muhimu wananchi wafahamu kwamba gharama za serikali ya 3 zitatoka mfukoni mwao na sii hazina maana kule hawavuni fedha.

Nitashukuru tu ikiwa kuna mmoja wenu ana majibu ya maswali nilouliza. Haya na Lipumba alisema nini ama Profesa Fulani hayajengi mjadala huu isipokuwa kuweka kiza zaidi. Maadam serikali ya Muungano itakuwa na serikali ya 3, itakuwa na bunge lake na mahakama yake ni lazima tujue kwanza muundo wa serikali hiyo na watumishi wake, gharama zake juu ya hizi zilizokuwepo. Kusema tu haitagharimu zaidi ni maneno tuloyazoea kwani misingi mingi ya mwalimu ilivunjwa huko nyuma na fikra kama hizi za ujuaji sana, lakini tumekuja kuyajutia na hatuwezi kurudi nyuma tena kusahihsiha. Hili ni moja kati ya hatari kubwa za sio tu kuuvunja muungano bali kuwepo maswali mengi yasiyokuwa na majibu sahihi lakini bado tunakazania iwe hivyo kwa sababu tu hatuipendi CCM. Sio kila alichokianzisha mwalimu kipigwe vita, hapana ni muhimu tuwe na majibu kamili kabla hatujachukua hatua zozote.

Kwa mfano Zanzibar ina watu mil.1.3 na bara tuna watu mil.45, ni kiasi gani cha kila serikali itachangia gharama za kuendesha serikali hii ya 3. Je, Tanzania bara itakuwa tayari kutoa asilimia 97.7 ya mchango wake kuendesha serikali hii ambayo kwa ujumla wake hawaihitaji? Tanzania bara na visiwani wakisha kuwa na serikali zao zenye mambo yoote makubwa isipokuwa saba ambayo wanaweza kuyaendesha wenyewe kwa nini kuwepo na Muungano? Kweli wananchi wa Tanzania bara wako tayari kugharamia asilimia hii ili kuuenzi muungano ambao ni gharama za ziada?

BAK, Ufafanuzi wa Lipumba ni maoni yake yeye ambayo sii rasimu hivyo kama wewe unayo mawazo hayo jenga hoja hapo nilipouliza kwa kuyajibu maswali yangu kupitia majibu yake. Jamani lini tutakuwa wakweli kwa nafsi zetu wenyewe? Kwa nini tunajenga mazoea ya Ubishi na hatutaki ku face ukweli pale tunapoona hatuna majibu? wewe nambie ulieweza nini kiasi kwamba unakubaliana na mapendekezo ya Lipumba na kama huyajui leo ina maana hujui..

ungefanya vema kama nawe ungeacha kuandika porojo bila kuonyesha japo kwa namba kile unachofikiri kitakuwa ndiyo ongezeko la gharama,
kama 30% ya bajeti yetu inaingia mifukoni mwa wachache huku tukiwa na serikali mbili ? gharama si jambo kubwa kuzuia muungano wa kweli.?
kwa nini tujikite kwenye serikali mbili au tatu na sio MOJA ? kisa ati kuenzi mauaji ya wasio hatia zanzibar myaitayo (mapinduzi)
 
Back
Top Bottom