Leo nikapita na movie ya kuitwa Custom Frontier toka huko Hong Kong. Picha linaanza tu! Nikaona bendera ya Tanzania, nikasema haa! Ina maana hii ngoma location yake ni TZ? Ila baadaye wakaitaja ile nchi ni Jamhuri ya Loklamoa.
Nkajiuliza, ina maana kuna nchi inaitwa Loklamoa na ina bendera inakaribia kufanana na ya TZ? Uvumilivu ukanishinda, nikastopisha muvi, nikaenda kugogo. Majibu yakaja kuwa hiyo ni nchi ya kubuni tu lakini kiundani walielezea nchi inayopatikana Afrika Mashariki. So, moja kwa moja nikajua wameamua kuitumia TZ lakini kama nchi ya kubuni tu. Sijui walikuwa hawana hela ya kuja huku au ndo vile tena, kile walichoigiza hakiendani na mazingira yetu.
Basi stori ya humu ni kama huu mgogoro wa Israel na Palestina tu. Nchi kama Israel ina silaha kali, inaipiga Palestina. Na Palestina sasa waamue kutafuta silaha kali kujibu mashambulizi. Basi na stori ipo hivyo. Jamhuri ya Loklamoa inapigwa na jirani yake nao wanatafuta silaha kujibu mashambulizi. Ndipo wanadondokea kwa mfanyabiashara wa Hong Kong ambaye anachukua almasi za Loklamoa halafu analeta silaha.
Sasa wale polisi wa Hong Kong ambao ndo hawa Custom Frontier, wanaingilia kati kuzuia usambazaji haramu wa silaha.
Nzuri kuitazama. Haina mbwembwe. Full nazi, full mijegejo.
nmeikuta sehemu nmeona nilete na humu
View attachment 3521402