Sensa 2012: Yanayojiri

Sensa 2012: Yanayojiri

Binafsi sioni umuhimu wa sensa,naomba serikali katika form zao zote waondoe vipengele vya makabila,dini.mfano katika nyumba za wagen,form za ajira(mikataba)polisi nk...huwa nachukia sana ninapo pewa form yoyote nikakuta hivyo vipengere.........?serikali imejianda miaka kumi katika swala la sensa bado limefeli...limeshindwa kulipa makalani kwa wakati hii ni haibu kwa serikali ya chama cha mapinduzi...madr,waalimu imeshindwa mpaka makalani wa sensa...inawalipa nusunusu...makalani wanavunjiana penseli.kapelo,vitambulisho hakuna....matangazo yanasema makalani watakuja na wamevaa sare,vitambulisho,hakuna chochote mimi nipo kigoma kskazin-mkigo
Nashangaa serikali iliwapa wabunge wote milioni moja moja kwa ajili ya kuamasisha sensa nashangaa sijawaona majimboni au wao wataisabiwa wapi?:spy:
 
Sensa ya mwanzo ya Tanzania huru iliyoungana iifanyika mwaka 1967 na hii ilikuwa ni sensa ya mwisho kuuliza swali la dini. Sensa zilizobaki zilifanyika mwaka 1978, 1988 na 2002. Sensa ya mwaka huu, 2012 itakuwa ni ya saba katika historia ya nchi yetu na ya tano ya Tanzania huru iliyoungana.

Sensa ya mwisho ya Tanganyika chini ya mkoloni wa Kiingereza katika mwaka 1957 ilionyesha kuwa Tanganyika ina Waislamu 58%, Wakristo 32% na Wapagani 10%. Uwiano kati ya Waislamu na Wakristo ilikuwa ni karibu 2:1 yaani kila penye watu watatu, 2 ni Waislamu na 1 ni mkristo, vile vile unaweza kusema waislamu walikuwa ni karibu mara mbili ya wakristo kiidadi Tanzania.

Mwaka 1967 ndio uliotoa matokeo ya ajabu ambayo mpaka leo sio tu Waislamu bali mtu yoyote aliye na akili timamu ana haki ya kuhoji matokeo hayo. Matokeo haya yalionyesha mgawanyiko wa kidini kama ifuatavyo: WAKRISTO: 33.5% yaani wameongezeka kwa 1.5% kulinganisha na sensa ya 1957. WAISLAMU: 31.4% yaani wamepungua kwa 26.6% katika kipindi cha miaka 10 tu. Hii haikuwahi kutokea sehemu yoyote Duniani iwapo sehemu hiyo haikukabiliwa na janga kama vile vita au jambo lolote lilisababisha idadi kubwa ya watu kufariki. Hata china ambayo imeweka sheria ya kuzaa mtoto mmoja tu basi haikuwahi kupungikiwa na watu au kundi fulani la watu katika nchi yao. WAPAGANI: 34.3% yaani wameongezeka kwa 24.3% kwa kipindi cha miaka 10.

Haya nayo ni maajabu, yaani unaweza ukadhani labda Tanzania ina tatizo la Waislamu kuwacha dini yao na kuwa wapagani. Hili nalo halina ushahidi wowote kuwa lilitokea katika kipindi hicho.

Hayo siyo maajabu, mnashindwa kuelewa kwamba wakristu waliachiwa kazi moja tu na YESU, "kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi" yaani kuhubiri injili na kuwaleta watu kwa YESU na wamekuwa wakiweka mipango yao vyema katika kutekeleza agizo hili. Katika miaka unayoeleza kuna uwezekano mkubwa wa uamsho mkubwa ulitokea na kuwafanya waislamu wengi kumgeukia YESU. Hata hivyo ni vyema kufahamu kwamba imani ya mtu yaweza kubadilika wakati wowote kulingana na vile atakavyo hubiriwa na kuamini, MKRISTO aweza kuamua kusilimu na kuwa mwislamu au MWISLAMU anaweza kubatizwa na kuwa mkristo na hiyo ni haki ya kila mmoja, huwezi kumlazimisha mtu kubaki na imani unayoamini wewe kwamba ndio sahihi, ndio maana kuna uwezekano mkubwa watu wengi katika nchi yetu hujiita WAKRISTO au WAISLAMU kwa sababu za kijamii na sio kwamba anaamini. Hivyo basi kuna uwezekeno mkubwa takwimu za kiimani kubadilika kwa kiwango kikubwa kulingana na wakati, jaribu kuangalia kwa kiwango gani katika miaka ya 2000 kumekuwa na uamsho mkubwa kwa wakristo katika kueneza injili na makanisa mengi makubwa kujengwa kama FULL GOSPEL (Kakobe), hawa wamekuwa na mkakati wa kuhakikisha wanakuwa na washirika na makanisa katika kila eneo, MWINGIRA...., NGURUMO YA UPAKO...., N.K. Hivyo basi ingekuwa busara zaidi kwa waislamu kuweka mikakati katika kueneza imani yao kwa njia ya amani, ili kadri miaka inavyosonga waweze kupata wafuasi wengi kuliko kubaki kung'ang'ania takwimu hizo za mwaka 1957.
 
JINSI ZOEZI LA SENSA LILIVYO POKELEWA KWA HISIA TOFAUTI


Publication1.jpg


MWAKA HUU TUTAONA MENGI NA KUSIKIA MENGI

sina uhakika kama watu wameelimika na kujua maana ya sensa ni nini.
Kama umefuatilia babu akiojiwa ITV- Babu baada ya Mahojioano na watu wasensa umejisikiaje? Jibu la Babu; Sijajisikia lolote kwani bado nasikia homa iko palepale
 
Zoezi la sensa linaloendelea kuanzia jumapili tarehe 26\08\2012 limekumbwa na changamoto na mkanganyiko mkubwa.Ikiwemo swala laudini kutoka upande wa Waislam,upungufu wa zana za utendea kazi n.k.Hilo la mwanzo la udini kwa baadhi ya waislamu kususia na kueneza kampeni za kususia zoezi hili muhimu kwa taifa,ni pigo kwa Mh.JK,CCM na serikali kwa ujumla.Haya ni matunda za siasa za chama tawala CCM baada ya kukosa sera na kuanza kupandikiza sera za udini na ukabila.Kwa upeo wao mdogo hawakujua ya kua hili linaweza kuligharimu taifa makubwa.Mkanganyiko katika zoezi la sensa kwa wWaisalam wengi kuiigomea ni mfano mmoja,swala hili kama alitatizamwa kwa undani linaweza likaleta madhara makubwa kwa taifa hapo baadae.MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Hayo siyo maajabu, mnashindwa kuelewa kwamba wakristu waliachiwa kazi moja tu na YESU, "kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi" yaani kuhubiri injili na kuwaleta watu kwa YESU na wamekuwa wakiweka mipango yao vyema katika kutekeleza agizo hili. Katika miaka unayoeleza kuna uwezekano mkubwa wa uamsho mkubwa ulitokea na kuwafanya waislamu wengi kumgeukia YESU. Hata hivyo ni vyema kufahamu kwamba imani ya mtu yaweza kubadilika wakati wowote kulingana na vile atakavyo hubiriwa na kuamini, MKRISTO aweza kuamua kusilimu na kuwa mwislamu au MWISLAMU anaweza kubatizwa na kuwa mkristo na hiyo ni haki ya kila mmoja, huwezi kumlazimisha mtu kubaki na imani unayoamini wewe kwamba ndio sahihi, ndio maana kuna uwezekano mkubwa watu wengi katika nchi yetu hujiita WAKRISTO au WAISLAMU kwa sababu za kijamii na sio kwamba anaamini. Hivyo basi kuna uwezekeno mkubwa takwimu za kiimani kubadilika kwa kiwango kikubwa kulingana na wakati, jaribu kuangalia kwa kiwango gani katika miaka ya 2000 kumekuwa na uamsho mkubwa kwa wakristo katika kueneza injili na makanisa mengi makubwa kujengwa kama FULL GOSPEL (Kakobe), hawa wamekuwa na mkakati wa kuhakikisha wanakuwa na washirika na makanisa katika kila eneo, MWINGIRA...., NGURUMO YA UPAKO...., N.K. Hivyo basi ingekuwa busara zaidi kwa waislamu kuweka mikakati katika kueneza imani yao kwa njia ya amani, ili kadri miaka inavyosonga waweze kupata wafuasi wengi kuliko kubaki kung'ang'ania takwimu hizo za mwaka 1957.

Hizo ni nadharia zako za kufikirika kaka, be analytic uwe kama GT! Unasoma lakini huelewi ni kwamba hicho kitu hakijawahi kutokea duniani pote!

Umeambiwa baada ya sensa ile na kuleta maswali mengi Nyerere aliamua kipengele cha dini kiondolewe mwaka 1978! Hakikuondolewa kwa makusudi kaka kwani ilishadhihirika kuwa Waislamu idadi yao ni kubwa na ingekuwa shughuli kwani waliofanya kusudi hiyo ya kupotosha takwimu walikuwa na uhakika wa kuteka asilimia 100 ya saikolojia ya walimwengu juu ya uwiano pogo wa kielimu na kimadaraka baina ya watu wa makundi ya dini iwapo sensa ingeficha utambulisho wa dini ili isijulikane Waislamu wako wangapi Tanzania.
Kwa upande mwingine, upotoshaji wa takwimu kuwa Wakristo ndio wengi nchini ulilenga, pamoja na mambo mengine, kuhalalisha dhulumu ya kimfumo dhidi ya Waislamu katika maeneo ya elimu na ajira za utumishi wa umma hasahasa katika ngazi za juu. Kwamba, wingi wa Wakristo katika maeneo hayo ni matokeo ya ukubwa wa idadi yao kulinganisha na makundi mengine ya jamii.
Ni hoja nyepesi kung’amulika kwamba kama wasingetoa takwimu za kuonesha kuwa Wakristo ndio wengi nchini, wabunifu na waasisi wa mfumo kandamizi wa kidini kwa misingi ya kisiasa wangeyajibu vipi maswali haya; ‘mbona Waislamu ni wachache katika maeneo hayo? Je wingi wa Wakristo mashuleni, vyuoni na madarakani umetokana na nini?
Mwanzo, ilidaiwa kuwa mfumo wa Kikoloni uliwabana Waislamu kielimu kwa sharti la kuritadi ili wapewe elimu, sawa kabisa, mtu angekubali kuwa katika miaka ya awali ya uhuru nafasi za madaraka zingejazwa na Wakristo waliopendelewa kielimu na mkoloni.
Lakini hoja ambayo ingewashinda Wabunifu wa mfumo wa dhuluma ni kwamba mbona hata baada ya uhuru Waislamu wameendelea kuwa wachache katika nyanja za elimu? Kama nyuma kulikuwa na sharti la kubatizwa, je baada ya uhuru sharti hilo lilikuwepo? Lakini bado hilo nalo lingesutwa na idadi ya watoto wa Kiislamu katika shule za msingi.
Waislamu waliandikisha watoto wao kwa wingi katika ngazi ya msingi nchini kote. Sasa, swali lingekomaa zaidi, kwa nini Waislamu waendelee kuwa wachache hata baada ya miaka mingi ya uhuru? Ni wazi mfumo wa dhuluma ungebainika kirahisi.

Ndio maana waasisi wake wakawa makini na sensa ya Taifa ili wajenge hoja ya jumla kuwa Waislamu ni wachache katika nyanja za elimu na madaraka kwa sababu jamii yao ni ndogo kama zilivyo jamii za watu wa makundi mengine madogo.

Na Wakristo ni wengi kwa sababu wao ndio wanaounda asilimia kubwa ya Watanzania. Angalau kwa kuficha takwimu za Waislamu walijiridhisha kuwa dhuluma waliyowafanyia Waislamu ingehalalika kwa mdadisi au mtafiti yeyote yule ambaye angetaka kuhoji kwa nini Waislamu ni wachache madarakani?



 
Baada ya kushangilia sensa kwa mbwembwe na kudhani wanawakomoa waislam, wameanza kula kichapo morogoro! kweli JK ni zaidi ya mwanasiasa.
 
[h=6]Waislam waandamana Mjini Bukoba wapo Mahakama kuu kushinikiza wenzao waliokamatwa kwa kugomea sensa waachiwe.[/h]
 
ALHAMDULILAHI. NIMEFAULU MTIHANI WA IMANI YANGU. NASHUHUDIA KUA HAPANA MOLA APASAE KUABUDIWA KWA HAKI ISPOKUA ALLAH(S.W) NA MTUME MUHAMAD (S.A.W) NI MJUMBE WAKE. LEO TAREHE 26 August,2012, mida ya 11:57 jioni, nimekataa kuandikishwa katika SENSA. NA AHIDI KUA NITABAKIA MUISLAMU MTIIFU KWA MOLA WANGU, NA VIONGOZI WENYE MAMALAKA MIONGONI MWETU SISI WAISLAMU. NIKOTAYARI KUITUMIKIA DINI YANGU YA KIISLAMU WAKATI WOWOTE NA MAHALA POPOTE NITAPO HITAJIKA. SIO GOPI MANENO WALA RISASI ZA MOTO. KILA NAFSI ITAONJA MAUTI. RABI TAKABALI.
tuko pamoja mkuu nipo radhi waniuwe lakini sio kuhesabiwa, ALLAH AKBAR, ALLAH AKBAR, ALLAH AKBAR
 
Jibu ni hakuna na hakuna kwasababu swali lako linajibu kuwa Sensa ya mwisho ya Tanganyika chini ya mkoloni wa Kiingereza katika mwaka 1957 ilionyesha kuwa Tanganyika ina Waislamu 58%, Wakristo 32% na Wapagani 10%. Uwiano kati ya Waislamu na Wakristo ilikuwa ni karibu 2:1 yaani kila penye watu watatu, 2 ni Waislamu na 1 ni mkristo, vile vile unaweza kusema waislamu walikuwa ni karibu mara mbili ya wakristo kiidadi Tanzania.

Sidhani kama sensa hii iliwafikia ''Watanganyika'' wote
 
Waislam waandamana Mjini Bukoba wapo Mahakama kuu kushinikiza wenzao waliokamatwa kwa kugomea sensa waachiwe.
Kesi ya kuku ipelekwe Mahakama kuu!? No way i don't trust you @ all.
 
...Sensa ya mwisho ya Tanganyika chini ya mkoloni wa Kiingereza katika mwaka 1957 ilionyesha kuwa Tanganyika ina Waislamu 58%, Wakristo 32% na Wapagani 10%.
...Sensa ya 1967 ilipokuja na takwimu WAKRISTO: 33.5% yaani wameongezeka kwa 1.5% kulinganisha na sensa ya 1957. WAISLAMU: 31.4% yaani wamepungua kwa 26.6% katika kipindi cha miaka 10 tu.
Ni kweli kuna tofauti kubwa ya idadi ya waumini wa dini hizo kati ya mwaka 1957 na 1967. Lakini inavyoonekana hapa ni kwamba waisilamu wanaamini kwamba sensa ya mwaka 1957 ndio yenye takwimu sahihi na ya 1967 haina takwimu sahihi. Mimi swali langu ni hili; je, haiwezekani kuwa kinyume chake; kwamba sensa ya mwaka 1967 ndio yenye takwimu sahihi na ya 1957 haina takwimu sahihi? Kama wanafunzi wawili wamekosa jibu la swali moja katika mtihani, iweje mmoja ang'ang'anie kwamba jibu la mwenzake sio sahihi (huku hata yeye akiwa amekosa)? Wanaojenga hoja kwa misingi ya sensa za 1957 na 1967 nashindwa kuwaelewa. Kama mtu ana nia hasa ya kujua idadi ya waumini, aangalie mchanganyiko wa sample mbalimbali kwenye makundi kadhaa ya kijamii, maybe atapata idea!
 
Nadhani zile kodi zetu zilizowapa posho hao watu wa sensa zimeenda bure.Maana nakaa hotelini kaja muhesabu sensa bahati mbaya akanikosa ikabidi ampe mlinzi taarifa kuwa nitakapotokea aniulize jina langu kamili ,Umri na uraia ,halafu asubuhi atapitia hizo details.

Sasa nikamuuliza mlinzi hivi, nikitoka hapo nje nikapigwa,kuporwa au kuumizwa nani wa kwanza kuulizwa?Akanijibu ni yeye (mlinzi) ,nikamuuliza sababu,akanijibu ninadetails zako zote.

Nikamalizia kwa kumuuliza hivyo inamaana huna haki ya kujua details hizo sababu wewe siyo afisa wa sensa na wala hautambuliki akasema ndio.

Nikamweleza tu wakija waambie amekataa kutoa details zake. Sasa jamani hebu nipeni taarifa maana huku niliko ni kijijini haswa,je, hili zoezi la safari hii ndiyo walivyoambiwa kwenye semina?Kama siyo,ina maana ripoti ya hiyo sensa haitakuwa na ukweli kwani data zitakuwa zimepikwa.
 
mohamed Shossi,

Hizo takwimu za uongo ndio zimekuwa zikitumiwa katika uteuzi na maamuzi kama ilivyo elezwa kuwa Tanzania haiwezi kujiunga na Jumuiya ya Kiislam ya OIC kwa sababu raia Wakiristo ni wengi kuliko Waislam.

Hizo takwimu za uongo ndio zimefanya hata serikali Wakiristo ni wengi...Wakuu wa Wilaya wapo 133. Waislam 42 Wakiristo 91 Mawaziri Waislam 9 Wakiristo 21. Manaibu Waislam 8 Wakiristo 17.

Hii nchi tunapoelekea tutakuja kupigana mitutu siku moja.
 
Last edited by a moderator:
Kwanza kero sasa hivi ni nyingi hata makelele ya maimamu kwenye maspika yao usiku kucha ni kelele, napendekeza misikiti yote iwekewe sound proof.
Tayari nchi inapita katika msukosuko wewe nawe unataka kuongeza balaa jingine, kwa nini usipendekeze kuwa Wakristo wasihamie katika miji ya Waislamu ambapo watakwepa kusikia sauti za adhana kila siku?

Juzijuzi mlikuwa na pendekezo la kutaka machinjioni pia wawepo Wakristo, liliishia wapi hili?......
kusanyeni mapendekezo yenu yote kwa pamoja na sisi Waislamu tuna mlolongo wa mapendekezo yetu pia.Halafu tuone kama mwisho wa siku kama kila mtu hatabakia kwake.
 
[JFMP3][/JFMP3]Mbona Mimi hawaji kunihesabu??? Ikifika kesho saa 12 jioni Kama sijahesabiwa nakata rufaa sensa irudiwe wallah!
 
Ni kweli kuna tofauti kubwa ya idadi ya waumini wa dini hizo kati ya mwaka 1957 na 1967. Lakini inavyoonekana hapa ni kwamba waisilamu wanaamini kwamba sensa ya mwaka 1957 ndio yenye takwimu sahihi na ya 1967 haina takwimu sahihi. Mimi swali langu ni hili; je, haiwezekani kuwa kinyume chake; kwamba sensa ya mwaka 1967 ndio yenye takwimu sahihi na ya 1957 haina takwimu sahihi? Kama wanafunzi wawili wamekosa jibu la swali moja katika mtihani, iweje mmoja ang'ang'anie kwamba jibu la mwenzake sio sahihi (huku hata yeye akiwa amekosa)? Wanaojenga hoja kwa misingi ya sensa za 1957 na 1967 nashindwa kuwaelewa. Kama mtu ana nia hasa ya kujua idadi ya waumini, aangalie mchanganyiko wa sample mbalimbali kwenye makundi kadhaa ya kijamii, maybe atapata idea!
Nakubaliana na wewe 100%. Unajua sisi tatizo letu ni ELUMU sii Waislaam wala Wakristu na ujinga huu ndio umepelekea kufika hapa tulipo. Hakuna uhakika wa takwimu zote zilizowahi kutolewa nyuma na kibaya zaidi tumeendelea kuamini kwamba tofauti zetu za kiimani zinaweza kusababisha UDINI kumbe kutokuwa na taarifa hizo ndiko kunajenga Udini zaidi.

Binafsi yangu sikubaliani na dhana ya baadhi Waislaam inayotafsiri kitendo cha Nyerere kuondoa kipengele cha imani ya dini ktk sensa. Yeye kama Mjamaa na mtu alotaka kujenga taifa moja lenye kuondoa tofauti zetu alifanya hivyo makusudi na kuhakikisha kwamba ni jukumu la serikali yake kupeleka maendeleo moja kwa moja kwa wananchi na ndio maana alitaifisha shule na hospital zote za dini akaacha zile za watu binafsi ili serikali ndiyo ipeleke huduma hizo kwa wananchi. Serikali ikawa ndiye mgawaji (sole supplier) wa vitu hivyo..Hivyo mfumo wake uliendana na dhamira yake na akaweka uzalishaji na usambazaji kuwa chini ya serikali..

Tatizo la leo lilofikia mimi kupingana na sensa hii ni kwa sababu vita hii muhimu ktk maendeleo ya WATU maskini vimerudishwa ktk mikono ya watu binafsi na hasa vyombo vya dini (kurudisha utengano), hivyo serikali ya Mwinyi, Mkapa na JK zote hazina mamlaka moja kwa moja na usambazaji wa Elimu na Afya kwa wananchi isipokuwa kuviwezesha vyombo na asasi mbali mbali kushiriki ktk kusambaza huduma hizi.

Hapa ndipo matatizo yanapoanzia, maana unapokataza Udini ni muhimu zaidi kufikiria utaweza vipi kuwahudumia wananchi wote sawa pasipo kupendelea. Maadam tumeondokana na Ujamaa wa Nyerere, hii dhana ya kujenga Taifa la Ujamaa na Kujitegemea wakati tunatumia sera za Kibepari, lazima pia iondoke kwa sababu tumerudisha mamlaka hayo mikononi mwa wananchi na kwa bahati mbaya tumerudisha mfumo wa kikoloni ulowadhalilisha Waislaam kabla ya Uhuru..

Leo tunawawezesha Matajiri wakati Wakulima na Wafanyakazi wakikwazwa halafu mnataka sisi tunamini kuwa nchi hii ni ya Wakulima na wafanyakazi?. Tupeni hesabu ya Wakulima na Wafanyakazi nchini halafu tuone juhudi zinazofanywa kuwaendeleza hapo ndipo tutaweza kupima maendeleo yao. Je ni wakulima na wafanyakazi kiasi gani wametoka ktk umaskini?. Kiasi gani wanategemea kilimo, na wafanyakzi wangapi hawana ajira ktk fani zote mbili. Kujua idadi ya wafanyakazi haina maana unajenga uhasama baina ya wenye kazi na wasiokuwa na kazi ama wafanya biashara, huu ni ujinga mwingine.

Matokeo ya mfumo huu mbovu uliopo, umerudisha Udini nchini na ipo kila sababu ya wananchi kuhesabiwa kwa dini, makabila, jinsia ili vyombo vya kidini na asasi tofauti zipate kuwa na takwimu kamili zitakazo wawezesha kusambaza huduma hizi kw awalengwa. Lazima tukubali yao makabila yanayosahaulika leo tofauti na wakati wa Nyerere na tumeendelea kutumia siasa za Ujamaa na Kujitegemea wakati tukitumia mbinu za kibepari kk maendeleo ya Kiuchumi..

Huwezi kuogopa kuwahesabu Waislaam na Wakristu kwa kuchelea Udini wakati tayari umesha ruhusu Utandawazi na soko huria kama ndizo njia za kukuza Uchumi. Leo shule na Hospital za Wakristu zinashirikiana na serikali kutoa huduma hizi wakati waislaam wameachwa nje, hii inatupa fursa sisi kujiuliza kama we are the minority or second citizen. Huwezi kusimamisha USAWA mahala ambapo hakuna HAKI kwa kutumia UHURU kuficha ukandamizaji wa wazi.

Nitarudia kusema UHURU, HAKI na USAWA ni vitu vinaendana sambamba huwezi kuacha kimojawapo kwa kuchelea matokeo wakati tupo ktk mfumo wa kibepari ambao unawapa nafasi na fursa wananchi wenyewe kusimamia uzalishaji na usambazaji wakati serikali ikijenga sera (policies na mikakati) kuwawezesha wananchi hao kuzalisha na kusambaza kulingana na mahitaji yao. Tusidanganyane, tunaweza kuwa wajinga lakini sii wajinga hivyo!.. Serikali haipeleki maendeleo kwa wananchi moja kwa moja ktk ubepari bali inawawezesha wananchi wake kwa sera na mikakati bora ili wao kujipatia maendeleo na ndio maana inakusanya kodi toka kwa wananchi..
 
Back
Top Bottom