Sensa 2012: Yanayojiri

Sensa 2012: Yanayojiri

Hayo ya lugha mbona wengine hatukuulizwa? Mtaalam wa sensa atusaidie kwa hili...

Mkuu kama hukuulizwa swali la kujua lugha ngapi basi amini kwamba hii sensa inaendeshwa kama COMEDY!! Swali hilo lipo Mkuu inaonesha M-sensishaji alikuwa amechoka hivyo akamua kuchakachua maana si unajua kwenye survey huwa kuna kujijazia tu ili kutimiza wajibu wa kumaliza madodoso!!!??

Pole sana Mkuu ndo sensa yetu hiyo! Serekali Legelege, sensa legelege, chama legelege sasa sijui tutafika kweli???
 
Kama hukumwelekeza mwanao kufanya hiyo kazi, hayo majibu ameyatoa wapi.Kama wasen sishaji wameridhika na majibu yake na hukumtuma basi shukuru Mungu umepata kichwa nyumbani kwako na hilo sio la ajabu sana kwa mazingira ya bongoland.
 
Yaani TZ usanii kila mahali. Na mwisho wa siku bajeti ya kutengeneza hayo madodoso ni mabilioni na mengi ya hayo madodoso ni hewa
 
Yaani TZ usanii kila mahali. Na mwisho wa siku bajeti ya kutengeneza hayo madodoso ni mabilioni na mengi ya hayo madodoso ni hewa
USANII mtupu! Unaulizwa maswali yakiwa mengi hayazidi 7! Kweli tumedhamilia kufanya sensa kwa ajili ya mipango ya maendeleo??!!1.Unaitwa nani?2.Unamiaka mingapi?3.Ulizaliwa wilaya gani4.Ulizaliwa Mkoa gani?5.Kiwango chako cha elimu?6.Kazi yako?7.Sijui mengine watajibu wenyewe kwa niaba ......!?Imeniacha hoi, sijui kwa taarifa hizi fupi wanakusudia kupata nini..duh!
 
USANII mtupu! Unaulizwa maswali yakiwa mengi hayazidi 7! Kweli tumedhamilia kufanya sensa kwa ajili ya mipango ya maendeleo??!!1.Unaitwa nani?2.Unamiaka mingapi?3.Ulizaliwa wilaya gani4.Ulizaliwa Mkoa gani?5.Kiwango chako cha elimu?6.Kazi yako?7.Sijui mengine watajibu wenyewe kwa niaba ......!?Imeniacha hoi, sijui kwa taarifa hizi fupi wanakusudia kupata nini..duh!

Yaani haya mabilioni nafuu yangetumika kujenga kituo cha kuzalisha umeme wa gesi ili tuwaondoe Symbion ingekuwa na maana zaidi na ingesaidia kuleta maendelao kuliko huu usanii usiokuwa na tija kwa taifa.
 
Nipo kijiji cha mpunguzi manispaa ya Dodoma ambapo kabla sijafika hapo nimepitia pia vituo vya Matumbulu, Mkulabi na Bihawana, kote huko nimekuta makarani wa sensa wamekaa chini baada ya kuishiwa madodoso ili hali nyumba nyingi bado hazijahesabiwa.

pia nimekuta makarani wengi wakiwa hawana sare wala kofia za sensa na nilipo wahoji kwa masharti ya kutotajwa majina yao walisema kwa masikitiko kuwa
1: hata penseli za huandikia imebidi wavunje kati ili wagawane kazi iende
2: hawana chaki ya kutikia milango iliyohesabiwa hali iliyosababisha watumie mkaa ku mark milango.
3: wamewasiliana na msimamizi mkuu wa mkoa, amewajibu kuwa hata mkoani wameishiwa dodoso na vifaa, hivyo amewataka wasubiri waagize Dar es Salaam.

My take:
Kama serikali ilikuwa haijajipanga kwa nini waliitisha sensa? Kwa hali hii sidhani kama idadi itakayopatikana itakuwa sahihi...

NAWASILISHA
 
Hilo linaonyesha dhahiri serikali tawala ilivyo legelege na DHAIFU kama alivyosema Pm wao ya kwmb LIWALO na LIWE!

Safi sanaaaaa!!
 
sio huko tu,hata mpwapwa,leo ni siku ya 3 hawafanyi kazi,kwa mfano mtu kapewa kaya 49 kuhesabu lakini amepewa makaratasi 10 tu.sasa tangu miaka 10 imepita kulikuwa hakuna maandalizi?

tunashukuru baadhi ya maeneo sensa yaenda vyema
 
sio huko tu,hata mpwapwa,leo ni siku ya 3 hawafanyi kazi,kwa mfano mtu kapewa kaya 49 kuhesabu lakini amepewa makaratasi 10 tu.sasa tangu miaka 10 imepita kulikuwa hakuna maandalizi?

tunashukuru baadhi ya maeneo sensa yaenda vyema
Poleni sana ,ndio mambo ya dhaifu hayo
 
sio huko tu,hata mpwapwa,leo ni siku ya 3 hawafanyi kazi,kwa mfano mtu kapewa kaya 49 kuhesabu lakini amepewa makaratasi 10 tu.sasa tangu miaka 10 imepita kulikuwa hakuna maandalizi?

tunashukuru baadhi ya maeneo sensa yaenda vyema
mkuu napata wasiwasi kama takwimu za sensa hii zitakuwa sahihi.
 
Mkuu siyo dodoma tu hata huku Arusha baadhi ya makarani hawana nilipowauliza ni nini sasa kinaendelea waliambiwa madodoso yamefuatwa dar es salaam kwa ndege na yatafika saa sita mchana cha ajabu mpaka nawasiliana na makarani jioni hii wanasema hawajaletewa hayo madodoso na wala hawana taarifa yoyote
 
Uke wako kama umeoa ana rangi gani, umewahi kutoka nje ya ndoa au?,unatumia kondomu au? Hela ya chakula unaacha kiasi gani nyumbani?
 
Itakuwa wamemuuzia Dr. kingwangala akiwa anatoa Rushwa ya Vitumbua wawe wanafungia hayo madodoso ya Sensa
 
Ni siku saba za kuhesabu Sensa, Hiyo Matumbuli imeshahesabiwa na Msimamizi ni Mtendaji wa Kata moja hapa mjini kanihakikishia tatizo hilo hakuna na Dodoso hazijafungiwa vitumbua.
Tatizo la sare lilishatatuliwa na sio lazima wavae, kweli hazikutosha na wananchi wa vijiji vya Matumbulu, Mpunguzi, Nkulabi na Chibelela kesho watamaliziwa wote
 
Hata huku Kilimanjaro vimekwisha, kuna jamaa hapa wanasema kesho hawataweza kuendelea na zoezi hilo
 
Wewe Ukwaju ni muongo na Mzushi mkubwa, nina shaka wewe utakuwa ni mmoja wa wadhaifu.Ukweli ni kwamba vifaa hakuna hata hapa Dodoma mjini hakuna na kama unakumbuka mimi jana nilizungumza kuhusu hilo na wenye akili timamu wote walielewa isipokuwa wewe tu ambae ni dhaifu
 
Hata huku Kilimanjaro vimekwisha, kuna jamaa hapa wanasema kesho hawataweza kuendelea na zoezi hilo
mkuu vifaa hakuna ,simu imepigwa mkoani nikiwepo makarani wameambiwa wangoje viagizwe dar coz dodoma mjini kote vimeisha.
 
Back
Top Bottom