Sensa 2012: Yanayojiri

Wewe Ukwaju ni muongo na Mzushi mkubwa, nina shaka wewe utakuwa ni mmoja wa wadhaifu.Ukweli ni kwamba vifaa hakuna hata hapa Dodoma mjini hakuna na kama unakumbuka mimi jana nilizungumza kuhusu hilo na wenye akili timamu wote walielewa isipokuwa wewe tu ambae ni dhaifu
naungana na wewe kaka, baada ya kupata hii habari nimewasiliana na jamaa hapa manispaa wamesema ni kweli TOOLS DOWN, vifaa hakuna mkoani wameagiza dar
 
Kwa nini dodoma vifaa viishe? isije ikawa hawa magamba wamepanga waharibu sensa dom makusudi ili idadi ya watu iwe feki wachakachue vizuri daftari la kudumu la wapiga kura? WAPI GREAT THINKERS
 
Ni siku saba za kuhesabu Sensa, Hiyo Matumbuli imeshahesabiwa na Msimamizi ni Mtendaji wa Kata moja hapa mjini kanihakikishia tatizo hilo hakuna na Dodoso hazijafungiwa vitumbua.
Tatizo la sare lilishatatuliwa na sio lazima wavae, kweli hazikutosha na wananchi wa vijiji vya Matumbulu, Mpunguzi, Nkulabi na Chibelela kesho watamaliziwa wote
kaka usichukulie rahisi hivyo, fikiria umehamasishwa na balozi wa mtaa kuwa kesho usiende shamba utapitiwa kuhesbiwa ,halafu jamaa wanakuja wanakwambia hawana karatasi, ukizingatia huu ni msimu wa kutayarisha mashamba (kubelega): pia wakazi wengine ni wafanyabiashara ya zabibu kusafirisha, unadhani hawa watasubiri vifaa?
 
Wewe Ukwaju ni muongo na Mzushi mkubwa, nina shaka wewe utakuwa ni mmoja wa wadhaifu.Ukweli ni kwamba vifaa hakuna hata hapa Dodoma mjini hakuna na kama unakumbuka mimi jana nilizungumza kuhusu hilo na wenye akili timamu wote walielewa isipokuwa wewe tu ambae ni dhaifu
Kila Mkazi wa Dodoma aliyesahauliwa leo Jumatano atahesabiwa, hilo shaka ondoa, na ni vifaa gani unavyovitaja hakuna? karatasi za dododso au pencil, mavazi si hoja na hata huko Matumbulu watu ni waelewa sana, inachotakiwa ww acha maagizo aliyebaki nyumbani awataje waliolala hapo tarehe 25 kuamkia 26/06/2012. kama kuna ka mgomo kwa waandikishaji hatujakasikia wakazi wote wanahesabiwa chini ya M<abalozi na Wenyeviti wa Mitaa, kwa wale waliosahauliwa wanapitiwa tena
 
*dodoma makarani wakosa vitambulisho, madodoso
*singida nako wakosa vitendea kazi na kofia
*dar makarani watishia kugoma, kisa posho
*jk, dk. Bilal, maalim seif, dk shein wahesabiwa

sensa ya watu na makazi iliyoanza jana nchini kote, iliingia dosari baada ya kutawaliwa na kasoro mbalimbali. Taarifa zilizopatikana jana kutoka katika maeneo mbalimbali nchini, zilisema baadhi ya makarani hawakuwa na vitendea kazi na hivyo kufanya kazi kwa wasiwasi wakihofia kutoaminika kwa wananchi.

Taarifa zilizopatikana kutoka mkoani dodoma zinasema kuwa, zoezi hilo la sensa lilikumbwa na dosari baada ya baadhi ya makarani kulalamika kutopewa vitambulisho.

Mbali na vitambulisho, makarani hao wamedai kuwa na uhaba wa madodoso hali iliyosababisha baadhi yao kupewa madodoso machache.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, baadhi ya makarani hao walisema kuwa, hali hiyo inaweza kusababisha washindwe kufanya kazi hiyo ya kuhesabu watu kwa ufanisi kutokana na kutoaminika kwa baadhi ya wananchi.

Akizungumza kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini, mmoja wa makarani katika kata ya hombolo, alisema hadi jana alikuwa hajapata kitambulisho wala fulana za kumtambulisha kuwa yeye ni karani wa sensa.

“sasa sijui kama tukienda huko kwenye kuhesabu watu watatuamini na kukubali wahesabiwe au watakataa kwa sababu hatuna vielelezo,” alisema.

Akizungumzia kasoro hizo, mkuu wa mkoa wa dodoma, dk. Rehema nchimbi, alikiri kuwepo kwa kasoro hizo.

Alisema kwa upande wa vitambulisho ni kweli vilikuwa havitoshi na kuwa vilitarajiwa kuwasili jana mchana.

“upo upungufu wa vitambulisho na majaketi ambapo vifaa hivi vilichelewa, lakini vitawasili leo mchana
010812.jpg
(jana),” alisema.

tutegemee madudu ya ukosefu wa vifaaa kujitokeza uchaguzi mkuu kwakuwa michakato ya zabuni ......inarudi wizi uliofanywa na makampuni yaliyopewa kazi za sensa ....
Tusije kukosa hadi karatasi za kupiga kura ..kama uchaguzi wa serikali za mitaa ulivyovurugwa ......
 
Back
Top Bottom