Sensa 2012: Yanayojiri

Sensa 2012: Yanayojiri

watu wataesabiwa X10, majumbani, kwenye train, mabasi, pikipiki, bicycle etc, ilimradi form zijae tu, mgomo uwe umefail

Tanzania mbona tunachekesha ulimwengu?? Kwa nn wasihesabiwe hao waliopo waliogoma tukatafuta mathematical formula ya kuwaingiza kuliko ku cheat? au kwa nn zoezi lisingeachwa kwanza hadi pawepo na muafaka kuliko kuchezea pesa za walipa kodi halafu mnatuletea takwimu za kupika??
 
Onyo! Nyumba hii ni ya waisilamu hatuhesabiwi! Awamu ya nne kazi kweli kweli!
 
Bamukunda inawezekana umechangia kwa Ustadh Ponda kuhesabiwa kama kweli ni jirani yako.Lakini inasemekana baadhi ya Wapinzani wa Sensa walipoitwa Ikulu na kupewa vidonge vyao walitoka wakiwa ndembendembe.Usishangae hilo ndio hali halisi ya baadhi ya Wabongo.
 
Ni punde Raisi wetu katoka kuelezea umuhimu wa sensa na kuwaomba na kuhimiza watu wahesabiwe. Ila kuna jambo moja kwa upande wangu sijamuelewa vizuri. kaulizwa swali na waandishi wa habari Je, watafanya nini kwa wanaosambaza sms kushawishi watu wasihesabiwe, jibu alilotoa ni rahisi kweli kwa hadhi yake, kasema "nasi tunatuma sms kuwashawishi wakubali kuhesabiwa, tutapambana nao hukohuko kwenye mitandao, tena zinatumwa kwa jina langu (raisi)" kiukweli pamoja na maelezo kuwa hao waliopo msikitini si watatoka tuu kama wamejifungia na wakitoka watahesabiwa. Binafsi naona kama kunamchezo wa kuigiza, kama kweli sheria ya uchaguzi inaelekeza nini cha kufanya kwa waliokiuka hili zoezi si muda wa kubembelezana. Kubembelezana sana huku kwa mambo ya msingi yanapoteza muda na kuchelewesha maamuzi ya msingi! NAPENDEKEZA HATUA KALI ZICHUKULIWE KWA WOTE WALIPOKIUKA WAZIWAZI.

MIMI NIMESHAHESABIWA, NAKUSHAURI NAWE UWE TAYARI KUHESABIWA!

Umesahau ili 62% iliyompeleka Magogoni ni ya waislamu. kwa hiyo lazima awe makini na majibu yake vinginevyo atapinduliwa na hiyo 62% ya waislamu. wewe hujiulizi kwanini CUF imeshuka daraja safari hii
 
tunawatakia sensa njema ila muangalie maana tanzania kila jambo linanasababu wanoogoma wanasababu zao nawanaokubali wanasababu zao kikubwa serikali haijaelimisha watu / wananchi maana halisi ya sensa na udini ndio uliochangia kuharibu sensa
 
Watu kwa ku copy na ku paste mko juu...ungeandika Kiswahili tungekuelewa wengi Mkuu..


..... kumbe..... wanaokataa kuhesabiwa wanaona weakness hii..... Chuwa was explaining about legal measures that could be instituted against individuals proved to have, in any way, sabotaged the exercise. Some Muslim activists told reporters about their plans to boycott that activity today. He said that the Statistics Act, 2002 does not clearly stipulate legal measures that can be taken against persons sabotaging that exercise.
Replying to a question on what action will be taken by NBS to individuals insisting on provision of numbers of Muslims and Christians, Dr Chuwa said the current act dated 2002 has no provisions for prosecuting anyone in that regard.
"The Statistics Act of 2002 page No 351 says nothing as to one who provides such statistics. Due to that weakness we seek that the Act be reformulated and sent to Parliament for amending, so as to get legal power to take action when such a situation occurs," he said.


 
Mpaka sasa bado waislam wengi wapo misikitini wanafanya ibada sijui makarani watawafauata?
Maana walilala msikitini na hawakufutwa usiku.

jk kawaambia hawawezi kukaa huko mda wote njaa itawauma watatoka tu na kuhesibiwa.!
 
Wakahesabu madawati kwenye shule za kata,hahesabiwi mtu hapa LIWALO NA LIWE KUDADADADEKIII!!!!
 
Unakumbuka Igunga ni viongozi gani wa dini walisimama na kusema waislam waichague ccm na siyo chadema? Sasa kitendo hicho ndiyo kilitokea sana kwenye misikiti 2010.
Kuhusu kuchaguliwa na wakristu au waislam: Viongozi wote hao wamechaguliwa na wakristu/waislam/wapagani lakini tofauti ya wakristu/wapagani ambao walichagua kwa utashi wao, waislam walihimizwa kuchagua viongozi wa ccm.
Ndiyo maana hata Igunga tuliona live vituko vya wale mashehe.

Ukileta mfano wa Igunga na mie takupa mfano wa Kanisa Sumbawanga unaukumbuka huo mgogoro au wewe unakumbuka Igunga, kwa hiyo kwa akili yako ndio unatuambia kura walizopata Chadema zilikuwa za Wakiristo tu.

Unaweza kutupa ushaidi kuwa mwaka 2010 Waislam Misikitini waliambiwa waipigie kura CCM? Kama kuropoka hata mie naweza kukuambia Wakiristo waliambiwa Makanisani waipigie kura Chadema.
 
Duh! Lumande tena,hivi sisi ambao tunaishi wenyewe hamna ata msaidizi kazini nako mpaka saa kumi ukiongeza na folen unafika saa mbili usiku ata lumande inabidi watuvumilie sababu kama leo hawajaonekana kwangu basi kuniona mpaka jpili la sivyo tutafukuzwa kazi.
 
Subiri 2015 kwenye mikutano ya kampeni ukomae na swali hili...usipopata jibu pigia kura chama kingine. Lakini nina wasiwasi itakapofika 2015 kama kawaida watu wataanza tena kutumiwa na kudanganyana kwenye nyumba zao za ibada na mwisho wa siku mtaipigia tena kura CCM kukikomoa chama kingine kama mlivyofanya 2010. Tukifika 2022 mtaanza tena kulalamika hivyo hivyo hatuoni maendeleo ya miaka 10 iliyopita lakini tukifika 2025 kwenye uchaguzi mtadanganyana zaidi na zaidi kwenye nyumba zenu za ibada na mpaipigia kura tena CCM kukikomoa chama kingine...Mzunguko unaendelea na jinsi siku zinavyokwenda ni hawahawa wanaolalamikia mfumo kristu ndiyo wanaotumika kuirudisha serikali ileile wanayoilalamikia madarakani...

Unazungumzia wale walio sema Jamaa Chaguo la Mungu (wakatoliki) na Malasusa au wale waliompamba Padri MZINIFU:spy:
 
Dakika tisini kwisha! Niece and the gang have invaded my space again, flipping through dvds, selects bunny dvd for viewing. Niece politely remainds me bbc news no good for your health watch more cartoons. Guess wengi wape. Nasubiri makarani wa sensa.

Asante kwa taarifa za kifo cha Neil Armstrong, jamaa alipenda sana anga, kumbe alipata leseni ya urubani kabla hajapata leseni ya kuendesha gari!
 
Tanzania mbona tunachekesha ulimwengu?? Kwa nn wasihesabiwe hao waliopo waliogoma tukatafuta mathematical formula ya kuwaingiza kuliko ku cheat? au kwa nn zoezi lisingeachwa kwanza hadi pawepo na muafaka kuliko kuchezea pesa za walipa kodi halafu mnatuletea takwimu za kupika??


Mkuu wa mkoa flani alisema Jana watakaogoma wataipata fresh ya Mwaka na wasipoonekana watakadiriwa maana wanazaa sana takwimu za awali zinaonyesha Tuko 45 million ivo kwa sasa wakikadiria 47-50 million watakuwa hawajakosea maana watz wanazaa Kama kuku Tehe Tehe Tehe Mimi sijabandika angalizo mlangoni kwani mwalimu wangu alinifundisha kuwa (don't trouble trouble unless trouble trouble you) ila hawafiki toka Jana usiku nawasubiria ila naambiwa wanapiga kazi mpaka Baa Naona bora wakanikute huko huko Baa.
 
Unakumbuka Igunga ni viongozi gani wa dini walisimama na kusema waislam waichague ccm na siyo chadema? Sasa kitendo hicho ndiyo kilitokea sana kwenye misikiti 2010.
Kuhusu kuchaguliwa na wakristu au waislam: Viongozi wote hao wamechaguliwa na wakristu/waislam/wapagani lakini tofauti ya wakristu/wapagani ambao walichagua kwa utashi wao, waislam walihimizwa kuchagua viongozi wa ccm.
Ndiyo maana hata Igunga tuliona live vituko vya wale mashehe.

Si ndio hao BAKWATA waliopewa millioni 100 ili kuhamasisha waislamu washiriki sensa na serikali hiyohiyo iliyowatumia mwaka 2010. Ndo upate picha Chombo cha BAKWATA kipo kwa ajili ya nani na si kukazani Mufti kasema ndo huyo huyo anaeipigia kampeni CCM.
 
Kuna karani mmoja rafiki yangu yeye kapangiwa Mwananyamala Kisiwani ananiambia mpaka saa 9 kaishahesabu nyumba 12 tu kila nyumba akiingia anakutana na upinzani mkali watu hawataki kuhesabiwa.
 
Wadau mi niko border Tunduma hapa navuka, kurudi huko mpaka baada ya wiki mbili itakuwaje?

Wewe ukirudi utakuwa umehesabiwa na uliowaacha nyumbani, si lazima uwepo physically wakati wa kuhesabiwa!
 
Back
Top Bottom