Kibirizi
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 604
- 149
Zoezi linakwenda vizuri tofauti na matarajio ya kundi fulani dogo, nimemsikiliza mkuu wa mkoa wa dar es salaam (TBC) amethibitisha kwamba zoezi linakwenda vyema mkoani Dar, sipendi kugeneralize kwamba waumini wa dini fulani wamegomea wote, kwa sababu mpaka sasa kuna ushahidi wa viongozi wa dini fulani wakihimiza watu wahesabiwe kwenye sensa na nimeona waumini wa dini hiyo wakiwapa ushirikiano makarani wa sensa, isipokuwa kuna kundi dogo la wahuni ambalo ndio wanakwamisha zoezi hili, nimetembelea misikiti zaidi ya mitano na hakuna muumini hata mmoja ambaye amekesha huko.