Ulishaona wangapi madikteta?


Nina marafiki wengi Wasukuma nawajua in and out na ni mifano mizuri sana katika ndoa zenye amani na maelewano. Mimi mwenyewe na miaka yangu hii 76 sijawahi hata kumfinya mwanamke na hata maeksi zangu wote tuliachana kwa upendo na amani sana; na mpaka leo baadhi yao bado tunasadiana katika ishu za hapa na pale.
Wasukuma wababe nadhani ni kizazi cha baba zetu kinachomaliza muda wake hiki. Hawa vijana wa sasa wengi angalau wamesoma na kidogo wanajua mambo. Labda tatizo ni nyinyi mabinti wa kisasa wasomi ambao hata hamjui nafasi ya mwanamke na mwanaume ni ipi katika nyumba. Full uanaharakati na kudai usawa uliopitiliza kimo. Usawa wenyewe hata mkipewa bado unawashinda. It is like you want to eat your cake and have it too. Na hii ndo sababu kuu wengi wenu hamuolewi sababu ya uanaharakati, usomi na kujifanya mnajua kila kitu. Hata mkiolewa mnaachika kwa sababu hamuwezi kuheshimu majukumu ya mume katika nyumba na kutimiza majukumu yenu kama wake.
Hakuna mwanaume mkorofi mbele ya mwanamke mwenye mutual respect na anayejua wajibu na majukumu yake na ya mume ndani ya nyumba; na kuyaheshimu.
Kizazi chenu hiki kimevurugwa ndo maana hata ndoa hazina maana tena. Na kila upande unautupia mpira upande mwingine.
Turudi kwa Mungu tuelewe lengo lake hasa la kuanzisha ndoa lilikuwa ni nini. Vinginevyo ni vurugu tupu na bila ndoa zenye amani na upendo, hakuna familia bora na matokeo yake jamii nzima inaangamia.
Mungu na Atusaidie kwa kweli!