Selfika na JF: Snap it. Show it

Umegusia jambo la msingi sana. Wenzetu wanapambania legacy. Yaani ni kitu cha muhimu sana kwao. Wakiondoka watakumbukwaje. Unakuta mtu anaishi maisha ya kawaida kumbe ana vimilioni vyake kadhaa ameviweka kwenye trust na ameandika will kabisa kuwa akifa vyote vipelekwe kwenye chuo au shule fulani vikajenge jengo ambalo litapewa jina lake iwe kama kumbukumbu ya kudumu. Ndiyo maana ukienda kwenye vyuo vikuu vyao utakuta majengo karibu yote ni majina ya watu. Utakuta SYB School of Economics. Ukiulizia huyo SYB alikuwa nani utapewa historia yake yote na kiasi cha pesa alichotoa kujenga jengo hilo. Na uzuri majimbo mengi pia wana matching program. Yaani SYB akitoa milioni 10 kujenga jengo serikali ya jimbo nayo ni lazima itoe milioni 10. Hivyo mjengo wa dola milioni 20 unajengwa lakini unaitwa kwa jina la SYB kwa vile ndiye initiator. Legacy!

Na tabia hii ya kukazania legacy ndiyo imewafanya kwa kiasi kikubwa waondokane na ufisadi huu wa kijinga kama tunaofanyiana huku. Huwezi kula hela za barabara au za visima vya maji kwa sababu kwanza utafungwa na utaharibu legacy yako mazima. Wenzetu hawawazi tu matumbo yao na familia zao. Ndiyo maana hata utajiri wao ni generational. Watoto, wajukuu, vitukuu, vilembwe....kamwe hawatakubali jina la familia life na watapambana kufa na kupona kuhakikisha kuwa biashara inaishi. Akina Ford. Akina Toyota. Akina Benz. Akina Boeing.....
 
Akiyanani nimecheka πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ
Eti Jehovah nikurudishie nini 🀣🀣🀣🀣🀣
 
Ah wee hawa wanakuchana live tuu. Sasa unakuta huyo demu ndio ulishampenda
 
Well articulated Mtumishi. Aisee na sisi tupambane tuache legacy.
 
Naona unaanza kunitangaza tararibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…