Selfika na JF: Snap it. Show it

Mimi ni yule mmoja, kati ya wale kumi,
Uliowaponya ukoma, kwako nimerudi
Wale tisa sijui,
Ila mimi nimekuja kusema Asante

Najiuliza, Nikulipe nini, kwa yote ulionitendea mimi,
Baba ni mengi, siwezi lipa hata kwa senti
Natafuta namna nzuri ya kukushukuru ninakosa,
Natafuta maneno mazuri ya kukushukuru ninakosa.
Ee Baba,
Nikulipe nini, nikulipe nini?

Uliyonitendea ni mengi,
Siwezi kuhesabu
Ila nina neno moja,
ASANTE (x5)

Nachojuaga, huwa unaongezaga
Kama ukimpa mtu kitu alafu akakushukuru
Nachojuaga, huwa unaongeza, zaidi.
Sikushukuru tu kwa haya uliyotenda,
Ila, Hata kwa yale ambayo hujayatenda
Huku nikiamini, Shukrani ni sauti ya imani

Fedha (Haitoshi kukushukuru)
Dhahabu (Haitoshi kukushukuru)
Ee Baba
Nikulipe nini, nikulipe nini

Ulionitendea ni mengi,
Siwezi kuhesabu
Ila nina neno moja,
ASANTE (x2).

Shukrani imebebwa kwenye neno moja,
ASANTE (Γ—4)
 
Good lyrics. Nizame mjini you tube niutafute
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…