Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Juzi kuna sehemu nilikaa nikasema ngoja niangalie ligi ya wadogo zangu karma na Anne. Mara Sauli huyo, nyuma yake K/njaro Express na Golden Deer bampa to bampa ; Golden Deer kamu-overtake mwenzie huyo kayeya. Muda kidogo kaja zake Imani taratibu; zikapita Sauli mbili tena, G.D nyingine na magari mengine mengii. Nimeshajisahau ndiyo namuona swahiba wako Al-Saedy anajikongoja, sijui nini kilimkuta siku hiyo. Tatizo hobby ya picha sina, nakuja kukumbuka baadaye mweeeh
Hapo kwenye hobby ya picha tuko wengi kwa kweli. Naweza kutana na tukio muhimu nikaliangalia kuanzia mwanzo ila likifika mwisho ndiyo nakumbuka eti sijalipiga picha.

Kwa mabasi hizo pitanapitana za njiani ni kawaida tu ila pale Mbezi ndiyo huwa panaamua nani mshindi. Mara nyingi anaanza Sauli then Al Saedy then Kilimanjaro then Imani Plus.
 
Selfika na Airtel ya buku X2.
IMG_20211217_124528.jpg
 
Alsaedy wa hovyo tu..basi ni vile analilazimisha tu kulipeleka lile gari.

Halina ulakshari wowote mule ndani
Basi ni vile ukipanda inabidi uungane nao kupambana na mengine.
Al Saedy kwa Mbeya mbona wanajitahidi kupeleka mabasi mazuri. Kuna siku nilipanda Al Saedy ya kwenda Dom aloooo abiria tulilalamika safari nzima.

Picha linaanza kila mtu katoa nauli yake yaani nauli wanakuchaji kwa kukuangalia muonekano wako. Al Saedy kwa Dom hamna kitu wanapeleka mikweche tu.
 
Hapo kwenye hobby ya picha tuko wengi kwa kweli. Naweza kutana na tukio muhimu nikaliangalia kuanzia mwanzo ila likifika mwisho ndiyo nakumbuka eti sijalipiga picha.

Kwa mabasi hizo pitanapitana za njiani ni kawaida tu ila pale Mbezi ndiyo huwa panaamua nani mshindi. Mara nyingi anaanza Sauli then Al Saedy then Kilimanjaro then Imani Plus.

Siku hiyo Al Saedy atakuwa alipata changamoto; aliachwa mbali sana na wenzie. Kwa kweli kwangu picha ni wito
 
Al Saedy kwa Mbeya mbona wanajitahidi kupeleka mabasi mazuri. Kuna siku nilipanda Al Saedy ya kwenda Dom aloooo abiria tulilalamika safari nzima.

Picha linaanza kila mtu katoa nauli yake yaani nauli wanakuchaji kwa kukuangalia muonekano wako. Al Saedy kwa Dom hamna kitu wanapeleka mikweche tu.
Hata Mbeya hamna kitu.
Gari nililopanda wakati wa kurudi yaani ni hovyo sijapata kuona.

Kwanza walipakia abiria wengi kuzidi seat...ikawa tukifika maeneo ya kukaguliwa wanawahamisha watu kwenye coaster...wanakuja kuwapandisha tena kwa mbele.
Gari baya hata AC halina..
Sipandi tena ile gari.

Kimbembe kikaja yule konda sijui aliniona nina hela,
Eti nimepakia unga ananidai hela na wakati chini ya 25kg ni bure..
Nilizinguana naye asubuhi,,ananiambia oh basi tushushe ukapande nao ndani,nikamwambia sawa tu ushushe nikakae nao kwenye seat.
Likapakia.

Kufika mbezi ananizingua,,nikamwambia tafuta mizani tupime,,ikizidi 25kgs nakupa hela..kama vipi nenda nao tu utaniletea kituo cha polisi.
 
Back
Top Bottom