Kisa kizuri .....
Alikuja mtu kwa Khalid bin Walid akamwambia "Fulani amekutukana..
Akamjibu "Hilo Ni gazeti lake alijaze anavyotaka..
Alisema mtu kumwambia Wahab bin Manbah "Hakika Fulani amekutukana..
Akamjibu: "Shetwani hakumpata wa kumtuma ispokuwa wewe??
Akasema mmoja kumwambia mtu "Fulani amekutukana..
Akamjibu: "Yeye amenirushia mkuki lakini haukunipata, kwanini wewe umeubeba huo mkuki Na ukauchoma moyoni mwangu??
Alikuja mtu Kwa Imam Shafi akamwambia "Fulani anakutaja kwa mabaya..
Akamjibu: "Kama Ni kweli basi wewe Ni mfitanishi, Na Kama Ni urongo basi wewe Ni Fasiq, akaona aibu akaondoka..
Usiniambie Nani ananichukia, Ama ananizungumza, niache nicheke Na nicheke Na watu wote, Na nihisi wote wananipenda, Na tuache yaliosemwa Na anayosema, napenda niondoke nikiwa Na Moyo uliosalimika..