Selfika na JF: Snap it. Show it

Ahsante,,,ya bamia unatumiaje?,nielekeze
Mahitaji
Bamia kumi (10)
Mafuta ya maji (African Black castor oil au coconut oil au olive oil)
Juice ya Tangawizi
Asali

Jinsi ya kuandaa
Osha bamia zako vizuri kuondoa uchafu wote
unaweza kukata kata kuwa vipande vidogo vidogo au ukamenya tu (kuexpose undani wake)
Weka kwenye sufuria yako safi
Ongeza maji kiasi (kikombe kimoja au viwili vinatosha) na ufunike
Chemsha kwa dakika 10 hadi 15 mpaka ile gelly au ute wa bamia uwe umetoka wa kutosha
Epua na uache ipoe kwa dakika kadhaa
Baada ya hapo chuja kuondoa vipeke na upate gelly tuu

Kama unatengeneza steaming
chukua ute ulioupata gawanya mara mbili
Nusu ya kwanza changanya na tangawizi na asali na mafuta yoyote ya kimiminika (hasa Castor oil)
Baada ya kuosha nywele kwa shampoo (hakikisha nywele zako ni safi) paka mchanganyiko kwenye nywele zote
Vaa shower cap au steamer na ukae kwa dakika 30+
Osha kwa maji mengi
Chukua ule mchanganyiko uliobaki changanya na mafuta kijiko kimoja hapa utakua umepata leave in conditioner
Nywele zako zikiwa mbichi na safi pakaa vizuri kuanzia kwenye ngozi hadi kwenye ncha.
Chambua vizuri nywele zako kidodgo kidogo kuhakikisha imeingia vizuri kwenywe nywele zote.
Unaweza kusuka mabutu (bantu knots) au twists za njia mbili au tatu au nywele za mistari kawaida nywele lazima ziwe na unyevu kabisa.
Ukiona zinakauka unanyunyiza maji tena.
Ukimaliza acha zikauke vizuri utaendelea kupaka mafuta yako kama kawaida ili kuzifanya zing’ae.
Ukifumua unapata mawimbi mazuri unaweza kubana utakavyo nywele zako.
 
Ahsante Sana,ubarikiwe naanza kazi
 
Process ndio ndefu hivi? Me nilimix bamia na maji tu.

Nikipata muda nitajaribu..
 
Dunia ina mambo hii jamani!! Watuhumiwa nao wanatuhumu wengine

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…