Selfika na JF: Snap it. Show it

Ungeingilia kati kidogo majirani gani nyie waoga hivyo mnataka mtu auliwe ndiyo mseme mtoe ushuhuda
 
Yaani lazima mtu hapo usitamani siku moja nilipopanga mdada huyo kapigwa na mchumba balaa toka saa moja asubuhi ni kichapo tu .

Nguvu zinatokea wapi , ama kweli wazazi wetu walivumilia sana ...
Jirani anapigwa hata hampigi simu polisi mnataka jamii iteketee, kama huko kagaera jana jamaa kampiga mke wake mpaka kaua, sasa mkikaa kimya mnakuza magomvi, ila na wakina mama nyie mpunguze maneno huwa mnaongea sana yani kipigo kinaanza nawe unajibu mashambulizi kwa mdomo
 
Wanawake hatuwezi ingilia ugomvi , Mimi navyoona unaweza ukaita watu wengine waje wasaidie au ndo uite polisi wafike eneo la tukio .
 
Well said ,

Maana imeandikwa katika Wakolasai 3:18
Enyi wake, watiini waume zenu, kwani ndivyo apendavyo Bwana. Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali kwao.

Asili ya mwanamke ni mdomo ona na hili andiko hapa linawakanya


Mwanamke mgomvi

Mithali 25:24:-Ni afadhali kukaa katika pembe ya darini , kuliko kukaa katika nyumba pamoja na mwanamke mgomvi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…