Selfika na JF: Snap it. Show it

Selfika na JF: Snap it. Show it

Sasa wewe kidogo ni kama mimi. Mimi mwenyewe maisha yangu yote ya shule nilikuwaga mpole yaani kiasi kwamba mtu anaweza akaninyang’anya mali yangu badala niichukue nabaki nalia na kusema kwa mwalimu napo nilikuwa naogopa.

Ila nilipofika chuo nikasema sasa basi acha na mimi nianze kuwa muongeaji niache huu ujinga. Ila cha ajabu uongeaji wenyewe eti umekuwa ni wa maandishi nyuma ya keyboard tu ila kuchambana au kubishana na mtu hivi live siwezi.

Nakumbuka kuna dada mmoja chuoni tuliwahi gombana kwenye group la darasani hadi akaleft group nikaona haitoshi nikamfuata inbox nikamchamba hadi akaniblock. Siku hiyo akaniona darasani akasema “enheee afadhali leo nimekuona haya ongea hapa yale yote uliyokuwa unaongea siku ile kwenye group” aisee alinichamba mbona nilinywea nilikuwa mdogo kama piriton ikabidi tu nimuombe msamaha yaishe.

So pamoja na kwamba nimekuwa muongeaji kwa kiasi chake ila bado nina uoga na aibu fulani hivi kwa watu. Nina confidence kwenye uandishi tu ila eti uniite uniambie ongea yale yote uliyokuwa unaandika hata kama ni mazuri nashindwa.
Duuuuuh upo km mie, mbele za watu nna uoga na aibu, siwezi kufanya hovyo, ila km n pembeni tobaaah naporomosha maneno km sie mie vile.
 
Sasa wewe kidogo ni kama mimi. Mimi mwenyewe maisha yangu yote ya shule nilikuwaga mpole yaani kiasi kwamba mtu anaweza akaninyang’anya mali yangu badala niichukue nabaki nalia na kusema kwa mwalimu napo nilikuwa naogopa.

Ila nilipofika chuo nikasema sasa basi acha na mimi nianze kuwa muongeaji niache huu ujinga. Ila cha ajabu uongeaji wenyewe eti umekuwa ni wa maandishi nyuma ya keyboard tu ila kuchambana au kubishana na mtu hivi live siwezi.

Nakumbuka kuna dada mmoja chuoni tuliwahi gombana kwenye group la darasani hadi akaleft group nikaona haitoshi nikamfuata inbox nikamchamba hadi akaniblock. Siku hiyo akaniona darasani akasema “enheee afadhali leo nimekuona haya ongea hapa yale yote uliyokuwa unaongea siku ile kwenye group” aisee alinichamba mbona nilinywea nilikuwa mdogo kama piriton ikabidi tu nimuombe msamaha yaishe.

So pamoja na kwamba nimekuwa muongeaji kwa kiasi chake ila bado nina uoga na aibu fulani hivi kwa watu. Nina confidence kwenye uandishi tu ila eti uniite uniambie ongea yale yote uliyokuwa unaandika hata kama ni mazuri nashindwa.
Aisee Mimi pia ugomvi siwezi sana sana ila sipendi kuona mtu anaonewa , Mara nyingi ikotokea ugomvi nabaki kimya .

Uwoga sio rahisi kutoka maana umeishi mpole muda mrefu na ndo hivyo ulivyo , Jitahidi uwe unaongea live pia na sio maandishi tu .
 
IMG_20200809_141146.jpg
 
Aisee Mimi pia ugomvi siwezi sana sana ila sipendi kuona mtu anaonewa , Mara nyingi ikotokea ugomvi nabaki kimya .

Uwoga sio rahisi kutoka maana umeishi mpole muda mrefu na ndo hivyo ulivyo , Jitahidi uwe unaongea live pia na sio maandishi tu .

Yeah hata mimi huwa sipendi kuona mtu anaonewa na huwa sipendi kununua ugomvi wa watu. Na mimi watu wanaweza wakawa wanaongea hivi mie nikawa nawasikiliza tu kama sipo yaani sichangii chochote kwa kuhofia labda nikichangia mawazo yangu yatadharauliwa tu ila eti nashangaa huku JF nachangia hata pumba bila kujali nitaonekanaje.

Nafikiri mimi upole ndiyo hulka niliyoumbiwa. Huku kuongeaongea sana huwa nalazimisha tu ili na mimi nionekane nina mdomomdomo ila hamna lolote.
 
Yeah hata mimi huwa sipendi kuona mtu anaonewa na huwa sipendi kununua ugomvi wa watu. Na mimi watu wanaweza wakawa wanaongea hivi mie nikawa nawasikiliza tu kama sipo yaani sichangii chochote kwa kuhofia labda nikichangia mawazo yangu yatadharauliwa tu ila eti nashangaa huku JF nachangia hata pumba bila kujali nitaonekanaje.

Nafikiri mimi upole ndiyo hulka niliyoumbiwa. Huku kuongeaongea sana huwa nalazimisha tu ili na mimi nionekane nina mdomomdomo ila hamna lolote.
Mara nyingine Bora ukae kimya ila Kuna muda kuongea pia inaweza kusuluhisha ugomvi huo . basi wewe utakuwa ni introvert
 
Halafu hata mimi nahisi ninakuwa huru zaidi ninapomzoea mtu. Kama mtu sijamzoea nakuwa kama bubu yaani sina cha kuongea zaidi ya kujibu atakachoniuliza tu basi.
Mie muongeaji naweza ongea na mtu yeyote yani bila kumzoea kihivyo nikijisikia... Rafiki zangu huwa wanasema Sina aibu ila najikuta tu nishaongea tuh ..
 
Yeah hata mimi huwa sipendi kuona mtu anaonewa na huwa sipendi kununua ugomvi wa watu. Na mimi watu wanaweza wakawa wanaongea hivi mie nikawa nawasikiliza tu kama sipo yaani sichangii chochote kwa kuhofia labda nikichangia mawazo yangu yatadharauliwa tu ila eti nashangaa huku JF nachangia hata pumba bila kujali nitaonekanaje.

Nafikiri mimi upole ndiyo hulka niliyoumbiwa. Huku kuongeaongea sana huwa nalazimisha tu ili na mimi nionekane nina mdomomdomo ila hamna lolote.
poleeeeh mam lol
 
Mimi siwezi kuwa mkorofi! Naogopa sana watu na hata mtu akinipiga huwa naogopa kumrudishia hata kama nina uwezo huo!

Kuna roommate wangu mmoja alikuwa anapenda sana kunionea kila akinikuta room lazima anizabue bao basi tu kunichokoza! Halafu akawa anasema eti anafanya vile sababu anajua mimi siwezi kumrudishia na kweli sikuwahi kumrudishia maana mtu mwenyewe ukimuangalia hata mkononi hajai basi tu ni vile alinikuta mimi mpole!
 
Back
Top Bottom