Umenikumbusha kitu aiseee!!
Maza mdogo muabeshi, sasa alikuwa na bwanaake mfipa. Basi bana kuna mashosti zake wakawa wanatafuta mganga wana mambo yao uko makazini kwao.
Maza si kapiga simu kaweka loudspeaker eeeee!!!
si nikasikia sauti ya bamdogo eti kapandisha majini kwenye simu anasema wale wadada mwaka haushi wanafukuzwa kazini wajitahidi wamuachie pesa mamdogo ya kununua vifaa vya kazi ili aje kuwafanyia kazi yao. Basi bamdogo anawaaga kwa kifipa aiseee!!!! Nilishindwa kuvumilia nilichekaaaaa mamdogo akakata simu faster alinikata jicho hilo la mwana ukome
Toka hapo siwaamini wafipa na nikimuona bamdogo nakauka kucheka