Selfika na JF: Snap it. Show it

Umeandika ukweli..

Nakumbuka nilipojiunga jf nilikutana na ugomvi wa wadada team fulani na team fulani walifikia hadi kutukanana..nikashangaa inakuwaje kuwaje..sawa wamekutana jf Sasa why hayo mapungufu yao ya nje ya jf wasiyamalize huko nje..

Kuna wakati huwa natamani rafiki kutoka jf lakini nikifiria Yale ya kusemezana vibaya kwenye Uzi..

Uwiii hapana..tubaki tusijuane tu
 
Dah yaani na wanapotea kweli aise kuna wakati nasomaga nyuzi za zamani nakutaga comments za watu ambao hata siwafahamu id zao najisemaga tu basi hawa watakuwa wamebadili id au wamepotea mazima

Hahahaha eti douchebags hilo neno umenikumbusha mbali aise
 
Umeona eenh?? Umenena vyema!!
 
True that, ila sasa sisi wanaume ni mende ujue since day one like tokea tunazaliwa...kila jalala tumo...lakini kwenu huwa inakuwa special

Nakumbuka nikiwa primary kuna kadada kazuri kazuri kenyewe kumbe kalikuwa kananikubali bila miminkujua, lkn rafikize walikuwa wanajua...

Sasa siku ndio tumeua std 7, that day tulipikiwa wali mchafu na soda za chupa, kale karembo kakaanza kunisaka.Kila nikipita kona hii, naambiwa fulani anakutafuta hahaha.
Basi ile kafanikiwa kuniona, she ran after me, na kunihug like how em girls do in movies.

Nikapewa vizawadi pale, mostly misosi misosi...yaani hapo nipo nashangaa shangaa tu, nilikuwa mpole sana na very shy, mtu wa kitabu sana. Kwanza hapo nawaza nitapata ngapi out of 150 ili niende shule kali.

So i never reacted the way she would expect, tukala kala pale, jamaa zangu wakatokea tukaondoka zetu maana tulikuwa tunakaa mbali na tulipoenda fanyia paper, enzi hizo kama unasoma shule A, std 7 mnapangiwa kwenda kufanya huko shule P kuepuka paper kuvuja.

Since then sikuwahi jua yupo wapi, until some few years back, kashaolewa na ako na watoto na ako anaishi +44
Yeah sana na hata wakaka pia lazima wanakuwaga na childhood crush
 
Sasa ninyi si mmekutana wote akili zenu zinafanana
yaani wewe na Shunie ni pipa na mfuniko,, kitu ukiongea wewe yeye atakuja kupigilia msumari na kitu akiongea yeye wewe utakuja kupigilia msumari vile vile

Sasa imagine unafahamiana na ndugu ambaye akili haziendani mimi mtu wa matani yeye yuko kauzu kila pumba nitakazoandika humu lazima aje inbox kuniuliza eti "Karma ni wewe kweli ndiyo umeandika vile??"
yamewahi kunikuta instagram hayo sina hamu mimi
Mbona mimi mejuana na ndugu yangu Shunie wala sina hofu kabisaa
 
Mnachukulia maisha serious sana. Mimi nishaonana na watu wengi humu kikazi na socially. Hadi kesho siogopi kukutana na yeyote nikiamua.
Nb: wengi wasemao hawataki au hawataonana na mwanajf....wanaongoza kuonana na watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…