Mwaka 2010, mama yangu mkubwa aliugua sana, alikuwa anaumwa ugonjwa wa ini tokana na kuwa alcoholic, kabla hajafariki aliugua coma, na hali haikuwa vizuri hata kidogo.
Huyo mama yangu amenisomesha, amenipa mwanga wa mambo mengi sana, maisha yake ya usichana ameishi ughaibuni, nikiwa mshamba kabisa nakwenda kumuona, nashangaa kila kitu, yeye alinipenda sana, na mie nilimpenda sana.
Nimekutana na marafiki wengi kwa sababu yake, na mambo mengine yote ni sababu yake.
Baada ya kuugua sana, watu walikata tamaa akiwemo baba yangu mkubwa ambae ni mmewe, kwa kweli nilimuomba sana Mungu ampe nafuu japo nipate kumuaga mama yangu kipenzi, hata nimwambie tu ahsante mama, anione mwanae anitambue roho yangu ifurahi.
Siku mbili baadae napata taarifa mama amepata nafuu yaani ametoka kwenye coma lakini ana wiki mbili ama mwezi kabla ini lake halija shutdown kabisa.
Namshukuru mungu nilimuona kwa mara ya mwisho , nilimshukuru kwa mema aliyonitendea, nilitoka hapo nalia, sikuamini kama kweli nimemuona akaniona mama yangu kipenzi, nilikua nae karibu sana kabla hajaanza ku hit bottles hard,namshukuru mungu alinipa wasaa kumuona mama yangu mara ya mwisho na kumwambia kwa heri.
Hakika mkuu naweza sema Mungu alisikia maombi yangu
Mungu hajibu kwa kile unachotaka bali unachohitaji.
1 Petro 3:12 NEN
Kwa maana macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza maombi yao. Bali uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu.
_King