Sawa mmeshindwa kujizuia kwenda kwenye mamipira, basi hata kusimama kuimba Wimbo wa Taifa?

Sawa mmeshindwa kujizuia kwenda kwenye mamipira, basi hata kusimama kuimba Wimbo wa Taifa?

Keynez

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2007
Posts
3,621
Reaction score
6,510
Labda mmeshindwa kujizuia kwenda kwenye hayo mamipira yenu. Labda ni addiction mnayoshindwa kuizuia. Labda wengine mnaona ni sehemu ya "kusahau" kwa muda machungu ya maisha. Sawa tunakubali.

Ila hata kujiorganize na wote kwa pamoja kusimama wakati mpira unaanza na kuimba Wimbo wa Taifa? Hili lingefanyika kila mechi lingetuma ujumbe mzito sana wa kizalendo bila kuonyesha mapenzi ya mtu binafsi ya kisiasa.

Tuone nani atakamatwa na kupewa kesi ya Uhaini kwa kuimba Wimbo wa Taifa!

N.B. Mkianza hilo zoezi, Azam wataambiwa waanza kuchelewesha kurusha matangazo katika mechi zote. Hapo mnajiongeza. Mnaimba kila baada ya dakika 15 hasa pale mpira ukianza tu, na kabla tu ya mapumziko. Mnaweza pia kuimba kila goli la timu yoyote likifungwa.

Wanategemea sana haya mamipira ili wananchi wapotezee yale yaliyotokea. Hapa ni kuwafuata huko huko wanapopategemea.
 
Wimbo wa taifa unawabariki viongozi wa nchi kitu ambacho kwa hawa viongozi wa sasa wa uchaguzi wa 2025 ni tusi kwa watanganyika, bora tuimbe ule wa Tanzania Tanzania nchi yangu.
Sikupingi na una hoja nzito ila Wimbo wa Taifa una uzito zaidi.
 
Back
Top Bottom