zomba
JF-Expert Member
- Nov 27, 2007
- 17,240
- 3,910
Nimeitoa hapa:Sudan - THE LEGAL SYSTEM
Bado utadai Sudan haifuati Sharia? Kwako wewe nchi inayofuata sheria ni Saudi tu?
Unasema wanaofanya uhalifu Saudi Arabia ni wageni tu. Je hao wa Saudi wanaobaka wafanyakazi wao wakike wakifilipino nao ni wageni? Je hao waSaudi waliombaka yule binti wa al-Qateef aliyebakwa mande mwaka 2006 ( angalia hapa: Saudi court ups punishment for gang-rape victim - CNN.com) nao walikuwa wamefoji bali walikuwa wageni? Ni kawaida wageni kuwasingizia wageni kwa maovu yote. Saudi Arabia hawana tofauti.
Utateteaje kitu ambacho haukijui? Utasemaje, wewe ambae bila shaka unajiona ni muumini safi, kuwa haujui kama hii adhabu iko kwenye Sharia au sheria? Unashindwa nini kusoma kitabu chako kitakatifu ili ujue ukweli uko wapi? Ni watu kama wewe ambao wanakubali kujitoa mhanga wanapoambiwa na mashehe uchwara kuwa peponi zawadi yao ni mabikira!
Amandla........
Mimi naitetea Sharia na kama kuna kifungu sikijui hukumu yake nnakuwa mkweli na muwazi kuwa hiyo hukumu siijui kwani mimi si mwana Sharia, mimi ni muumin wa uIslam.
Na pia nimetetea sheria, na nimesema kama ni Sharia au sheria ndio iliyotowa hiyo hukumu ya viboko kwa huyo mwanamke basi ni sawa kabisa. Huyo mwanamke alitakiwa afate Sharia au sheria za nchi anayoishi.
Au hujui kusoma? au mradi ubishane tuu?
Jee, wewe unazijuwa sheria zote zilizo kwenye Biblia au for this matter za nchi unayoishi? Hata ungekuwa ni mwana sheria basi ng'oo.