Nono
JF-Expert Member
- Feb 11, 2008
- 1,543
- 664
Naona mantiki ya hoja yako. Nilijiuliza sana wakati wa uteuzi wa wakurugenzi mbalimbali akiwepo aliyekuwa wa Kilombero ambaye alihamishiwa Bagamoyo. Pindi ushindi wa kesi ya uchaguzi ulipotoka na kumpa ushindi mgombea wa upinzani, yule mkurugenzi alitumbuliwa!! Wengi wa wakurugenzi walichauliwa kutokana na wanachama wa ccm, na kwa mwendo huu wa kuwapandisha vyeo wale wanaodaiwa kuchezea rafu wapinzani, haitii shaka hata kidogo kuwa hawa wateule hawatakuwa tayari kumkwaza muajiri wao kwa vyovyote. Wasiwasi wangu, ni kama tukienda na mdundo huu hadi 2020 (hakuna dalili ya kubadilika), ni wazi kuwa wakurugenzi wote watawatangaza wabunge wote na madiwani wote wa ccm kuwa ndio washindi (hii iwe kwa kuagizwa au kutokuagizwa).Kuna kitu kinanishangaza sana kuhusu CHADEMA, bado hawaamini kuwa uhuni wanaofanyiwa unatokea mbali zaidi ya polisi, zaidi ya wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa. Nilikuwa nikiwasikiliza Lema na Nassari walivyokuwa wakidai watampelekea mh. Rais ushahidi wa madiwani kuhongwa nikasikia kichefuchefu!
Nafikiri nilisema mahali ninyi toeni huo ushahidi, in public, sasa baada ya kubezwa na TAKUKURU na Mnyeti kupewa ukuu wa mkoa, kupandishwa, nadhani akili itawajia. Maana walichokuwa wakikifanya ni kumtumia mtu ujumbe kuwa, "The magic of fear is working"
Na kama hawatakuwa na mkakati wa pamoja wa kujua namna ya kupambana kisiasa very forcefully, 2020 wakibakizwa wabunge 5 wa CHADEMA niiteni mbwa!
Why I say so!
1) Kama mwenzenu anapigwa risasi mchana kweupe, reaction inakuwa ni unyonge, ukishinda ubunge wakamtangaza mwingine utafanyaje?
2) Kama Kigaila anakamatwa na polisi kwa kuhoji kwanini Makonda anazunguka na wenye bunduki reaction yenu inakuwa hii, mkinyang'anywa ubunge mtaweza kufanya nini?
3) Kama mtu bustani zako zinaharibuwa unalia lia unajibu uhuni kwa sheria ukinyang'anywa ubunge hata kama umeshinda kwa asilimia 90% utafanyaje!
4) Hivi neno, " Jecha apewe tuzo" linaashiria nini kwenu?
5) Hivi pamoja na kuonyesha wazi Mnyeti alihusika kuhonga madiwani na bado akapandishwa cheo inaashiria nini kwenu!
Endeleeni kulia goodluck, pengine mtaonewa huruma! Guys mnachokifanya ni kutuma ujumbe kuwa hata mfanyiwe nini hamwezi fanya lolote, "And the envelopes will be pushed real far in 2020 by the look of things"
Halafu acheni madharau!
Hivyo nadhani ni vyema kuanza kutafuta uwanja wa kupata muafaka wa kitaifa katika hili kabla ya kufika huko kwani inaweza kuzorotesha utengamano wa Watanzania.