Samahani walimu hivi mna mgomo?

Samahani walimu hivi mna mgomo?

Shule ya mugabe sekondari sinza vyoo havina maji na kuna wanafunzi wa kike.
 
Uko wapi huo mgomo????
Mkigoma tutawafukuza wote na kuajiri wapya. Mtaani kuna idadi sawa na muliopo serikalini. Leteni mchezo sasa.
tobaa..! tatizo umekariri migomo myengine sio mpaka utikise bahari no unapita chini kwa chini ila madhara yake mtaisoma tu!
 
Hivi inawezekanaje mwanafunzi wa darasa la tano hajui kusoma..?
unamwambia nionyeshe W anakuonyesha R duh! mpaka nimechoka kabisa!! sasa hapa mtu anasoma au anapita tu..?!

hawa ndo wataalum tunaowategemea miaka ijayo kweli ama kweli waafrika tunahitaji kutawaliwa!! elimu ndo inatakiwa itukomboe lkn ndo inapita kama mpita njia tupu!

Serikali hebu wajalini walimu watengeneze watu wanaostahili msipowajali ama kuijali hii sekta ya elimu tutakapofikia patakuwa hapatamaniki for sure..
Nani hajui dunia ya sasa yahitaji wasomi..? Sasa kwa dizaini hii tutawapata kweli miaka 50+ sasa bado tunasuasua dah!

Lile shipa la aibu limetoka kabisa!.


Tunaandaa wataalamu watakaosimamia Nchi yetu ya Vi-Wonder au huelewi ndugu
 
Msingi mbovu katika elimu utasababisha kuzaliwa Taifa la wajinga.Huwezi kuniambia watoto wamefaulu darasa la saba kwa kupata 70 katika maksi 250.Na 80% wamepata 70-100/250.Hii maana yake 20% ya darasa la saba ndio walistahili kwenda sekondari.Baada ya miaka kadhaa tutapigwa sindano tumboni kwa kuumwa tumbo.
 
Sasa hivi hata kile kidogo walichokuwa wanapata walimu wamenyang'anywa, hata ile heshima imepotea now hata mwenyekiti wa kijij anamfukuza shule mwalimu, sasa hivi hata kile kijiheshima cha mwalimu mtaani hakipo tena, tegemea kubwa zaidi ya hilo itafika mahali hata mwanafunzi atajishangaa shule anaenda kufanya nini, elimu ipo kaburini bado kufukiwa tu.
 
Nawewe jiulize. Walimu wanalipwa ?
Serikali Ina pretend kulipa walimu
Na walimu wana pretendi kufanya kazi
Ni wachache sana watakao elewa hii lugha yako


Kauli hiii
28a86e659c30f62d2794915e8aa60480.jpg
inahitaji nguvu hata za wanyama kuielewa aseee



Na tumeanza kuelewa hasara za hasira za mnyonge
 
Tumekua tukiwatukana sana walimu na walivumilia na manyanyaso mengi,
Mathalani mwalim alimfundisha mtu mpaka kuvaa akafaulu mpaka labda kufanya kazi tofauti na ualimu, halafu huyo huyo anamtukana mwalimu ni kilaza na wakati ana mtoto unategemea huyo mtoto afundishweje kwa mfano,


Na sasa hivi watameza sana matango pori

Na kama ni kweli walimu watawansweka watoto wenu nyinyi mnaowatukana jera kwa kuwafelisha na wao kufunguliwa mashtaka kwa kufuja fedha za serikali
 
Hivi inawezekanaje mwanafunzi wa darasa la tano hajui kusoma?
unamwambia nionyeshe W anakuonyesha R duh! Mpaka nimechoka kabisa sasa hapa mtu anasoma au anapita tu?

Hawa ndo wataalum tunaowategemea miaka ijayo kweli ama kweli waafrika tunahitaji kutawaliwa, elimu ndo inatakiwa itukomboe lakini ndo inapita kama mpita njia tupu.

Serikali hebu wajalini walimu watengeneze watu wanaostahili msipowajali ama kuijali hii sekta ya elimu tutakapofikia patakuwa hapatamaniki for sure.

Nani hajui dunia ya sasa yahitaji wasomi? Sasa kwa dizaini hii tutawapata kweli miaka 50+ sasa bado tunasuasua.

Lile shipa la aibu limetoka kabisa!
Afadhali na wewe umeliona, mm nilikuwa mwalimu nikaachana nao, na mara nyingi zikitokea mada zinazohusu elimu huwa nachangia sana, watu wengi wanawaona walimu kama vile mazoba na hawajielewi, hawatazami athari mbaya kabisa inayozalishwa na hawa walimu, mm naamini sana kuwa walimu walishagima kitambo sana tangu miaka ya mwanzoni kabisa ya 2000, kile kipindi mwalimu anaheshimika na kuthaminika na jamii.

Mtu anayemuona mwalimu kuwa hajitambui na hajui hadhi yake na ni mtu mnyonge afanye tathmini kazi wanazofanya walimu, watoto wanaenda kucheza na kurudi nyumbani sio kujifunza.
 
Na wazazi inabidi kufatilia maendeleo ya mtoto kwa mfano hilo swali ulitakiwa umuulize akiwa darasa la kwanza sasa lakini ndo hivyo hakufatiliwa kama anajua au hajui kupata elimu bora ni collaboration ya wazazi +walimu +mwanafunz mwenyewe
Kwa hizo shule hata ukienda kufuatilia unajiumiza tu, utasmbiwa elimu ni bure hata kutojua kusoma ni bure hauziwi na mtu. Utaambiwa mwanao anasinzia darasani sasa tumfanyeje na elimu ni bure? Au uje na beseni la maji ya baridi kwa ajili ya kupunguza usingizi,

Kama elimu ni bure unafikiri ujinga utauzwa?
 
Itafika hadi sekondari hajui kusoma km shule zikiwa za mwisho wakuu wa shule, maafisa elimu n. K wanapigwa chini kwa nn zisifanyike mbinu zozote hata za kuwahonga wasimamizi ilimradi wapite tuu.
Usiseme itafika, nenda huko maporini kidogo kaka, mtu yuko form two hajui chochote, wanafanya mitihani ya ramli wakiwa std 7, wanasiliba siliba hata asiyejua anaweza kufaulu na kwenda form one ila hajui chochote, ili kuficha aibu wakashusha ufaulu form two na wanampango elimu ya lazima iwe form four yaani hakuna kufeli std 7 wala form two.
 
Kweli kuna tatizo katika ufundisha kutokana na kile ukikitaja leo hapa unafungwa na wizara ya anayelala la shuka ya taifa ila hata zamani kuna wengi tu walimaliza shule bila kujua kusoma na kuandika. Wengine hawakujua kiingereza hata cha kuombea maji na kumkaribisha mgeni licha ya kusoma hadi chuo kikubwa sijui walifikaje huko
 
Sasa kama gvment inawabana kila kona wafanyeje? Hutakiwi kuwa na biashara,kufundisha private na serikalini ni kosa la jinai.Mshahara mdogo kuliko kada zingine,Who i'll care about your baby? Stress za maisha zinawafanya walimu wengi wanashindwa kudeliver material in effective way.Huu ni UKWELI na msema kweli ni mpenzi wa MUNGU.
In weed's voice
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom