Samahani walimu hivi mna mgomo?

Samahani walimu hivi mna mgomo?

Hivi inawezekanaje mwanafunzi wa darasa la tano hajui kusoma..?
unamwambia nionyeshe W anakuonyesha R duh! mpaka nimechoka kabisa!! sasa hapa mtu anasoma au anapita tu..?!

hawa ndo wataalum tunaowategemea miaka ijayo kweli ama kweli waafrika tunahitaji kutawaliwa!! elimu ndo inatakiwa itukomboe lkn ndo inapita kama mpita njia tupu!

Serikali hebu wajalini walimu watengeneze watu wanaostahili msipowajali ama kuijali hii sekta ya elimu tutakapofikia patakuwa hapatamaniki for sure..
Nani hajui dunia ya sasa yahitaji wasomi..? Sasa kwa dizaini hii tutawapata kweli miaka 50+ sasa bado tunasuasua dah!

Lile shipa la aibu limetoka kabisa!.
Hilo ni kosa lako mzazi kumpeleka mtoto st.kayumba..Upuuzi wa namna hyo school bus hamna.
 
Na bado hiyo ni introduction tu
Km drs moja lina watoto 120 unatarajia wataelewa kitu gn hapo?! Sasa hilo ni kosa la Mwalimu. Na mzazi pia huchangia sn mtoto anafikaje mpk la tano bila mzazi kujua kuwa miaka yote hii mtoto hajui kusoma?! Lakin utakuta lawama zote anatupiwa walimu. Kwa kweli nawapa pole walimu kwa kazi ngumu
 
Hilo ni kosa lako mzazi kumpeleka mtoto st.kayumba..Upuuzi wa namna hyo school bus hamna.
hivi zinakutosha kweli wewe..? binafsi sina hata mtoto huko za skul bus unadhani watz wote wanaweza kustahimili hizo bei? yani we mbipi kabisa wewe
 
Ukiona mwanao hajui kusoma na kuandika ujue tatizo ni wewe mzazi
Wewe unakuwa unafanya nini hadi mtoto wako anashindwa kutofautisha kati ya R na W?
Shule ni sehemu ya kumsogeza mwanafunzi asonge mbele zaidi lakini mtu anayetakiwa kuhakikisha mtoto anajua kusoma na kuandika ni mzazi. Kwa mzazi aliye makini na anayependa elimu kweli mtoto huanza kufunzwa nyumbani na husimamia hilo na uzuri kuna vitabu vinauzwa mitaani ambavyo vinaweza kumsaidia mtoto kusoma na kuandika.
Mzazi ndio mwalimu wa kwanza wa mtoto na mtoto anapo feli lazima uanze kwanza kujiangalia wewe kama kweli unatimiza wajibu wako ipasavyo.
Mtoto unampeleka kuanza shule hajui hata kusoma a,e,i,o,u halafu umpe lawama mwalimu? hivi unafikiri kuna wanafunzi wangapi wa namna hiyo? Mzazi umechukua jitihada gani?
Watoto wote wa wakubwa wanasoma shule ya FEZA&the likes.

Watoto wa nyerere walisoma Tabora boys.

Safi kabisaaaaaa.
 
Unamshangaa wa std 5?, njoo secondary uone maajabu ya dunia.Kusema kweli, Ili niwe Mwalim halisi, natakiwa nifanye kazi Massa 24 kwa mchanganuo ufuatao,
1.SAA 07:30am-15:30pm. Huu ni mda wa kukimbizana na topics/maada kulingana na mpango kazi wangu wa mwaka mzima.
2.16:00-nakuendele ni mda wa kuwasaidia wale SLOW LENERS kama kuna maeneo hawakuelewa ktk mda wa kawada wa vipindi darasani.
3. Pia kama Mwalim natakiwa nikutane na angalau wanafunzi 2 au 3 kwa siku for private talk.Hii ni kwa wale watakao gundulika kuwa na msongo wa mawazo kwa siku hiyo.n.k huu ni mfano tu, Sasa serikar inanilipa 716000/= na wakichukua makato yao nabaki na kama 47..../=(degree holder) na hatunaga posho yoyote zaidi ya mshahara. Hivyo nalazimika kufanya kazi masaa 8 tuuuu! then naelekea dukani kwangu kukusanya pesa ya kumchekeshea shemeji yenu!
 
Hivi inawezekanaje mwanafunzi wa darasa la tano hajui kusoma..?
unamwambia nionyeshe W anakuonyesha R duh! mpaka nimechoka kabisa!! sasa hapa mtu anasoma au anapita tu..?!

hawa ndo wataalum tunaowategemea miaka ijayo kweli ama kweli waafrika tunahitaji kutawaliwa!! elimu ndo inatakiwa itukomboe lkn ndo inapita kama mpita njia tupu!

Serikali hebu wajalini walimu watengeneze watu wanaostahili msipowajali ama kuijali hii sekta ya elimu tutakapofikia patakuwa hapatamaniki for sure..
Nani hajui dunia ya sasa yahitaji wasomi..? Sasa kwa dizaini hii tutawapata kweli miaka 50+ sasa bado tunasuasua dah!

Lile shipa la aibu limetoka kabisa!.
Mkuu elimu bora ni gharama inanunuliwa bei ghali. Hali itakuwa MBAYA zaidi na hii elimu bure iliyijaa siasa za kipuuzi. Mkuu mwenyewe anakiri kuwa "Mzee bure" alifariki halafu upande wa pili anakufanyia sanaa kuwa suala nyeti kama ELIMU ni bure. Elimu ni gharama.
 
Waweza kuthibiti mtumishi yeyote utakavyo ila si Mwalimu, ukimlazmisha kuingia darasani ataingia tu ila utaelewa baadae kaenda kufanyaje.Walimu wa serikali hutumia 10%tu ya taaluma Yao nyngne ni ktk mambo mengne ya kujikimu kwa kipato. Mtasema Sana tu.
 
Rutashoborwa et all:-
Jibu tu kwa usahihi kuwa ni Sera ya chama chetu kuwaandaa wapiga kura wasiojua kusoma na kuandika ili wakati wa uchaguzi ukifika tumteue kada wetu awasaidie kuweka tick kwa mgombea wa chama chetu.
Mwisho wa siku chama chetu kinatangazwa kushinda kwa kishindo!
Ila kwa wale wanaojua kusoma na kuandika watawekewa ulinzi wa mbwa na maji ya kuwasha na hata kukataliwa kuwa siyo wakazi wa eneo husika ili mradi tu chama chetu kishinde.
Waambie pia kuwa walimu ni muhimu wakati wa kukierejesha chama chetu kitukufu madarakani na wakishasimamia uchaguzi wanawekwa pending wakisubirishwa kwa uchaguzi.
Maslahi ya walimu in kusimamia chaguzi zetu tu basi!
 
he he! bado tunakazi sana nchi hii mambo mengine unaweza kusema ikawa kama unatukana!
kama walimu wanakumbwa na yote hayo(watu wanao noa bongo za watoto ambao ndio taifa la kesho)hawajaliwi tutegemee madudu tu na mang'amng'am ya hovyohovyo tunatengeneza taifa la wenye navyo ndo wawe juu maskini tutajiju dadeki!!
 
mkuu me kwanza sina mtoto badobado haya nimeyaona kwa mtoto wa fulani...
ndio mzazi lzm amuangalie mtt lkn mkuu nini maana ya mwalimu..?
Hili swali iulize serikali kama inajua ni nini maana ya mwalimu!!!? Kama serikali haijui hiyo kitu basi jibu ni hicho ulichokiona kwa huyo mtoto.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom