Sam Mahela sasa ndani ya TBC1

Sam Mahela sasa ndani ya TBC1

Mpaka leo ni Wakala tena mkubwa tu na anayetambuliwa na FIFA Mkuu. Jamaa ni mjanja mjanja na Mtoto wa mjini sana. Kala sana Pesa za Manji miaka mitatu iliyopita ambapo Simba SC tumeshafanya vibaya sana huku akishirikiana na Kiongozi mmoja Mkuu wa Simba SC mwenye jina la ' Tabaka ' fulani la Wazungu la Afrika ya Kusini ambalo liliwatesa mno Waafrika huko na hasa hasa Hayati Mzee Mandela.

Wawili hawa ndiyo walikuwa wakimuuzia Manji na yule wa TFF Ramani zote za Vita za Simba SC hadi kupelekea Simba SC kuteseka mno katika hiyo miaka na Mwenyezi Mungu akasikia Kilio chetu ambapo yule yule Nyoka aliyekuwemo ndani ya Simba SC yakamkumba ya kumkumba na huku tena na yule wa TFF nae yamemkuta huku Simba SC yetu sasa ikichanja tu mbuga kimafanikio. Amini usiamini Wawili wote hawa ni wana Yanga SC wa Kufa Mtu ila wana Simba SC wengi hawajui.
namjua sam(salumu) mahela kiundani...alisoma kule mkoani tabora shule moja ya kanisa
 
Tatizo lake anajipodoa saana na kutinda nyusi kabla hajaingia studio
Sasa kuna mwanaume gani mwenye kutinda nyusi?
 
Mpaka leo ni Wakala tena mkubwa tu na anayetambuliwa na FIFA Mkuu. Jamaa ni mjanja mjanja na Mtoto wa mjini sana. Kala sana Pesa za Manji miaka mitatu iliyopita ambapo Simba SC tumeshafanya vibaya sana huku akishirikiana na Kiongozi mmoja Mkuu wa Simba SC mwenye jina la ' Tabaka ' fulani la Wazungu la Afrika ya Kusini ambalo liliwatesa mno Waafrika huko na hasa hasa Hayati Mzee Mandela.

Wawili hawa ndiyo walikuwa wakimuuzia Manji na yule wa TFF Ramani zote za Vita za Simba SC hadi kupelekea Simba SC kuteseka mno katika hiyo miaka na Mwenyezi Mungu akasikia Kilio chetu ambapo yule yule Nyoka aliyekuwemo ndani ya Simba SC yakamkumba ya kumkumba na huku tena na yule wa TFF nae yamemkuta huku Simba SC yetu sasa ikichanja tu mbuga kimafanikio. Amini usiamini Wawili wote hawa ni wana Yanga SC wa Kufa Mtu ila wana Simba SC wengi hawajui.
Kaburu!!
 
Kitambo sana sijamsikia Sam Mahela, mtangazaji mahiri sana IPP Media hasa ITV na Radio One. Napenda sana akiwa anareport ITV Habari saa 2 usiku. Ana kisauti fulani hivi kizuri sana ila siyo kama cha Kivuyo.

Sam Mahela popote ulipo kaka yangu… big up sana !
Yuko TBC na si unajua TBC huwa hatuiangalii sana kivile ndiyo maana humuoni. Ukiwa mpenzi wa TBC utamuona sana.
 
Bora angeenda Azam au hata star Tv huko alipoenda naweza pita miaka 2 sijafungua hiyo channel sababu vipindi vinaboa taarifa zao picha sio clear yaani ni yakizee haswaaa mara ya mwisho kuangalia Tbc kipindi cha chereko kilipokuwa hot mtangazaji sijui glory nani alivyotoka yule mtangazaji nikapotea na mie Sam hukuona nafasi hata Efm au TV1 kweliiii au ungeenda hata sibuka tv

Ingekuwa wewe uchague kati ya laki nne uliyoizoea kila siku na milioni moja ya uhakika yenye security yakutosha kwa kazi yako unafkiri utaenda wapi?
 
Back
Top Bottom