Mtanzania,
Ninakubaliana na wewe kwa asilimia nyingi sana kwenye hoja yako. Lakini kuna sehemu ndogo tu ambayo tunatofautiana. Mifano yako wa Jews ambao wamehamia kwenye nchi nyingine na kwenda kushika nyadhafa kubwa kubwa ninaikubali kabisa. Nadhani kitu unachokikosa kwenye hoja yako ni kimoja, hao wahamiaji walifuata taratibu zote za nchi na kuhakikisha wamepata uraia wao kwa njia halali.
Keil,
Ndio maana nimetumia mfano wa Jews ili wengine muelewe. Jews walikuwa wanatoroka kwa kutumia njia mbalimbali, wengine walikuwa wanazamia USA na hapa UK. Walivyoingia wengi wao
wala hawakushughulikia uraia wao. Wanao waliozaliwa walikuwa
wanajua ni raia na wameendelea hivyo. Hata pale ilipogundulika kwamba kuna tatizo basi wahusika walisaidiwa kufuata utaratibu.
Mfano mzuri ni Howard aliyekuwa kiongozi wa Tories ambaye mwenyewe alishakiri kwamba babake alizamia kutokea Romania na kuingia UK kwa kudanganya. Sikusikia Blair akishangilia na kusema kwasababu baba yako hakuwa raia halali na wewe sio raia. Lakini ingelikuwa sisi Afrika hapo tungekuwa tumepata sababu.
Tofauti yetu Tanzania ni kwamba ubinafsi na roho mbaya vimetuzidia kiasi kwamba serikali na rais wake wanaweza kumwambia Ulimwengu sio raia. Sasa wengine tumeingia kumwandama
Rweyemamu kuwa sio raia. Sikubaliani na Rweyemamu lakini siwezi kudiriki hata kusema sio raia kwa mtu ambaye najua kazaliwa Tanzania na kakulia Tanzania miaka yote hiyo.
Kule mipakani watu wote ambao waliingia TZ kutoka sehemu zingine hakuna aliyekuwa anaenda serikali kujisajili, kwanza hata walikuwa hawaelewi kuna kujisajili. Uongozi wa vijiji ndio ulikuwa unawakaribisha na kuwapatia maeneo ya kuishi. Mnachoongelea sasa ni kama kilichompata Kaunda kule Zambia, hivi kweli mtu mwenye akili na asiyejaa chuki kichwani atasema Kaunda hakuwa raia wa Zambia?
Kwa kweli nashindwa kuelewa msingi wa hoja ya kumwambia mtu ambaye kazaliwa TZ na kukaa Tanzania miaka yote hiyo kwamba sio raia. Hata kama kuna makosa basi wazazi ambao ndio walifanya makosa ndio waadhibiwe na sio watoto.