Baada ya kupitia thread hii yote nimegundua yafuatayo:
Mosi, watanzania hatuelewi umuhimu wa uraia, kama jinsi ambavyo nchi nyingine zina thamini uraia. Dunia nzima hakuna mahali mtu ambaye si raia anaweza kupewa kazi serikalini na hasa kama kazi yenyewe ni sensitive. Ikulu ni sehemu nyeti sana, na mtu aliye kwenye post kama ambayo amepewa Salva ana uwezo wa ku-access info nyingi sana ili aweze kujua namna ya kujenga na kutetea hoja zake pindi anapokutana na wana media ambao wako makini. Kama Ikulu ikishindwa kumpa info za kutosha maana yake ni kwamba atashindwa kuwasiliana na wana habari na hilo litaifanya serikaali iwe na wakati mgumu zaidi. Kwa hiyo hoja ya uraia mpaka hapo naona bado iko valid. Una imani gani na mtu ambaye huna uhakika na uraia wake, je akitumia hizo info kwa nia mbaya utamlaumu nani? Kazi aliyopewa Salva huwezi kulingaanisha na kazi za kubeba box za UK au US ambako illegal immigrant yeyote anaweza kuifanya na wala kusiwe na shida yoyote.
Mbili, hoja ya uraia imekuwa ikiibuka pindi linapokuja swala la maslahi. Kumbukumbu yangu inasema kwamba Jenerali Twaha Ulimwengu alikuwa kwenye timu ya kampeni ya BWM, lakini pindi alipoanza kuikosoa serikali, rungu la uraia lilimshukia. Kwa maneno mengine serikali ilijua wazi kwamba the guy was not a citizen lakini wakaja kuibua hoja hiyo ili kummaliza. Marehemu Nabwa aliwahi kuwa mwandishi wa Makamu wa Rais, alipokuja kuwa mwiba mkali kwa serikali ya Mapinduzi ya Zenji akashukiwa na rungu la uraia. Salim ili kukatwa makali ya ushindani kwenye kinyang'anyiro cha urais, alishukiwa na rungu la uarabu ambao una uhusiano mkubwa sana na swala la uraia. The list goes on ... swali, kama Salva aliweza kumdunda Salim na rungu la uraia ili akose urais kwanini na yeye asidundwe? Dhambi ya kula nyama ya binadam ukishaitenda itakuandama kila utakapoenda, Salva alianzisha mwenyewe na sasa ni zamu yake kushughuliwa, sioni kama ni dhambi kujadili uraia wake na hasa ikizingatiwa kwamba ni yeye ndie aliyeanzisha haya mambo na sioni sababu ya watu kumtetea. (Mtazamo wangu kwenye hili ni kwamba linatumiwa kimakosa, objective si ulinzi na usalama bali ni kukomoana na kumalizana, lakini kwa kuwa nae alicheza mchezo mchafu ngoja aonje machungu ya mchezo huo)!
Tatu, kuna watu wamekuja na swali la why now? Ni sawa na illegal immigrant akiamua kujilipua na kufanya kazi za kubeba box, hakuna mtu atakayemfuatilia. Lakini siku huyo illegal immigrant akionekana anapewa kazi sensitive ya akina Tony Snow, hakuna Mmarekani hata mmoja ambaye atakubaliana na hilo. Kama mtu ana doubt na uraia wa Salva ni bora aseme mapema ili achunguzwe na ijulikane wazi kwamba jamaa siyo raia. Kuuliza kwamba kwanini watu hawakuhoji hapo awali, jibu lake ni rahisi sana. Tulikuwa tunamuona kama mbeba box tu wa Bongo na kuwepo kwake Tanzania hakuwezi kuhatarisha usalama wa nchi. Kwa hiyo watu wameuliza uraia baada ya kuona amekwaa post nyeti ambayo ikishikwa na foreigner ni hatari maana huwezi kujua kama ana uchungu na Tanzania. Dr. Laurian Rutayisire alifundisha Mlimani miaka mingi mpaka akawa Associate Prof lakini alipoitwa kurudi Rwanda alienda mbio bila hata kuaga. Ukichunguza sana utakuta kwamba alisomeshwa na hela ya Tanzania, yet akashindwa kulipa fadhila kwa watanzania waliotoa kodi ya yeye kusoma. Je, mtu huyo ana uchungu gani na Tanzania? Suppose huyo mtu angekuwa alishafanya kazi Ikulu ya Tanzania, ungekuwa na uhakika gani kwamba siku ikitokea Kigali na Dar wametofautiana hawezi kutoa nyeti za Ikulu ya Dar? Tusiwe na mtazamo finyu wa ku-analyze mambo halafu siku yakija kulipuka ndipo tunaanza kulia lia kwamba ilikuwaje na huku watu walikuwa wamekaa kimya.
Makala ya gazeti la The East African iko wazi, Kamanzi amesema ana ndugu wengi wako Bongo, je tunajua wako ofisi zipi? Siku Kamanzi akihitaji info kutoka Ikulu yetu na kama kuna ndugu yake Ikulu unadhani atashindwa kuzipata? Let us be serious kwenye haya mambo na siyo kutanguliza mawazo kwamba mtu akija na hoja ya uraia basi inalenga kwenye wivu au kumharibia mtu kitumbua chake!