Salome: Diamond Platnumz ft Rayvanny - General Views

Salome: Diamond Platnumz ft Rayvanny - General Views

Mkuu sawa sasa nyimbo mpya imetoka badala watuletee mashabiki tuione wao wanakazana kuleta habari za kiba sijui huyo kijana kawafanya nini?
Mkuu mbona nyimbo za Mfalme Simba zikitoka kila binadamu anazipata automatically haina haja ya kuletewa hapa.. kama upo ndani kwa nje utasikia ikipigwa kwenye ma-speaker makubwa.. JUZI TULIMLETA DOGO KIBA PALE WASAFI KU-RECORD ALIKUA ANASHANGAA NA KUOGOPA, IKABIDI DIAMOND AMWAMBIE USIOGOPE KUWA HURU KIJANA...
 
Kama kaikubari ni jambo jema hizi bifu zikaisha wakawa wanapongezana kwenye mziki mzuri
 
Huyu bwanamdogo anafanya investment za kutosha, haugopi kuwekeza katika muziki wake!

Atafika mbali saana, Kiba ajifunze kitu hapo, sio zile 800Million tunazosikiaga anaishia kuhonga tu, awekeze atupeleke waTZ mbele zaidi, manaake kwenye michezo yoote tushafeli labda muziki utatutangaza wabongo,

Nasubiria kwa hamu nione Kiba atajibu vp
 
nimesoma youtube eti original version ilikua ya mfalme kabaka na sio saida karoli
 
niseme tuu kutoka moyoni platnum nilikua cmkubaliii kivileee ila kwa hiii ngoma nime kaaa ila ina bidi amlipe saida
 
Mnajitekenya halafu mnacheka wenyewe domo ana roho mbaya sana kama ruge
 
[Verse 1: RayVanny]

Kioo hakidanganyi mama
Umejipodoa umepodoka
Mwendo na shape vyote mwanana
Mi suruali yanidondoka
Tukimbizane nini Salome wangu?
Hiyo michezo ya jogoo
Mbona watizama chini Salome wangu?
Ukimuona jongoo
Inama kidogo
Shika magoti
Mi nimesimama kama ngongoti
Mtoto jojo sio roboti
Chumbani bingiribingiri 'samasoti'

[Chorus: Diamond Platnumz]

Unantenkenyaga ukinyonga Salome
(Unantekenyaga ukinyongaa)
Unantenkenyaga ukinyonga kweli
(Unantekenyaga ukinyongaa)
Aaah orera bakuru vani
Orera ngambee
Orera na Zari ma
Orera ngambe

[Verse 2: Diamond Platnumz]

Utamu kolea a porokoto
Ting'ali ting'ali ndani kwa moto
Ntamnyongea msokoto
Nteme sumu kali kama koboko
Eeh mapenzi yananipa shida
(Shida mama)
Ni donda lisilokuwa na tiba
(Tiba bwana)
Usije baby ukanicharanga
Ukanichambua moyo kama karanga
Mie baby kwenye msambwanda
Huwa siendagi nge nge ni nga nga nga

[Chorus: Diamond Platnumz]

Unantenkenyaga ukinyonga Salome
(Unantekenyaga ukinyongaa)
Unantenkenyaga ukinyonga kweli
(Unantekenyaga ukinyongaa)
Aah orera bakuru vani
Orera ngambee
Orera na Zari ma
Orera ngambe

[Verse 3: RayVanny]

Miee mwenzako nyang'anyang'a
Miee binzari we ndio nyanya
Baby kwang'waru
Nisimamie kama kangaroo
Ibane kangwaru
Babu Juma mpige kwakwaru
(Kwakwarukwa)

[Bridge]
Asa chambua kama karanga sasa
(Chambua kama karanga)
Ichambue kama karanga Salome
(Chambua kama karanga)
Asa washa, washa, moto washa, washa
Songa, songa, ugali songa, songa
Mpaka chini ka chi
Mpaka chini ka chi

Wenye wivu wajinyonge leo
(Wenye wivu wajinyonge)
Aaah wenye wivu wajinyonge sana
(Wenye wivu wajinyonge)
Wenye wivu wajinyonge kweli
(Wenye wivu wajinyonge)
Oooh wenye wivu wajinyonge sana
(Wenye wivu wajinyonge)

[Outro]

Wanakodoa kodo!
Wanakodoa
(Macho kodo!)
Wanakodoa kodo!
Wanakodoa
(Wale kodo!)
Wanakodoa kodo!
Wanakodoa
(Ukinyonga)
Wanakodoa kodo!
Wanakodoa
(We ukisonga)
Wanakodoa kodo!
Wanakodoa
 
Ndio nimetoka kuipakua nyimbo mpya ya Mond.
Dahhh.....
Kiukweli kijana ameifanya poa sana, hata nikirejea kwa waliokua wakisema amecopy Saida......
Mhhhh.....
Hapana, ebu ngoja nikatae aiseeee.... ninachoweza sema ni, kijana kakoleza kwa vionjo vya kiafrika.
Na hata wanaosema ambana kwa Salome, Naahhhh basi tuseme pia Mr Flavor pia ameibiwa.
Nimeaskia kijana kamtaja na Zari ndani
 
Diamond alitakiwa kupata ruhusa kwa saida,.Duniani kote wasanii wakubwa wana utaratibu huu,.mfano ngoma aliyofanya mayunga na akoni chorus ilikuwa ya msanii wa zamani kutoka afrika ya kusini..walipata kibali(walitoa mtonyo) ndio wakapewa ruhusa ya kuachia ngoma
Saida ameshtaki kuwa kaibiwa???
 
Sasa usiwe unaongea bila kujua saida kalori na management yake washapewa hela yao nashangaa ww kulalamika mkuu
Hapo chacha utadhani wamepokea malalamiko kutoka kwa saida hawa sijui wa wapi hawa
 
Ebwana hii wimbo ni nomaa aseee, nimeisklza karibia mara 50 na bado haichoshi, audio nzuri video ndo balaaaa.

Hiyo video nyengine ya version ya club aache kwanza maaanaa
 
HIP _is the movement
HOP_is the intelligent
So HIP_HOP is the Intelligent Movement
 
Leo ndo nimeamini kuwa kweli mimi ni hater...Maana watu wote humu wanausifia huu wimbo but naona kawaida sana...Yani sioni jambo kusifia kabisa...I must be a hater
 
Yaani kaimba wimbo wa asili yetu halafu video Ina asili ya Nigeria na Yale majuba aloyavaa hahaa poor diamond , alikosa kushona hata vitenge aendane na tamaduni yetu watz, najua mtapinga ila kiukweli hajawatendea haki wabongo huo sio utamaduni wetu japo wimbo ni wa kwetu
Well said
 
Diamond kakopi nyimbo za watu hizo
1474259856248.png
 
Back
Top Bottom