Haya mambo tuna kila sababu ya kuangalia kwa kina kuwa ni kwanini yanatokea sasa ,
\kwani ukiangalia kwa kina utaanza kujiuliza kuwa wale wana NEC ambao walitaka mafisadi wa EPA wachukuiw hatua hawatakuwa na mjadala kikao cha keshokutwa huko Dododma maana sasa issue itakuwa NNAPE.
Wenzangu na miye wa Zanzibar na hoja yao kuwa ni nchi ama laa na mjadala ambao huenda ungeweza hata kubadilisha historia ya taifa hili sionio kama utakuwepo tena kwani issue sasa ni Nnape.
Wale waliohoji kuhusu Richmond ,mjadala huo hautakuwepo tena kwani umezimwa kisayansi na kwa kutumia mbinu za kikomunist kwelikweli.
Kwani sioni kama ni kweli kuwa hawa wazee akiwemo kawawa eti wanaweza wakawa wamefanya walichofanya bila kufanya political calculations za kutoshga na haswa kuhusiana na madhara ambayo wanaweza kuyapata baada ya uamuzi huo.
Nnape , anapaswa kuamua moja na kama kweli alikuwa ni mtu anayepingana na ufisadi hana budi sasa kufanya maamuzi mazito ,na hilo litampa kinga ya kuendelea kuishi kwani akiwa humohumo kikitokea chochote atakuwa amemalizika kwa stsil ile ile.\
\
Najaribu kuijitahidi kuangalia haya mambo kwa upana wake na haswa hao waliojihusisha kumngoa ,naona baraka za Mwenyekiti wa Chama taifa yaani Kikwete mwenyewe, ama pia wanaweza kuja kesho na kusema kuwa CC imeamua kumrejesha kwani vijana waliamua kwa jaziba ila kutokana na ukweli kuwa vijana hawamtakio basi hawezi kuwa kiongozi wao na hivyo asiwe mgombea.