Naona dhana ya uwajibikaji bado ni ngeni kwetu! Kazi ipo!
Rais ameishasema kwamba sakata la mahujaji lilitokana na sababu ndogo ndogo kwa kuwa ATCL bado haijawa na ndege za kwake na hivyo yaliyotokea yangeweza kutokea. Kama hawakuwa na ndege za kwao au kwa maneno mengine kama hawakuwa na uwezo wa kuwasafirisha mahujaji kwanini walijiingiza kwenye hiyo shughuli? Hiyo hasara ya milioni 160 italipwa na nani kama si kutoka kwenye kodi za walalahoi? Nyang'anyi akisikia kauli hiyo hata kama alikuwa na nia ya kujiuzulu unatarajia ajiuzulu? Maana mtu aliyemteua tayari kaishasema kwamba tatizo lilikuwa ni dogo na kwamba serikali inafanya jitihada za kuhakikisha wanarudi mara baada ya hijja. Kwa mwendo huu sidhani kama kuna watu watakuja kuwajibika chini ya utawala wa JK labda kama jamaa akiboronga sana kiasi cha kushindwa kumbeba! Tusitarajie chochote si Nyang'anyi ama Mattaka atakayejiuzulu ... Mkuu wa Kaya ameishawatetea, na hivyo Chenge nadhani anatwanga maji kwenye kinu tu!