Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Sakata la Kafulila na wenzake CHADEMA

Dr Slaa alishatoa ufafanuzi, si akaunti zote mwenyekiti anasaini. Lakini pia, haisaini maombi wala kuidhinisha matumizi. Yeye anachosaini ni kwa nia ya kudhibiti benki fedha kutoka. Maandalizi ya malipo yanafanywa na Mkurugenzi wa Fedha na kuidhinishwa na Katibu Mkuu. Hivyo, kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA accounting officer ni Katibu Mkuu hivyo kama kuna matatizo kwenye matumizi ya CHADEMA wa kuhojiwa ni Dr Slaa sio Mbowe.

Umetaja suala la fedha za Conservative, Dr Slaa alishaeleza kwamba toka mwaka 2005 CHADEMA haijawahi kupokea fedha toka chama hicho. Sasa fedha za Conservative wakati huo Mkurugenzi wa Mambo ya Nje alikuwa Zitto Kabwe. Na ni fedha kidogo sana, na Zitto alishazitolea ufafanuzi humu humu JF kuwa ni kiwango gani na zilitumikaje, hayo uliyoyataja hakuyasema kabisa. Hebu fanya search tu hapa utaona. Sasa kama unasema zilijenga Bilicanas au kuanzishia Tanzania Daima unataka kutuambia kwamba Zitto alitudanganya humu kumlinda Mbowe?

Asha


billcanas je?
 
Nawaambieni Hakuna mtu anayetea maslahi ya Taifa akatetea CCM na akatetea CHADEMA .

CHADEMA ni kihiyo cha ajabu sana , hakuna hata mjinga mmoja atakaye kubaliana na maneno eti amesema vibaya ktk vyombo vya habari ihiali kila mmoja anatambua bayana ni vita ile ile .

Hapa hakuna cha Slaa wala nini Slaa naye ni kihiyo tu kama vihiyo vingine.NUKTA
anaendeshwa na fisadi Mbowe kama karagosi lilokosa mwelekeo.
Afadhali wewe uliyekwenda nchi za ulaya mashariki kufuta ukihiyo! na inaonekana kama hujafuta ukihiyo na wewe nadhani umeandika haya kwa sababu ni kihiyo!
 
Afadhali wewe uliyekwenda nchi za ulaya mashariki kufuta ukihiyo! na inaonekana kama hujafuta ukihiyo na wewe nadhani umeandika haya kwa sababu ni kihiyo!

teh teh teh teh

CHADEMA ni kihiyo cha kutisha
Mbowe fisadi .
Slaa fisadi.
kihiyo wa kwanza ni Mbowe maana hata mwaka mmoja ka DISCO ,ulaya wa kiku DISCO wewe jua ni mjuha wa kutisha, maana ma prof wa ulaya hawana chuki wanakupa nafasi ku SUP.

Sasa kihiyo Mbowe kilipigwa chini within NO SECOND.Sishangai sana hata anavyoendesha kampuni yake CHADEMA.
 
KAKASLAA.jpg



Mwangilie huyu fisadi utafikiri anawaza la maana


Vipi mkuu kuna mtu ameiba password yako?, maana naona unaandika vitu ambavyo ni tofauti na yule niliyemzoea.

Dr Slaa amefanya UFISADI upi tena?, tuhabarishe.

Kuwa na heshima kidogo..
 
Vipi mkuu kuna mtu ameiba password yako?, maana naona unaandika vitu ambavyo ni tofauti na yule niliyemzoea.

Dr Slaa amefanya UFISADI upi tena?, tuhabarishe.

Kuwa na heshima kidogo..
Hakuna mtu kaiba password yake lakini kama kawaida ni mmoja wa low thinkers wa jf, pamoja na kwenda shule ulaya mashariki.
Hapa sijui yeye shule imemsaidia nini? Ni bora angekaa hapa kuliko kupoteza pesa ya walipa kodi!
 
Mmh hapo patakua hapatoshi kisiasa Tanzania, maana kwa hakika CHADEMA imeshachukua umaarufu vya kutosha na inahitajika busara katika kufanya kila jambo kabla ya kuonesha mpasuko wa namna hii - kama hizi habari ni za kweli - basi dunia yangu siasa inaisha.
 
Vipi mkuu kuna mtu ameiba password yako?, maana naona unaandika vitu ambavyo ni tofauti na yule niliyemzoea.

Dr Slaa amefanya UFISADI upi tena?, tuhabarishe.

Kuwa na heshima kidogo..


Heshima gani
fisadi ni fisadi tu ,sasa unataka niwe na heshima gani?

Huyu jamaa alishiriki kumsimamisha Wangwe na akatetea sana ule uamuzi , binafsi mimi kama mimi nilifikiri jamaa wenda kawastahi viongozi wenzake ama ni mapungufu ya kibinadamu.

Jamaa karudia tena yale yale ,sasa namwiita rasmi SLAA ni FISADI lilokomaa na MNAFIKI wa KUTUPWA.

Heshima gani huyu FISADI anastahili kuita wenzake SISIMIZI??
 
Kamati Kuu ya Chadema kujadili uamuzi wa Dk Slaa
broken-heart.jpg
Exuper Kachenje na Fidelis Butahe

KAMATI ya Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa kukutana kati ya Novemba 27 na 28 mwaka huu, kujadili pamoja na mambo mengine, pepo baya la kisiasa lililoanza kukikumba chama hicho cha upinzani.

Pepo hilo, linafuatia uamuzi wa Katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa, kuwafuta kazi maafisa wawili wa Chadema kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.

Kufutwa kazi kwa maafisa hao David Kafulila aliyekuwa Ofisa habari wa chama hicho na Danda Juju, aliyekuwa akishughulikia mambo ya Bunge katika chama hicho, kulitangazwa juzi na Dk Slaa.

"Tena andika mwandishi wala usiogope ni kwamba leo, (juzi) kulikuwa na kikao, nimekiongoza mwenyewe na maamuzi nimeyatoa mwenyewe, tumetengua uteuzi wao. Sasa ni wanachama wa kawaida," alinukuliwa Dk Slaa katika mahojiano na gazeti hili juzi.

Hatua hiyo imeibua majeraha ya kisiasa yaliyotokana na uchaguzi wa viongozi ndani ya chama hicho, uliofanyika Septemba mwaka huu.

Tayari Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amepinga vikali hatua ya kufukuzwa kwa watendaji hao, wanaotajwa kuwa ni washirika wake wakubwa kisiasa, tangu mbio za uchaguzi uliomtikisa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Jana Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema, Bob Makani alisema, "suala hilo tutalijadili katika kikao cha Kamati Kuu ambayo itakutana kabla ya mwisho wa mwezi huu. Bahati mbaya sijawasiliana na uongozi siwezi kujua ni tarehe gani."

Hata hivyo alielezea matumaini yake kuwa haki itakuwa imetendeka kwa wanachama hao ambao walikuwa waajiriwa wa Chadema na kwamba ndiyo maana walipewa nafasi ya kujitetea.

Makani alifafanua kwamba, kimsingi, mwajiriwa anapaswa kufuata sheria na kanuni za mwajiri wake na kwamba, kama Kafulila na Juju hawakuzingatia hayo na kuendekeza majungu ndani ya chama na kuvunja katiba, hawawezi kuvumiliwa.

"Hao ni waajiriwa, katika ajira kuna maadili, sheria na kanuni, kama ni kweli wameleta majungu ndani ya chama hawawezi kuvumiliwa," alisema Makani.

Hata hivyo vyanzo huru vya habari, vilidokeza kuwa mkutano huo unatarajiwa kufanyika kati ya Novemba 27 na 28 mwaka huu.

Habari hizo zimekuja huku kukiwa na habari nyingine kuwa Mwenyekiti wa chama hicho (Mbowe), Dk Slaa na maafisa wao kadhaa walitarajiwa kukutana jana katika kikao cha siri, kujadili upepo ulivyo ndani ya Chadema.

Habari zaidi zilisema baadhi ya wanachama wa Chadema mikoani wakiwemo wenyeviti wao, wamekerwa na kitendo cha Dk Slaa, kumlinganisha Kafulila na mdudu sisimizi.

Kwa mujibu wa habari hizo, wanachama hao wamekuwa wakihoji kama ndani ya Chadema kuna sisimizi na tembo na kwamba kama yapo basi chama kina matabaka ya watu, jambo ambalo si la haki.

Akizungumzia kuwepo kwa mpasuko ndani ya Chadema , Makani alisema haoni kama uamuzi huo unaweza kuathiri chama wala kuzidisha ufa.

Alisema mpasuko unaweza kujitokeza zaidi kama tuhuma dhidi ya maafisa hao zitathibitika kuwa ni za kweli na wakaachwa ndani ya chama.

Katika uamuzi wake Dk Slaa alisema ametengua ajira za wanachama hao wawili kwa maslahi ya chama, hatua iliyotangazwa siku kadhaa tangu kuvuja kwa siri za kikao kati ya Mbowe na baadhi ya viongozi wa Chadema.

Habari za awali zilisema kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma, kilijadili pamoja na mambo mengine, nidhamu ya wanachama hao pamoja na mama mzazi wa Zitto, Shida Salum.

Habari tulizopata wakati tunakwenda mitamboni zilisema baadhi ya wazee wa Kigoma, wamemtaka Kafulila kuwa jasiri na kutokata tamaa ili hatimaye awanie ubunge katika Jimbo la Kigoma Kusini.

Vyanzo vya habari za kuaminika, vilifafanua kwamba wazee hao walikutana na Kafulila juzi usiku baada ya kuvuliwa wadhifa aliokuwa nao.

Habari hizo zilieleza kwamba, wazee wakiwemo viongozi wa dini wameelezea kuchukizwa na uamuzi wa Dk Slaa, kumvua Kafulila wadhifa wake.

Kafulila alipoulizwa kuhusu mkutano huo na wazee, alijibu: "Hapana kaka hakuna kitu kama hicho, mimi bado naombea Chadema kiwe chama kimoja."

Hata hivyo, habari hizo za ndani zilikariri wazee hao wakitaka Kafulila na mwenzake Juju warejeshwe kwenye nafasi zao mara moja ili kuleta amani na utengamano katika chama.

Wakati mzee Makani akiweka matumani ya uhai wa Chadema, hali ya kisiasa ndani ya chama hicho ni tete kufuatia kuwepo kwa kambi zinazopingana.

Hali hiyo tete kisiasa inatokana na baadhi ya wanachama kuona, uamuzi huo wa Dk Slaa, kuwa umefanywa kwa chuki zilizotokana na majeraha ya uchaguzi wa viongozi ndani ya chama.

Katika uchaguzi huo wa Septemba, Zitto alimtikisa Mbowe, baada ya kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti. Mpasuko mkubwa ambao ulijitokeza katika kipindi hicho unaonekana kuisumbua Chadema
 
Hakuna mtu kaiba password yake lakini kama kawaida ni mmoja wa low thinkers wa jf, pamoja na kwenda shule ulaya mashariki.
Hapa sijui yeye shule imemsaidia nini? Ni bora angekaa hapa kuliko kupoteza pesa ya walipa kodi!


Heri mimi nimemaliza shule je Mbowe kufeli na kurudi home hajapoteza hela za walipa kodi??
 
KAMATI ya Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa kukutana kati ya Novemba 27 na 28 mwaka huu, kujadili pamoja na mambo mengine, pepo baya la kisiasa lililoanza kukikumba chama hicho cha upinzani.

Hiyo Kamati kuu itakuwa imepoteza mwelekeo kama hata katibu mkuu akifukuza ofisa wa chama wanajadili basi hawana la kujadili na wamepoteza mwelekeo.

Jana Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema, Bob Makani alisema, "suala hilo tutalijadili katika kikao cha Kamati Kuu ambayo itakutana kabla ya mwisho wa mwezi huu. Bahati mbaya sijawasiliana na uongozi siwezi kujua ni tarehe gani."

Hapa hili gazeti inaonyesha kuwa habari zao ni za kutunga hivi kweli Bob Makani ni mwenyekiti wa baraza la wazee? Mwananchi linakoelekezwa siko kwani linaonekana kabisa kuwa linafanya zaidi spinning.

Habari hizo zimekuja huku kukiwa na habari nyingine kuwa Mwenyekiti wa chama hicho (Mbowe), Dk Slaa na maafisa wao kadhaa walitarajiwa kukutana jana katika kikao cha siri, kujadili upepo ulivyo ndani ya Chadema

utabiri ule ule wa sheikh yahaya , hata gazeti makini kama hili linaandika habari kama hizo? mbona ni spinning za kitoto sasa mhariri utatuulia gazeti.

Hali hiyo tete kisiasa inatokana na baadhi ya wanachama kuona, uamuzi huo wa Dk Slaa, kuwa umefanywa kwa chuki zilizotokana na majeraha ya uchaguzi wa viongozi ndani ya chama.

Kama ni kweli kuwa Kafulila aliita kikao kilichofanyika Dodoma kama alivyonukuliwa na gazeti la mwananchi jumapili kuwa ni kikao cha gheto anastahili kuchukuliwa hatua alizochukuliwa kwani kama ni afisa habari anaenda public na kusema kuwa kikao ni cha gheto huo ni uhuni na mtu kama huyo hafai kuwa afisa habari wa chama .

Ushauri CHADEMA nendeni hapo kwa wanangangari buguruni wawape mkakati wa jinsi ya kushughulikia watu hawa.
Nikija nitawasaidia .
 


Kama ni kweli kuwa Kafulila aliita kikao kilichofanyika Dodoma kama alivyonukuliwa na gazeti la mwananchi jumapili kuwa ni kikao cha gheto anastahili kuchukuliwa hatua alizochukuliwa kwani kama ni afisa habari anaenda public na kusema kuwa kikao ni cha gheto huo ni uhuni na mtu kama huyo hafai kuwa afisa habari wa chama .

Huyo Ndiye Afisa Habari wa CHADEMA, afadhali kaka umeliona hilo
 
KAMATI ya Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa kukutana kati ya Novemba 27 na 28 mwaka huu, kujadili pamoja na mambo mengine, pepo baya la kisiasa lililoanza kukikumba chama hicho cha upinzani.

Hiyo Kamati kuu itakuwa imepoteza mwelekeo kama hata katibu mkuu akifukuza ofisa wa chama wanajadili basi hawana la kujadili na wamepoteza mwelekeo.

Jana Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema, Bob Makani alisema, "suala hilo tutalijadili katika kikao cha Kamati Kuu ambayo itakutana kabla ya mwisho wa mwezi huu. Bahati mbaya sijawasiliana na uongozi siwezi kujua ni tarehe gani."

Hapa hili gazeti inaonyesha kuwa habari zao ni za kutunga hivi kweli Bob Makani ni mwenyekiti wa baraza la wazee? Mwananchi linakoelekezwa siko kwani linaonekana kabisa kuwa linafanya zaidi spinning.

Habari hizo zimekuja huku kukiwa na habari nyingine kuwa Mwenyekiti wa chama hicho (Mbowe), Dk Slaa na maafisa wao kadhaa walitarajiwa kukutana jana katika kikao cha siri, kujadili upepo ulivyo ndani ya Chadema

utabiri ule ule wa sheikh yahaya , hata gazeti makini kama hili linaandika habari kama hizo? mbona ni spinning za kitoto sasa mhariri utatuulia gazeti.

Hali hiyo tete kisiasa inatokana na baadhi ya wanachama kuona, uamuzi huo wa Dk Slaa, kuwa umefanywa kwa chuki zilizotokana na majeraha ya uchaguzi wa viongozi ndani ya chama.

Kama ni kweli kuwa Kafulila aliita kikao kilichofanyika Dodoma kama alivyonukuliwa na gazeti la mwananchi jumapili kuwa ni kikao cha gheto anastahili kuchukuliwa hatua alizochukuliwa kwani kama ni afisa habari anaenda public na kusema kuwa kikao ni cha gheto huo ni uhuni na mtu kama huyo hafai kuwa afisa habari wa chama .

Ushauri CHADEMA nendeni hapo kwa wanangangari buguruni wawape mkakati wa jinsi ya kushughulikia watu hawa.
Nikija nitawasaidia .


Mkuu tuchukulie ni kweli jamaa iliita GHETO hicho kikao, na mwezake adhabu yake inatokana na kukiita kikao hicho jina gani?
 
Heri mimi nimemaliza shule je Mbowe kufeli na kurudi home hajapoteza hela za walipa kodi??

Hivi Chiligati angetokea na Kusema kwamba Kikao cha Kamati ya Mzee Mwinyi na wabunge wa CCM kilikuwa ni Kikao cha GHETO hivi JK au Makamba wangechekelea tu bila kumchukulia Hatua yeyote ya Kinidhamu?
 
Hivi Chiligati angetokea na Kusema kwamba Kikao cha Kamati ya Mzee Mwinyi na wabunge wa CCM kilikuwa ni Kikao cha GHETO hivi JK au Makamba wangechekelea tu bila kumchukulia Hatua yeyote ya Kinidhamu?

mimi ninavyofamu afsa wa habari lazima afahamishwe habari ndani ya taasisi anayoihabarisha.

Kama afsa habari wa taasisi hakufahamishwa kinachoendelea na alipoulizwa kuhusu habari hizo yeye kama afsa habari hafahamu na kusema kama kilikuwepo kikao cha namna hiyo basi ni cha ki GHETO maana kama kingekuwepo kikao cha kitaasisi basi yeye kama afsa habari angekifahamu kuwepo.

Hapo hakuna kosa lolote.

Chilingati kama afsa habari alifahamishwa kuwepo kwa kikao hicho.
kwa hiyo hawezi kusema vinginevyo na ikitokea akasema basi itakuwa kakiuka maadili.
 
mimi ninavyofamu afsa wa habari lazima afahamishwe habari ndani ya taasisi anayoihabarisha.

Kama afsa habari wa taasisi hakufahamishwa kinachoendelea na alipoulizwa kuhusu habari hizo yeye kama afsa habari hafahamu na kusema kama kilikuwepo kikao cha namna hiyo basi ni cha ki GHETO maana kama kingekuwepo kikao cha kitaasisi basi yeye kama afsa habari angekifahamu kuwepo.

Hapo hakuna kosa lolote.

Chilingati kama afsa habari alifahamishwa kuwepo kwa kikao hicho.
kwa hiyo hawezi kusema vinginevyo na ikitokea akasema basi itakuwa kakiuka maadili.

Sasa kama hakufahamu uwepo wa kikao Hicho ilikuwaje akakilabel as Gheto Meeting!

Kama hilo ni jibu ambalo alilitoa kutoka Moyoni kwake na akiamini kwamba ni Correct answer then atakuwa na Matatizo ya Kukosa Busara na Mtu wa namna hiyo hafai hata kupewa Mke aishi naye.

Kama ni Kweli alijibu hivyo just because hakujua kama kuna meeting Idodomya then Hana Merrits za kuwa Kuwa Kiongozi ni vyema amewekwa Pembeni ili ajifunze namna bora ya Kuongoza na kujibu maswali katika Circumstance yeyote
 
Sasa kama hakufahamu uwepo wa kikao Hicho ilikuwaje akakilabel as Gheto Meeting!

Kama hilo ni jibu ambalo alilitoa kutoka Moyoni kwake na akiamini kwamba ni Correct answer then atakuwa na Matatizo ya Kukosa Busara na Mtu wa namna hiyo hafai hata kupewa Mke aishi naye.

Kama ni Kweli alijibu hivyo just because hakujua kama kuna meeting Idodomya then Hana Merrits za kuwa Kuwa Kiongozi ni vyema amewekwa Pembeni ili ajifunze namna bora ya Kuongoza na kujibu maswali katika Circumstance yeyote


Huyu kama alikiita kikao hicho kilikuwa GHETO basi atakuwa na na busara sana ,tena ingebidi achwe hapo chadema ili angalau hii kampuni ingekuwa na watu wanaofuata presedura.

Sasa Ndugu yangu kikao ambacho si halali kikao cha ki GHETO GHETO unataka akiiteje?
Najua saizi wako buzz kutengeneza makaratasi ili ionekane kikao kilikuwa halali tetetethhh
MAFISADI BWANA
 
Huyu kama alikiita kikao hicho kilikuwa GHETO basi atakuwa na na busara sana ,tena ingebidi achwe hapo chadema ili angalau hii kampuni ingekuwa na watu wanaofuata presedura.

Sasa Ndugu yangu kikao ambacho si halali kikao cha ki GHETO GHETO unataka akiiteje?
Najua saizi wako buzz kutengeneza makaratasi ili ionekane kikao kilikuwa halali tetetethhh
MAFISADI BWANA


Mabadiliko ya Mtu yanaanzia Kichwani, wewe huwezi badilika mkuu wangu Naona napoteza Mb zangu bure kujaribu kuelimisha mtu ambaye hataki kuelimishwa.

Wewe ni MBISHI
 
Mabadiliko ya Mtu yanaanzia Kichwani, wewe huwezi badilika mkuu wangu Naona napoteza Mb zangu bure kujaribu kuelimisha mtu ambaye hataki kuelimishwa.






Mwenye uelewa anaelewa

Wewe ni MBISHI

wewe ulidhani mabadiliko yanaanzia miguuni??

najaribu kukueleza kuwa hakuna kikao ambacho kinaweza fanyika bila afsa wa habari kufahamishwe.

Huo ndo utawala na uongozi wa sheria ,kanuni na taratibu , unachojaribu wewe kueleza kadamnasi ni kanuni za kosmosi ambazo hazipo dunianiani hapa waelewa wake ni wanazi tu kama wewe.
 
Kamati Kuu ya Chadema kujadili uamuzi wa Dk Slaa
broken-heart.jpg
Exuper Kachenje na Fidelis Butahe

KAMATI ya Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), inatarajiwa kukutana kati ya Novemba 27 na 28 mwaka huu, kujadili pamoja na mambo mengine, pepo baya la kisiasa lililoanza kukikumba chama hicho cha upinzani.

Pepo hilo, linafuatia uamuzi wa Katibu mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa, kuwafuta kazi maafisa wawili wa Chadema kwa sababu ambazo hazijawekwa wazi.

Kufutwa kazi kwa maafisa hao David Kafulila aliyekuwa Ofisa habari wa chama hicho na Danda Juju, aliyekuwa akishughulikia mambo ya Bunge katika chama hicho, kulitangazwa juzi na Dk Slaa.

"Tena andika mwandishi wala usiogope ni kwamba leo, (juzi) kulikuwa na kikao, nimekiongoza mwenyewe na maamuzi nimeyatoa mwenyewe, tumetengua uteuzi wao. Sasa ni wanachama wa kawaida," alinukuliwa Dk Slaa katika mahojiano na gazeti hili juzi.

Hatua hiyo imeibua majeraha ya kisiasa yaliyotokana na uchaguzi wa viongozi ndani ya chama hicho, uliofanyika Septemba mwaka huu.

Tayari Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, amepinga vikali hatua ya kufukuzwa kwa watendaji hao, wanaotajwa kuwa ni washirika wake wakubwa kisiasa, tangu mbio za uchaguzi uliomtikisa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.

Jana Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa Chadema, Bob Makani alisema, "suala hilo tutalijadili katika kikao cha Kamati Kuu ambayo itakutana kabla ya mwisho wa mwezi huu. Bahati mbaya sijawasiliana na uongozi siwezi kujua ni tarehe gani."

Hata hivyo alielezea matumaini yake kuwa haki itakuwa imetendeka kwa wanachama hao ambao walikuwa waajiriwa wa Chadema na kwamba ndiyo maana walipewa nafasi ya kujitetea.

Makani alifafanua kwamba, kimsingi, mwajiriwa anapaswa kufuata sheria na kanuni za mwajiri wake na kwamba, kama Kafulila na Juju hawakuzingatia hayo na kuendekeza majungu ndani ya chama na kuvunja katiba, hawawezi kuvumiliwa.

"Hao ni waajiriwa, katika ajira kuna maadili, sheria na kanuni, kama ni kweli wameleta majungu ndani ya chama hawawezi kuvumiliwa," alisema Makani.

Hata hivyo vyanzo huru vya habari, vilidokeza kuwa mkutano huo unatarajiwa kufanyika kati ya Novemba 27 na 28 mwaka huu.

Habari hizo zimekuja huku kukiwa na habari nyingine kuwa Mwenyekiti wa chama hicho (Mbowe), Dk Slaa na maafisa wao kadhaa walitarajiwa kukutana jana katika kikao cha siri, kujadili upepo ulivyo ndani ya Chadema.

Habari zaidi zilisema baadhi ya wanachama wa Chadema mikoani wakiwemo wenyeviti wao, wamekerwa na kitendo cha Dk Slaa, kumlinganisha Kafulila na mdudu sisimizi.

Kwa mujibu wa habari hizo, wanachama hao wamekuwa wakihoji kama ndani ya Chadema kuna sisimizi na tembo na kwamba kama yapo basi chama kina matabaka ya watu, jambo ambalo si la haki.

Akizungumzia kuwepo kwa mpasuko ndani ya Chadema , Makani alisema haoni kama uamuzi huo unaweza kuathiri chama wala kuzidisha ufa.

Alisema mpasuko unaweza kujitokeza zaidi kama tuhuma dhidi ya maafisa hao zitathibitika kuwa ni za kweli na wakaachwa ndani ya chama.

Katika uamuzi wake Dk Slaa alisema ametengua ajira za wanachama hao wawili kwa maslahi ya chama, hatua iliyotangazwa siku kadhaa tangu kuvuja kwa siri za kikao kati ya Mbowe na baadhi ya viongozi wa Chadema.

Habari za awali zilisema kikao hicho kilichofanyika mjini Dodoma, kilijadili pamoja na mambo mengine, nidhamu ya wanachama hao pamoja na mama mzazi wa Zitto, Shida Salum.

Habari tulizopata wakati tunakwenda mitamboni zilisema baadhi ya wazee wa Kigoma, wamemtaka Kafulila kuwa jasiri na kutokata tamaa ili hatimaye awanie ubunge katika Jimbo la Kigoma Kusini.

Vyanzo vya habari za kuaminika, vilifafanua kwamba wazee hao walikutana na Kafulila juzi usiku baada ya kuvuliwa wadhifa aliokuwa nao.

Habari hizo zilieleza kwamba, wazee wakiwemo viongozi wa dini wameelezea kuchukizwa na uamuzi wa Dk Slaa, kumvua Kafulila wadhifa wake.

Kafulila alipoulizwa kuhusu mkutano huo na wazee, alijibu: "Hapana kaka hakuna kitu kama hicho, mimi bado naombea Chadema kiwe chama kimoja."

Hata hivyo, habari hizo za ndani zilikariri wazee hao wakitaka Kafulila na mwenzake Juju warejeshwe kwenye nafasi zao mara moja ili kuleta amani na utengamano katika chama.

Wakati mzee Makani akiweka matumani ya uhai wa Chadema, hali ya kisiasa ndani ya chama hicho ni tete kufuatia kuwepo kwa kambi zinazopingana.

Hali hiyo tete kisiasa inatokana na baadhi ya wanachama kuona, uamuzi huo wa Dk Slaa, kuwa umefanywa kwa chuki zilizotokana na majeraha ya uchaguzi wa viongozi ndani ya chama.

Katika uchaguzi huo wa Septemba, Zitto alimtikisa Mbowe, baada ya kuingia kwenye kinyang'anyiro cha uenyekiti. Mpasuko mkubwa ambao ulijitokeza katika kipindi hicho unaonekana kuisumbua Chadema

Huyu kama alikiita kikao hicho kilikuwa GHETO basi atakuwa na na busara sana ,tena ingebidi achwe hapo chadema ili angalau hii kampuni ingekuwa na watu wanaofuata presedura.

Sasa Ndugu yangu kikao ambacho si halali kikao cha ki GHETO GHETO unataka akiiteje?
Najua saizi wako buzz kutengeneza makaratasi ili ionekane kikao kilikuwa halali tetetethhh
MAFISADI BWANA

Kama hiyo ndio akili yako basi kumbe huna maana .
 
Kama hiyo ndio akili yako basi kumbe huna maana .

WEwe maana uliyonayo ni ipi? kumbe wewe unamaana

Wewe maana yako ni ipi hapo Fisadi wenu alipomwita binadamu mwenzie SISIMIZI MDUDU

Na bahati yake tu Tanzania hakuna utawala wa sheria kama ingelikuwapo basi ingembidi athibitishe jinsi Daud alivyo mdudu sisimizi
 
Back
Top Bottom