Nimesoma kwenye gazeti la Mwananchi Kafulila anasema "Ninakipenda sana chama changu, ninamheshimu sana Dr Slaa...najua tatizo la msingi halijapatiwa jibu..Ninatafakari! " .nikajiuliza kama tatizo la Kafulila ana mgogoro na Mbowe au CHADEMA? maana kafukuzwa na Slaa lakini bado anaonesha imani kubwa kwa slaa. tatizo ni nani? nini?....
1.Nimemsikia kijana aliyeshinda umakamu mwenyekiti wa BAVICHA akisema tatizo la kafulila ni misimamo...na mbowe anapenda vijana wa kuburuza....au wa kabila lake kama alivyo John Mrema
2.Kafulila amekuwa akidai vikao vya kujadili matumizi ya ruzuku ya chama kila mwezi pesa zinapoingia...ambazo ni zaidi ya milioni60..kitu ambacho mbowe hayuko tayari...Na huu ndio mgogoro mkubwa ndani ya CHADEMA.kwamba ni Mwenyekiti pekee katika vyama vya siasa vikubwa nchini ambae ni signatory wa chama ni yeye tu...Kikwete sio, Lupumba sio..
3.Inasemekana kafulila analalamika kuwa slaa anaburuzwa na mbowe, nakwamba slaa anafaa kabisa kuwa hata rais kwakuwa atakuwa juu ya wote...kwamba mwenyewe slaa hana hatia katika madili ya pesa...na kwamba hata kwenye viti maalumu, baada ya mbowe kubadilisha majini ya waliopendekezwa na baraza kuu kwa mujibu wa kanda zao, slaa aliagizwa akatetee kwenye kikao cha baraza kuu...wajumbe wakakataa....wakatishia kumfukuza, ndipo mbowe akaingilia kati kuomba radhi....ndipo slaa akasema "kama mwenyekiti aliyeagiza majina yabadilishwe amekiri kosa, basi na mimi nakiri kosa....
4.Nashukuru nimewahi kumwona kafulila akiwa na Dr Kitila Mkumbo nadhani ilikuwa mwezi wa nne kabla ya uchaguzi wa busanda. lakini anatisha...yani alianguka gorofa ya kumi lakini akapona kwa siku nane...na wala hakuwa amechubuka hata kidogo kicwani...isipokuwa miguuni..Du Kigoma????
5.Nimesikia alitakiwa kufukuzwa mara kwanza alipofuatilia sana matumizi ya milioni35 za desemba 2008, ambazo ni siri kubwa mpaka sasa...ila kesho ntaambiwa....maana jamaa anasema hiyo ni siri kubwa kwani vikao zaidi ya vinne vilikaa kutaka taarifa ya matumizi ya fedha hizo bila mafanikio...ndipo alipozidi kuhojiwa akatishiwa kufukuzwa.
NINAENDELEA KUCHUNGUZA MGOGORO HUU, NA NITAENDELEA KUTOA TAARIFA KILA NINAPO NUSA...HIZO NDIZO NIMENUSA LEO KUTOKA SAKATA HILO