FaizaFoxy
Platinum Member
- Apr 13, 2011
- 92,883
- 109,212
Kuvamiwa kwa Isael ni mpango uliosukwa ukasukika kama ulivyosukwa mpango wa 9/11. Kinachotafutwa ni Saudi Arabia siyo Gaza wala Palestina wala Iran.
Naamini kuwa Israel na Palestina na yanayoendelea huko Gaza ni uwakala (proxy) tu wa kutafutwa Saudi Arabia. MBS wa Saudi Arabia" alimtowa nishai" sana Biden mara kadhaa. Alipotembelea Saudi Arabia miaka miwili nyuma alidharauliwa sana na MBS. Kafanya donge. Kumbuka MBS anawiza sana na Trump.
Kama hiyo haitoshi, Saudi Arabia kuikomowa USA, kaanza kukata biashara kwa kiwango kikubwa na USA na kahamia China na Urusi, kajiunga mpaka BRICS
MBS na Biden, picha haziendi kabisa toka Biden kaingia madarakani. Kwa mnaofatilia siasa za duniani, hilo haliwapi shida, lipo wazi kabisa.
Siamini kuwa kikundi kidogo kama Hamas, kiweze kufanya mashambulizi yale ya tarehe 7/10 bila Wayahudi kujuwa. Ile ni mipango iliyopangwa ikasukika kama ya 9/11, matokeo ya 9/11 ikavamiwa Iraq na Afghanistan. ikapigwa Sudan, Ikapigwa na kusambaratishwa Libya, zote hizo hazikuwa na hatia yoyote 9/11.
Saudi Arabia iliyosemekana vijana wake ndiyo waliohusika kwa zaidi ya 90% na shambulio la 9/11 haikuguswa kabisa bali ikawa inatemeshwa fedha zote za vita vya Iraq na Afghanistan, kibabe, ikipenda isipende.
MBS alivyogoma tu kutowa fedha na kubadilisha msimamo wake kwa kuwa yenyewe ilikuwa inakabiliwa na janga la Yemen, USA na NATO hawakubaki Afghanistan, wakajiondowa Afghanistan mbiombio.
MBS na Saudi Arabia ndiyo wanaoonekana nuksi kwa USA na NATO sasa hivi, Israel na Palestina wanatumika kama "proxy" tu.
Sasa hivi uchokozi wote uanelekezwa Saudi Arabia, wanatiwa uchungu Waarabu na Waislam waishinikize Saudi Arabia ijiingize kwenye mzozo liwageukie. Anachotakiwa Saudi Arabia sasa hivi ni arushe japo risasi moja au aseme hovyo tu aanze kutandikwa mpaka MBS aondolewe kabisa ili USA waweke vibaraka wao Saudi Arabia.
Bila MBS kuondoka Saudi Arabia, kwa hiyari au kwa nguvu, na vibaraka wa 'hewala bwana' kwa USA kuwepo, Israel na Palestina vita havitosimama elo wala kesho.
Hilo MBS alilielew, siyo mjinga, alipomfanyia ujeuri tu USA, tukaanza kuona, miaka miwili mitatu sasa, Saudi Arabia inajiingiza kwa nguvu kwenye uhusiano na Urusi na China. Tusishangae tukoona pia anaingia uhusiano na Kiduku.
Tanzania kama nchi tunatakiwa tuchukuwe fursa zilizopo za kinachoendelea hivi sasa. Tuendelee kulaani mauwaji ya raia wasio na hatia na tuendelee kubaki hatufungamani na upande wowote, huku tukizitumia fursa kuzifanya faida (Resilience).
Naamini kuwa Israel na Palestina na yanayoendelea huko Gaza ni uwakala (proxy) tu wa kutafutwa Saudi Arabia. MBS wa Saudi Arabia" alimtowa nishai" sana Biden mara kadhaa. Alipotembelea Saudi Arabia miaka miwili nyuma alidharauliwa sana na MBS. Kafanya donge. Kumbuka MBS anawiza sana na Trump.
Kama hiyo haitoshi, Saudi Arabia kuikomowa USA, kaanza kukata biashara kwa kiwango kikubwa na USA na kahamia China na Urusi, kajiunga mpaka BRICS
MBS na Biden, picha haziendi kabisa toka Biden kaingia madarakani. Kwa mnaofatilia siasa za duniani, hilo haliwapi shida, lipo wazi kabisa.
Siamini kuwa kikundi kidogo kama Hamas, kiweze kufanya mashambulizi yale ya tarehe 7/10 bila Wayahudi kujuwa. Ile ni mipango iliyopangwa ikasukika kama ya 9/11, matokeo ya 9/11 ikavamiwa Iraq na Afghanistan. ikapigwa Sudan, Ikapigwa na kusambaratishwa Libya, zote hizo hazikuwa na hatia yoyote 9/11.
Saudi Arabia iliyosemekana vijana wake ndiyo waliohusika kwa zaidi ya 90% na shambulio la 9/11 haikuguswa kabisa bali ikawa inatemeshwa fedha zote za vita vya Iraq na Afghanistan, kibabe, ikipenda isipende.
MBS alivyogoma tu kutowa fedha na kubadilisha msimamo wake kwa kuwa yenyewe ilikuwa inakabiliwa na janga la Yemen, USA na NATO hawakubaki Afghanistan, wakajiondowa Afghanistan mbiombio.
MBS na Saudi Arabia ndiyo wanaoonekana nuksi kwa USA na NATO sasa hivi, Israel na Palestina wanatumika kama "proxy" tu.
Sasa hivi uchokozi wote uanelekezwa Saudi Arabia, wanatiwa uchungu Waarabu na Waislam waishinikize Saudi Arabia ijiingize kwenye mzozo liwageukie. Anachotakiwa Saudi Arabia sasa hivi ni arushe japo risasi moja au aseme hovyo tu aanze kutandikwa mpaka MBS aondolewe kabisa ili USA waweke vibaraka wao Saudi Arabia.
Bila MBS kuondoka Saudi Arabia, kwa hiyari au kwa nguvu, na vibaraka wa 'hewala bwana' kwa USA kuwepo, Israel na Palestina vita havitosimama elo wala kesho.
Hilo MBS alilielew, siyo mjinga, alipomfanyia ujeuri tu USA, tukaanza kuona, miaka miwili mitatu sasa, Saudi Arabia inajiingiza kwa nguvu kwenye uhusiano na Urusi na China. Tusishangae tukoona pia anaingia uhusiano na Kiduku.
Tanzania kama nchi tunatakiwa tuchukuwe fursa zilizopo za kinachoendelea hivi sasa. Tuendelee kulaani mauwaji ya raia wasio na hatia na tuendelee kubaki hatufungamani na upande wowote, huku tukizitumia fursa kuzifanya faida (Resilience).