Webabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,186
- 10,922
Huku upepo tufani la Al Aqsa ukizidi kupiga kote kote.Saudi Arabia imeionya Marekani juu ya kihere here chake cha kuwatibua wapganji wa Houth kwenye bahari nyekundu.
Wakati huo huo taifa hilo mashuhuri kwa kusafirisha mafuta duniani limesisitiza juu ya haja ya kusitishwa vita vinavyoendelea Gaza mara moja.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vilivyonukuu onyo hilo,hofu ya Saudi Arabia ni kuwa kujiingiza kwenye vita hivyo kunaweza kukavisambaza vita vya Palestina na Israel kwa eneo lote la mashariki ya kati na kwa haraka sana.
Saudi Arabia inaelewa sana ushujaa wa wapiganaji wa Houth ambao wao hawakuweza kuumaliza kwa njia ya vita juu ya kumilika silaha kali dhidi yao.
Mara kadhaa droni za Houth na makombora mengine viliwahi kupiga maeneo muhimu ya kiuchumi ya Saudi Arabia pamoja na viwanja vya ndege vya kimataifa kitu ambacho hakikuzoeleka huko Saudi Arabia kwa miongo kadhaa.
Hatimae Saudi Arabia ilitiliana saini na watawala hao wa Yemen kusitisha vita na kurudisha udugu wao.
Wakati huo huo taifa hilo mashuhuri kwa kusafirisha mafuta duniani limesisitiza juu ya haja ya kusitishwa vita vinavyoendelea Gaza mara moja.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vilivyonukuu onyo hilo,hofu ya Saudi Arabia ni kuwa kujiingiza kwenye vita hivyo kunaweza kukavisambaza vita vya Palestina na Israel kwa eneo lote la mashariki ya kati na kwa haraka sana.
Saudi Arabia inaelewa sana ushujaa wa wapiganaji wa Houth ambao wao hawakuweza kuumaliza kwa njia ya vita juu ya kumilika silaha kali dhidi yao.
Mara kadhaa droni za Houth na makombora mengine viliwahi kupiga maeneo muhimu ya kiuchumi ya Saudi Arabia pamoja na viwanja vya ndege vya kimataifa kitu ambacho hakikuzoeleka huko Saudi Arabia kwa miongo kadhaa.
Hatimae Saudi Arabia ilitiliana saini na watawala hao wa Yemen kusitisha vita na kurudisha udugu wao.