Sagini aagiza Miradi ya Vyombo vya Ulinzi na Usalama Mkoani Geita kukamilika kwa wakati

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,988
r.JPG
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini (Mb) amewataka Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na wakandarasi wanaosimamia miradi ya ujenzi Mkoani Geita kukamilisha Ujenzi wa Miradi yote kwa wakati na kuzingatia ubora.

Mhe. Sagini ametoa maagizo hayo Novemba 25, 2023 katika ziara yake ya kikazi ya kutembelea na kukagua Miradi mbalimbali ya Ujenzi inayotekelezwa chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na kusikiliza na kutatua kero mbalimbali zinazojitokeza katika utekelezaji wa miradi hiyo

"Niwatake wakandarasi kuongeza nguvu kazi ili kuwahisha utekelezaji wa miradi kwa kuzingatia ubora unaotakiwa na ikiwezekana ongezeni muda wa kufanya kazi na hakikisheni vifaa vyote vimenunuliwa ili kurahisisha Ujenzi," Amesema Mhe. Sagini
r1.JPG

rr.JPG
Pia ameziomba Mamlaka zote za Miji kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kuweka visima vya maji (fire hydrat) kwa ajili ya kurahisisha uzimaji moto.

Aidha Mhe. Sagini ametembelea na kukagua Ujenzi wa Kituo cha Polisi, Kituo cha Zimamoto na Uokoaji, Nyumba Sita za Askari Polisi, Mradi wa Ufyatuaji tofali wa Gereza Geita.
 
Back
Top Bottom