Naibu Waziri Sagini amaliza ziara yake Kanda ya Ziwa, apongeza Vyombo vya Usalama

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,813
11,991
00.JPG
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini amemaliza ziara yake ya kikazi kutembelea na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Vyombo vilivyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na kusikiliza na kutatua kero zinazojitokeza lengo likiwa ni kuboresha utendaji kazi na kuvipongeza Vyombo vya Usalama, Maafisa na Askari kwa kuendelea kuchapa kazi licha ya ugumu wa mazingira na changamoto mbalimbali zinazowakabili.



Akizungumza na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mwanza, Vyombo vilivyopo chini ya Wizara yake, Maafisa na Askari katika kikao cha majumuisho, Sagini amesema katika ziara yake amejifunza mambo mengi, ikiwemo moyo wa kujituma na uchapaji kazi kwa bidiii, pamoja na usimamizi mzuri wa miradi ya ujenzi inayoendelea na mwenendo mzuri wa malezi bora kwa wafungwa na mahabusu katika Magereza yetu.
00.JPG
“Nimejionea ubunifu mkubwa uliofanywa na Taasisi zetu katika kuboresha mazingira ya kazi, utunzaji wa mazingira, ukarabati wa majengo, umaliziaji wa ujenzi wa miradi pamoja na ujenzi wa miradi mipya, utajiri mkubwa wa ardhi na hali ulinzi na usalama kuimarika kwenye maeneo yetu, ushirikiano mlionao baina yenu, wadau na viongozi wa kiserikali,” amesema.

Akihitimisha ziara yake Mkoani Mwanza, Naibu Waziri Sagini alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maghorofa ya Polisi Mabatini, mradi wa ujenzi wa nyumba za Polisi pamoja na kituo cha Polisi Nyamuhongoro, kituo cha Polisi Malya Wilayani Kwimba, kituo cha Polisi Kwimba, Chuo cha Polisi wanamaji Mwanza, mradi wa ujenzi wa mfumo wa majitaka Gereza Kuu la Butimba, Kiwanda cha Ushonaji na Useketaji cha Gereza Kuu Butimba na baadaye kupokea taarifa ya hali ya usalama Mkoani humo pamoja na utendeji kazi wa Vyombo vilivyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
 
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Jumanne Sagini amemaliza ziara yake ya kikazi kutembelea na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na Vyombo vilivyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi pamoja na kusikiliza na kutatua kero zinazojitokeza lengo likiwa ni kuboresha utendaji kazi na kuvipongeza Vyombo vya Usalama, Maafisa na Askari kwa kuendelea kuchapa kazi licha ya ugumu wa mazingira na changamoto mbalimbali zinazowakabili.

Akizungumza na Kamati ya Usalama ya Mkoa wa Mwanza, Vyombo vilivyopo chini ya Wizara yake, Maafisa na Askari katika kikao cha majumuisho, Sagini amesema katika ziara yake amejifunza mambo mengi, ikiwemo moyo wa kujituma na uchapaji kazi kwa bidiii, pamoja na usimamizi mzuri wa miradi ya ujenzi inayoendelea na mwenendo mzuri wa malezi bora kwa wafungwa na mahabusu katika Magereza yetu.
“Nimejionea ubunifu mkubwa uliofanywa na Taasisi zetu katika kuboresha mazingira ya kazi, utunzaji wa mazingira, ukarabati wa majengo, umaliziaji wa ujenzi wa miradi pamoja na ujenzi wa miradi mipya, utajiri mkubwa wa ardhi na hali ulinzi na usalama kuimarika kwenye maeneo yetu, ushirikiano mlionao baina yenu, wadau na viongozi wa kiserikali,” amesema.

Akihitimisha ziara yake Mkoani Mwanza, Naibu Waziri Sagini alitembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa maghorofa ya Polisi Mabatini, mradi wa ujenzi wa nyumba za Polisi pamoja na kituo cha Polisi Nyamuhongoro, kituo cha Polisi Malya Wilayani Kwimba, kituo cha Polisi Kwimba, Chuo cha Polisi wanamaji Mwanza, mradi wa ujenzi wa mfumo wa majitaka Gereza Kuu la Butimba, Kiwanda cha Ushonaji na Useketaji cha Gereza Kuu Butimba na baadaye kupokea taarifa ya hali ya usalama Mkoani humo pamoja na utendeji kazi wa Vyombo vilivyopo chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Milioni 802 jengo la ofisi jimboni kwake liko vizuri Sana. Mradi uko katika hatua nzuri Mheshimiwa Naibu Waziri.
 
Back
Top Bottom