Safari yangu ya jana imenisaidia kuitafakari imani yangu kwa dakika kadhaa

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,595
215,272
Jana nilipanda treni kwa safari ya masaa manne. Mlangoni alikuwepo mhudumu na kipima joto na kuhakikisha wote tuna barakoa kabla ya kuingia ndani pia kulikua na meza yenye sanizer pembeni.

Tuliambiwa tukae mbali na abiria wengine la kama mmetoka nyumba moja mnaweza kukaa pamoja. Sasa alikuja mwanaume mmoja aliomba ku charge simu kwani nilipokaa kulikuwa na socket ambayo sikuitumia.

Alisema ni muhimu awe na simu kwani kuna maombi anaendelea nayo kupitia You Tube. Niliposikia maombi nilimdadisi zaidi, alisema ni maombi ya Bhudaism. Nilimuuliza wewe ni Bhuddist? Alisema yeye hana dini ingawa alizaliwa Mkristu wa Anglicana na kupata sakramenti zote.

Wakati huo maongezi yetu ya yamekolea na barakoa tumeziweka videvuni, alisema baada ya kuzunguka dunia kikazi amegundua nguvu ya sala na maombi ya dini nyingine ambazo wala hazina uhusiano na Yesu. Anaamini kuwa kuna Mungu na anaamini jua lina nguvu sana. Aliniambia kuna ibada inayohusisha jua na ukimaliza hiyo ibada unaweza usilale kwa masaa 72, unakuwa na nguvu za ajabu.

Kwakweli nilimueleza kwangu mimi Ukristu nimerithi kutoka kwa wazazi. Kama walionileta duniani wameishi kwa imani hiyo na kunifundisha mema kwenye muongozo huo sioni sababu ya kuachana nao, pia mimi binafsi umenijenga kumjua Mungu na maombi.

Mwisho wa safari yetu tuliagana. Nilijifikira sana nikiwa nyumbani kuwa Yesu alisema yeye ni njia ya kweli, sasa hawa wanaoabudu kupitia jua siku ya hukumu itakuwaje kwao?
 
Endelea kuamini unachoamini, dunia hii ina mengi na mambo ya kusitajabisha. Wapo wanaopinga uwepo wa Mungu . Hii ni sambamba na mawazo ya kiyumanisti(hali ya kuabudu binadamu badala ya Mungu) na kimatirialisti( hali ya kuabudu mali ya dunia badala ya Mungu. Wahiumanisti huamini kuwa mwanadamu hujisimamia mwenyewe na utukufu wake ndio wa manufaa zaidi. Wanaounga mkono dhana ya kimatirialisti wana imani tu katika mambo ya ulimwengu huu ndio kama hao wanaoamini jua.

Lakini kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vyatoka Kwake na kwa
ajili Yake sisi twaishi na kuna Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa Yeye vitu vyote
vimekuwepo na kwa Yeye sisi tunaishi ( 1 Wakorintho 8:6).

Endelewa kubarikiwa
 
Hao ni waabudu jua au sun worshipers, wanaabudu kiumbe wanaacha kumwabudu muumba. Ndivyo zilivyo dini nyingi kama Buddhism, Hinduism, nk. Kwa kifupi nakuhakikishia hakuna Mungu wa kweli isipokuwa yule aliyejitambulisha kwa kupitia Yesu Kristo.

Hili Jina linapita majina yote. Ukiwa na imani na ukalitumia jina la Yesu huwezi kushindwa na shetani hata siku moja. Kwangu wachawi wanateseka siku hizi. Watu wengi hawajui ukweli huu.
 
Hao ni waabudu jua au sun worshipers, wanaabudu kiumbe wanaacha kumwabudu muumba. Ndivyo zilivyo dini nyingi kama Buddhism, Hinduism, nk. Kwa kifupi nakuhakikishia hakuna Mungu wa kweli isipokuwa yule aliyejitambulisha kwa kupitia Yesu Kristo. Hili Jina linapita majina yote. Ukiwa na imani na ukalitumia jina la Yesu huwezi kushindwa na shetani hata siku moja. Kwangu wachawi wanateseka siku hizi. Watu wengi hawajui ukweli huu.
Yeye anaamini jua ni kiunganishi kati ya Mungu na mwanadamu na nguvu ya jua hitoka kwa Mungu. Kwakua Mungu anatupenda ndiyo maana ametuletea jua na bila ya jua hakutakua na uhai duniani.
 
Nje ya mada: Tunapaswa kuogopa kifo kama tu tunavyo muogopa adui mwingine na kuchukua hatua sahihi kujilinda!
Hatupaswi kuogopa kifo eti kisa mafundisho fulani ya kidini yenye vitisho vya kuchomwa moto baada ya kufa.
 
Endelea kuamini unachoamini, dunia hii ina mengi na mambo ya kusitajabisha. Wapo wanaopinga uwepo wa Mungu . Hii ni sambamba na mawazo ya kiyumanisti(hali ya kuabudu binadamu badala ya Mungu) na kimatirialisti( hali ya kuabudu mali ya dunia badala ya Mungu. Wahiumanisti huamini kuwa mwanadamu hujisimamia mwenyewe na utukufu wake ndio wa manufaa zaidi. Wanaounga mkono dhana ya kimatirialisti wana imani tu katika mambo ya ulimwengu huu ndio kama hao wanaoamini jua.


Lakini kwetu sisi yuko Mungu mmoja, aliye Baba, ambaye vitu vyote vyatoka Kwake na kwa
ajili Yake sisi twaishi na kuna Bwana mmoja tu, Yesu Kristo, ambaye kwa Yeye vitu vyote
vimekuwepo na kwa Yeye sisi tunaishi ( 1 Wakorintho 8:6).

Endelewa ku






Amina
 
Huyo tayari ameikana Imani yake,au yawezekana kabla ya kuingia huko aliko alikuwa hajaisoma vizuri Biblia na kuilewa.Pia ipo shida nyingine ambayo kuna watu wengi sana wanafuata dini kwa ajili ya miuijiza ambapo pengine angesimamam vizuri pale alipo angeweza kuiona miujiza mkubwa kuliko hiyo ya jua lake...
 
Ila kwa Yesu ni kugumu wadau.Tuwe wakwel.Mi mwenyewe nimeokoka na namuamini Mungu ila dah kuna time unajikuta tu ushachanganya "makaratee" mengine ya "kimaghumashi" ilimradi life lisonge.
Ila naamin Mungu ananipenda hivyo hivyo.
Ntafanyaje sasa????
Sijui nisemeje!nimecheka!
Ila endelea hivyohivyo Yesu hatakuacha!na usimuache!

JESUS IS LORD
 
Ila kwa Yesu ni kugumu wadau.Tuwe wakwel.Mi mwenyewe nimeokoka na namuamini Mungu ila dah kuna time unajikuta tu ushachanganya "makaratee" mengine ya "kimaghumashi" ilimradi life lisonge.
Ila naamin Mungu ananipenda hivyo hivyo.
Ntafanyaje sasa????
Ndio maana Yesu alisema kuwa hakuna mtakatifu hapa duniani isipokuwa Mungu peke yake,na hii inaonyesha alijua kuwa kuanguka kupo ila usikate tamaa,unapoanguka inuka uendelee kusonga mbele kwa maombi na sala,huku ukiombea Mungu akutoe hapo ulipo ili uwe mahala salama zaidi,kwani ukimuacha Mungu wako ndio anguko lako liliko...
 
Back
Top Bottom