Mimi ni Mkristo mlokole, nimeanza kukosa Imani na ukristo nahisi Uislam ndiyo dini ya kweli

Mganguzi

JF-Expert Member
Aug 3, 2022
1,032
2,769
Napenda sana ibada, naamini kupitia ibada mambo mengi yanaweza kuwa sawa! Napata shida kidogo na Imani yangu ya ukristo, miaka ya 1980 -1990 ibada ilikuwa nzuri sana kokote utakakoenda kusali na kanisa lolote utakaloingia Ibada zilikuwa na nguvu halisi ya Mungu.

Hapakuwa na makorombwezo Wala mbwembwe kama Sasa! Huwa navurugwa sana nikiingia kanisani mambo mengi yamebadilika! Kanisa la Sasa imekuwa sehemu ya disco,dance na mitindo ya hovyo ya mavazi, wanawake wanavaa nguo ambazo hata kwenye baadhi ya bar hawavai na wachungaji wako busy na mapato na matumizi. Mahubiri asilimia tisini ni fedha na mipasho! Nimechoka na miujiza ya zana kama uganga, kanisa la Leo mchungaji anaamini lazima abebe zana ndio apande madhabahuni ,ukristo unabadilika Kila mwaka ,sura ya kanisa sio Ile ya 1990 ,2000.

Kila mwaka kanisa linavaa sura nyingine, wachungaji wetu wanavita kubwa ya kugombea waumini kiasi hawana ushirikiano Tena ! Ni maadui na hawana maombi ya pamoja Tena kama zamani. Kila mchungaji yaonekana kama ana mbingu ya kwake. Kuna kundi wanajiita mitume na manabii na Kuna kundi la maaskofu na wachungaji ,maaskofu na wachungaji wanahisi wao nao wanambingu Yao ambayo mitume na manabii hawataenda ! Na mitume na manabii pia wanaona wachungaji na maaskofu hawana nguvu ya mungu Tena!

Hizi ni dalili mbaya sana kwa miaka 20 ijayo ya ukristo, mpaka Sasa asilimia 70 waislam wako sawa na unaweza kuwaelewa! Lakini wakristo wamefeli kabisa , naikubali sana ibada ya hija na Ile ya kuchinja waislamu wanaungana Duniani kote kwa ajili ya Allah!

Lugha Yao inakuwa Moja na kauli Yao ni thabiti kabisa ,wanavaa vizuri sana wanapokuwa kwenye ibada na hata ,huwezi kuyaona mapaja ya mwanamke msikitini yakiwa nje sijui kama nitaweza kuuvumilia ukristo kwa miaka michache ijayo mungu aturehemu !
 
Shida ilianzia kwenye nakanisa ya kilokole,waprotestanti walivyoona walokole wanachuma waumini wao na wenyewe ikabidi wabadilike. Shida ya pili ikaanzia tena huko huko kwa walokole, wachungaji wa kiprotestanti walivyoona wachungaji wa kilokole wanapiga hela kupitia mahubiri yao ya sadaka na wenyewe upepo umehamia huko.
 
Shida ilianzia kwenye nakanisa ya kilokole,waprotestanti walivyoona walokole wanachuma waumini wao na wenyewe ikabidi wabadilike. Shida ya pili ikaanzia tena huko huko kwa walokole,wachungaji wa kiprotestanti walivyoona wachungaji wa kilokole wanapiga hela kupitia mahubiri yao ya sadaka na wenyewe upepo umehamia huko.
Umenena vema sana
 
Napenda sana ibada ,naamini kupitia ibada mambo mengi yanaweza kuwa sawa! Napata shida kidogo na Imani yangu ya ukristo ,miaka ya 1980 ---1990 ibada ilikuwa nzuri sana kokote utakakoenda kusali na kanisa lolote utakaloingia Ibada zilikuwa na nguvu halisi ya mungu ...

Wewe ni mamluki wa mudi umekuja kuleta propaganda hata muandiko unaonyesha.

Kimsingi dini ya kiislam ni dini inayoamini sana katika matendo ili upate wokovu,ndio mana wanapambania sana maisha ya utu wa nje sio utu wa ndani,ndio maana wengi wao wamejaa husuda,wivu,chuki na ubaguzi baina yao na hata kwa wasio waislamu wenzao.

Wokovu unapatikana kwa neema na haki ya kristo pekee,na kama unaenda kanisani kukitegema uipate hiyo neema na haki kupitia viongozi wa dini au waumini jua wewe sio mkristo wa kweli bali ni mkristo jina.

Kuna makanisa mengi still ibada zao ni njema za za kumtukuza Mungu. Kristo awe mfano kwako kuuishi ukristo.

Ila kama umeona huko kuko sawa ukristo haumlazimishi mtu kutoka ni wewe na mawazo yako.

Kila jema.
 
Wewe ni mamluki wa mudi umekuja kuleta propaganda hata muandiko unaonyesha.

Kimsingi dini ya kiislam ni dini inayoamini sana katika matendo ili upate wokovu,ndio mana wanapambania sana maisha ya utu wa nje sio utu wa ndani,ndio maana wengi wao wamejaa husuda..
Hahahaha hujajibu hoja ila umenishambulia ,usiweke mvinyo mpya kwenye chombo Cha zamani
 
Back
Top Bottom