Ryan The King
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 2,789
- 2,704
Ikitokea kwa bahati mbaya kuwa kuna Mungu, basi itampsa Mungu awaombe watu msamaha kwa udhaifu wa uwepo wake ambao ni uharibifu mtupu.
Mungu yupo Mkuu sema hakuna aliyewahi kumuona.
Si Shetani si malaika wote hawamjui wala hawajawahi kumuona ndio maana hafananishwi na çhochote ila yupo.
Shida ni kwamba watu hudhani wakifika huko mbinguni watamuona Mungu kumbe wanajidanganya. Shetani mwenyewe hajawahi kumuona ndio maana akamkadiria nguvu zake akidhani atashinda matokeo yake ndio haya.
Hata ukisoma katika kitabu cha historia ya wayahudi kiitwacho Biblia. Utaona Nyoka akimdanganya Hawa kuhusu kufanana na Mungu ambaye Shetani mwenyewe Alitamani kufanana naye. Hawa anaingia tamaa ya kutaka kuingia katika daraja la juu lisilo na mfano yaani lisilo onekana. Yaani Mungu aliyeumba kila kitu.
Hivyo kijana acha kuhangaika kubisha vitu ambavyo huvijui. Ni bora ukae kimya. Lakini simanianishi upelekwe pelekwe na ngonjera za Hawa watu wanaojifanya wanajua kumuelezea Mungu wakati hata waliowapa hizo habari hawamjui. Hata manabii hawamjui. Hata waliowapa ufunuo manabii yaani Malaika hawamjui. Hata huyo wanayemuita Shetani hamjui huyo Mungo japo anatambua kuwa yupo na nmheshimu.
Kwa ufupi hakuna anaemjua Mungu. Hakuna aliyewahi kumuona. Kama Shetani angebahatika kumuona Mungu asingeshindwa kuvujisha jinsi alivyo.
Kilichotokea mbinguni ni kugombania Mamlaka baina ya viumbe waishio huko ambako wanadamu Kwa lugha zao hukuita Mbinguni.