Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Sababu zinazonifanya nisimpende Mungu

Mungu hakosei na wala hampangii baya binadam yeyote
Mungu kawaachia binadam wajitawale na akili zao binafsi
Sio mambo yote yanayotokea ni mipango ya Mungu
Kama ingekuwa hvyo kila moja angeenda mbinguni baada ya mauti
 
Kuna maswali mengi kuhusu Mungu huwa najiuliza, mpaka SAA nyingine huwa namkasirikia Mungu (maybe nakufuru lakini acha iwe hivyo).Bcoz kwa ninavomuwazia Mungu ingekuwa ni heri nisingezaliwa.

1) Kama kweli Mungu ni upendo, kwanini aumbe jehanamu ya kutuchoma milele sisi tulio waovu (lyk for billions and trillions of years). Si heri angetumaliza tu kuliko kututesa milele? Kwenye shuhuda nyingine wakristo huenda motoni kwa dhambi moja tu ambayo hawakutubu. (I know hell was originally intended for the devil and his demons & not 4 humans)

2) Kwanini alimruhusu shetani kumjaribu Adam ikiwa alijua kuwa wanadamu wengi tutateseka duniani, tutaanguka maovuni, na atatutupa Jehanamu?

3) Kama Mungu anatuambia tukitenda dhambi na tusipomtii tutachomwa motoni, Je wakristo na waislamu (baadhi yetu) tutakuwa tunamtumikia Mungu kwasababu tunampenda na tunataka kumjua zaidi? au tutakuwa tunamtumikia kwasababu tunaogopa kwenda Jehanamu?

4) Mungu husema mawazo yake si kama ya kwetu, na njia zake zipo juu zaidi, nakubaliana na hilo. Maybe kutuchoma motoni it's in his nature, that's the way He is and we have to live with it.

5)All in all Mungu ana hekima kuliko mimi, coz ni muumba wa kila kitu. Maybe katika hekima yake yote, hii ndo decision bora aliokuja nayo. Labda ana reason nzuri behind all this ambayo mm siijui. Maybe Mungu mwenyewe akinijibu face 2 face, nitabadili mtazamo wangu kuhusu yeye.

6) Kingine kinachonikasirisha pia ni yeye kuruhusu mimi kuja hapa duniani, naona ni heri nguvu aliotumia kuniumba mimi angetumia kufanya kitu kingine, nachukia + najuta kuwa hapa duniani to see all this, dunia imejaa waovu (mm nikiwa mmoja wapo) pamoja na mateso ya kila namna.

Haya ndo mawazo yangu nimeamua ku-share nanyi, najua hata povu linitoke vipi it won't change the facts. Samahani kwa ntakaekuwa nimewakwaza humu jukwaani, naamini Mungu alishayajua mawazo yangu kuhusu yeye toka kitambo. So im just keeping it real.


Unamchukia Mungu???,

Fanya toba kuanzia leo. Funga na usali sana, toa sadaka.

Jinyime sana wakati wa kufunga kwako, usamehewe hii dhambi, maana itatafuna vizazi vyako vvyote,

Eeeh Mwenyezi Mungu, Mungu wa Rehema, Mungu wa Ibrahim, Mungu wa Yakobo, umsamehe mtu huyu bure maana hajui anenalo!

Amina
 
Inaonekana uko stressed muda huu (point yako ya sita) as if kuna jambo baya umefanya,linakuumiza,unalijutia

Kama iko hivyo kweli ni heri ukatubu kwa imani yako na kuamini sisi binadamu hakuna mkamilifu,wote tunamkosea Mungu

Kwa imani yangu nafahamu Mungu ni pendo na huwa hakusudii baya lolote litutokee
Sasa kama humpendi yeye manake hata ndani yako hakuna upendo

USHAURI
Usipende kumuongelea Mungu kiboya boya kama unawongelea wachumba zako huko

Hayo maswali # 1,2&3 nimeshindwa kuyajibu kwasababu sipo into dini kabisa

Hii mada sijaiandika nikiwa under stress, hayo mawazo sikuanza kuwa nayo Leo, mm huwa na-question vi2 vingi ninavyoona na kuvisikia. Nia yangu si kumwandika Mungu kiboya, Bali ni kuujua ukweli halisi wa mambo.

Wewe mwenyewe kwa juu juu unaweza kujiona kuwa unampenda, unamuogopa, na unamuheshimu Mungu, lakn ukijichunguza vizuri matendo yako, hayaendani na huyo unaempenda..

Honestly nijibu, kama kweli unampenda na kumuheshimu Mungu asilimia ngapi ya muda wako kwa kila wiki unaitumia kumwaza Mungu? na mambo ya mbinguni? Sana sana utakachokuwa unawaza ni mambo ya hapa duniani, lyk kufanikiwa kipesa, kuolewa, ngono etc..

Maybe ulinielewa vibaya along the way, Mimi simchukii Mungu (coz hakuna baya kubwa ambalo amenifanyia) ila tu simpendi (partly because kuna vitu kuhusu yeye ambavyo sijavielewa) na najitahid kutafta ukweli halisi kuhusu yeye, nimjue zaidi.

Pia mm ni mtenda dhambi wa kukusudia Mara kwa Mara so siwez ku-claim kuwa nampenda Mungu, huo utakuwa ni uongo joanah
 
WEWE ENDELEA HIVYO HIVYO MKUU.

WACHA SISI TUENDELEE KUMUABUDU NA KUMUIMBIA MUNGU WETU ANAYETUFANYA KUPUMUA NA KUWA HAI LEO HII.

TUTAPEANA MAJIBU SIKU TUKIFA NA KUJIONEA UKWELI.
 
Ukiona watu wanaanza kuhoji na kuchukua tahadhari za namna hii, ujue IQ za watu zinaongezeka.
Tuendako taifa litakuwa na watu makini wasio laghaiwa kirahisi kwa mawazo mfu kama vile uwepo wa Mungu.
Hata kama Mungu angekuwepo angeshajinyonga kwa aibu.
Hahahaha we jamaa sikuzote unahasira sana na Mungu. Hebu nikuulize kidogo... unahisi sisi binadamu na Mungu, ni nani mwenye kumhitaji zaidi mwenzake?
 
Mungu hayupo so point zako ni invalid.

Kama yupo basi anavyosema ni mwenye rehema na upendo kuliko binadamu yeyote anatudanganya maana angekua nao dunia isingekua kwenye mess hii.

Ana paradox nyingi mno kiasi kwamba his own existence can't be possible in anyway. Anasema anajua yote yatakayokuja na yaliyokuwepo,hehe meaning story ya adam n eve ka ni kweli then anamlaumu eve bure tu maana yeye alijua wazi watakachokifanya na bado akaweka mti pale, kosa ni la kwake 100% ni sawa na mzazi kujua mtoto ukimpa wembe atajikata alafu unampa then anajikata unamtupia lawama na kumuongezea adhabu juu.

Siku nilipoachana na fix za dini akili ilifunguka, kuishi kwa uoga uoga tena hakuna, mtoto ukimjaza kitu utotoni anakishika kama kilivyo, acheni watoto wenu wakue then wachague, hamtobaki na mtu anayeamimi haya maduduwasha
Asa mtu akifa...what next
 
Mtu hujui chochote alafu unajifanya eti unajua.



Wapo viumbe ambao wana uwezo mkubwa kiasi cha kudhani ni miungu na wanamheshimu Mungu lakini wewe usiyejua hata dakika moja mbele unaropoka kama kichaa.

Subiri zamu yako. Naamini unayo akili ambayo Mungu amekupa ambayo hiyo hiyo ndio utajionea kuwa ulikuwa kichaa
Ikitokea kwa bahati mbaya kuwa kuna Mungu, basi itampsa Mungu awaombe watu msamaha kwa udhaifu wa uwepo wake ambao ni uharibifu mtupu.
 
Mim ni mwana science,Ulimwengu una aproximately bilion 900 za galaxies,dunia hii tuliyomo ipo kwenye moja ya galaxies hizo,inaitwa milky way,.galaxies hiz zina nyota zake,(JUA LETU,ni moja ya nyota)..ukubwa wa galaxy ndio una determine uwingi wa nyota,..mfano galaxy yetu ina nyota zake nying tuu moja wapo ndo hili jua,hii tena ni nyota ndoogo saana ambayo,(jua ni kubwa kuliko dunia mara milion1),galaxy yetu ni moja ya galaxy ndogo saaaana.kuna galaxy zenye nyota zaid ya 10,..so kila nyota hubaatika kuzungukwa na sayari,mfano nyota yetu jua inazungukwa na sayar zijulikanazo ambazo ni almost 9,sayari hizi zina miaka bilion na ma bilioni,mfano sayar yetu dunia ina miaka almost 4.5bilion na ni sayar ndoogo sana kulinganisha na hizo zilizoko kwenye galaxies zingine..sasa mifumo yooote hii inalindwa na nguvu za asili ambazo inazifanya zi balance bila kuingiliana ama kuleteana mushker zenyew kwa zenyew,..nikimaanisha zna self control ambayo iko systematic.,na well balanced..kwa sayansi hii peke yake,inakupa kitu,..ok tuje kwa viumbe,tukiacha wanyama wengne na mimea na bacteria na virus na wadudu wengne amba wana mifumo yao,..kila binadam umuonae dunian hapa ana kitu kwenye seli yake kinaitwa DNA,..cha ajab kila bnadam ana aina yake pekee ya hii kitu,yan huwez fanana na mwenzio,..tuko bil.7,kila mtu ana take pekee,na mifumo yetu ya mwili iko systematic,moyo ,ubongo,mapafu,damu,mifupa etc,..hii pia ni vilevile kwa mimea na wanyama na wadudu,..pia tukija kwa vitu ambavyo sio viumbe hai,ni same thing,kila rock/miamba ina identity yake pekee.so..kwa science hii kubwa na uwezo huu mkubwa,..Mungu wa ukweli ambae huenda sio huyu tunaefundishwa au kusikia ambae kwa mafundisho yaliyopo yanamfanya awe kama wa kawaida i mean kama bnadam vile,na ndomana kunakua na controversies nying watu wanakua hawaelew, hii ni very wrong,..Huyu alietuumba ,yan original Creator of all atakua anatushangaa sana.tunahangaika inshort...huyu creator ni very powerful,na science yake na phylosophy yake si ya kitoto,hana kwanza mda wa ku kedeal na mihemko ya watu wasio elewa au niseme kaumba kila kitu kiwe na self control kwasabab hakupenda kumuingilia mtu.so haya tunayo experienc ulimwenguni ni matokeo ya the life we choose n decide by ourselves,mfano,kufa,kuzaliwa,ulemavu,njaa,shibe,..etc n thts y leo hii ukiamua kujitoa dunian ,u can do tht,or kusitisha maisha ya mtoto alie tumbon,u can do tht.so doctrine aliyonayo the creator of all,ni kuubwa kuliko unavyodhani,.na projects anazozifanya the creator(We call him GOD) ni huuge ambazo haziko kwenye upeo wa mwanadamu.so The creator hajaumizwa na alichoandika huyu bwana sabab anajua hafaham the truth..The creator hana mda wa kumchoma mtu or sjui nin,sjui jehanam,etc na story nyiing za uongo,he created,n the creation goes on and on and on kwan sis wenyew we do sub creations humu humu ulimwengun...niishie hapo,kuna meng sana
Duh! hivi vitu ndo vinachanganya zaidi. So what if uyo Sub God ndo akawa chanzo cha mafundisho hayo ya Jehanamu, shetani n.k , sisi binadamu sasa tunapaswa kuobey au tuishi tupendavyo. Just want to know your thoughts.
 
Hahahaha we jamaa sikuzote unahasira sana na Mungu. Hebu nikuulize kidogo... unahisi sisi binadamu na Mungu, ni nani mwenye kumhitaji zaidi mwenzake?
Mungu anamuhitaji mwanadamu ili awepo ilihali mwanadamu hamuhitaji Mungu ili awepo.
Kuna watu wapo ambao tangu kuzaliwa kwao hawajawahi kumsikia wala kumtegemea Mungu.Lakini kama watu wata acha kumpa Mungu promo, basi Mungu hatakuwepo maana hakuna kitu kingine chenye kuthibitisha uwepo wake zaidi ya kelele za watu waliokuwa deluded.
 
Usichanganye dini na Imani.

Kama havina uwiano sasa dini kibao za nini? Hizo imani za uwepo wa Mungu zinaanzia wapi? Wanaojifanya wanaelewa si wamesoma?Kama uliwahi kuona muislam anasoma semonari,basi dini na imani ni tofauti
 
Mimi nilishaandika mengi kama haya nikaambiwa na wanaJF nitakufa ndani ya wiki mbili..wakatawa wanatag kuona kama niko hai..watu humu waoga hata kujadili
sio waonga tu...... there religious "fanatics" wamekalilishwa religious dogma believe without reason.
 
Wewe ni devil worshipper so hayo yote waambie wenzio wanaomwabudu shetani. Ushindwe kwa jina Yesu kristo aliehai.
 
Jamani naombeni niseme ivi,mnataka kujua kua tunachezewa akil na huyu mtu,nenden google then mkaandike hiko kichwa cha habar cha huo uzi ndio mtajua kua kafanya copy paste, kufurahisha jukwaa,tangu 2013 io topic ililetwa,na 2016 pia ililetwa mpk ktk magazetin, sasa sjui nani anamlisha ayo matango.
 
Back
Top Bottom